Nakala

UTANGULIZI


Shukurani zote zinamstahiki Allah peke yake,Rehma na amani


zimwendee Mtume(s.w.a) pamoja na ahli zake na swahaba wake wote.


Amma baad:


Hakika sababu za msingi zilizo nipelekea kuandika ki tabu hiki na


hali iliyo jionyesha ya kushamiri kwa harakati za Raafidhwa za


kuwalingania watu katika dhehebu hili potofu na harakati hizi zimekuwa


kiulimwengu, na kutokana na hatari kubwa ya kundi hili kwa dini ya


uislamu na kutokana na hali ya kughafilika na kuji sahau kwa waislamu


wengi kutokana na hatari ya kundi hili, na kutokana na itikadi yao iliyo


jaa ushirikina, na kuitukana Qur-an na Maswahaba-Radhi za Mwenyezi


Mungu ziwe juu yao-na kupituka mipaka juu ya Maimamu wao, ndio


maana nimeazimia kuandikakitabu hiki na kuyajibu mambo yanayo


watatiza watu kuhusu kundi hili kwa muhtasari, nikufuata nyayo za


Sheikh wetu Sheikh Abdallah bin Abdurahman-aljibrin- Mungu


amuhifadhi-katika kitabu chake "Atlaaliiqaat alaa Matni lumuatiliitiqaad"


na kwa kunukuu katika vitabu vya Raafidhwa ambavyo ni


maaraufu na mashuhuri kwao, na katika vya Ahlusuna miongoni mwa


wema walio tangulia na walio kuja baaada yao amabao waliwajibu


Raafidhwa na kubainisha ubovu wa itikadi zao zilizo simama juu ya


ushirikina, na uongo, na kuchupa mipaka, na matusi.


Na nimejaribu kwa kadri ya uwezo wangu katika kitabu hiki


kuwasimamishia hoja,kupitia vitabu vyao wanavyo vitegemea, kama


alivyo sema Sheikh Ibrahim bin Sulaiman Aljab-han-Mwenyezi Mungu


amrehem-"Nitakusimamishia hojakupitia mdomowako ewe Shi'a.


Mwisho na muomba Allah awanufaishekupitia kitabu hiki wenye


mazingatio kama alivyo sema Allah "Hakika katika hayo mna ukumbusho


kwa wenye kuwa na nyoyo zinazo zingatia, aumwenye kutega sikio na


hali moyo wake uko hadhir" Qaf:37


Natoa shukrani kwa kila alie changia katika kitabu hiki,namuomba


Allah awalipe kila la kheri.


Rehma na amani zimuendee bwana wetu Muhammad na ahli zake


na Maswahaba zake.


Imeandikwa na Abdallah Muhammad Assalafy.


- 4 -


NI LINI LIMEDHIHIRI KUNDI LA RAAFIDHWA?


Lili anza kundi la Raafidhwa wakati alipojitokeza Myahudi


mmoja aitwae (Abdallah bin sabai) akidai kuwa ni Muislam, na kwa


madai ya kuwapenda Ahlul bayt (watu wa nyumbani kwa Mtume) na


akapituka mipaka katika kumtukuza Ally (r.a) na akadai kuwa mtume


alimuusia kuwa khalifa baada yake, kisha akamnyanyua na kumuweka


katika daraja ya uungu na haya yanathibitishwa na vitabu vya kishia.


Kwa mfano Alqmmy katika kitabu chake (Almqaalatu walfiraq)


(1): Anakiri kuwepo kwake (Ibnu sabai) na anamzingatia kwamba ndie


mtu wa mwanzo aliesema kuhusiana na uimamu wa Ally na kurejea


kwake, na akaanzisha kuwatukana Abubakari na Omar na Uthmani na


maswahaba wengine, kama alivyosema Annuubkhty katika kitabu chake


(Firaq Shia) (2). Nakama alivyosema pia Alkushiy katika kitabuchake


maarufu ( Rijaalul-kushiy) (3). Na katika mashia wa sasa hivi wanaosema


kuwepo kwa Abdalla bin Sabai ni Muhammad bin Ally Al muallim


katika kitabu chake ( Abdallah bi Sabai Alhaqiikatul-majuhuula) (4). Na


mtu kukubali jambo ndio dalili kubwa, nahawa wote tulio wataja ni


katika Mashekhe wakubwa wa kiraafidhwa.


Amesema Albaghdaadiy: "Assabaiyya ni wafuasi wa Abdallah


bin Sabai ambae alichupa mipaka katika kumtukuza Ally (r.a) na kudai


kuwa alikuwa ni Nabii, Kisha akachupa mipaka zaidi mpaka akadai kuwa


alikuwa ni Mungu".


Na amesema Albaghdaadiy vilevile: "Na alikuwa Ibnu Saudaiyaani


Ibnu Sabai- Asili yake ni Myahudi katika watu wa Aliirah,


akadhihirisha Uislamu kwa kutaka awena ukubwa kwa watu wa Alkuufa,


akawaambia(watu wa kuufa) kwamba amekuta katika Taurati kwamba


kila Mtume anae waswiy (mrithi) na kwamba Ally (r.a) ndie mrithi wa


Mtume (s.a.w)".


Na amesema Ashihristany kuhusu Ibni Sabai kwamba ndie mtu


wa kwanza aliesema kwamba kuna nasswi (dalili) juu ya uimamu wa


Ally (r.a), na akaeleza kuhusu kundi la Sabaiya kwamba ndilo kundi la


kwanza lililo anzisha itikadi ya kutoweka kwa Imamu wao wa kumi na


mbili(Almahd Almuntadhwar) na kurejea kwake, kisha Shia wakarithi


itikadi hiyo baada yao, pamoja na kutofautiana kwa makundi yao,kuhusu


uimamu wa Ally na ukhalifa wake. Na hayo ni katika athari za Ibni Sabai,


na yaliongezeka makundi ya Shia na itikadi zao na kauli zao yakawa


makundi mengi sana.


Nahivi ndivyo walivyo zua Mashia itikadi ya Alwaswiy, Arrajaa,


Alghaiba, bali itikadi ya kwamba maimamu wao wanasifa za uungu (5)


kwa kumfuata Myahudi Ibnu sabai.


- 5 -





(1) Rejea: Almaqaalaatu wal firaq cha Alqummy uk.10-21


(2) Rejea: Firaqu Shia cha Anuubakhty uk. 19-20


(3) Rejea: aliyoyataja Alkushiy katika riwaya zake mbalimbali kutoka kwa Ibni Sabai na itikadi zake, tazama namba:


170,171,172,173,174 katika uk. 106-108


(4) Na kitabu hiki ni majibu ya kitabu alichokitunga mshia aitwae Murtadhwa Al-askary kwa anuani (Abdallah bin Sabai wa


asaatwiru ukhra) ambae alipinga katika kitabu chake kuwepo kwa Abdallah bin Sabai.


(5) Rejea Usuulu i-itiqaad Ahli Sunna waljamaa cha Allaalakaaiy (1/22-23).


- 6 -


KWANINI SHIA WAMEITWA RAAFIDHWA?


Jina hili kalitaja Sheikh wao Almajlisy katika kitabu chake


(Bihaarul-anwar) akasema katika mlango alio uita, mlango kuhusu (


Ubora wa raafidhwa na uzuri wa kujiita jina hili), kisha akataja kutoka


kwa Sulaiman Al-aamash kuwa amesema: niliingia kwa Abii Abdillah


Jaafar bin Muhammad nikasema kumwambia: Hakika watu wanatuita


Raafidhwa, nini maana ya Raafidhwa? Akasema: wallahi sio wao walio


kuiteni hivyo bali Mwenyezi Mungu alikuiteni hivyo katika Taurati na


Injili kupitia ulimi wa nabii Mussa na nabii Issa. (1)


Na imesemekana kuwa: wameitwa raafidhwa kwa sababu


walikuja kwa Ally bi Hassan wakamwambia: Jitenge na Abubakari na


Omar ili tuwe pamoja nawe, akasema: wao ni vipenzi wa Babu yangu,


siwezi kujitenga nao bali niko pamoja nao, wakasema: hivyo basi


tumekukataa, ndipo wakaitwa Raafidhwa, na akaitwa kila alie muunga


mkono Zaid kuwa ni Zaydiyya. (2)


Na inasemekana:wameitwa Raafidhwa kwa kupinga kwao utawala


wa Abubakari na Omar. (3)


Na imesemekana: Wameitwa hivyo kwa kukataa kwao Dini. (4)





(1) Tazama kitabu (Bihaarul-anwar) cha Almajlisy 65/97. (ambacho ni miongoni mwa marejeo yao muhimu katika vitabu vyao


vya sasa)


(2) Rejea: Attaaliqaat alaa matni lum-atul iitqaad cha Sheikh Abdallah Aljibriin uk.108.


(3) Tazama Maqaalaatul-Islaamiyiin cha muhyi ddiin Abdulhamiid (1/89)


(4) Maqaalatul Islamiyiin 1/89


- 7 -


RAAFIDHWA WAMEGAWANYIKA MAKUNDI MANGAPI?


