Nakala




Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


3


UTANGULIZI


Vipi tusome Tarekhe ya Masahaba?


Sifa zote njema zimemthibitikia Allah aliyejaalia historia ya waislamu


waliotangulia kuwa yenye kung’ara na iliyo safi, na Sala na Salamu


zimshukie yule aliyepelekwa na Allah kuwa Mtume na Nabii muongowaji


pia sala ziwashukie jamaa na masahaba wake, na kila aliyekuwa mchaji.


Ama baada ya hayo: Kwa hakika kuhifadhiwa kwa Historia yetu iliyosifika,


na kuihifadhi kutokana na mikono ya wachafuaji, na uongo wa wenye chuki


na ujinga wa wasioelewa, ni katika mambo ya wajibu juu ya wenye elimu na


maarifa, hivyo isiachiwe kuwa kwenye mikono ya Mustashrikina wakaifanya


kitambaa cha kufutia uchafu, wala kwenye mikono ya waliouacha mkono


uislamu –kwa kusahau au kwa makusudi –ili iwaondoe toka kweye njia


waliokuwa mababu na watukufu, wakachukuwa hili na kuwacha hili, kwa


ajili ya haja zilizomo kwenye nafsi zao na Allah ni mwenye kufichuwa


waliyokuwa wameyaficha.


Na katika zama hizi tunaona mataifa na umma zinazojaribu kujifanyia


historia yake, zinakusanya mawe na nyaraka, wanachimbuwa mabaki ya kale,


wanavunja majumba na kuharibu misikiti, kwa madai kwamba humo imo


historia na kumbukumbu, jambo lililowafanya watobowe, wachunguze na


kuteketeza wakiwa na matarajio ya kupata historia inayodaiwa. Na hii siyo


hali ya umma hizi tu ,bali ndiyo hali ya mataifa mengi katika zama hizi, bali


katika kila zama.


Jee ni ipi hali ya umma wetu; ulio na historia ing’arayo na iliyochapishwa


wala hawaipi umuhimu wowote ?!


Kwa kuanzia hapa ni lazima juu yetu kusoma Historia yetu kisomo cha utafiti


na uhakiki, kuisafisha kutokana na taka zilizopakaziwa, kuitakasa kutokana


na yaliyochanganyiwa, ili itoke ikiwa safi yenye kung’ara, watu wanufaike


nayo, na iwe kama alivyosema Mola wetu (Subhanahu Wataalah) :{Ama


povu basi hupotea, ama kile kinachowafaa watu basi hubakia kwenye


ardhi, hivi hivi Allah hupigia mifano}[Ar Ra’d:17]


Abdil Kariim bin Khaalid al ‘Harby.


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


4


Mlango wa Mwanzo


Sababu za kufanya mapungufu katika kusoma Historia inawezekana


kuyarejesha mapungufu yaliyopo kwenye darasa nyingi za historia za


zama za kisasa kwenye sababu tatu1 :


Sababu ya mwanzo


Hakika watoto wengi wa Kiislamu wameangukia kuwa mihanga kwa


yale waliyoandika baadhi ya Mustashrikina, waathirika wao miongoni


mwa kizazi chetu na waandishi wengineo wasioaminika, ambao


hujikumbatizia uongo na uzushi uliozushwa kwenye Historia yetu ya


kiislam kwa ujumla, na yale yanayoambatana na Aalil Beit Nabii


(S.A.W) waliotoharika na Masahaba watukufu (r.a).


Batili hizi huzifanya kuwa ni nguzo kwa wanayoyaandika, kama


kwamba ni vyenye kusalimika, wakihamasisha usomaji wa maandishi


hayo toka kwa wasomaji wasioona kitu ndani yake, wakitegemea


sababu ya kuandikwa kwake kwenye vitabu vya kihistoria, kama


kwamba kuwa kwake kwenye matumbo ya vitabu inatosheleza


kupakia rangi sifa za ukweli na kuthibitishia upakaji matope kutokana


na uongo na batili, wakijisahaulisha kufanyia kazi misingi ya utafiti


wa kielimu na kupatikana kwa uhakika yale wanayoyakaribisha usiku


na mchana. Pamoja na kwamba mengi ya wanayoyanukuu na


kuyataja, ima yanakuwa ni yenye sanad dhaifu, uzushi, au yasiyokuwa


na asili kabisa kabisa.


Na wengi miongoni mwao wanauelewa uhakika huu isipokuwa


wanajisahaulisha tu, kwa ajili ya kutia kasoro na kuiangusha historia


yetu tukufu, wao huanza kuandika wakiwa na niya mbaya, malengo ya


kiadui, yakilenga kwenye upakaji matope, kutia shaka kwenye nguzo


za umma huu, kueneza fitina na kuanzisha uadui baina ya watoto wa


umma huu, jee vipi itajuzu kwa muislamu awafanye hawa na


1 Sababu hizi zimetajwa na Daktariri ‘Abdil ‘Aziz Khan Allah ampe salama


kwenye kitabu chake –Matukio na Matukio ya Fitna zenye kuenea –


uk. (73-74) na tumezidisha juu yake kutolea baadhi ya dalili muhimu na


maalumati ya lazima.


