Nakala

MASWALI 60 KWA WAKRISTO


UTATU


Kwa mujibu wa Wakristo wengi, Yesu amekuwa ni Mungu-mtu, mtu kamili


na Mungu kamili. Je, kitu chenye mwisho na kile kisicho na mwisho


vinaweza kuwa ni kimoja? Kuwa “Mungu kamili” maana yake ni kutokuwa


na mwisho na kutohitajia msaada, na kuwa “mtu kamili” maana yake ni


kutokuwa na uungu.   


1. Kuwa mtoto ni kuwa chini ya daraja ya uungu na kuwa na uungu ni


kutokuwa mtoto wa yoyote. Vipi Yesu atakuwa na sifa ya utoto na


uungu kwa wakati mmoja?


2. Wakristo wanadai kwamba Yesu alidai kuwa yeye ni Mungu wakati


walipomnukuu katika Yohana 14:9: “…Aliyeniona mimi amemwona


Baba…” Je, Yesu hakusema wazi wazi kwamba: kamwe watu


hawakumuuona Mungu, kama inavyosema Yohana 5:37: “Naye Baba


aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wowote,


wala  sura yake hamkuiona”?


3. Wakristo wanasema kwamba Yesu alikuwa ni Mungu kwa sababu


alikuwa anaitwa mtoto wa Mungu, Mtoto wa mwanadamu, Masiha, na


“mwokozi.” Ezekiel aliandikwa katika Biblia kama ni mtoto wa


Mungu. Yesu alinena kuhusu “waletao amani” kuwa ni Watoto wa


Mungu. Mtu yoyote aliyefuata matakwa na Mipango ya Mungu


alikuwa akiitwa MTOTO WA MUNGU katika utamaduni wa


Kiyahudi na katika lugha yao (Mwanzo 6:2,4; Kutoka 4:22; Zaburi


2:7, Warumi 8:14) neno “Messiah” ambalo kwa Kiebrania


linamaanisha “Mpakwa Mafuta wa Mungu” sio “Kristo”, wala


“Cyrus” na mtu huitwa “Messiah” au “mpakwa mafuta”. Ama kuhusu


neno “mwokozi” liliopo katika Wafalme wa pili 13:5, watu wengine


walipewa jina hilo vile vile bila ya kuwa miuungu. Kwa hivyo, katika


maneno hayo uko wapi uthibitisho unaoonesha kuwa Yesu ni Mungu


wakati neno mtoto halikutumiwa kwake peke yake?


4. Wakristo wanadai kwamba Yesu alikiri kwamba yeye na Mungu


walikuwa ni kitu kimoja kwa maana ya Kimaumbile pale anaposema


katika Yohana 10:30; “Mimi na Baba tu umoja.”, Baadae katika


Yohana 17:21-23, Yesu alinena kwamba wafuasi wake, yeye


mwenyewe na Mungu ni kitu kimoja katika sehemu tano. Sasa kwa


nini walipe neno “Kitu kimoja” la kwanza maana nyingine tofauti na


yale maneno “kitu kimoja” katika sehemu tano nyinginezo?


5. Je, Mungu ni watatu-katika-mmoja na ni mmoja katika watatu kwa


wakati mmoja au ni mmoja kwa wakati huo huo?


6. Ikiwa Mungu ni mmoja na watatu kwa wakati mmoja, kwa hiyo


hakuna hata mmoja kati ya hao watatu ambae ni Mungu kamili.


Tukikubali kwamba huo ndio ukweli, sasa je, wakati Yesu alipokuwa


duniani, hakuwa Mungu kamili, wala “Baba aliyembinguni” hakuwa


Mungu kamili. Je, hilo halileti mkanganyiko kwa kile alichokuwa


akikisema Yesu kila siku kuhusu Mungu wake na Mungu wetu


aliyembinguni, Bwana wake na Bwana wetu? Je, hilo vile vile


halimaanishi kwamba hakukuwa na Mungu kamili, katika kipindi cha


kati ya dai la kusulubiwa na dai la kufufuka?


7. Ikiwa Mungu ni mmoja na watatu kwa wakati mmoja, sasa nani


aliyekuwa Mungu huko mbinguni wakati Yesu alipokuwa aridhini?


Je, hili halileti mkanganyiko na yale aliyokuwa akiyasema mara


nyingi juu ya kuwa Mungu aliyembinguni ndiye aliyemtuma?


8. Ikiwa Mungu ni mmoja na watatu kwa wakati mmoja, je, nani


aliyekuwa Mungu huko mbinguni katika zile siku tatu zilizo kati ya


dai la kusulubiwa na dai la kufufuka?  


9. Wakristo husema kwamba: “Baba (B) ni Mungu, Mwana (M) ni


Mungu na Roho Mtakatifu (R) ni Mungu, lakini Baba si mwana, na


Mwana si Roho Mtakatifu, na Roho Mtakatifu si Baba”. Kwa hesabu


rahisi na kwa kanuni inakuwa hivi, ikiwa B = G, M = G na R = G;


kwa kufuatanisha inakuwa B = M = R, wakati sehemu ya pili ya


maelezo hayo inaonesha kuwa B№ M№ R (inamaanisha haziko


sawa). “Sasa je, huo si mkanganyiko na imani ya Wakristo juu ya


utatu wenyewe?