Imekuja katika kitabu (Daairatul-maarif) kuwa "Makundi ya Shia


ambayo ni mashuhuru yako zaidi ya sabini na tatu"(1)


Bali imepokewa kutoka kwa Raafidhwa Mir baaqir Addaamand


(2) kwamba makundi yote yaliyotajjwa katika Hadithi, Hadithi ya


kugawanyika kwa Umma wa Muhammad katika makundi sabini na tatu


yamekusudiwa makundi ya Mashia, na kwamba lililotajwa kuwa ni kundi


lililosalimika ni kundi la imaamiyya.


Na ametaja Almaqriizy kuwa makundi yao yanafikia mia tatu .


Na amesema Ashihristany: "Hakika Raafidhwa wamegawanyika katika


makundi matano:Alqiisaaniyya, Azaydiyya, Al imaamiyya, Alghaaliyya,


Al ismaailiyya," (4)


Na amesema Albaghdaady: " Hakika Raafidhwa baada ya zama za


Ally (r.a) wako makundi manne: Zaidiyya, Imaamiyya, Kiisaaniyya, na


Alghulaatu" (5)


Lakini yakupasa kutambua kuwa Zaydiyya si katika kundi la


Raafidhwa ispokuwa kundi la Aljaaruudiyya.





(1) Rejea: Daairatul Maarif (4/67)


(2) Ni Baaqir bin Muhammad Al-istiraabaady, Maarufu kama Al-miir Addamaad, amekufa mwaka 1041.Tazama maelezo yake


katika kitabu (Alkunaa-wal-alqaab) cha Abbaas Alqummy 2/226


(3) Ni Almaqriizy (2/351)


(4) Rejea: Almilal wannihal cha Ashihristaany uk.147


(5) Rejea: Alfarqu bainal-firaq, cha Albaghdaady uk.41


- 8 -


NI IPI ITIKADI YA ALBADAA WANAYO IAMINI RAAFIDHWA?


Al badaa maana yake ni kudhihiri baada ya kutoweka, au kwa


maana ya kuanzishwa kwa rai mpya. Na neno hili (Albadaa kwa maana


zote mbili linamaanisha kuwepo hali ya kutojua jambo kisha kujua


kunakuja baadae, na mambo yote haya mawili kwa Allah ni muhali, aliki


Raafidhwa wanainasibisha sifahii ya ( Albadaa) kwa Mwenyezi Mungu.


Imepokewa kutoka kwa Rayyaani bin Asswalt kwamba


amesema:" nilimsikia Arridhwaa akisema: hajapata Mwenyezi Mungu


kumtuma nabii yoyote ispokuwa kwa kuharamisha pombe na kukiri


(Albadaa) kuwa ni katika sifa za Allah" (1)


Na kutoka kwa Abdalla amesema: 'Hajapata kuabudiwa


Mwenyezi Mungu kwa jambo lolote kama Albadaa" (2) katukuka


Mwenyezi Mungu na hayo kutukuka kukubwa kabisa.


Tazama ndugu yangu Muislam jinsi wanavyo mnasibishia Allah


sifa ya ujinga. Ilihali Mwenyezi Mungu anasema: " Hakuna alioko katika


Mbingu na Ardhi ajuae Ghaibu (yasio onekana au hayaja tokea) ila


Mwenyezi Mungu" Annaml 65


Badala yake wanaitakidi kuwa Maimamu wao wanajua elimu


zote, wala halifichikani kwao jambo lolote. Je hii inaweza kuwa itikadi ya


Uislamu aliyo kujanayo Muhammad (s.a.w)?





(1) Rejea; Usuullkaafi uk.40


(2) Rejea: Usuululkaafi cha Alkulayny katika kitabu tauhiid (1/331)


- 9 -


NI IPI ITIKADI YA RAFIDHWA KUHUSU SIFA ZA ALLAH?


Raafidhwa ndio watu (kundi) wa mwanzo waliopinga sifa za Allah na


kudai kuwa kumthibitishia baadhi ya sifa ni kumfanya kuwa ana


kiwiliwili. Sheikhul-islamu ibnu taymiya kamtaja mtu wa kwanza kuleta


itikadi hii katika Raafidhwa kuwa ni Hisham bin Al-hakam(1) na Hishamu


bin Saalim aljawaliiqiy na Yunusi bin Abdirahamani Alqummiy na abuu


jaafari al-ahwal(2).


Wote waliotajwa hapo juu ni katika mashekhe wakubwa wa


Ithnashariya,kisha wakawa jahmiyya wanaopinga sifa za Allah,kama vile


wengi wao katika riwaya zao nyingi walivyomsifu mwenyezi mungu kwa


sifa mbaya ambazo waliziambatanisha na sifa ambazo zinathibiti kwa


Allah(s.w)


Amepokea Ibnu Baabawaihi zaidi ya riwaya sabini (70) zinazosema


kuwa Allah, "hasifiki kwa zama,wala sehemu,wala namna,wala


kutikisika, wala kuhama toka sehemu hadi sehemu nyingine,wala hana


sifa miongoni mwa sifa za kimaumbile,wala huwezi kumuhisi,wala yeye


si kiwiliwili,wala hana sura".(3)


Na kwahiyo mashekhe wao wakafuata njia hii potofu,pamoja na


kuzikataa sifa za Allah zilizo thibit katika Qur-an na Sunna za mtume


(s.a.w)


Vilevile wanapinga na kukataa kuteremka kwa Allah (s.w)katika


mbingu ya dunia katika theluthi ya usiku kama ilivyo thibiti katika


hadithi sahihi,na wanasema kwamba Qur-an imeumbwa (sio maneno ya


Allah) na wanapinga kumuona Allah siku ya kiyam(hataonekana).


Imekuja katika kitabu (Bihaarul-an-waar) kwamba Abuu Abdillah


Jaafar Asaadiq,aliulizwa kuhusu Allah(s.w) je ataonekana siku ya


Qiyama?


Akasema ametakasika mwenyezi mungu na hilo kutakasika kuliko


kukubwa,hakika macho hayaoni isipokuwa kitu chenye rangi na


umbile,na mwenyezimungu ndie muumbaji wa rangi na maumbile(4).


Bali wamesema, lau kama mtu atamnasibisha Allah na baadhi ya


sifa, kama vile kuonekana, basi anahukumiwa kama ameritadi (katoka


katika uislamu). Haya yamepokewa kutoka kwa shekhe wao Jaafar


Annajafy(5).





(1)Rejea;Minhaaju sunna(1/20) cha sheikh Ibnu Taymiya.


(2)Rejea Itiqaadaatu firaqulmuslimiin walmushrikina uk.97


(3)Rejea; attauhiid cha Baabawayhi uk 57


(4)Rejea: Bihaarul-answer cha al majlis (4/31)


(5)Rejea: kashful ghitwai ukurasa wa 471


- 10 -


Lakini ni muhimu utambue (ndugu msomaji wa kitabi hiki)


kwamba Allah kathibitisha mwenyewe katika Qur-ani kuwa waumini


watamuona siku ya qiyama kama ilivyo kuja katika suratl qiyama "Nyuso


sikuhiyo zitakuwa ni zenye kung'ara.ni zenye kumtazama mola


wake."alqiyama:22-23.


Naimethibiti katika sunna sahihi za mtume,kama ilivyo katika


sahihi al bukhari na muslim,katika hadithi ya Juraiji bin Abdillah


Albajaly, kasema: "Tulikuwa tumeketi na mtume (s.a.w)akautazama


mwezi usiku wa tarehe 14 akasema:" "Hakika mtamuona mola wenu


kama mnavyouona mwezi huu, hampati shida katika kuuangalia."(1)


Na aya na hadithi zinazothibitisha jambo hili ni nyingi hatuwezi


kuziorodhesha zote.





1-Rejea katika bukhari no(544) na muslim no:(633) kwa faida


- 11 -


NI IPI ITIKADI YA RAAFIDHWA KUHUSU QUR-ANI HII TULIYONAYO


AMBAYO ALLAH KACHUKUA AHADI YA KUIHIFADHI?


Hakika Raafidhwa,ambao katika zama zetu ndio wanaitwa (SHIA)


wanasema: Hakika Qur-ani tuliyonayo siyo Qur-ani ile aliyoiteremsha


Allah(s.w) kwa mtume (s.a.w) bali imebadilishwa, ikazidishwa na


kupunguzwa.


Na jamuhuri wa wanachuoni wa hadithi wa kishia wanaitakidi


kwamba Qur-ani imebadilishw, hii ni kwa mujibu wa maneno ya Annuri


attwabrisiy katika kitabu chake (Faslul-khitwaab fii tahriif kitabu rablarbaab)(


1)


Na amesema Mohammad ibn Yaaqub Alkulayny, katika kitabu


chake (Usuulul kafi) katika mlango aliouita (Hawakuikusanya Qur-ani


yote isipokuwa maimamu)(anakusudia maimamu wao) kisha akaleta


riwaya ifuatayo: "Kutoka kwa Jaabir, amesema:nilimsikia Abu Jaafar


akisema: Hajapata kudai mtu yoyote kuwa kaikusanya Qur-ani yote kama


alivyo iteremsha Allah ispokuwa atakuwa ni muongo. Hakuna


alieikusanya na kuihifadhi kama alivyoiteremsha Allah ispokuwa Ally


bin Abii Twaalib na maimamu baada yake"(2).


