
FADHILA ZA SIKU KUMI
(ZA MWANZO) ZA DHUL-HIJA
Kiswahili
Kamati ya Kielimu ya Jumuia ya Kuhudumia Maudhui
za Kiislamu kwa Lugha Mbalimbali.
FADHILA ZA SIKU KUMI (ZA MWANZO)
ZA DHUL-HIJA
FADHILA ZA SIKU KUMI (ZA MWANZO)
ZA DHUL-HIJA
Utangulizi
Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu
Mola Mlezi wa walimwengu, na rehema na amani
zimfikie yule aliyetumwa kuwa rehema kwa
walimwengu, na kwa watu wake, na Maswahaba
zake, na wale waliofuata mwenendo wake, na
wakaongoka kwa muongozo wake, mpaka siku ya
Malipo. Ama baada ya hayo:
Huu ni ujumbe mfupi, uliokusanya mambo
muhimu anayoyahitaji Muislamu katika fadhila za
siku
kumi za mwanzo wa Dhul-Hija.
Tumezikusanya kwa ajili ya mwenye kutembelea
Misikiti Miwili Mitukufu, mwanamume na
mwanamke; ili wawe na elimu na utambuzi na
mambo ya dini yao, tukitaraji kutoka kwa
Mkarimu, Mwingi wa kuneemesha awanufaishe
kwa ujumbe huu, na aufanye kuwa wenye kufaa, na
uwe kwa ajili ya kutaka uso wake tu. Kwani, Yeye
ndiye mbora wa wenye kuombwa na Mkarimu
zaidi anayetarajiwa.
Kamati ya Kielimu ya Jumuia ya Kuhudumia Maudhui
za Kiislamu kwa Lugha Mbalimbali.
1
Fadhila za siku kumi (za mwanzo) za
Dhul-Hija:
Siku kumi (za mwanzo) za Dhul-Hija, ubora
wake ni mkubwa mno. Ameubainisha Mwenyezi
Mungu Mtukufu katika kitabu chake, na
akaubainisha Mtume wake Muhammadi, rehema
na amani ziwe juu yake, katika mafundisho yake.
Nazo ndizo zile siku ambazo ameapa kwazo
Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani ya Kitabu
chake katika kauli yake:
"Ninaapa kwa (wakati wa) Alfajiri. Na kwa
usiku kumi (wa mwanzo wa Dhul-Hija)." [Surat
Al-Fajri: 1-2] .
Nazo ni siku kumi (za mwanzo) za Dhul-Hija,
kama alivyosema (Abdullahi) bin Abbas,
(Abdullahi) bin Zubairi, Mujahid, (imamu) bin
Kathiri, (imamu) bin Al-Qayyim na zaidi ya
mmoja katika wema waliotangulia na wale
waliofuata baada yao.(1)
Nazo ni siku ambazo kufanya matendo ndani
yake huwa bora zaidi kuliko hata kupigana vita
katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu; kwa
hadithi ya (Abdullahi) bin Abbas, radhi za
Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, kwamba
(1) Tazama Tafsiri bin Kathiri 4/106, na Zaadul-Ma'aadi 1/56.
2
alisema: Alisema Mtume, rehema na amani ziwe
juu yake: "Hakuna siku ambazo kufanya matendo
mema ndani yake hupendeza zaidi kwa Mwenyezi
Mungu kuliko hizi siku kumi." Wakasema: "Ewe
Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Hata kupigana
Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu?" Akasema
Mtume, rehema na amani ziwe juu yake: "Hata
kupigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu,
isipokuwa mtu aliyetoka kwa nafsi yake na mali
yake, na akawa hakurudi na chochote katika
hivyo."(1)
Matendo bora zaidi katika siku kumi (za
mwanzo) za Dhul-Hija:
1- Kutekeleza Hija na Umra. Haya ni katika
matendo bora zaidi ndani ya siku kumi hizi; kwa
kauli ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake:
"Atakayehiji na akawa hakusema maneno
machafu wala kutenda matendo machafu, atarudi
kama siku aliyozaliwa na mama yake (akiwa hana
dhambi)."
Na katika tamko la Muslim: "Atakayeiendea
nyumba hii, na akawa hakusema maneno
machafu wala kutenda matendo machafu, atarudi
(1) Kaipokea Bukhari, na Tirmidhi na tamko hili ni lake.
3
kama siku aliyozaliwa na mama yake (akiwa hana
dhambi)."(1) Kauli yake: "Atakayeiendea nyumba
hii", inajumuisha kwa muktadha wake Hija na
Umra, na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu.