10. Ikiwa Yesu alikuwa Mungu, kwa nini alimwambia yule  mtu


aliemwita Yesu “Bwana Mwema” alimwambia asimwite “mwema”


kwa sababu hakuna mwema ila Mungu wake aliyembinguni peke


yake?  


11. Kwanini Wakristo wanasema kwamba Mungu ni watatu katika mmoja


na mmoja katika watatu, wakati Yesu alisema katika Marko 12:29.


“Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja” kama ilivyo katika sehemu


nyingi ndani ya Biblia.


12. Ikiwa kuamini utatu lilikuwa ni jambo la lazima ili uwe Mkristo, kwa


nini Yesu hakulifundisha na wala hakulisisitiza jambo hilo kwa


Wakristo katika zama zake? Je, vipi hao wafuasi wa Yesu


wachukuliwe kuwa ni Wakristo bila ya kulisikia neno utatu? Kama


ingekuwa utatu ndio uti wa mgongo wa Ukristo, Yesu angeliufundisha


na angeliusisitizia na angeliufafanua kwa watu wake kikamilifu.


13. Wakristo wanadai kwamba Yesu alikuwa Mungu kama


walivyomnukuu katika Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno,


naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”. Hayo


ni maneno ya Yohana na si maneno ya Yesu, vile vile, neno la kwanza


la Kigiriki kwa ajili ya Mungu ni “HOTHEOS” ambalo linamaanisha


“Mungu” likiwa na M kubwa, wakati neno la pili la Kigiriki kwa ajili


ya Mungu ni “TONTHEOS” ambalo linamaanisha “mungu” likiwa na


“m” ndogo. Je, huko si kukosa uaminifu kwa wale waliotafsiri Biblia


ya Kigiriki? Je, nukuu hiyo ya Yohana 1:1 iliyotambuliwa na kila


mwanazuoni wa Kikristo aliyeisoma Biblia kwamba imeandikwa na


Myahudi aitwae Philo Alexandria kabla ya Yesu na Yohana?


14. Je, neno “god” au “TONTHEOS” pia halikutumika kuashiria wengine


kama ilivyo katika Wakorinto 2  4:4 (Na Shetani ndie) mungu wa


ulimwengu huu na katika Kutoka 7:1 “Angalia, nimekufanya wewe


kuwa kama Mungu kwa Farao; ?


WOKOVU:


Wakristo  wanasema kwamba “MUNGU AEMTOA” mwanawe wa pekee


ili kutuokoa sisi”. Je, Mungu alimtoa Yesu kumpa nani wakati yeye Mungu


ndiye mmiliki wa ulimwengu wote?


15. Ikiwa ilikubalika kwa utukufu wa Mungu kuwa awe na watoto, basi


angeumba mamilioni ya watoto kama Yesu. Sasa kuna jambo gani


kubwa kumhusu huyu mtoto wa pekee?


16. Kwa nini Biblia inasema kwamba Yesu alitaka kufa msalabani, huku


yule mtu aliyesulubiwa pale msalabani alikuwa anapiga kelele


“Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” kwa mujibu wa


Matayo 27:45 na Marko 15:33?


17. Ikiwa Mungu alitaka kutuokoa, Je, angeshindwa kutuokoa bila


kumtoa muhanga Yesu?


18. Mungu yeye mwenyewe ni haki, na haki inataka kusiwepo na mtu


anayepaswa kuadhibiwa kwa madhambi ya wengine, vile vile


haipaswi kuadhibiwa watu wengine kwa kuwaokoa wengine: Je! Dai


la kwamba Mungu amemtoa muhanga Yesu ili kutuokoa haliteti


mkanganyiko kama kweli Mungu ni mpenda haki? Je, Dai hilo


halitofautiani na maana halisi ya haki?


19. Watu wanatoa muhanga vitu vyao ili kupata vitu vingine


wasivyokuwa navyo ikiwa haiwezekani kuwa navyo vyote viwili kwa


wakati mmoja. Wakristo wanasema kwamba “Mungu alimtoa


muhanga mtoto wake wa pekee ili kutuokoa; Tunajua kwamba Mungu


ni Mwenye nguvu; Mungu alimtoa Muhanga Yesu kwa nani?


20. Kutoa muhanga kitu maana yake ni kwamba huwezi kukipata tena


kile ulichokitoa; sasa kuna siri gani katika kutolewa Muhanga Yesu


wakati Mungu aliweza kumrudisha Yesu baada ya kusulubiwa (kwa


mujibu wa maneno ya Wakristo)?


21. Ikiwa  


 Wakristo wote wameokoka kwa kupitia Yesu na


wanakwenda Peponi (kwenye uzima wa milele) bila kujali matendo


yao, kwa hiyo mafundisho ya Yesu hayana umuhimu wowote na


maana ya maneno “uovu” au “wema” hayana umuhimu wowote.


Ikiwa hali sivyo hivyo, kwa hiyo wale Wakristo ambao wanamwamini


Yesu lakini hawafuati mafundisho yake wala hawajatubu watakwenda


motoni?


22. Vipi Wakristo wanayachukulia matendo kama kitu kisicho na


umuhimu baada ya kuwa kitu kimoja wakati Yesu aliposema katika


Matayo 12:36; “Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana,


watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya


hukumu.”?