Na imepokewa toka kwa Jaabir toka kwa Jaafar (mwenyezimungu


amrehemu) kwamba amesema: "Hawezi kudai mtu yoyote kwamba


anayo Qur-ani kamili ispokuwa walioachiwa wasia"(3)





1-Rejea: Faslulkhitwab cha Hussein bin Mahdi Taqiyyun-nuury Ahwabrasy uk.32


2-Rejea: Usululkaafi cha Alkulayn (1/228)


3-Rejea: Usululkafi cha Alkulayn (1/285)


- 12 -


Na imepokewa kutoka kwa Hisham bin Saalim, toka kwa Abii


Abdillah (Jaafari) amesema: "Hakika Qur-ani aliyokujanayo Jibrilu kwa


mtume (s.a.w) ni aya 17,000."(1)


Maana ya maneno hayo ni kwamba Qur-ani wanayoidai


Raafidhwa ni zaidi ua Qur-ani hii tuliyonayo, ambayo Allah kachukua


ahadi ya kuihifadhi zaidi ya mara tatu. Tunamuomba Allah atukinge na


upotevu wao.


Na ametaja Ahmadi Attwabrisi katika kitabu chake (Al-ihtiyaaJ)


kwamba Omar alimwambia Zaid bin Thaabit: Hakika Ally alikuja na


Qur-ani, ndani mnafedheha za muhajiriina na answari, na tumeonelea


tutaje Qur-ani_ nyingine_na tuyaondoe mambo yote ya fedheha za


muhajirin na answari, Zaid akakubaliana nae katika hilo.


Kisha akasema: Endapo mtamaliza kuiandika Qur-ani kama jinsi


mtakavyo nyinyi, halafu Ally akadhihirisha Qur-ani aliyonayo, je


hatakuwa kabatilisha kazi mliyoifanya?. Omar akasema: hivyo ni lipi la


kufanya? Zaid akasema: wewe ndio utajua ufumbuzi, Omar akasema:


Hakuna ujanja zaidi ya kumuuwa Ally ili tupate kupumua, akafanya


mipango ya kumuuwa Ally kupitia Khaalid bin Waliid, lakini hakuweza.


Pindi Omar alipotawala ukhalifa, alimuomba Ally awape Qur-ani


ili waibadilishe,akasema Umar: Ewe abal hassan(Ally) Waonaje


ungetuletea Qur-ani uliyokuwa umeileta kwa Abuu Bakari ili


tuwaunganishe watu katika msahafu mmoja? Akasena (Ally) Hakuna


uezekano wa jambo ulitakalo, kwani nilikuwa nimeuleta kwa Abuu


Bakari ili kunsimamishia hoja na ili msijekusema siku ya Qiyama


"Hakika sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo" Surat al aaraaf: 172 au


msijekusema "Haikutujia" Al araaf: 129, hakika hii Qur-ani hawaigusi


isipokuwa walio twaharika, na wale waliousiwa katika wanangu(kizazi


changu). Omar akasema: je kunamuda maalumu wa kuidhihirisha? Ally


akasema: Ni pale atakapo simama mtoto katika watoto wangu


akiidhihirisha na kuwaamrisha watu kuifuata.(2)





1-Rejea: usululkaaf cha alkulayny (2/634) kathibitisha shekhe wo riwaya hii katika kitabu chake (Qiraatu al-uquul) (12 525)


Akasema: hadithi hii ni thiqa(yakutegemewa)


2-Rejea: Al-ihtijaaj cha Attwabrisy, uk. 225 na kitabu Faslulkhitwab uk. 7


- 13 -


Na kwa vyovyote vile watakavyo jidai Mashia kukikana kitabu


(Annur) cha Attwabrisy, Kwa itikadi yao ya (Taqiya), Hakika kitabu


hicho kimejaa(kimesheheni) mamia ya dalili toka kwa wanazuoni wao


katika vitabu vyao tegemezi, zinazothibitisha kwamba wao wanaitikadi


na kuamini kuwa Qur-ani imebadilishwa isipokuwa hawapendi kuamsha


makelele ( na malumbano) kuhusu itikadi yao hii juu ya Qur-ani.


Na inabain kuwa kuna Qur-ani mbili, moja inayojulikana kwa


waislamu wote, na nyingine ni makhsusi(maalumu) imefichwa, na hiyo


ndio kunapatikana ndani yake surat Al wilaya, ambayo mashia wanadai


kwamba iliondolewa katika Qur-ani.


Pia katika aya ambazo wanadai kufutwa katika Qur-ani, ni ile


aliyoitaja Amry Attwabrasy katika kitabu chake (Faslulkhitwab fii tahriif


titab rabil arbaab) ambayo ni (Na tukainua utajo wako kwa ally ambaye


ni mkwe wako) Wanadai imeondolewa katika suratl-inshiraah(alam


nashrah) wala hawaoni haya katika madai yao haya hali yakuwa wanajua


wazi kuwa sura hii ni makkiyyah(imeteremshwa makkah) na Ally


hakuwa mkwe wa mtume makkah.


- 14 -


NI IPI ITIKADI YA RAAFIDWA KUHUSU MASWAHABA WA MTUME


(S.A.W)


Imejengeka itikadi ya Raafidwa juu ya kuwatukana na


kuwakufurisha masahaba wa mtume (s.a.w) rehema na amani zishuke juu


yao, Ametaja alkulayn katika kitabu(Furuul-kaafy) kutoka kwa Jaafary


(a.s) "waliritadi watu woote baada ya mtume (s.a.w) isipokuwa watu


watatu,Nikasema: ni kina nani hao watatu? Akasema ni Miqdaad ibnu


As-wad, na Abudhari al-ghifariy, na Salmaan al-faarisy".(1)


Na ametaja Almajlisy katika kitabu (Bihaarul-an-waay) kwamba


mtumishi wa Ally ibnul-Husain kasema: Nilikuwa naye (a.s_ katika


baadhi ya sehemu alizokuwa akijitenga, nikasema kumwambia: Hakika


mimi ninashakia baadhi ya haki kwako,naomba nieleze kuhusu watu


hawa wawili, Abubakari na Omar, Akasema: Nimakafiri na kila mwenye


kuwapenda ni kafiri". Pia imepokewa toka kwa Abi Hamza Athumaly


kwamba alimuuliza Ally bin Alhusain kuhusu Abubakari, Akasema;


"Nikafiri na kila atakaemuunga mkono pia ni kafiri.(2)1


1-Rejea: FURUUL-KAAFY cha Alkulayny uk.115 1


2- Rejea:BIHARUL-AN-WAR cha Almajlisy 69/137-138.


- 15 -


Na katika tafsiri ya Alqummy katika kauli yake mwenyezi mungu


"Na mwenyezi mungu anakataza kutenda kila makosa, na hasa madhambi


yaliyo pita mipaka kwa ubaya, na kila kisicho pendeza, hali kadhalika


anakataza kumfanyia ubaya mtu."nnahl ;90" Wametafsiri (Faahisha)Kuw


ni Abubakari na (Munkari) Kuwa ni Omar) na (Albagh-yi) Kuwa ni


Uthmani.(1)


Na ametaja Almajlisy katika (Biharul-an-war) Kuwa:Habari


zinazo onesha(elezea) ukafiri wa Abubakari na Omari na mfano wao, na


juu ya malipo ya kuwalaani na kujitenga nao, na habari zinazoelezea


uzushi wao ni nyingi kiasi kwamba haitoshi kuelezea katika kitabu hiki


au katika vitabu mbalimbali, lakini haya machache tuliyoyataja yanatosha


kwa mtu ambae Mwenyezi Mungu kataka kumuongoza katika njia iliyo


nyooka.(2)


Bali kataja Almajlis katika (Biharul-an -war) Riwaya mbalimbali


kwamba Abubakari na Omar na Uthmani na Muawiya (wenyezi mungu


awarehemu) kwamba watakuwa katika masanduku ya moto.(3)


- 16 -


Na wanasema(Raafidhwa) katika kitabu chao (Ihqaaql-haq) cha


Al-mar-ashy:"Ewe mwenyezi mungu mrehemu muhammad pamoja na


ahli zake, na walaani masanamu wawili wa kiquraish, na matwaaghuti


wao, na mabinti wao..." (4) wakiwa wanawakusudia Abubakari na Omar


na bibi Aisha na Hafswa bint Omar, mwenyezi mungu awarehemu.


1


1-Rejea: Tafsiri ya Alqummy uk 1/390


2-Rejea: Biharul-an-war cha Almajlisy30/230


3-Rejea: Biharul-an-war cha Almajlisy 30/236


4-Rejea: Ihqaaqul-haq 1/337.angalia dua ya masanamu wawili mwisho wa kitabu.