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


5


wanayoyaandika kuwa ni viwakilishi baina yao na kumbu kumbu, dini


na historia yake ?!Na hii haimaanishi kwamba mustashrikina wote


wako sawa, wapo wa aina mbali mbali.


Wapo miongoni mwao wanaokusudia kubadilisha, kutia kasoro na


kutia watu kwenye shaka; kwa sababu ya chuki na husuda na malengo


ni ustashriki wa kiadui wa kutawalia na kupora nchi kuuwa waja, na


kudidimiza maendeleo ya kiislamu na utamaduni wake.


Na miongoni mwao –nao ni wachache- ni wale walioingilia


kumbukumbu zetu kama kazi ya kielimu na utafiti, juu ya


kudhihirisha mapungufu wanapokuwa kwenye mazingatio machache


tu kutokana na ugeni wao kwenye dini hii, na ukosefu wa maarifa


mazuri wa Lugha yake ambayo (ndio msingi wa mwanzo wa kumbu


kumbu hizi na usukani wake), na katika haya ni uchapishaji wa kitabu


(Al Waafii bil Wafayaati) cha Swalaa’hid Diini as Swafadiyyi, na


utunzi wa (Muujamul Mufahras Lialfaadhil ‘Hadiithin Nabawiyyi


Shariif ).


SABABU YA PILI


Kuondoka kwa elimu ya kisheria, upungufu wa hima na maarifa,


kujingikiwa na njia ya maulamaa wa historia na misingi yenye


uhusiano na uandishi na kupanga riwaya ya kihistoria.


Hivyo baadhi ya maulamaa mfano wa Maimamu wawili (At Tabary


na Ibn Kathir) kamwe hawashurutishi kuleta riwaya sahihi kwenye


vitabu vyao na kupuuza dhaifu kutoka na na riwaya za visa dhaifu vya


matukio na mambo yaliyozuka, bali walifuata mpango maalum


waliouashiria kwenye tangulizi za vitabu vyao; ili msomaji awe


kwenye bayana ya jambo hili.


Lakini wengi wa mufakirina, waandishi na walioendelea kwa ujumla


walikuwa kwenye kifungo na bado wako kwenye misingi hiyo na


vitangulizi, hivyo imekuwa kutoielewa na kuipuuza ni sababu ya


kupotea tafiti zao na maandishi yao yenye kusadikisha –usahihi – na


kufikia kwenye haki ..


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


6


Hivyo ni katika mambo ya umuhimu kusoma utangulizi wa mtunzi wa


kitabu chochote kile ili tupate uwazi wa sera ya kitabu chake. Na kwa


kubainisha uhakika wa tuliyotanguliza; tunakuletea mfano wa


umuhimu wa kuzingatia misingi na sera za wanahistoria, nayo ni sera


ya Imam Ibn Jarir Tabary (r.a) kwenye kitabu chake cha Tarekhe.


Ubainishaji wa Sera ya Imam Tabary kwenye kitabu chake


( Taarekhul Umam wal Muluuk)


Huyu hapa Imam Ibn Jaririt Tabary2 anafichua sera yake kwenye


utangulizi wa kitabu chake anasema "Zilizomo kwenye kitabu changu


katika habari kutoka kwa baadhi ya waliotangulia, miongoni mwa yale


yanayokataliwa na msomaji, au yanayochukiwa na msikilizaji wake,


kwa kuwa hakuelewa njia katika usahihi wake, na wala haina maana


kwa uhakika, hivyo ieleweke kwamba haikuja toka kwetu, ila imekuja


toka kwa baadhi ya wanukuuji, na kwamba sisi hiyo tumeileta kwa


namna tulivyofikishiwa.3mpaka hapa.


Imam Tabary (r.a) anambainishia msomaji kwa uwazi kwamba


kamwe hakushurutisha usahihi katika yale anayoyaleta kwenye kitabu


chake hichi katika riwaya zake, na kwamba dhamana katika


anayoyanukuu iko kwa wasimulizi walionukuu kabla yake, nae


kwenye kitabu hichi alikuwa mnukuuji na muaminifu, na sio mhakiki


mkosoaji. Hivyo baadhi ya aliyoyasimulia Tabary toka kwao


walikusanya baina ya uongo na wingi wa riwaya, na miongoni mwao


Tabary:ni Imam :Muhammadbin Jariir bin Yaziid Abu Jaa’far


Tabary.Mfasiri ,Muha’haddith ,mwanahistoria ,na mwanazuoni wa Usuli


Fiqhi na mwanafiqhi ,Imam mujtahid .Alizaliwa Aamaal ‘Tabaristaan mwaka


(224) na kufariki (310H).Miongoni mwa tunzi zake ni (Tarekhe l Umam wal


Muluuk)na Jaami’iBayaan fii Ta-awiilQur-aan).