23. Wakristo wanasema kwamba watu wanakwenda Peponi kwa kupitia


Yesu tu! Wakati Paulo anasema katika 1 Wakorintho 7:8-16 kwamba


Mume asieamini anakubalika kwa Mungu kwa sababu anaunganishwa


na mke wake na kinyume chake, na watoto wao wasio na dini vile vile


wanakubalika kwa Mungu. Kwa hivyo kumbe watu wanaweza


kwenda Peponi bila ya kumwamini Yesu; kutokana na maneno hayo.


24. Vipi Biblia inasema kwamba Waisraeli wote wameokoka ingawa


hawamwamini Yesu? Je, Hili halipingani na dai la Biblia ya kuwa njia


ya pekee ya kwenda Peponi ni kwa kupitia Yesu tu?


25. Kwa mujibu wa Wakristo, wale wote ambao hawakubatizwa


watakwenda motoni. Kwa hivyo hata watoto wachanga nao


watakwenda motoni kwa vile walikufa kabla ya kubatizwa; kwa vile


walizaliwa na dhambi la asili la kurithi? Je, hili halipingani na maana


ya neno haki; kwanini Mungu awaadhibu watu kwa madhambi


wasiyoyatenda?


ROHO MTAKATIFU


Sehemu pekee katika Biblia alipotajwa Roho Mtakatifu ni katika Yohana


14:26; “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba


atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote niliyowaambia. “Ni kipi kile


ambacho Roho Mtakatifu ameleta au kufundisha kwa miaka 2000 iliyopita?


26. Wakristo wanasema kwamba Msaidizi maana yake ni Roho Mtakatifu


(Yohana 14:26) Yesu alisema katika Yohana 16:7-8. “Lakini mimi


nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana


mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu;” Hii haiwezi


kumaanisha Roho Mtakatifu; kwa vile Roho Mtakatifu inasemekana


kwamba alikuwepo hata kabla ya Yesu hajazaliwa kama ilivyo katika


Luka 1:41 “Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu”. Hapa, Roho


Mtakatifu vile vile alikuwepo wakati wa Yesu: sasa vipi hii imaanishe


kwamba  ni sharti aondoke Yesu ndipo Roho Mtakatifu aweze kuja?


27. Katika Yohana 16:7-8, inasema; “Bali mimi nikienda zangu,


nitampeleka kwenu. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha


ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.” Je, hii


“Yeye” hapa inamaanisha nini? Je, viwakilishi hivyo havimaanishi


mtu mwanamume?  


28. Je, Roho Mtakatifu anazungumza na Wakristo wema na waovu vile


vile? Je, Roho Mtakatifu yu pamoja nao wakati wote au wakati fulani


tu? Je, ni wakati gani anaanza kumtembelea mtu atakaye kuwa


Mkristo?


29. Utasemaje kuwa wewe ni Mkristo ikiwa Roho Mtakatifu yu ndani ya


Mkristo mwingine? Inakuwaje Wakristo wengi wanawapumbaza watu


kwa kudai kwamba Roho Mtakatifu yu ndani yao tu! Na baadaye


wanabadilisha dini?


30. Je, Roho Mtakatifu anaamuru kile ambacho Wakristo wanapaswa


kukifanya bila ya uhuru wa kuchagua hata kidogo au anawaongoza tu


na wao wana uhuru wa kufuata au kuto fuata?


31. Ikiwa Roho Mtakatifu anaamuru kile Wakristo wanachopaswa


kukifanya, kwa nini Wakristo wanafanya maovu na madhambi? Vipi


unaweza kuuelezea ubadilishaji wa dini na kuingia dini na imani


mbali mbali kunakofanywa na Wakristo wengi? Je, Wanaambiwa


kufanya hayo na Roho Mtakatifu?   


32. Ikiwa Roho Mtakatifu anawaongoza Wakristo tu, na wako huru


kufanya wanavyotaka, sasa ni vipi tutajua kwamba waandishi wa


Biblia hawakufanya makosa wakati walipoziandika?


33. Ikiwa Wakristo wanaamini kwamba Roho Mtakatifu huwajia na


kuzungumza nao kila siku, kwanini hawamuulizi Roho Mtakatifu


kuhusu chapisho lipi la Biblia wanalopaswa kulifuata kwa vile kuna


machapisho mengi?


KAZI  YA UJUMBE WA YESU


Hivi bila ya kuazima kutoka katika dini na mifumo mingine, Ukristo


unaweza kuwapa wanadamu mfumo kamili wa maisha? Huku Ukristo ukiwa


umefungika kwa maisha ya kiroho tu na hautoi sheria, sasa vipi jamii


itaweza kuamua sheria zipi ni sahihi na zipi ni makosa?


34. Kwa nini Wakristo wanasema kwamba Yesu alikuja kwa ajili ya


ulimwengu mzima wakati yeye alisema kuwa alitumwa kwa


Mayahudi tu? Alimwambia yule mwanamke Mkananayo


aliyemuomba amtibie bintiye aliyekuwa anasumbuliwa na mapepo:


“Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” na pia


alisema; Si vyema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”


(Matayo 15:21-28).


KUFUFUKA KWA YESU


Ikiwa utasoma Matayo (28: 1-10), Marko (16:1-20), Luka (24:1-12), na


Yohana (20:1-18) utakuta habari zenye kutatanisha: Maandika yote hayo


yanakubali kwamba kaburi lilikuwa linalindwa kwa muda wa siku tatu. Hata


hivyo, maandiko hayo yanaonesha kugunduliwa kwa kaburi kuwa ni tupu


katika hali tofauti.  