- 17 -


Na ametaja Almajlisy katika risala yake aliyo iita"Al-aqaaid" akasema: Na katika mambo


yanayozingatiwa kuwa ni muhimu sana katika dini ya Imaa miyyah ni kuhalalisha Mut-a, na Hajj


tamatui, na kujitenga mbali na watu watatu(Abubakari na Omar na Uthumani na Muawiya na Yazid


bin Muawiya, na kila aliye mpiga vita Amiril-muuminina Ally) (1)


Na katika siku ya Ashuraa (Rafidhwa)huleta mbwa na wakamita Omar, kisha wanaanza kumpiga


kwa fimbo na mawe mpaka anakufa, kisha wanaleta mtoto wa Mbuzi kisha wanamuita Aishan na kisha


wanaanza kumnyonyoa manyoya yake na kumpiga hadi anakufa.(2)


Pia huwa wanasherehekea siku aliyo uwawa Omar bin Alkhatwaabi, na wanamuita Abuu luu lu atilmajuusy


ambae alimuuwa Omar kuwa ni shuja wa dini(3)


Tunamuomba mwenyezi mungu awarehemu maswahaba wote pamoja wake zake mtume (s.a.w) ambao


ni mama w waumini.


Hebu tizama ndigu msomaji ubaya na chuki zilizo bebwa na kundi hili potofu lililo toka katika


uislamu, na mambo wanayosema juu ya watu wema kama hawa, ambao ndio watu bora baada ya


mitume, watu ambao mwenyezimungu kawasifu, na mtume wake pia, na umma wa kiislamu


umekubaliana juu ya uadilifu wao na ubora wao, bali hata historia inashuhudia ubora wao na juhudi


zao kubwa katika dini hii ya uislamu.





1-Rejea: Risaalatul-aqaaidi cha Almajlisy uk 85


2-Rejea: Tabdiil dhwalaam wa tanbii haan-myaam cha shekh Ibrahim aljabhaan uk 27


3-Rejea: Abbaasul-qummy (Alkunaa wal-alqaab 2/55


- 18 -


RAAFIDHWA WANAFANANA NA MAYAHUDI


Amesema sheikhul islamu bin taymiyyah mungu amrehemu,(ushahidi


juu ya hilo ni kwamba,Matatizo ya Rafidhwa ndio matatizo ya


Mayahudi,Kwa sababu Mayahudi wanasema:Ufalme haupaswi kuwa


isipokuwa katika kizazi cha Daudi,Na Raafidwa wanadai kuwa


utawala(al imama) haupaswi kuwa isipokuwa kwa mtoto wa Ally (R.A).


Pia mayahudi wanasema:Hakuna jihadi katika njia ya Allah mpaka


atakapo kuja Masihi Dajjali ashuke na upanga.Na Raafidwa wanasema:


Hakuna jihadi katika njia ya Allah mapaka atakapokuja Mahdi na utoke


wito wa jihadi kutoka mbinguni.


Pia Mayahudi huchelewesha sala zao mpaka nyota zinapo kusanyika,


Vilevile Raafidwa nao huchelewesha magharibi mpaka nyota


zikusanyike,Ilhali hadithi ya Mtume(S.A.W) Inatufundisha


kwamba(Hautaacha kuwa ummati wangu katika kheri muda wa kuwa


hauicheleweshi sala ya magharibi mpaka kukusanyika kwa nyota)1


Mayahudi waliigeuza Taurati,Vilevile Raafidwa nao wameigeuza Qurani.


Mayahudi wanapinga jambo la kupangusa katika khofu: Vilevile


Raafidhwa wanalipinga jambo hilo.


Mayahudi wanamchukia Malaika Jibrilu, Wanasema: Huyo ni adui yetu


miongoni mwa malaika.Vilevile Raafidwa wanasema: Jibrilu alikosea


kuleta utume kwa Muhammad(S.A.W).1


Vilevile Mayahudi na Wakristo wamewashinda Raafidwa kwa mambo


mawili,Kwanza: waliulizwa Mayahudi: Ni nani aliye bora katika watu wa


mila yenu? Wakasema: wabora kwetu ni wafuasi wa Musa.Nawa


wakristo wakaulizwa:ninani aliebora katika mila yenu? Wakasema: Ni


wanafunzi wa nabii Issa(Yesu).


Raafidwa wakaulizwa ninani M-baya zaidi na muovu katika mila yenu?


Wakaema wafuasi wa Muhammad(S.A.W)1


Na ametaja Sheikh Abdallah al-jamiily katika kitabu chake (Badhlul


majhuud fii mushabahati arrafidwa lil yahuud) Kwamba katika mambo


mbayo Raafidwa wamefanana na Mayahudi ni,Mayahudi na


Maraafidhwa wanawakufurisha watu wote wasiokuwa miongoni mwao


na kuzihalalisha damu zao na mali zao,Kisha sheikh akasema: Mayahudi


wanawagawa watu katika mafungu mawili tu(Mayahudi na


ummamiyuun) Ummamiyuun ni kila asiekuwa Yahudi,na wanaitakidi


kwamba wao ndio waumini pekeyao,Ama Ummamiyuun wao ni makafiri


- 19 -


NI IPI ITIKDI YA RAAFIDWA JUU YA MAIMAMU?


Raafidwa wanadai maimamu wao ni (Maasuumiin) yaani


wamehifadhiwa na madhambi, na kwamba wanajua ghaibu. Kayanukuu


haya alkulayniy katika kitabu (usuulul-kaafy) : "Kasema Imamu Jaafar


Asswadiq : Sisi ni hazina ya elimu ya Mwenyezimungu, Sisi ni wafasiri


wa amri za Mwenyezi Mungu,Sisi ni watu tuliokingwa na dhambi,


Imeamrishwa tutiiwe, na imekatazwa tusiasiwe, Sisi ndio hoja ya


Mwenyezi Mungu ya wazi kwa viumbe vilivyo chini ya ardhi na mbingu


na vilivyo juu ya Ardhi". (1)


Pia kasema Alkulayny katika (Alkaafy) Katika mlango aliouita


mlango kuhusu (kwamba maimamu pindi wanapotaka kujua jambo basi


hujua tu), Imepokewa toka kwa Jaafar kwamba amesema "Hakika imamu


anapotaka kujua basi hujua tu, na kwamba wao wanajua muda wa kufa


kuwa ni lini, na kwamba wao hawafi ila kwa hiyari yao wenyewe" (2)


Na amesema Alkhumainiy katika kitabu chake (Tahriirul-wasla)


kwamba "Hakika Imamu anayo nafasi tukufu, na daraja ya juu, na


utawala wa kufanya kila kitu viko chini ya utawala wake vyote vilivyo


katika ulimwengu" na akasema pia "Hakika sisi (anakusudia maimamu


wa ithnasharia) tunazo hali Fulani kwa Mwenyei Mungu ambazo hazipati


malaika wala nabii yoyote".(3)





(1)Rejea: Usuululkaafy cha Alkulayniy 1/165


(2)Rejea: Usuululkaafy cha Alkulayniy 1/258


(3)Rejea: Tahriirul-walah cha Alkhumainy uk.52,94


tu wala hawamjui Allah (s.w).Imekuja katika kitabu chao (Attilmuud)


Kwamba: Mataifa yoote wasiokuwa Mayahudi ni washirikina.


Wamemkufurisha hata Nabii Issa (A.S),Kama ilivyokuja katika


Attilmuud, wamemsifu na kumtaja kuwa ni kafiri,wala hamjui Mungu.


Raafidwa nao wanaitakidi kwamba wao ndio waumini pekeyao,na kila ambae si Raafidwa basi ni kafiri wala


hana fungu lolote katika uislamu.


Ama kuhusu sababu za Raafidwa kuwakufurisha wailamu ni kwakuwa hawaitakidi(Al wilaya) Ambayo ndio


itikadi ya Raafidwa, na kwamba jambo hili ni nguzo katika nguzo za Uislamu na kila asie itakidi hivi basi huyo ni


kafiri kwa mujibu wa imani yao ni kama ambae hajatamka shahada mbili,au ni sawa na alie acha sala tano, bali


Alwilaya kwao ni jambo ambalo limetangulizwa juu ya nguzo zote za Uislamu.


Amepokea Albarqiyu kutoka kwa Abdallah(a.s) kwamba amesema(hakuna yoyote anaefuata mila ya Ibrahimu


isipokuwa sisi tu na wafuasi wetu, Ama watu wengine wote wamejitenga na mila yake.)