 Tarekhe l Umam wal Muluuk.(52/1)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


7


1-Muhammad bin Hamiid Ar raazy sheikhe wa Tabary :


Tabary amesimulia kwa wingi toka kwake kwenye kitabu chake (At


Taariikh) na (At tafsir) pamoja na kwamba Muhammad huyu


amerembewa kuwa ni muongo na mzushi wa hadithi, nae ni dhaifu


mwenye hadithi zisizofaa toka kwa As Sawaadil A’adhwam toka kwa


maulamaa wa Jerhe na Ta’adiil 4


2-Luut’ bin Ya’yaa Abuu Mikhnaf;


Anazo riwaya nyingi kwenye (Taariikh Tabary ) zimefikilia riwaya


(585), kwenye riwaya hizo ameingia kwenye matukio na mambo


muhimu yaliyozuka kwenye historia ya kiislamu yakianzia kwenye


kifo cha Nabii (S.A.W), mpaka kuanguka, kwa Dola ya Umawiyyah,


na Lut huyu ni mwenye kutiwa ila mbele ya maulamaa wa Hadithi.


Amesema Ibn Maiyn


Amesema ibn Ma’iin" -   - sio chochote "-


Na akasema Ibn ‘Hibbaan "anasimulia hadithi za uongo toka kwa


wenye kukubalika .


Nae Adh Dhahaby akasema:” mtowaji wa habari zilizofisidika”5”":


Kutokana na mfano huu umedhihiri umuhimu wa kuangalia sera na


masharti ya maulamaa na kuyafahamu katika uandishi wa historia, na


umuhimu wa kuzihudhurisha nyoyoni wakati wa kutalii kitabu cha


Imam huyu au yule.Hali hii inahusika pia na vitabu vyengine vya


habari na historia, bali pia kwenye vitabu vya kumbu kumbu na fani


zake tofauti .


Baadhi ya wanahistoria hawa sera yao ilikuwa ni kunukuu riwaya na


habari hizi zikiwa na sanad zake bila ya kuzingatia hali za watu wala


sanadi zake, kwa kwenda kwenye kauli iliyoenea :”Yeyote aliyeweka


sanad basi huyo ameshategemeza kauli –hiyo-”, kwa kufuata hikaya


4 Angalia Miizaan wal I’itidaal)(530/3-531).


5 Angalia kitabu :Marwiyyaat Abii Ma’hnif (Luutw’ bi nYa’yaa Abuu


MakhnafAl Azdy ) Kwenye Tarekhe at Tw’wabary :zama za khilafti


Raashidiah) (uk. ) cha Daktari Ya’hya bin Ibrahim Al Yahya (Chapa


.1.Daarul ‘Aaswimah /Ar Riyaad1410 H.)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


8


za baadhi ya maulamaa wa hadithi katika uandishi wa hadithi, kwani


wao huandika kila riwaya kwa sanad yake ikiwa kama hatua ya


mwanzo; ama hatua inayofuatia – ni yenye kutofautisha baina ya


wanahistoria na wanahadithi –ambapo hushughulika na kuzichuja na


kuzitafiti, kuzihakiki na kuzitenganisha baina ya sahihi na dhaifu .


Imam Ibn Hajar ameashiria hilo akibainisha njia na sera za wengi wa


waliotangulia anasema "Wengi wa Muhadithina katika zama zilizopita


toka kwenye mwaka wa mia mbili na kuendelea mbele walitaja


hadithi kwa sanadi zake, wakiitakidi kwamba wamejiondolea


dhamana yao.”


Kwa kawaida Al-haafidh anakusudia wasimulizi wanukuuji, sio


maimamu wadadisi maulamaa wa Jerhe na Taadiil, walinzi wa dini


kutokana na kuchafuliwa na kubadilishwa, wenye kutumia misingi na


kanuni madhubuti za kukubalika na kukataliwa kwa msimulizi na


chenye kusimuliwa, hiyo ni misingi isiyokuwa na shubuha wala


mifano kwenye uzoefu wa kibinadamu na maendeleo yake .


Ni wajibu wa msomaji-akiwa ni mwenye kufaa-ahakikishe simulizi za


kitabu hichi au kile juu ya mwangaza wa misingi ya Muhaddithina


wadadisi, nao ni ule unaoitwa "Elimu ya Mustalahi-alhadithi"


uliojengeka juu ya kutafiti hali za masimulizi na habari na wanukuuji


wake katika hali ya kukubalika na kukataliwa, kwa kukaa kati ya


mambo mawili :


Mosi :Utafiti na upekuzi kuhusiana na wasimulizi wanukuuji wa


riwaya hizi wakitegemea kauli ya mabingwa wadadisi miongoni


mwao, maimamu wa Jarhu na Taadili 6;hivyo anaefaa huwa ni thiqah;


riwaya zake hukubalika, na asiefaa huwa dahifu riwaya zake


hazikubaliki wala hazina hadhi yoyote ile.