1 Matayo (28) na Yohana (20) zinaeleza kwamba Maria Magdalena na


Maria wengine walikuwa ndio  watu wa kwanza kuliona lile kaburi.


2 Marko (16) inaeleza kwamba Maria Magdalena, Maria mama, James


na Salome walikuwa wa kwanza kuliona kaburi likiwa tupu.


3 Marko (28) inaeleza kwamba kulikuwa na tetemeko la ardhi ambalo


lililoondosha jiwe lililokuwa juu ya kaburi. Anasema kwamba


Malaika ndie aliesababisha hivyo: Maandiko mengine hayataji


kuwepo kwa tetemeko la ardhi.  


4 Matayo na Marko wanasema kwamba mwanamume mmoja tu


aliyevaa mavazi meupe ndiye alikuwa malaika.


5 Luka inasema wanamume wawili waliovalia mavazi meupe, ambao


walikuwa malaika, ndio waliokuwa wamekaa juu ya kaburi. Yohana


inasema kwamba wale wanawake wawili hawakumkuta mtu yoyote


kwa mara ya kwanza walivyokwenda kwenye kaburi, lakini


waliporudi tena, waliwaona watu wawili, mmoja alikuwa Malaika na


mwingine alikuwa Yesu.


6 Matayo inasema kwamba, wakati walinzi walipotoa taarifa hizi kwa


Kuhani mkuu, yule Kuhani mkuu aliwalipa kiasi kikubwa cha pesa, na


kuwaambia “Mnapaswa kusema kwamba wafuasi wake walikuja


nyakati za usiku na kuiba mwili wake”. Alidai kwamba askari


walichukua pesa na kusambaza habari hiyo na toka hapo, hadithi


ilikuwa ni yenye kuzunguka kati ya Wayahudi; mpaka leo (kwa


mujibu wa Matayo). Maandiko mengine hayasemi chochote kuhusu


jambo hilo.  


35. Ni maelezo yapi ambayo ni ya kweli?


36. Kwa nini Yesu alipojitokeza baada ya tendo la kusulubiwa


inachukuliwa kama ndio kigezo (uthibitisho) wa kufufuka kwake


wakati kuna maelezo yasemayo kwamba si yeye aliyesulubiwa wala


aliyekufa kwani aliyesulubiwa ni mtu mwingine wakati Mungu


akimwokoa Yesu?


37. Vipi Matayo alijua dai au hoja ya makubaliano kati ya wale askari na


yule kiongozi? Hivi mtu hawezi kusema kwamba kuna mtu


aliyewalipa wale wanawake kiasi kikubwa cha pesa na akawaambia


waeneze maneno yale ya kwamba Yesu alifufuka, pamoja na uthabiti


huo huo kama ule wa habari ya Matayo.


38. Kwanini walimwamini yule mtu aliekuwa na mavazi meupe? Kwa


nini walimuamini kwamba alikuwa ni malaika? Maelezo ya Yohana


ni ya kustaajabisha sana, kwa vile yeye alisema kuwa Maria


hakumtambua Yesu (ni yupi kati ya wale watu wawili) wakati


alipokuwa akizungumza nae, hali alimtambua tu wakati yule mtu


alipomwita Maria kwa jina lake?


39. Vipi lile kaburi lililokuwa tupu lina thibitisha kwamba Yesu


alisulubiwa? Je, Mungu hawezi kumtoa mtu mwingine kutoka


kaburini na kumfufua?


40. Injili inaaminiwa kuwa ni maneno asilia ya Mungu, yanasadikiwa


kwamba   yalisemwa na Roho Mtakatifu kwa wafuasi wake ambao


waliyaandika. Ikiwa chanzo chake ni kimoja, kwanini yasilingane


katika kulizungumzia tukio lile muhimu? (la kufufu Yesu).


41. Vipi  Matayo, Marko, Luka na Yohana waliweza kuchukuliwa kama


mashahidi walioona Yesu akifufuka wakati Biblia inatuambia


kwamba hakuna mtu aliyemuona Yesu akitoka ndani ya kaburi?


BIBLIA


Ikiwa Wakristo wanachukulia Agano la Kale kwamba ni maneno ya Mungu,


kwa nini walibatilisha baadhi ya maandiko katika Agano la Kale ambayo


yalikuwa yakizungumzia adhabu (kwa mfano adhabu ya uzinzi)?


42. Kwanini Marko 16:9-20 haipo kwenye machapisho mengi ya Biblia


wakati katika baadhi ya machapisho imejitokeza kama tanbihi ya


chini ya ukurasa tu au imewekwa katika mabano? Je, tanbihi ya chini


ya ukurasa katika Biblia nayo inachukuliwa kuwa ni maneno ya


Mungu, hasa hasa wakati inapozungumzia jambo muhimu kama la


kupaa kwa Yesu?


43. Kwa nini Biblia ya Kikatoliki ina vitabu 73 ndani yake wakati Biblia


ya Kiprotestanti ina vitabu 66 tu ndani yake? Wakati zote mbili ya


Kikatoliki na Kiprotestanti zinadai kuwa na maneno kamili ya Mungu,


ipi inatakiwa iaminiwe na kwa nini; kwa kigezo gani?