Na imekuja katika tafsiri ya Alqummy, kuwa imepokewa kutoka kwa Abdallah(a.s) kwa amesema(Hakuna


yoyote alie katika mila ya Uislamu isipokuwa sisi,mpkaka siku ya Qiyama)1


- 20 -


Bali imefikia hali kwa Maraafidhwa waliochupa mipaka katika


kuwatukuza na kuwafadhilisha (kuwafanya bora) maimamu


wao,wamewafanya bora juu ya manabii wote isipokuwa Muhammad


(s.a.w) (1)


Hawakuishia hapo tu, bali wanasema kuwa maimamu wao


wanautawala wa mwisho kabisa. Ameyataja haya Alkhui katika kitabu


chake (Misbaahul-faqaaha) akasema: Ni wazi kwamba hakuna shaka


kabisa juu ya utawala wao juu ya viumbe wote, kama ilivyo bainisha


katika maneno yao, kwa kuwa wao ndio sababu ya ulimwengu, na wao


ndio sababu ya kupatikana viumbe, maana kama si wao basi watu wote


wasingeliumbwa, bali wameumbwa kwa ajili yao, na kuwepo kwao ni


kwaajili yao….. na utawala walionao maimamu ni kama utawala wa


Mwenyezi Mungu juu ya viumbe wake".(2)


Tunamuomba Mwenyezi Mungu atulinde na upotevu wao huu!!


Vipi maimamu wawe ndio sababu ya kupatikana viumbe? Vipi wawe


sababu ya kuwepo ulimwengu? Vipi watuwote waumbwe kwaajili ya


maimamu wao, ilhali Mwenyezi Mungu anasema katika sura


Adhaariyaati 56 "Sikuwaumba majini na watu ila tu wapate kuniabudu".


Tunamuomba Mwenyezi Mungu atukinge na itikadi potofu kama


hii inayopingana na qur-ani na suna za Mtume (s.a.w).


Kasema Sheikhul-islamu bin Tayimiya (Wanadai Raafidwa kuwa


dini inafuata matakwa ya wanachuoni wao,halali ni ile wanao ihalalisha


wao, na haramu ni ile wanao iharamisha wao,na dini ni yale


wanayoyataka wao".





(1) Rejea: mir-aatul-uquul fii shar-hi akhbari rasuul cha Almajlisiy 2/290


(2) Rejea: mis-baulfuqaaha cha Abil-qaasim Alkhui 5/33


(3) Rejea: minhaajusunna cha IbnuTayymiya 1/482.


- 21 -


NI IPI ITIKADI YA KUREJEA WANAYO IAMINI RAAFIDWA?


Raafidwa wamezua bid-a (uzushi) wanayoiita (AR-RAJ-A),


Kasema Almufiid kuwa: "Wamekubaliana Imamiya juu ya kurudi


(kufufuka) wengi katika watu waliokufa".(1)


Na itikadi hii inakusudia kufufuka kwa imamu wao wa mwisho


wanaemuita (Al-qaaim) atatoka katika zama za mwisho akitokea katika


pango, ambaye atakuja kuwauwa wapinzani wake wote na kuwarejeshea


mashie haki zao walizo porwa na makundi mbalimbali katika historia ya


kuwepo kwao.(2)


Amesema Assayid almurtadhwa katika kitabu chake (Almasaailu


annaaswira) kwamba Abubakari na Omar, watasulubiwa katika zama


hizo(za kutoka kwake) huyo imamu wao wa kumi na mbili wanaimuita


(Qaaim ahali Muhammad) na kwamba mti utakuwa mbichi kabla ya


kusulubiwa kwao lakini baada ya kusulubiwa kwao utakauka.(3)


Na amesema Almajlisy katika kitabu (Haqul-yaqiin) kutoka kwa


Muhammad Albaaqir: " pindi atakapodhihiri Almahdi, basi atamfufua


bibi Aisha kisha amsimamishie hadd (adhabu)". (4)


Kisha wakayapanua makusudio na maana ya Arraj-a na kudai kuwa


Mashia wote watafufuka na maimamu wao, na wagomvi wao nao


watafufuka na maimamu wao.


Itikadi hii potofu inatubainishia chuki kubwa zilizo fichika katika


nafsi zao ambazo zinawapelekea kueleza upotofu kama huu, na itikadi hii


ndio iliwapelekea As-abaiyya wakakanusha kuwepo siku ya mwisho.





(1) Rejea:Awaailul-maqaalaat cha Almufiid uk.5


(2) Rejea:Alkhtuutul-ariidhwa, cha muhibuddin alkhaatwib uk.80


(3) Rejea: Awaailul-maqaalsst cha Almufiid uk.95


(4) Rejea: Haqul-yaqiin cha Muhammadul-baaqir Almajlisy uk.347


- 22 -


Na madhumuni ya kurejea ni kulipiza kisasi kwa wagomvi wao,


lakini ni akina nani wagomvi wao? Riwaya ifuatayo itakubainishia ndugu


msomaji chuki waliyonayo Raafidhwa dhidi ya Ahlusunna, na jinsi


walivyo karibu zaidi na Mayahudi na Manaswara: Ameeleza Almajlisy


katika kitabu chake (Biharul-anwar),kutoka kwa Abii baswiir kapokea


toka kwa Abu Abdillah(a.w) amesema: alisema: Ewe abu muhmmad:


kanakwamba ninatazama kushuka kwa (alqaim) katika masjidis-sahla


akiwa na watu wake na familia yake….mpaka akasema…


nikamwambia,Atakuwa na msimamo gani kuhusu Ahlu dhimma?


Akasema:Atawapa amani kama alivyowapa amani mtume (s.a.w), na


watatoa kodi hali ya kuwa ni madhalili,nikasema, je waliokufanyieni


uadui? Akasema :Hapa ewe Abu muahammad,yeyote alietukhalifu katika


dola yetu hatakuwa na nafasi yoyote, hakika Mwenyezi mungu


katuhalalishia damu zao, wakati atakapokuja Alqaim, lakini pindi


atakaposimama huyo msimamaji wetu, atalipiza kisasi kwa ajil ya


Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kwaajili yetu pia.91)


Hebu tazama ndugu muislamu jinsi gani huyo Mahdi wa Mashia


atawapa amani Mayahudi na Manaswara, halafu awapige vita Ahlu


sunna!





(1) Rejea: Biharul-anwar cha Almajlisy 25/376.


- 23 -


NI IPI ITIKAD YA "TAQIYYAH" KWA RAAFIHDHWA?


Amesema taqiya mmoja wa wanazuoni wao wa zama hizi kuwa


"Taqiya ni kitendo cha mtu kusema au kufanya kinyume na vile anavyo


itakidi, kwa lengo la kujikinga na madhara yeye au mali yake au kulinda


utu na heshima yake" (1)


Na wanadai kwamba mtume (s.a.w) alifanya (Taqiya) wakati


alipokufa kiongozi wa wanafiki Abdallh bin Ubayi bin Saluul, pindi


alipokuja kumswalia, kisha Omar (r.a) akamwambia Mtume (s.a.w) Hivi


Mwenyezimungu si kakukataza kumsalia mtu huyu mnafiki?, Mtume


(s.a.w) akamwambia wewe unajua ni nini nimesema? Nimesema : Ewe


mola wangu mjaze ndani yake moto, na ulijaze kaburi lake moto, na


umuingize motoni" (2)


Hebu tazama nduguyangu muislamu vipi wanamzulia na


kumnasibisha Mtume (s.a.w) na uwongo?! Hivi inaingia akilini kwamba


maswahaba wa mtume (s.a.w) wanamtakia reham na Mtume (s.a.w)


akimlaani?!.


Na amenukuu Alkulayny katika (Usuulul kafii):"kasema Abu


Abdillah : Ewe Omar hakika asilimia tisa ya dini ipo katika taqiya, na


hana dini asiyekuwa na Taqiya, na Taqiya inaingia katika kila kitu


isipokuwa katika pombe na kupangusa juu ya khofu".


Na amenukuu vilevile Alkulayny toka kwa Abi Abdillah kwamba


amesema "icheleeni dini yenu, na ikingeni kwa Taqiya, kwa hakika hana


imani asiyekuwa na Taqiya"(3)





(1) Rejea: Ashiatul miizaan, cha Muhammad JawadMughniyat uk.47


(2) Rejea: Furuu-ulkafii, kitabul janaiz uk 188


(3) Rejea: Usuulul kafii uk 482-483.


- 24 -


Bali imefikia hali kwa Raafidwa wanajuzisha kuapa kwa asiye kuwa


Mwenyezi Mungu kwa mujibu wa Taqiya!!


Ameyaeleza hayo Alhurul aamily katika kitabu chake (Wasaailu shia)


kuwa imepokewa kutoka kwa ibu Bukhari, toka kwa Zuraara toka kwa


Abi Jaafar (r.a) amesema: nilisema kumwambia Abu jaafar : Hakika sisi


tunapita kwa watu wanatutaka tuape juu ya mali zetu na ilhali


tumeshakwisha zitolea zaka, akasema (Abujaafar): Ewe Zurara pindi


utakapo chelae hilo basi wewe apa kwa vyovyote vile


watakavyotaka,Nikamuuliza : Hata kuapa kwa talaka? Akasema kwa


chochote watakacho taka.