Pili :Kuangalia kwenye matini za riwaya hizi na kuzifanyia upekuzi


kwa kuzilinganisha na kitabu cha Allah na Sunna iliyo sahihi


iliyothibiti na misingi ya ujumla yenye kutegemewa kuhusiana na


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


9


mambo mawili hayo, ili kuelewa zisizofaa toka zile zenye kufaa,


zilizofuta –nasikh- toka kwenye zilizofutwa –mansukh- .


Hivyo msomaji akiwa ni mwenye sifa ya kustahikiwa na kuendesha


tafiti hizi na kuzifanyia uhakiki akiangalia wenye kushikamana na


elimu hii tukufu na ya kina; na vyenginevyo itamlazimu kumuogopa


Allah na jambo hili kulitegemeza kwa wanaofaa, watu maalum, watu


wa utafiti na maarifa ya mathiqa waadilifu .


SABABU YA TATU :


Kile wanachofanyia danadana baadhi ya waandishi ya uwezekano wa


kufanyiafanyia wepesi kwenye riwaya hasa zinazohusiana na zama za


mwanzo katika Historia ya Kiislamu zikilinganishwa na ukali katika


riwaya za Hadithi za Nabii (S.A.W) nalo wallahi likiwa ni katika


makosa makubwa yanayotokea kwa watu wetu waliostaarabika, kwa


vile ni aina katika aina za kuathirika na sera za kimagharibi ambazo


hazitilii mkazo kwenye unukuuji wa sanadi, na mfano mkubwa wa


hilo ni kwamba isnadi baina yao na (Injili) ni yenye kukatika kwa


mamia ya miaka, nacho ndicho kitabu chao kitakatifu basi unaona vipi


kwenye vitabu vyengine?!


Hakika historia ya Ahlil Beit ya Nabii (s.a.w) na Masahaba (r.a) ni


sehemu ya dini yetu na kamwe haisihi kuifanya sawa baina yake na ile


historia nyengine, au kufanyia uzembe katika kuichukuwa na


kuisimulia kwake, hivyo uzembe au kasoro yoyote katika haki ya


Historia hii na kuithibitisha kwake basi athari yake kwa vyovyote vile


itarejea kwenye dini, na juu ya kusihi kwa hadithi na usalama wake


kutokana na ubadilishwaji na ugeuzwaji wake .


Nasi tunao mfano wa wazi kwenye utiaji kasoro wa yule ambae ndani


ya moyo wake muna chuki kwenye riwaya ya kusilimu kwa Abu


Huraira Sahaba huyo mkubwa (r.a). Hakika watafiti wanajitahidi kwa


mapana katika kujadili baadhi ya matukio na mambo ya kihistoria


yaliyozuka zamani na sasa, wapo wanaothibitisha na wapo


wanaopinga, na kila upande unatanguliza dalili na hoja zake


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


10


zilizowapelekea kuona hivyo, pamoja na kwamba baadhi ya matukio


haya kamwe hayapelekei faida yoyote na amali kubwa, unadhania vipi


kuhusiana na Historia ya Aalil Bait na Masahaba (r.a) wabebaji wa


Sheria na ngome madhubuti ?!


Hii haimanishi uwajibu wa kutendea habari zote za (zama za


mwanzo) katika Historia yetu kama zinavyotendewa Hadithi katika


hali ya kukubalika na kukatalika, bali ni wajibu kutofautisha baina ya


habari na riwaya.


-Hivyo ikiwa habari na athari hizi ni kutoka kwa Aalil Bait na


Masahaba (r.a) wanasimulia zuhudi, ushujaa, ukarimu, kujitowa kwao


muhanga na wema wa tabia zao, mienendo yao bora na upole wa tabia


zao na mambo hayo hayakutoka kwenye misingi mikuu ya kisheria,


wala sio yanayokataliwa na maumbile yaliyo salama, hivyo hakuna


pingamizi kutajwa, kusimuliwa na kuandikwa kwake, kwani mambo


hayo hayagusi au kutikisa asili ya kisheria, na kamwe kwenye


kusimulia kwake hakuna madhara au mguso kwa hadhi ya Aalil Bait


na Masahaba (r.a) .


-Ama iwapo habari hizo ndani yake zimo fitina, au baadhi ya


misimamo ya kihamasa, au baadhi ya yanayochafua hadhi ya Aalil


Bait na Masahaba (r.a), au ndani yake kimo kitu kinachokwenda


kinyume na Misingi ya ujumla ya kisheria, au kumuingiza baadhi ya


kasoro zenye kukatalika na maumbile yaliyo sawa.


Hivyo aina hii ya habari ni lazima kuangaliwa kwenye sanad zake


muangalio wa umakini na wa kina na kuhukumiwa kwa hukumu ya


uadilifu .


Mikakati hii mitatu ambayo ndani yake kumeingia mapungufu katika


kusoma, kuonyesha na kunukuu historia ya kiislamu .