Na amesema Mtume, rehema na amani ziwe juu
yake. "Kufanya Umra mpaka Umra nyingine
kunafanya
mtu kusamehewa madhambi
yanayofanyika baina ya Umra hizo mbili. Na Hija
iliyokubalika haina malipo isipokuwa Pepo."(2)
2- Kufunga siku tisa (za mwanzo za Dhul
Hija) au zitakazowezekana katika hizo. Hili ni
kwa kauli ya Mtume, rehema na amani ziwe juu
yake: "Hakuna siku ambazo kufanya matendo
mema ndani yake hupendeza zaidi kwa Mwenyezi
Mungu kuliko hizi siku kumi." Na swaumu ni
miongoni mwa matendo mema matukufu zaidi
ambayo alihimiza juu yake Mtume, rehema na
amani ziwe juu yake, na akahamasisha juu yake.
Miongoni mwake ni kauli yake, rehema na amani
ziwe juu yake: "Hakuna mja yeyote atakayefunga
siku moja katika njia ya Mwenyezi Mungu,
isipokuwa Mwenyezi Mungu atauweka mbali kwa
(1) Kaipokea Bukhari na Muslim.
(2) Kaipokea Bukhari na Muslim.
4
siku hiyo moja uso wake na moto misimu
sabini."(1)
3- Ni sheria kuchinja udhuhiya siku ya
kuchinja na siku za Tashriiq (kubanika
nyama). Imethibiti kuwa Mtume, rehema na
amani ziwe juu yake: "Alichinja siku ya Idi kondoo
wawili weupe wenye pembe. Aliwachinja kwa
mkono wake, akataja jina la Mwenyezi Mungu juu
yake, akatoa takbira na akaweka mguu wake juu
ya shingo zao."(2)
Na imesimuliwa kutoka kwa Aisha, radhi za
Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwamba
alisema: Alisema Mtume wa Mwenyezi Mungu,
rehema na amani ziwe juu yake: "Hajawahi
kufanya mwanadamu tendo lolote siku ya
kuchinja (siku ya Idi) linalopendeza zaidi kwa
Mwenyezi Mungu kuliko kumwaga damu. Na
hakika kitaletwa kichinjwa hicho siku ya Kiyama
kikiwa na pembe zake, nywele zake na kwato
zake. Na hakika damu hiyo hufika kwa Mwenyezi
Mungu katika mahali (pa kukubalika) pake kabla
(1) Ameipokea Bukhari na Muslim.
(2) Ameipokea Bukhari na Muslim.
5
haijadondoka katika Ardhi. Basi zisafisheni
kwavyo (vichinjwa) nafsi zenu."(1)
Na zinapoingia siku kumi (za mwanzo) za Dhul
Hija; atajizuia aliyekusudia kuchinja kunyoa
nywele zake na ngozi yake; kwa mujibu wa
hadithi ya Ummu Salama, radhi za Mwenyezi
Mungu ziwe juu yake, kutoka kwa Mtume,
rehema na amani ziwe juu yake, ya kwamba
alisema: "Mtakapouona mwezi mwandamo wa
Dhul-Hija, na akataka mmoja wenu kuchinja;
basi ajizuie kunyoa nywele zake na kupunguza
kucha zake." Na katika tamko jingine: "...basi
kamwe asichukue chochote katika nywele zake
wala katika kucha zake mpaka atakapochinja
dhabihu wa Idi."(2)
4- Takbira (kusema: Allaahu Akbaru), na
tahlil (Laa ilaaha illa llaahu), na kumtaja
Mwenyezi Mungu ndani ya siku hizi kumi na siku
za Tashriiq (kubanika nyama); kwa hadithi ya
Abdallah bin Omari, radhi za Mwenyezi Mungu
ziwe juu yao, kutoka kwa Mtume, rehema na
amani ziwe juu yake, kwamba alisema: "Hakuna
siku tukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu
wala zinazopendeza zaidi kufanya matendo
(1) Kaipokea Tirmidhi.
(2) Kaipokea Muslim.
6
ndani yake, kuliko siku hizi kumi (za mwanzo za
Dhul-Hija). Basi zidisheni sana ndani yake:
Tahlili - yaani kusema: Laa ilaaha illa llaah
(hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu),
na Takbiri - yaani kusema: Allaahu Akbaru
(Mwenyezi Mungu ni Mkubwa), na Tahmidi -
yaani kusema: Alhamdulillaah (sifa njema ni za
Mwenyezi Mungu)."(1)
Na takbira zina aina mbili, kama ifuatavyo:
Aina ya kwanza: Takbira zisizo na mipaka. Nazo
ni zile ambazo hazihusiani na baada ya swala;
bali zinaruhusika nyakati zote.