Na imepokewa toka kwa Sumaa toka kwa Abii Abdillah (a.s) amesema:


"Pindi mtu atakapo apa kwa Taqiya hakuna tatizo maadam kalazimishwa,


na kalazimika kufanya hivyo".(1)


Raafidhwa wanaitakidi kuwa Taqiya ni faradhi ambayo madhehebu yao


hayasimami bila ya Taqiya, na wanaitumia hasahasa katika mazingira


magumu, hivyo inatakiwa ndugu muislamu utahadhari sana na hawa


Raafidhwa.





(1) Rejea: wasaailu shia cha Al-hurril-omily 16/136-137.


- 25 -


NI IPI ITIKADI YA UDONGO WANAYOIAMINI RAAFIDHWA?


Makusudio ya udongo katika itikadi ya Raafidhwa, ni udongo wa


kaburi ya Hussein (r.a) Ameeleza mmoja wa wapotevu miongoni mwao


aitwae Muhammad Amnuumanul-haarithy,ambae wanamuita (Asheikhul


mufiid) katika kitabu chake (Al mazaar) imepokewa kutoka kwa Abi


Abdillah kwamba amesema:" katika udongo wa kaburi ya


Hussein,kunapatikana ponyo la kila maradhi,nao ndio dawa iliyo kubwa


kabisa'.


Na amesema Abdallah : wafanyieni tahniki ( yaani watilieni


mdomoni mara tu baada ya kuzaliwa kwao) watotowenu kwa udongo wa


kaburi ya Hussein.


Na akasema vilevile: Alitumiwa Abdul Hussein Arridhwa mzigo


(furushi la nguo) kutoka khurasaan ndani yake mkiwa na


udongo,akaulizwa alie tumwamzigo huo, Ni kitu gain hiki?


Akasema:Huu ni udongo kutoka katika kaburi ya Hussein.Hapakuwa


panatumwa mzigo wowote isipokuwa ndaniyake panawekwa udongo,


anasema:Udongo huu ni amani kwa idhini ya Mwenyezi mungu. Na


inasemakana kwambamtu mmoja alimuuliza swaadiq kuhusu kutumia


udongo wa kaburi la Hussein, akajibu kumwambia: Pindi utakapoula basi


sema hivi: Ewe Mola wangu hakika mimi nakuomba kwa haki ya ufalme


ulioushika,na kwa haki ya Mtume aliye hifahiwa,nakuomba umpe rehma


Muhammda (s.a.w) pamoja na watu wa nyumba yake, na ujaalie udongo


huu kuwa ni ponyo la kila ugonjwa,na uwe ni kitulizo cha amani


kutokana na kila khofu, na niulinzi kutokana na kila baya.


Pia Raafidhwa wanadai kwamba, Mashia wameumbwa kwa


udongo maalum,na Sunni wameumbwa kwa udongo mwingine kisha


ukachanganywa udongo huo wote,basi maasi na maovu yanayofanya


Mshia yeyote ni kutokana na athari ya udongo walioumbiwa Masunni. Na


kheri na uongofu anaekuwanayo Sunii yeyote ni kutokana na athari za


Udongo walioumbwa shia.Pidni itakapofika siku ya qiyama, basi maovu


ya Mashia watabebeshwa Masunni, na mema ya Masunni watapewa


Shia.(1)





(1) Rejea: Ilaalu asharaa uk. 490-491. Biharul anwar 5/247-248


- 26 -


NI IPI ITIKADI YA RAAFIDWA KUHUSU AHLU SUNNAH?


Miongoni mwa itikadi mbaya za Raafidwa ni kwamba


wanahalalisha damu na mali za Ahlu sunnah Amepokea aswadiq katika


(Al-ilal) kutoka kwa Daa-uudi bin Farqad amesema: "Nilimuuliza abu


abdillah, unasemaje kuhusu Naasiby? (Naswibi wanakusudia


Ahlusunnah), akasema:Damu yake ni halali, hatakama utaweza


kumuangushia ukuta au kumzamisha baharini basi fanya


hivyo.Nikamuuliza vipi kuhusu mali yake? Akasema pindi utakapoweza


kuichukua basi ichukue".(1)


Pia Raafidhwa wanaitakidi kwamba kizazichao ndio kizazi safi,


Ameeleza Hashimu Albaharany katika tafsiri yake(Alburhan) imepokewa


toka kwa maytham bin Yahya,kutoka kwa Jaabir bin Muhammad,


amesema"Hakuna mtoto yoyote azaliwaye isipokuwa Ibilisi anakuwa


haadhir katika kuzaliwa kwake,anapojua mtotohuyo ni katika Shia basi


shetani mkubwa anamkinga huyo mtoto kutokanan na ibilisi, na kama sio


katika shia basi shetani huingiza kidolechake katika sehemu zake za


nyuma(katika makalio ya mtoto), nah ii ndio sababu ya kuwa mtoto wa


kiume huzaliwa kaelekea chini, na kama ni mtoto wa kike basi shetani


huingiza kidole chake katika utupu wake, hivyo anazaliwa akiwa ni


muovu, na ndio maana mtoto huzaliwa analia sana"(2)


Bali mashie wanaitakidi kwamba watu wote ni watoto wa zinaa


isipokuwa Shia peke yao!! Ameeleza Alkulayny katika kitabu chake


(Arraudhwatu minalkafi) kutoka kwa Abi Hamza,kutoka kwa Abu Jaafar


(a.s) kwamba amesema: "Nilisema kumwambia, hakika baadhi ya jamaa


zetu wanazua uwongo na kuwatuhumu wasio waungu mkono, akamjibu


kuwa, kuachana nao ni bora zaidi, kasha akasenma: Wallah ewe Abu


Hamza hakika watu wote ni watoto wa zinaa isipokuwa Shia".(3)





(1) Rejea: almahaasin Annafsaaniya uk166


(2)Rejea: Tafsirul burhani cha Hashim Albahrany 2/300


(3) Rejea: Arraudhwatul minalkafi cha Alkulayny 8/285.


- 27 -


Na katika itikadi za raafidwa wanaona kwamba Ahlusunna ukafiri


wao ni mkubwa zaidi kuliko ukafiri wa Mayahudi na manaswara, kwa


sababu wao asili yao ni Makafiri, ama Ahlisunna kwamba wao


wameritadi,na ukafiri wa kuritadi ni mkubwa zaidi, hii ni kwa mujibu wa


ijmai, na ndio mana wanakuwa bega kwa bega dhidi ya waislamu, kama


historia inavyojieleza.(3)


Imekuja katika kitabu (wasaailu shia) kutoka kwa Alfudhwail bin


yasaar amesema: "Nilimuuliza Abu Jaafar je naruhusiwa kumuozesha


Naswibii mwanamke wa kirafidwa? Akasema: Hapana, kwa sababu


Naswibii ni kafiri" (4)


Na manaswibii kwa ahlusunna ni wale ambao wanamchukia Ally


bin Abitwaalib(r.a), lakini Raafidwa wao wanawaita ahlusunna Naswibii,


kwa sababu wanamtanguliza Abubakari na Omar na Uthmani juu yaAlly,


pamoja na kwamba kumtanguliza Abubakari na Omar n Uthmani juu ya


Ally ndivyo ilivyo kuwa zama za Mtume (s.a.w), na ushahidi wa haya ni


kauli ya ibni Omar: ". Na amezidisha Attwabrani katika Alkabiir:


"Tulikuwa tukifadhilishwa baina ya watu katika zama za (s.a.w)


tunamfadhilisha Abubakari kisha Omar Kisha Uthmani " Amepokea


bukhari. Na amezidisha Attwabrani katika alkabiir: "Na Mtume (s.a.w)


alikuwa akilijua hilo wala hatukemei katika hilo". Pia ibnu Asskir


amesema :"tulikuwa tukimfadhilisha Abubakari na Omar na Uthmani na


Ally".


Amepokea imamu Ahmad na wengineo kutoka kwa Ally bin Abi


twalib kwamba amesema: Mbora wa umma huu baada ya Mtume (s.a.w)


ni Abubakari kisha Omar, na laiti ningependa ningemtaja wa tatu".


Amesema Imamu Ahnad kwamba athari hii ni mutawaatir.(5)





(4) Rejea: wasaail shia cha Alhurul aamily (7/431) Attahdhiib (7303)


(5)Attaaliqaat alaa matni lumuatul-iitqaad cha sheikh Jibrin uk.910


- 28 -


NI IPI ITIKADI YA RAAFIDHWA KUHUSU NDOA YA MUT'A NA INA


UBORA GANI KWAO?