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


11


MLANGO WA TATU


Kanuni kuhusiana na kujibu shubuhati kuhusiana na Ahlil Bait:


Inampasia muislamu awe na tahadhari juu ya mambo sita


muhimu yanayoambatana na Aalil beit (r.a)


Jambo la Mosi :


Kwamba hadhi ya Ahlil Bait ni kubwa na imesaidia baadhi ya maadui


wa uislam kujipenyeza baina ya waislam, nako ni kukuza kielelezo


cha mapenzi ya Ahlil Bait na mawalii (wawachwa huru wao), kuzua


hadithi kwenye ubora wao, kama ni matokeo ya watu kukubali fadhila


za Ahlil Bait na mapenzi yao kwao kwa ujumla kwani wao walikubali


hadithi hizo za uzushi bila ya kuzifanyia upekuzi na utafiti na hivyo


tunaona Maimamu wa Aalil Bait ( r.a) wanalitaja jambo hili kwa kila


uwazi, na kwamba ni uhakika uliotokea hivyo inawapasa vipenzi vya


Aalil Bait ( r.a) kuchukuwa tahadhari miongoni mwa yaliyozuliwa juu


ya Aalil Bait ( r.a) katika athari na habari zilizozushwa .


Huyu hapa imamu miongoni mwa maimamu wa Aalil Bait tukufu (r.a)


nae ni Jaafari Sadiq (r.a) anasema "Hakika watu wamependezeshewa


uongo juu yetu "7 Naye (r.a) akiita kwa jina la Madwiyyatu


akasema:"Hakika ni sisi Aalil Bait (a.s) ni wa kweli kamwe


hatutovuka kutokana na muongo na anayotuzulia, basi ukweli wetu


huporomoka kwa sababu ya uongo wake juu yetu"8


Msikilize Shariih bin Abdil Lahil Qaadhy akiisifu kaumu iliyokaa


pamoja na Jaafar, na kudai kusimulia toka kwao:"Amesema Abu


Amril Kishy: Amesema Yahya bin Abdil Majid Al Hamany, kwenye


kitabu chake Al Muallafu fii ithbaati Imaamati 'Ali bin Abi Talib ( r.a)


"nilimwaambia Shariik Hakika watu wanadai kwamba Jaafar bin


7 Bihaarul Anwaar cha Al Majlisy (246/2)


8 (Jaamiur Ruwaat ) cha Muhammadil Ardiby Al Haairy (221/2) na


(Kuliyyaat fii 'ilmir Rijaal ) cha Jaafar As Sabhaany (uk.26)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


12


Muhammad ni mdhaifu wa hadithi, akasema "Ninakupa habari ya


kisa, Jaafar bin Muhammad alikuwa mtu mwema, muislamu mchaji


basi akakumbatiwa na watu wajinga wakawa wanaingia na kutoka


kwake" na wanasema ametuhadithia Jafar bin Muhammad hadithi na


zote ni Munkarat walizozizuwa toka kwa Jaafar, ili wawatake watu


chakula kutokana na kufanya hivyo, na huchukuwa dirhamu toka


kwao, waliokuwa wakileta kila hadithi munkar, hayo yakasikiwa na


wasiokuwa na elimu, basi miongoni mwao wamo walioangalia, na


wengine wapo waliozikataa .


Vile vile akasema Imam Jafar Saadiq (r.a) :"Mughira bin Said alikuwa


akitegemea kumzulia uongo baba yangu, huchukuwa vitabu vya


wafuasi wake, na wafuasi wake walikuwa wamemficha ndani ya


wafuasi wa baba yangu" huchukuwa vitabu vya wafuasi wa baba


yangu na kuvipeleka kwa Mughira, akawa humo anaweka kufuru na


uzandiki, na kuyategemezea kwa baba yangu, kisha anayapeleka kwa


wafuasi wake na kuwaamrisha wayaeneze."9


Jambo la Pili:


Hakika hadithi za uongo zilizozushwa kwenye fadhila za Masahaba


(r.a) hatua kwa hatua – zinazidi idadi ya Hadithi sahihi kwa makumi


ya mara, hivyo sio wajibu kukubali hadithi za fadhila na kuzieneza na


kuvukia kwazo mpaka wa sifa ila baada ya kuzitafiti sanadi zake na


kuthibitisha usahihi wake.


Jambo la Tatu :


Hakika fadhila zilizothibiti kwenye haki za Aalil Bait (a.s)


hazimaanishi kupwekeka kwao kwa fadhila hizo zilizokuja bila ya


kuwashirikisha wengineo, na hivyo ni kwa kufata kanuni inayosema:(


Kufanyiwa umakhsusi kwa makarama hakumaanishi kuondolewa


kwa mwengine).