Zinaanza takbira zisizo na mipaka katika Idil
Adhha kuanzia siku ya kwanza ya siku kumi (za
mwanzo) za Dhul-Hija mpaka siku ya mwisho
katika siku za Tashriiq (kubanika nyama), katika
nyakati zote: usiku, mchana, barabarani, sokoni,
msikitini, nyumbani na maeneo yote yanayofaa
ndani yake kutajwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Aina ya pili: Takbira zenye mipaka: Nazo ni zile
zinazofungamanishwa na swala katika idil
(1) Kaipokea Ahmad.
7
Adhha hasa. Na wakati wake na namna yake ni
kama ifuatavyo:
Kwanza: Zitaanza takbira zenye mipaka baada
ya swala ya Alfajiri siku ya Arafa, na zitamalizika
baada ya swala ya Laasiri siku ya tatu katika siku
za Tashriiq (kubanika nyama). Hili ni kwa
asiyekuwa hujaji. Na ama hujaji, yeye zitaanza
takbira zenye mipaka kuanzia Adhuhuri ya siku
ya kuchinja.
Pili: Namna ya kufanya takbira: Allaahu
Akbaru, Allaahu Akbaru. Laa ilaaha illa
llaahu, wallaahu Akbaru, Allaahu Akbaru
walillaahil Hamd. Yaani: Mwenyezi Mungu ni
Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. Hakuna
mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa
Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni
Mkubwa. Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, na kila
sifa njema ni zake Yeye Mwenyezi Mungu.(1)
5- Pupa ya kutekeleza swala ya Idi kwa
asiyekuwa hujaji, kutoa takbira wakati wa
kuiendea na kusikiliza hotuba. Kwani, hilo ni
miongoni mwa alama kubwa za Uislamu.
Na kwa sababu ya ukubwa wa jambo lake,
wameamrishwa kuiendea wanawake mpaka
mabikira na wenye hedhi. Imesimuliwa kutoka
(1) Tazama: Al-Mughni, cha bin Qudama 3/290, na Ashsharhul
Kabiir pamoja na Al-Muqni wal-Inswaaf 5/380.
8
kwa Ummu Atwiya, radhi za Mwenyezi Mungu
ziwe juu yake, kwamba alisema: "Tulikuwa
tukiamrishwa kutoka siku ya Idi mpaka tukawa
tunawatoa
mabikira
majumbani
mwao
wanamojihifadhi, vile vile mpaka tukawa
tunawatoa wenye hedhi, kisha wanakaa (uwanjani)
nyuma ya wanawake. Wakawa wanatoa takbira
kwa takbira zao, na wanaomba kwa dua zao, na
wanataraji baraka za siku hiyo na utakasifu wake."
Na katika tamko jingine: "Na aliwaamrisha
wenye hedhi wajitenge mbali na mahali
wanaposwalia Waislamu."(1)
6- Kukithirisha matendo mema, miongoni
mwa ibada za sunna: Kama vile swala, sadaka,
kusoma Qur'ani Tukufu, kuamrisha mema na
kukataza mabaya, kumtendea wema jirani,
kuunga udugu na mengineyo miongoni mwa
matendo mema, kwa ujumla wa kauli yake
rehema na amani ziwe juu yake: "Hakuna siku
ambazo kufanya matendo mema ndani yake
hupendeza zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko hizi
siku kumi." Wakasema: "Ewe Mjumbe wa
Mwenyezi Mungu! Hata kupigana Jihadi katika njia
ya Mwenyezi Mungu?" Akasema Mtume wa
Mwenyezi Mungu, rehema na amani ziwe juu yake:
"Hata kupigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi
(1) Ameipokea Bukhari na Muslim.
9
Mungu, isipokuwa mtu aliyetoka kwa nafsi yake na
mali yake, na akawa hakurudi na chochote katika
hivyo."(1)
Na Mwenyezi Mungu pekee ndiye mwenye
kuombwa atunufaishe kwa yale tuliyojifunza, na
atufunze yale yenye kutunufaisha. Hakika Yeye
ndiye Mpaji, Mkarimu. Na rehema na amani
nyingi zimuendee Nabii wetu Muhammadi na
watu wake.
(1) Kaipokea Bukhari na Tirmidhi, na tamko hili ni lake.
10
Yaliyomo
Utangulizi ................................................................................... 1
Fadhila za siku kumi (za mwanzo) za Dhul-Hija: .... 2
Matendo bora zaidi katika siku kumi (za mwanzo)
za Dhul-Hija: ............................................................................. 3