Ndoa ya mut'a inafadhila kubwa kwa Raafidhwa, kama wanavyo


dai, imekuja katika kitabu (Manhaju sswadiqiin) cha fat'hullah


Alkaashan, kapoke a toka kwa Asswaadiq: Hakika Mut'a ni katika dini


yangu na dini ya baba yangu, basi mwenye kuifanya hiyo anatekeleza


dini yetu, na mwenye kuipinga,huyo atakuwa anaipinga dini yetu, bali


huyo anaifuata dini nyingine isiyokuwa dini yetu, Na mtoto anaezaliwa


katika ndo ya mut'a ni bora kuliko anaezaliwa katika ndoa ya kawaida,


Na mwenye kuipinga mut'a huyo ni kafiri ameritadi, (1)


Amenukuu Alqummy katika kitabu (Man laa yahdhuruhul- faqiih)


kutoka kwa abdallah bin sinani, kutoka kwa Abdillah amesema: "Hakika


mwenyezi mungu mtukufu katuharamishia kinyaji chochote chenye


kulevya, na akatupa badalayake mut'a" (2)


Naimekuja katika (Tafsiri ya manhaju sswaadiqiin) ya Mullah


Fat'hullah Alkaashaany: "Amesema mtume (s.a.w) Mwenye kufanya


mut'a mara moja, basi huachwa huru na moto theluthi yake, na mwenye


kufanya mara mbili huachwa huru na moto theluthi mbili, na mwenye


kufanya mara tatu,basi huachwa huru na moto yeye mzima"


Na katika kitabu hichohicho, imekuja kuwa "kasema Mtume


(s.a.w) mwenye kufanya mut'a mara moja, basi huyo kasalimika na


ghadhabu za Mwenyezi mungu, na atakae fanya mara mbili atafufuliwa


pamoja na watu wema, na atakaefanya mara tatu huyo atakuwa nami


peponi".


Pia katika kitabu hichohicho kwamba amesema Mtume(s.a.w)


mwenye kufanya mut'a mara moja, anakuwa katika daraja ya Hussein, na


mwenye kufanya mut'a mara mbili yuko katika daraja ya Hassan, na


mwenye kufanya mut'a mara tatu, anakuwa katika daraja ya ally bin


Abitwaalib, na mwenye kufanya mara nne daraja yake ni kama daraja


yangu"(3)





(1) Rejea: manhaju sswaadiqiin cha Mullah Fut'hullah Alkaashany 2/495


(2) Rejea;man laa yah dhuruhulfaqiih cha ibnu baabawaihi Alqummy uk. 330


(3) Rejea: Tafsir Manhaju sswaadiqiin cha mullah Fut'hullah Alkaashany 2/ 492-493


- 29 -


Na marafidhwa hawakuainisha idadi maalumu katika swala la


mut'a, imekuja katika (Furuu ul kaafy) na (Attahdhib) na (al-istibuswari)


kutoka kwa Zuraara kapokeya toka kwa Abiabdillah, kasema :"Aliulizwa


kuhusu mut'a kwamba je nikatika wanawake wa nne walio ruhusiwa?


Akasema:waweza kuowa mpaka elfu moja, kwa sababu wao ni mwenye


kukodiwa. Na pia imepokewa kutoka kwa Muhammad bin muslim,


kutoka kwa Abi Jaafar kwamba, alisema kuhusu ndoa ya mut'a: kwamba


hao sikatika wale wa nne, kwa sababu mwanamke anaye olewa ndoa ya


mut'a hapewi talaka, wala hana fungu lolote katika mirathi,bali yeye ni


mwenye kukodiwa tu ".(1)


Vipi hali hii na ilihali Mwenyezi Mungu anasema "Na wale ambao


tupu zao wanazilinda.Isipokua kwa wake zao au kwa (wanamwake) wale


iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao ndio wasio


laumiwa.(Lakini)Anaye taka kinyume cha haya basi hao ndio warukao


mipaka (Ya Mwenyezi Mungu).(Almu-uminun 5-7).


Kwa hiyo aya hizi zinatubainishia kwamba ndoa zinazo ruhusiwa


ni mke na wale iliyo wamiliki mikono ya kuume,na kinyume na hawa


basi ni haramu, hivyo mut'a ni zinaa, tunamuomba Mwenyezi Mungu


atukinge na shari.


Amesema sheihk Abdallah bin Jibrin kwamba (Raafidhwa katika


kuhalalisha mut'a wanaitumia aya iliyokuja katika suratun nisaai aya ya


24 " Na pia (mmeharamishiwa)wanawake wenye(waume zao) isipokua


wale iliyo wamiliki mikono yenu ya kuume(ndio)sheriya ya Mwenyezi


Mungu juu yenu.Na mmehalalishiwa(kuowa wanawake)wasio hawa


muwatafute kwa mali zenu, kwa kuwaowa bila ya kufanya zinaa. Basi


wale mnao waowa miongoni mwao wapeni mahari yao yalyio lazimishwa


.Wala si vibaya kwenu katika (kutoa) yale mliyo ridhiana badala ya yale


yaliyo tajwa.Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi na mwenye


hekima."Annisaai:24





(1) Rejea: Alfuruu minal kaafi cha Alkulayny 5/451 na Attahdhib 2/188.


- 30 -


Na jawabu la hoja hii ni kwamba: Hakika aya zote hizi kuanzia


aya ya 19 hadi aya ya 23 zinazungumzia ndoa, kisha baada ya kutaja wale


walio haramishwa kwa nasabu na kwa sababu zingine akasema


Mwenyezi Mungu "Mmehalalishiwa wanawake wengine wasio kuwa


hawa walio tajwa, basi pindi mtakapo waoa ili kustarehe nao kihalali,


basi wapeni mahari zao mlizo kubaliana, na kama wakisamehe chochote


katika hizo mahari zao kwa ridhaa zao basi hakuna ubaya katika hilo."


hivyo ndivyo walivyo ifasiri aya hii kongamano la maswahaba na walio


kuja baada yao".(1)


Hata Shekh wa kundi la Attusy katika kitabu chake (Tahadhiibulahkaam)


ameitaja kwa ubaya ndoa ya Mut`a, anasema:"Kama akiwa


mwanamke anatoka katika nyumba ya watu watukufu basi haifai kumuoa


katika ndoa ya mut`a, kwa kuchelea aibu itakayo ipata familia yake na


udhahalili utakao mpata yeye". (2)


Bali hali imefikia kwa hawa Rafidhwa wanahalalisha kumuendea


mwanamke kinyume cha maumbile.Yamekuja haya katika (Alistibswaar)


kutoka kwa Ally bin Alhakam amesema;"Nilimsikia swaf


wani anasema:Nilimuuliza Ar-ridhwaa nikasema:Hakika mmoja katika


wafuasi wako kanituma nikuulize jambo ambalo yeye kaogopa na kaona


aibu kukuuliza,akasema;nilipi ?akasema:Je inafaa mtu kumuingili mke


wake kinyume cha maumbile? Akasema:Ndio inafaa." (3)





(1) Ni katika maneno ya Shekhe Ibnu Jibrin.na dalili nyingine ya kuharamisha mut`a katika suna za Mtume(s.a.w) ni Hadithi ya


Rabiu bin Sabura Aljuhany kwamba babayake alimuhadithia kwamba alikuwa pamoja na Mtume (s.a.w) akasema:"Enyi watu


hakika mimi nilkuwa nimekuruhusuni kufanya Mut`a ,hakika Mwenyezi mungu ameiharamisha mpaka siku ya Qiyama,yoyote


ataye kuwa na mwanamke ambaye kamuoa ndoa ya Mut`a basi na amuache,na wala asichukue chochote alichokuwa kampa".


Kaipoke Muslim Nnambari (1406).


(2)Rejea: Tahdhiibul-ahkaam cha attusy 7/227 .


(3) Rejea: Al-istibswaar cha Attuusy (3/243).


- 31 -


NI IPI ITIKADI YA RAFIDHWA KUHUSU NAJAF NA KARBALAA,


NA JE KUNA FADHILA GANI KATIKA KUZURU SEHEMU


HIZI?


Mashia wanaitakidi sehemu yalipo makaburi ya watu walio dai


kuwa ni maimamu wao, au ambao ni maimamu kweli, kwa sehemu hizo


ni sehemu takatifu,hivyo Alkuufa ni haram(sehemu takatifu),pia Karbalaa


ni haram,na Qumm nayo ni haram. Na wanayo riwaya wanayo dai


kuwa imepokelewa kwa Asswaadiq kwamba, Mwenyezi mungu anayo


haram yake ambayo ni makka,na Mtume wake anayo haram yake ambayo


ni Madina,na amiiril-mu`uminiina anayo haram yake ambayo ni


Alkuufa,na sisi tunayo haram yetu ambayo ni qumm.