9 (Al Hadaaiqin Naadhira h) cha Yusuful Bahry(50/1) Bihaarul Anwaar ccha


Al mjlisy(250/2)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


13


Lau tutasema: Hakika Nabii (s.a.w) amesema kuhusiana na haki ya


Ali ( r.a) – nae ni katika Aalil Bait ( r.a)-: "Bendera hii nitampa mtu


ambae Allah atakomboa juu ya mikono yake anayempenda Allah na


Mtume wake, naye anampenda Allah na Mtume wake"


Jee kwenye hadithi hii ichukuliwe kwamba makarama haya


yameondoshwa na hayawezekani juu ya Aalil Bait waliobakia (r.a), na


kwamba Al Hassan na Al Hussein wao hawampendi Allah na Mtume


wake (s.a.w)


Kwa maumbile tu ni kwamba haiwezekani, bali wao ni mabwana wa


vijana wa watu wa Peponi na hakuna shaka kwenye mapenzi ya Allah


na Mtume wake (s.a.w) kwao, na kwamba lengo la habari ni kwamba


Allah amempa hadhi na kumnyanyulia cheo chake kwa kufanyiwa


umakhususi ya kutajwa, kwa mfano :


Amesema Allah Taala kuhusiana na Aalil Bait (r.a) {Hakika Allah


anataka kuwaondoshea takataka Aalil Bait na kuwasafisha


msafisho ulio bora} [Al Ahzaab :33]


Na akasema kuhusiana na Masahaba {Kamwe Allah hataki


kukufanyieni uzito lakini anataka kukusafisheni na kukutimizieni


neema zake kwenu }[Al Maaidah :6]


Usafishaji ni wenye kuenea kwa waumini wote, lakini Allah


amewafanyia umaalum Aalil Bait (r.a) kutokana na ubora wao, nawe


pima juu ya hili, na hakuna shaka kwamba baadhi ya Aalil Bait ( r.a)


wanayo mambo maalum na yanayowatofautisha na wengine ambayo


kwayo hawashirikiani na yeyote yule, kama ambavyo baadhi ya


Masahaba (r.a) wanayo mambo maalum na sifa za ziada


wasizoshirikiana kwazo na mwengine yeyote yule hivyo ni wajibu


kumpa kila mwenye haki; haki yake, na jambo lenyewe ni pamoja na


Hadithi ya Kisaai mashuhuri ambayo ndani yake imo sifa kubwa kwa


baadhi ya Aalil Bait ( r.a) na kuingiza baadhi ya watukufu wa Aalil


Bait ( r.a) kama vile Hassan na Hussein, nao ni katika jamaa wa


Mtume (s.a.w) ambao hawakuwa wakiishi kwenye nyumba ya Mtume


(s.a.w) kwenye hukumu ya aya tukufu, hivyo haifahamiki sio katika


wa karibu au wa mbali toka katika hadithi hii kubinya Ualil Bait ( r.a)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


14


kuwa wa Ali pekee, Fatma, Hassan na Hussein (r.a) na tukawakusanya


pamoja nao, na pia katika hadithi hii haifahamiki kuingizwa na


kutolewa kwa wengine, sio katika sharti la kuingizwa hawa ni


kutolewa mama wa waislamu - Allah awaridhie wote- na rehema za


Allah zimepanua kila kitu, hivyo kamwe hazimbinyi mmoja kwa ajili


ya mwengine, lau mtu angesema nae anao ndugu kumi; Omar, Ali na


Khalid ni ndugu zangu. Jee hii inamaanisha kwamba saba waliobakia


sio ndugu zake? Haya huja kwenye maneno ya waarabu kwa wingi


bali hata kwenye Quran Tukufu, mfano wa kauli yake Taala :{Hakika


idadi ya miezi mbele ya Allah ni miezi kumi mbili kwenye Kitabu


cha Allah siku Allah aliyoumba mbingu na ardhi miongoni mwao


imo minne mitukufu (hurum), hiyo ndiyo dini iliyonyooka } [at


Tawbah :26], yaani hiyo ndiyo dini iliyonyooka, na kwamba dini


iliyonyooka imefupishwa kwenye idadi ya miezi na kuwa miongoni


mwao imo miezi mitukufu, basi kadhalika kauli yake (s.a.w) kwenye


hadithi ya Kisaa –nguo-"Hawa ni Ahlil Bait yangu " Anamaanisha


watu wa nyumba yangu kama tulivyobainisha.