44. Ni wapi zinakotoka hizo tafsiri mpya za Biblia wakati ile Biblia ya


asili haipo au haipatikani popote? Maandiko ya kizamani ya Kigiriki


ambayo yenyewe ni tafsiri hayafanani na yanatofautiana yenyewe kwa


yenyewe.


45. Unawezaje kuyachukua maandiko ya waandishi ambao kamwe


hawakumuona Yesu kwamba   ni sahihi, kama vile Marko na Luka?


46. Kwa nini nusu ya Agano Jipya imeandikwa na mtu ambae kamwe


hakuonana na Yesu katika maisha yake? Paulo anadai alionana na


Yesu alipokuwa njiani toka Jerusalemu kuelekea Damaskasi bila


kutoa ushahidi wowote wa kuonana naye? Paulo alikuwa ndie adui


mkubwa wa Ukristo; Je, hilo halitoshi kutilia shaka juu ya usahihi wa


kile alichokiandika? Kwa nini Wakristo wanayaita maandiko ya


vitabu hivyo vya Agano la Kale kwamba ni “MANENO YA


MUNGU”  wakati wale waliyoyapitia Biblia ya RSV wanasema


kwamba mwandishi wa SAMWELI hajulikani na yule alieandika (na


kuyakusanya)


maandishi


 ya


kale


 (KUMBU KUMBU)  


“HAJULIKANI HUENDA YALIKUSANYWA NA KUHARIRIWA


NA EZRA”.!!!


UTATA


47. Kulingana na mambo yanayotatanisha katika Biblia, ni vipi Wakristo


wanaweza kuamua kwa wingi wa theluthi mbili yapi ni maneno ya


Mungu na yapi si maneno ya Mungu kama tangulizi ya baadhi ya


Biblia zinavyosema kama ilivyosema ile ya RSV?


48. Kwanini Luka katika maandiko yake anazungumzia kupaa kwa Yesu


kuwa ilikuwa ni siku ya Pasaka, na katika Matendo ya Mitume,


maandiko ambayo yanajulikana kama yeye ndiye mwandishi,


anasema alipaa siku arobaini baadae?


49. Ukoo wa Yesu umetajwa katika Matayo na Luka tu. Matayo


iliorodhesha vizazi 26 kutoka Joseph hadi Daudi wakati Luka yeye


iliorodhesha vizazi 41. ni Joseph tu anayeungana na Daudi katika


orodha zote mbili. Hakuna jina jingine hata moja lingana! Ikiwa hayo


yalitolewa na Mungu neno kwa neno, vipi yatofautiane? Baadhi


wanadai kwamba moja ni kwa ajili ya Maria na moja ni kwa ya


Joseph, lakini ni wapi alipotajwa Maria katika maandiko yote mawili?


50. Ikiwa Musa aliandika vitabu vya kwanza kabisa vya Agano la Kale,


Musa aliwezaje kuandika taarifa ya kifo chake mwenyewe? Musa


alikufa katika kitabu cha tano akiwa na miaka 120 kama ilivyotajwa


katika Kumbukumbu la Torati; 34:5-10


51. Katika chapisho la King James, kwa nini linaeleza miaka 7 (saba) ya


ukame katika Samweli 2  24:13 huku likieleza miaka 3 (mitatu) tu ya


ukame katika Mambo ya Nyakati 1- 21:12? Kwa nini yote yalibadilika


katika chapisho jipya la kimataifa na machapisho mengine?


52. Vile vile Katika chapisho la King James, kwa nini inasema kwamba   


JEHOIACHINI alikuwa na miaka minane wakati alipoanza kuongoza


katika Mambo ya Nyakati 2 (21:12) huku ikisema alikuwa na miaka


kumi na nane katika Wafalme 2  24:8? Kwa nini baadae zote


zilibadilika na kuwa 18 katika chapisho jipya?


53. Katika machapisho yote, kwa nini yanasema kwamba Daudi aliwauwa


waendesha magari ya Farasi MIA SABA wa Kisyria na wapanda


farasi arobaini elfu kama ilivyooneshwa katika Samweli 2 10:18 huku


ikisema watu elfu saba ambao walipigana kupitia magari ya farasi na


wapiganaji wa miguu 40 elfu katika Mambo ya Nyakati 1 19:18?


54. Katika machapisho yote, kwa nini yanasema kuwa majosho elfu mbili


katika Wafalme 1 7:26 huku katika Mambo ya Nyakati 2 4:5 linasema


ni majosho elfu tatu?


55. Katika chapisho la King James, kwa nini linasema kwamba Solomoni


alikuwa na vikalio vya farasi elfu nne katika Mambo ya Nyakati 2


9:25, huku likisema kwamba


  Solomoni alikuwa na vikalio vya


farasi arobaini elfu katika Wafalme 1 4:26? Kwa nini yalibadilika yote


mawili na kuwa arobaini elfu Katika chapisho jipya?


56. Mwanzo 1, uumbaji wa Mungu umeanzia majani kisha miti, ndege,


nyangumi, ng`ombe na vitambaavyo na mwisho mwanamume na


mwanamke. Mwanzo 2, hata hivyo, inauweka uumbwaji wa


mwanamume kabla ya ng`ombe na ndege na mwanamke. Baadaye na


wanyama. Vipi itawezekana kufafanua haya?