Na Kar-balaa kwa Mashia ni bora kulikko Alqaaba. Imekuja katika


kitabu(Bihaarul-anwar)kutoka kwa Abii Abdillah kwamba kasema;


"Hakika Mwenyezi mungu aliiteremshia Alqaaba wahyi(ufunuo)lau kama


si udongo wa Kar-balaa nisingelikufanya bora ,na lau kama si mwili wa


yule aliyeko katika udongo wa Kar-balaa nisingekuumba,wala nisinge


umba nyuba ambayo kwayo umejifakharisha,basi tulia na uwe ni Mkia


dhalili na si mwenye kibri kwa ardhi ya kar-balaa,la sivyo nitakutupa


katika Jahannam" (1)


Bali rafidhwa wanaona kuzuru kaburi la Husein huko karbalaa ni


bora kuliko nguzo ya tano ya uislamu(Hijja)!!. Amesema Almajlisy


katika kitabu chake (Bihaarul-anwar)Kutoka kwa bashiir addahaan


amesema;"Nilimuuliza Abuu Abdillah(a.s) Endapo itanipita hijja alafu


nikaenda katika kaburi ya Husein? Akasema:Vizuri sana ewe


Bashir,muumini yeyote atakae liendea kaburi la Husein hali ya kutambua


haki yake,katika siku ambayo sio siku ya idd,basi huandikiwa thawabu za


Hijja 20 na Umra20 zenye kukubaliwa,na thawabu za kushiriki katika


vita 20 vya Jihadi pamoja na Mtume au Imamu muadilifu, na atakaye


liendea siku ya Arafa hali ya kujua haki zake basi huandikiwa thawabu za


Hijja 1000 na Umra 1000 zenye kukubaliwa,na thawabu za kupigana


Jihadi 1000 pamoja na Mtume au Imamu muadilifu.





(1)Rejea kitabu Albihaar(10/107)


- 32 -


Pia katika kitabu hicho hicho wametaja kwamba wanao zuru kaburi


la hussein huko karbalaa ni watu safi,na wanaokuwa wamesimama Arafa


ni watoto wa Zinaa!!"imepokewa toka kwa Ally bin Asbaatwi kwamba


kapokea toka kwa Abi Abdillah(a.s) kuwa kasema:Hakika Mwenyezi


mungu Mtukufu anaanza kuwatazama wanao zuru kaburi la hussein usiku


wa kuamkia Arafa.Akasema:Nikamuuliza,Kabla hajawatazama walioko


katika kisimamo cha Arafa?akasema;Ndio,nikamuuliza,kwanini iwe


hivyo? akasema: Kwa sababu katika watu walioko Arafa mna watoto wa


zinaa tofauti na wale walioko Karbalaa hakuna mtoto wa zinaa kati yao".


(1)


Bali kiongozi wao mkuu Ally Assistaany katika kitabu


chake(Minhaajus-swaalihina)Amefadhilisha kuswali katika makaburi


kuliko kuswali katika Miskiti!! Kasema katika mas-ala nambari


562:Inapendeza kuswali katika makaburi ya maimamu (a.s)bali


imesemekana kuwa ni bora kuliko kuswali miskitini, na imepokewa


kwamba kuswali katika kaburi la imamau ally bin Abi twaalib(a.s)ina


ubora wa swala laki mbili. (2)


Bali Shekh wao Abbas Alkaashaany katika


kitabuchake(Maswaabiihul-jinaani)kapituka mipaka katika kuitukuza


Karbalaa mpaka akasema:" Hapana shaka kwamba Karbalaa ndio sehemu


takatifu zaidi katika uislamu,na imepewa utukufu ambao haikupewa


sehemu yoyote ardhini,na hii ni kwa mujibu wa dalili nyingi zilizo


pokewa kuhusu jambo hili,hivyo ikafanywa ndio ardhi ya Allah(s.w)iliyo


tukuzwa na kubarikiwa,na ni ardhi iliyo nyenyekea, na ni ardhi iliyo


teuliwa na ndio haram ya Alla yenye baraka na amani,na ndio haram ya


Mtume,na ndio kitovu cha uislamu,na ni katika sehemu ambazo Allah


anapenda kuomba na kuabudiwa katika sehemu hizo,na ndio ardhi


ambayo udongo wake ni tiba, hakika sifa hizi na nyinginezo zilizopo


katika ardhi ya karbalaa,hazipatikani katika sehemu yoyote ardhini,hata


katika alkaaba". (3)





(1) Rejea;Bihaarul-anwar cha Almajsliy 85/98


(2) Rejea:Minhaajus-swalihiin cha Assisaany 1/187


(3)Rejea; Maswaabiihul-jinaan cha Abbaasi Alkaashaany uk 360.


- 33 -


Pia imekuja katika kitabu(Almazaar) cha Muhammad


Annuumaan,wenyewe wanamuita (Ashaikhulmufiid) akielezea ubora wa


Masjid alkuufa:Imepokewa toka kwa Abii Jaafar Albaaqir amesema:"Lau


watu wangejua fadhila zinazo patikana katika masjidulkuufa basi


wangeliuandalia matumizi na vipandwa kutoka sehemu mbalimbli ili


kuuendea,hakika swala ya faradhi katika msikiti huo ni sawa na Hijja ,na


swala ya sunna ni sawa na umra."(1)


Pia imekuja katika kitabu hicho hicho katika mlango aliyo uita


(Yasemwayo wakati wa kusimama katika kaburi) kwamba mwenye


kumzuru Hussein anatakiwa kuashiria kwa mkono wake wa kuume, na


aseme katika dua ndefu kabisa,miongoni mwake maneno


yafuatayo:"Nimekujia kukuzuru,nikitaraji uthibitishwe unyayo wangu,na


nina yaqini kwamba Mwenyezi mungu Mtukufu anawaondolea waja


wake matatizo yao kupitia kwenu, na kwa sababu yenu anateremsha


rehma,na kupitia nyinyi anaizuia ardhi isiwadidimize watu wake,na


kupitia nyinyi kayathibitisha mjabali yake.Ninamuelekea Mola wangu


kupitia kwenu ili mnikidhie haja zangu,na mnisamehe madhambi yangu."


(2)


Hebu tazama ndugu msomaji jinsi watu hawa walivyo tumbukia


katika ushirikina ,kwa kumuomba asiye kuwa Allah awakidhie haja


zao,na kuomba kusamehewa madhambi yao kwa asiye kuwa Allah, vipi


wamefikia katika hali hii,na ilihali Mwenyezi Mungu anasema"Hakuna


anaye samehe madhambi ila Allah".Al-imraan: 135. Tunamuomba Allah


atukinge na ushirikina.





(1)Rejea:Kitaabul-mazaar cha sheikh Almufiid uk. 20.


(2)Rejea:kitaabul-mazaar cha sheikh Almufiid uk. 99.


- 34 -


NI MAMBO GANI AMBAYO RAAFIDHWA WAMETOFAUTIANA NA


AHLU SUNNAH?


Amesema Nidhwaamud-diin muhammad al-a`adhwamy katika


utangulizi wa kitabu chake (Ash-shiiatu wal-mut`a) :"Hakika tofauti


zilizopo kati yetu na Ahlusunnah sio tofauti za kifiqhi peke yake, kama


vile mas`ala ya Mut`a n.k hapana,bali asili ya tofauti zetu ni katika


mambo ambayo ndiyo misingi ya dini(Mambo ya kiitikadi) kama haya


yafuatayo:


(1)Rafidhwa wanadai kwamba Qur-ani imebadilishwa,hivyo ina


mapungufu. Nasisi tunasema:hakika Qur-ani ni maneno ya Allah


yaliyo timia wala hayana mapungufu


yoyote,hayakubadilishwa,wala hayatabadilishwa aidha kwa


kupunguzwa au kuongezwa mpaka siku ya Qiyama. Kama alivyo


sema Allah "Hakika sisi tumeuteremsha ukumbusho(Qur-ani),na


hakika sisi tutauhifadhi". Alhijri 9


(2)Rafidhwa wanadai kuwa maswahaba wa Mtume(s.a.w) waliritadi


baada ya kufa Mtume(s.a.w)ispokuwa wachache tu,na wakafanya


khiyana katika dini hasa hasa Makhalifa watatu;Abubakari,Omar


na Othman. Na kwa hiyo Makhalifa hawa watatu ni Makafiri na ni


wapotevu kwa mujibu wa imani ya kishia. Nasisi tunasema;Hakika


maswahaba wa Mtume(s.a.w) ndio viumbe bora baada ya


Mitume,na kwamba wote ni waadilifu,hawawezi kumsingizia


Mtume(s.a.w),na ni wakweli katika yale waliyo yanukuu kutoka


kwa Mtume(s.a.w).


(3)Rafidhwa wanadai kuwa:Hakika maimamu wao kumi na mbili ni


maasuumiin(wamehifadhiwa na madhambi),na kwamba wanajua


ghaibu na wanayo elimu yote waliyo pewa Malaika ,Manabii na


Mitume,na kwamba wanajua mambo yote yaliyo pita na


yajayo,halifichikani kwao jambo lolote,na kwamba wao wanazijua


lugha zote za ulimwenguni na kwamba dunia yote ni ya kwao. Na


sisi tunasema kwamba: Wao ni viumbe kama viumbe


wengine,wamo miongoni mwao wanachuoni,na Makhalifa.Wala


haifai kuwanasibisha na jambo ambalo wao hawakujinasibisha nalo


bali wao walikataza mambo hayo na kujitenga mbali nayo kabisa.



 



Machapisho ya hivi karibuni

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI

KWANINI UISLAMU? UZU ...

KWANINI UISLAMU? UZURI NA FAIDA ZA UISLAMU