Nasi tunaweza kusema kuwa iwapo Hadithi ya Kisaai inazuwia


kuingia mmoja wa Ahlil Bait, basi vipi kaingia humo Ali bin Hassan


bin Muhammad, Muhammadi al-baaqir, na Jaafar Sadiq na wengineo?


miongoni mwa Itra watukufu waliobakia, na hawa bila shaka asilani


hawakuwepo kwenye tukio la kutukuza kwa ajili ya Kisaa.10


Jambo la nne:


Kwamba kutegemea nasabu pekee haitoshi;


Kama ilivyo kuwa ni wajibu juu yetu mapenzi ya (Aalil Bait mmoja ),


kwa sababu ya imani yake kwa Allah na nasabu yake na ujamaa wake


kwa Nabii (s.a.w), basi ni wajibu pia kwetu kumchukia kwa kiwango


cha maasi yake, hali yake ni hali ya mtu mmoja mmoja wa umma huu


10 Angalia 9Aayatu tathiir cha 'Abdil Haadil Husseiny (uk. 20)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


15


na "Na yeyote yule aliefanya upole wa amali yake basi kamwe nasabu


yake haitomuharakisha."11


Jambo la Tano:


Ufanyaji wa Ualil Bait ( r.a) kuwa wa Ali, Fatma, Hassan na Hussein


(r.a) na kwenye watoto tisa wa Hussein tu, kwa hali yoyote ile haisihi,


ufanyaji wa Ualil Bait ( r.a) kuwa wao peke yao ni kinuyume na


uhakika wa mambo . Na katika ufanyaji wa Ualil Bait ( r.a) kuwa wao


peke yao wamefutwa wengi wa walio Aalil Baitin Nabawy


iliyotukuka, na ndani yake umo unyimwaji wao wa nasabu hii


iliyotoharika, na haki zinazotokana nazo kiibada, kimazingatio na


kimali kwao na juu yao, Allah alizowateulia na kuwakadiridhia juu


yao, hapa sipo pahala pa kuzielezea kwa urefu .


Na katika yaliyokuwa hayana shaka ni kwamba ufupishaji wa ujamaa


wa juu ya waliotajwa (r.a), kwa vyovyote vile kunapelekea upunguzaji


wa kizazi cha Mtume (s.a.w) na haingii akilini mtu yeyote yule kuwa


mtu anaweza kuleta jambo hili .


Inatupasa kukuwauliza watu hawa :


• -Wako wapi maami wa Mtume (s.a.w) ?


• -Jee Hamza (r.a) sio katika watoto wa Abdil Muttalib?


• Upo wapi utajo wake jee yeye siye simba wa Allah na Mtume


wake, shahidi wa Uhud na shujaa wa Badri? Na pale


alipostashhadi Nabii (s.a.w) akahuzunika huzuni ambyo


hajawahi kuhuzunika kabla yake ?


• -Jee Nabii (s.a.w) hakusema "Bwana wa mashahidi mbele ya


Allah siku ya kiama ni Hamza"!?12


11 Sehemu ya Hadithi :aliyoismulia Muslim :Mlango wa fadhila za


kukusanyika kwenye kisomo cha Qur-n ikatika Hadithi ya Abi Hureirah(r.a)


nam. (2677)


12 Ameisimulia Hakim kwenye (mustadrak )( 120/2 ) na akasema (Swahihul


Isnad) na Dhahaby akampinga kwenye (Talkhis ) .Na Muhaddith albany


ameihukumu kwenye (As silsilati as Swahiha ) nam.(716 /nam 374)kuwa ni


sahihi kutokana sanad zake na shahid .


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


16


• Jee Abbas (r.a) sie katika watoto wa Abdul Muttalib na


ameshuhudia ukombozi wa Makka, na mwenye kuthibiti siku


ya Hunein pamoja na waliothibiti?


• Jee haikusimuliwa "Hakika Abbas (r.a) ni katika mimi na


mimi ni katika yeye?"


• Jee vile vile Nabii (s.a.w) hakusema:" Enyi watu !Yeyote


aliemuudhi ami yangu basi huyo ameniudhi mimi ; hakika


ami wa mtu ni mfano wake" 13


• Wako wapi watoto wa maami wa Mtume (s.a.w).?


• Jee Jaafar At Tayaaru – mwenye kuruka kwa mbawa – (r.a)


mtu mwenye mambo bora na yenye kushukuriwa?


• Jee yeye siye aliyesemewa na Nabii (s.a.w) (umeshabihi


umbile na tabia zangu )? 14


• Jee Yeye hakuwa mmoja wa watangulizi kwenye uislamu ?


• Jee hakuwa miongoni mwa waliohamia Uhabeshi, na


kuendelea kuwa huko mpaka Mtume (s.a.w) alipohamia


Madina, akaja siku ya ukombozi wa Khaibar, na Nabii (s.a.w)


akafurahi furaha kubwa na kumkumbatia na kumbusu baina


ya macho yake ?


Imesimuliwa kwamba alimwambia :"Sielewi ni kwa jambo lipi mimi


ni mwenye kulifurahia zaidi;ukombozi wa Khaibar au kuja kwa


Jaafar?"15


Pale Nabii (s.a.w) alipompeleka Muuta kuwa naibu wa Zaid bin


Haaritha (r.a) alifanya kazi kubwa kwenye njia ya Allah, akapigana


13 Ameismulia At Tirmidhy akasema (Hassanun Swahihun ) na (Ahmad )


(165/4), akadhoofishwa pia na Muhadith Albaany . kwenye Silsialti


Dhaiifah(446/2 nam .806 ).