QURAN NA WAKRISTO


Ketengo hiki hakihitaji wala hakihoji, lakini sana sana kunampatia msomaji


baadhi ya aya za Quran ambazo zinauelekeza Ukristo kwa upekee, na watu


wa kitabu kwa ujumla. Sehemu kubwa ya Quran inahusika na au


inafungamana na Wakristo na Wayahudi na nimeamua kuchagua aya


zinazofungamana na maudhui ya makala hii.


1 “Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam;


Alimuumba kwa udongo kisha Akamwambia: “Kuwa”; basi akawa.”


(Quran 3:59)


2 “Sema: “Enyi watu mliopewa Kitabu (cha Mwenyezi Mungu.


Mayahudi na Manasara)! Njooni katika neno lilio sawa baina yetu na


baina yenu: ya kwamba tusimwabudu yoyote ila Mwenyezi Mungu,


wala tusimshirikishe (Mwenyezi Mungu) na chochote; wala baadhi


yetu tusiwafanye wengine kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu


(au pamoja na Mwenyezi Mungu). Wakikengeuka, semeni:


“Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu, (tumenyenyekea amri za


Mwenyezi Mungu).”


3 “Enyi watu mliopewa Kitabu! Mbona mnabishana juu ya Ibrahimu, na


hali Taurati na Injili havikuteremshwa ila baada yake? Basi je,


hamfahamu?”  


4 “Ibrahimu hakuwa Myahudi wala Mkristo, lakini alikuwa mwongofu,


mtii; wala hakuwa katika washirikina.”  


5 “Watu wanaomkurubia zaidi Ibrahimu ni wale waliomfuata yeye


(katika zama zake) na Mtume huyu (Muhammad) na waliomwamini


(Mtume huyu). Na Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wa wenye


kuamini.”  


6 “Baadhi ya watu waliopewa Kitabu wanapenda wakupotezeni; lakini


hawapotezi ila nafsi zao; na (hali wenyewe) hawatambui.”  


7 Enyi mliopewa Kitabu! Mbona mnazikataa Aya za Mwenyezi Mungu,


hali mnajua (kuwa ndiyo ndizo)?


8 Enyi mliopewa Kitabu! Mbona mnachanganya haki na batili, na


mnaficha haki, hali mnajua?” (Quran 3:64-71)


9 “Na anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa kwake.


Naye Akhera atakuwa katika wenye khasara (kubwa kabisa).” (Quran


3:85)


10 “Na kwa (ajili ya) kusema kwao: “Sisi tumemuua Masihi Isa, mwana


wa Maryamu, Mtume wa Mungu,” hali hawakumwua wala


hawakumsulubu, bali walibabaishiwa (mtu mwengine wakamdhani


Nabii Isa). Na kwa hakika wale waliokhitalifiana katika (hakika) hiyo


(ya kumwua nabii Isa)wamo katika shaka nalo (jambo hilo la kusema


kauawa). Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo) hili (la kuwa


kweli wamemwua Nabii isa), ispokuwa wanafuata dhana tu. Na kwa


yakini hawakumwua. Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua Kwake, na


Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu (na) Mwenye hikima.” (Quran


4:157-158).


11 “Enyi watu wa Kitabu! Msipindukie mipaka katika dini yenu, wala


msiseme juu ya Mwenyezi Mungu ila yaliyo kweli. Masihi Isa bin


Maryamu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na (ni kiumbe aliyeumbwa


kwa) tamko Lake (tu Mwenyezi Mungu) alipompelekea Maryamu. Na


ni roho iliyotoka Kwake (Mwenyezi Mungu kama roho nyengine).


Basi mwaminini Mwenyezi Mungu na Mitume Yake; wala msiseme


“watatu …” Jizuieni (na itikadi hiyo); itakuwa bora kwenu. Bila shaka


Mwenyezi Mungu ni Mungu Mmoja tu. Ni mbali na Utakatifu Wake


kuwa ana mwana. Ni vyake (vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo


ardhini; na Mwenyezi Mungu ni Mlinzi wa kutosha. Masihi (Nabii


Isa) hataona unyonge kuwa mja wa Mwenyezi Mungu, wala Malaika


waliokurubishwa (na Mwenyezi Mungu hawataona unyonge kuwa


waja wa Mwenyezi Mungu). Na watakaoona unyonge uja wa Mungu


na kutakabari, basi Atawakusanya wote Kwake (Awatie Motoni). Na


ama wale walioamini na kufanya vitendo vizuri, basi Atawapa ujira


wao (sawa sawa), na kuwazidishia fadhila zake. Lakini wale walioona


unyonge na kufanya kiburi, basi Atawaadhibu kwa adhabu iumizayo,


wala hawatapata rafiki wala msaidizi (yoyote) mbele ya Mwenyezi


Mungu. (Quran 4:171-173)  


12 “Na kwa wale waliosema: “Sisi ni Wakristo,” Tulichukua ahadi kwao,


lakini wakaacha sehemu (kubwa) ya yale waliyokumbushwa, kwa


hivyo Tukaweka baina yao (wenyewe kwa wenyewe) uadui na


bughudha mpaka Siku ya Kiama. Na Mwenyezi Mungu atawaambia


walivyokuwa wakiyafanya. Enyi watu wa Kitabu! Amekwisha


kufikieni Mtume wetu, anayekudhihirishieni mengi mliyokuwa


mkiyaficha katika Kitabu, na husamehe mengi. Bila shaka imekwisha


kufikieni nuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Kitabu


kinachobainisha (kila jambo). Kwa (Kitabu) hicho Mwenyezi Mungu


huwaongoza wenye kufuata radhi Yake katika njia za salama, na


huwatoa katika kiza kuwapeleka katika nuru kwa amri Yake, na


Huwaongoza katika njia iliyonyooka. Kwa yakini wamekwisha kufuru


wale waliosema: “Mwenyezi Mungu ni Masihi bin Maryamu.” Sema:


“Ni nani atakayemiliki (kuzuilia) chochote mbele ya Mwenyezi


Mungu kama Yeye angetaka kumwangamiza Masihi mtoto wa


Maryamu, na mama yake na vyote vilivyomo katika ardhi?” Na


ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake ni wa Mwenyezi


Mungu (tu peke yake). Huumba Apendavyo. Na Mwenyezi Mungu ni


Muweza juu ya kila kitu.” (Quran 5:14-17)   


13 “Bila shaka wamekufuru wale waliosema, “Mwenyezi Mungu ni


Masihi (isa) bin Maryamu.” Na (hali ya kuwa) Masihi alisema: “Enyi


wana wa Israili! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola


wenu. Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi


Mungu atamharamishia Pepo, na mahali pake (patakuwa) ni Motoni.


Na madhalimu hawatakuwa na wasaidizi (wa kuwasaidia Siku ya


Kiama).”


14 Kwa hakika wamekufuru wale waliosema: “Mwenyezi Mungu ni


mmoja katika (wale waungu) watatu; (Yeye ndiye wa tatu wao).” Hali


hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja (tu peke yake). Na kama


hawataacha hayo wayasemayo, kwa yakini itawakamata – wale


wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao – adhabu iumizayo.


15 Je! Hawatubu kwa Mwenyezi Mungu na kumwomba msamaha? Na


Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa


kurehemu.


16 Masihi bin Maryamu si chochote ila ni Mtume (tu). (Na) bila shaka


Mitume wengi wamepita kabla yake. (Hawajaona)? Na mamake ni


mwanamke mkweli. (Na) wote wawili walikuwa wakila chakula (na


wakenda choo. Basi waungu gani wanaokula na kwenda choo)?


Tazama jinsi wanavyogeuzwa (kuacha haki).


17 Sema: “Je! Mnawaabudu – badala ya Mwenyezi Mungu (peke yake) –


wale ambao hawawezi kukudhuruni wala kukunufaisheni? Na


Mwenyezi Mungu ndiye Asikiaye (na) ndiye Ajuaye.”


18 Sema: “Enyi watu wa Kitabu! Msipindukie mipaka katika dini yenu


bila haki, wala msifuate matamanio ya watu waliokwisha potea toka


zamani; (nao ndio hao wanavyuoni wenu) na wakawapoteza wengi, na


(sasa) wanapotea njia iliyo sawa, (hawataki kumfuata Nabii


Muhammad).” (Quran 5:72-77)   


19 Na (kumbukeni) Mwenyezi Mungu atakaposema: “Ewe Isa bin


Maryamu! Je, wewe uliwaambia watu: ‘Nifanyeni mimi na mama


yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu?” aseme (Nabii


Isa): “Wewe umetakasika na kuwa na mshirika. Hainijuzii mimi


kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uwongo).


Kama ningalisema bila shaka Ungalijua; Unayajua yaliyomo nafsini


mwangu, lakini mimi siyajui yaliyo nafsini Mwako; hakika Wewe


ndiye Ujuaye mambo ya ghaibu.


20 “Sikuwaambia lolote ila yale Uliyoniamrisha: ya kwamba,


‘Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wenu.’ Na nilikuwa shahidi juu


yao nilipokuwa nao; na Uliponikamilishia muda wangu, Wewe ukawa


Mchungaji juu yao, na Wewe ni Shahidi juu ya kila kitu.


21 Ikiwa Utawaadhibu, basi bila shaka hao ni waja wako; na


Ukiwasamehe basi kwa hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu (na)


Mwenye hikima; (Hutaambiwa kuwa wamekushinda kuwatia adabu).”


22 Mwenyezi Mungu atasema: “Hii ndiyo Siku ambayo wakweli


utawafaa ukweli wao. Wao watapata Bustani zipitazo mbele yake


mito. Humo watakaa milele. Mwenyezi Mungu amewawia (amewapa)


radhi; nao wawe radhi Naye. Huku ndiko kufaulu kukubwa.” (Quran


5:116-119)  


23 Na Mayahudi wanasema: “Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu;” na


Wakristo wanasema: “Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu”; haya


ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasi na kuyapima). Wanayaiga


maneno ya wale walio kufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu


awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa!


24 Wamewafanya wanavyuoni wao na watawa wao kuwa ni miungu


badala ya Mwenyezi Mungu na (wamemfanya) Masihi mwana wa


Maryamu (pia mungu), hali hawakuamrishwa ispokuwa kumuabudu


Mungu Mmoja, hakuna anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Yeye.


Ametakasika na yale wanayomshirikisha nayo.


25 Wanataka kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao,


lakini Mwenyezi Mungu amekataa ispokuwa kuitimiza nuru Yake,


ijapokuwa makafiri wanachukia.


26 Yeye ndiye Aliyemleta Mtume Wake kwa uongofu na Dini ya haki ili


Aijaalie kushinda (Dini hii) dini zote; ijapokuwa watachukia hao


washirikina.


27 Enyi mlioamini! Wengi katika makasisi (wanavyuoni wa Mayahudi


na Manasara) na watawa (wao) wanakula mali za watu kwa batili na


kuwazuilia njia ya Mwenyezi Mungu. Na wale wakusanyao dhahabu


na fedha wala hawazitoi katika njia ya Mwenyezi Mungu, wape


habari za adhabu inayoumiza (inayowangoja)


28 Siku (mali yao) yatakapotiwa moto katika Moto wa Jahanamu, na kwa


hayo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo


yao, (na huku wanaambiwa): “Haya ndiyo (yale mali) mliojilimbikia


(mliyojikusanyia) nafsi zenu, basi onjeni (adhabu ya) yale mliyokuwa


mkikusanya.” (Quran 9:30-35)


MUHAMMAD AU YESU?     


Wakristo wanadai kwamba utabiri wa Kumbukumbu la Torati 18:18


unamuhusu Yesu na sio Muhammad. Hiyo aya inasema: "Mimi


nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami


nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote


nitakayomwamuru.” Kumbukumbu la Torati 18-18 Hoja ya pekee


wanayoikimbilia katika tafsiri hiyo ni kuwa wote wawili Musa na Yesu


walikuwa Mitume. Ingawa hoja hiyo inapingana na madai yao ya kuwa


Yesu alikuwa ni Mungu na si Mtume. Mitume wengi wa Kiyahudi


walifanana na Musa. Hata hivyo, kama tutamlinganisha Muhammad na


Musa, tupata kuwa:  


Muhammad alikuwa ni Mwarabu, na Waarabu wanatokana na Ismaili, mtoto


wa Ibrahimu, huku Musa alikuwa ni Myahudi, na Wayahudi wanatokana na


Isaka, mtoto wa Ibrahimu, kwa kuwa neno NDUGU ZAO linaashiria watoto


wa mtoto wa kwanza kuwa ndugu wa mwingine. Hili halikubaliki kwa Yesu,


kwa kuwa alikuwa ni Myahudi.


Kwa mujibu wa Wakristo, Yesu alienda Motoni kwa siku tatu huku Musa


akiwa hajaenda. Kwa hiyo, Yesu si kama Musa. (Katika Uislamu, hakuna


yoyote katika hao Manabii watatu aliyeingia Motoni)


Musa na Muhammad walizaliwa na baba na mama huku Yesu alizaliwa na


mama tu.


Musa na Muhammad walioa na kuwa na watoto, huku Yesu akiwa hajaoa


kabisa.


Musa na Muhammad walipata matatizo na mambo magumu kutoka kwa


watu wao mara ya kwanza, lakini mwishoni walikubaliwa na watu wao.


Huku Yesu alikuwa amekataliwa na watu wake mwanzoni na anaendelea


kukataliwa na Wayahudi hadi leo hii. “Alikuja kwake, wala walio wake


hawakumpokea.” Yohana 1:11


Musa na Muhammad walikuwa na nguvu, kando na kuwa Mitume. Wote


wawili walitekeleza adhabu kubwa, hilo likiwa ni mfano, huku Yesu hakuwa


na madaraka kwa watu wake. “Yesu akajibu, ufalme wangu sio wa


ulimwengu huu”, Yesu amesema katika 18:36.


Musa na Muhammad walileta sheria mpya huku Yesu hakuleta.


Musa alilazimishwa kuhama alipokuwa mkubwa aende Median huku


Muhammad pia, alilazimishwa ahame alipokuwa katika hatua moja ya


maisha yake, kuelekea Madina. Huku Yesu hajalazimishwa kuhama katika


utuuzima wake.


Musa na Muhammad wote wawili walikufa vifo vya kawaida na kisha wote


walizikwa, huku jambo hilo haliwezi kuongelewa kwa Yesu. Yesu


hakuuliwa wala hakusulubiwa kabisa kabisa, kwa mujibu wa Quran na


hakufa kwa kifo cha kawaida kama ilivyothibitishwa na Wakristo ambao


wanaamini kasulubiwa.


MASWALI YA MWISHO


57. Kwa nini, ewe kiongozi wa Kikristo, huji kusikiliza na kujifunza dini


ya kweli ya Yesu?


58. Ukiwa kama Mkristo, uliyeusoma Uislamu na ikiwa ni hivyo, je,


uliusoma kutoka kwa Waislamu wa kweli?


59. Kama  Mkristo, je, unakubali kwa uadilifu na wema kuwa ni lazima


uchunguze kile kinachosemwa na Uislamu juu ya Mungu, Yesu,


pamoja na maisha haya na ya baadae?


60. Kwa kuwa ni Mkristo, je, pia, waamini  kile tunacholazimika


kuhesabiwa kwa Muumba wetu na kwamba Muumba ni mkamilifu na


Muadilifu? Kama muumini mwaminifu kwa Mungu. Je, hulazimiki


kutafuta ukweli usiobadilishwa bilia kujali matokeo yake?      





 



Machapisho ya hivi karibuni

FADHILA ZA SIKU KUMI ...

FADHILA ZA SIKU KUMI (ZA MWANZO) ZA DHUL-HIJA

Mafungamani ya Shahad ...

Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.