14(Hakim kwenye Mustadrak) (325/3) (Swahihul Isnaad )


Ameismulia At Tirmidhy


15 Imesimuliwa na Bayhaqy kwenye (Sunanil Kubra) (101/7) kwa Sanad


yake ni mpaka kwa shaaby toka kwa Nabii(s.a.w) kwa hiiyo.Na aksema:"Hii


ni Mursal"


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


17


mpaka akakatwa mikono yake miwili na akastashhadi, Allah


akamlipa mbawa mbili kwa sababu ya mikono yake hiyo miwili


Peponi, kama alivyotolea habari Assadiqul Masduq (s.a.w) basi tokea


siku hiyo duniani akapewa jina "Attayaar" ?


Nabii (s.a.w) zilipomfika habari za kustashhidi kwake alihuzunika


huzuni kubwa na kusema "Usiku wa jana niliingia Peponi nikamuona


Jaafar anaruka pamoja na Malaika. "16


Na akasema (s.a.w) (Jaafar alinipita kwenye kundi tukufu la Malaika,


huku mbawa zake mbili zikiwa zimepakwa damu zikiwa nyeupe).17


Hivyo baadhi ya sifa zake zinazojulisha ukubwa wa hadhi yake na


utukufu wa cheo chake duniani na akhera, Allah amridhie yeye na


yeye amridhie.


Jee Abdillah ibn Abbas wino wa umma –huu- na mfasiri wa Quran


aliyeitwa wino kutokana na wingi wa elimu yake, fahamu zake na


ukamilifu wa akili na wingi wa fadhila zake. Kwanini isiwe hivyo,


wakati Mtume (s.a.w) alimuombea dua ya kuwa na fiqhi ya dini na


elimu ya utambuzi? 18 nae alikuwa katika walioshuhudia Jamal na


Swifin pamoja na Ali (r.a), na Masahaba wakuu (r.a ) na Matabiina


walikiri ubora huu kwake –Allah awaridhie kwa wema-.!


Kiko wapi kizazi cha Ali (r.a) nacho ni wengi ?


Kiko wapi kizazi cha Hussein (r.a) kilichobakia na miongoni mwao ni


wajukuu wa Shahidil Kuufah, Zaidi bin Ali bin Hussein, na kizazi cha


watoto wake waliobakia ?


16 (Hakim kwenye Mustadrak) (196-209) na akasema (Swahihul Isnaad ) na


akahukumui usahihi wake kwenye (Mukhtaararah ) Muhadith Albaany .


kwenye (Swahiih Jaamii :3358 ) angalia Silsialt Swahiiha (227/3 chini ya


nam.1226) .


17 (Hakim kwenye Mustadrak) (312/3) na kusema (iko kwenye sharti la


Muslim ) na kuafikiwa na Muhadith Albaany . kwenye (Silsialt Swahiiha)


(226/3 chini ya nam.1226) .


18 Muttafaqun 'Alaihi


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


18


• Zipo wapi haki zao hawa ?


• Jee wao ni katika Aalil Bait ( r.a) au sio ?


• Na iwapo wao hawamo basi ni nani huyo aliyewatowa?


• Na kwa dalili na hoja ipi inajusurishia tendo hili ?


• Jee ipo njama nyuma ya ovu hili ? 19


Mjadala wa maudhui hii na uwazi wake hapa sio pahala pake, ila


tumetaja hayo kwa lengo la kumtanabahisha msomaji mpendwa


kwamba Historia ya Aalil Bait ni pana, kubwa na tukufu kuliko


wanavyoitaja baadhi.


Aalil Bait ni wengi Allah awazidishe na kuwabariki, nao ni wale


walioharamishiwa sadaka, ambao ni: Bani Hashim, wake wa Mtume


(s.a.w) nao ni katika ahli zake –jamaa wa kufuatia sio kwa uasili kama


ambavyo makumi ya nasi zilizothibiti zilizowazi zilivyojulisha hivyo;


hivyo ni kwamba kabla hawajaolewa na Mtume (s.a.w) hawakuwa


kati aali wa nyumba yake na nasi mutawatiri ni nyingi kwenye vitabu


na nasi ambazo zinabainisha tuliyoyataja ni kutowafunga Aalil Bait (


r.a) kwenye Ali, Fatmah na baadhi ya kizazi cha Hussein Allah wote


awaridhie, amesimulia Muhammad bin Sulaiman al Kuufy :" Hussein


bin ‘Uqbah alimuuliza Zaidil Aram :"Ni nani Aalil Bait yake ( r.a) jee


wake zake sio Aalil Bait wake ( r.a) ?


Akasema :"Hakika wake zake ni ahli zake, lakini Ahli beit yake ni


wale walioharamishiwa sadaka juu yao baada ya yeye akamwambia


Hussuein "Ni nani hao ewe Zaid?" akasema ni jamaa wa Jaa'far, jamaa


wa Aqiil na jamaa wa Abbas "20


Khuily nae ameeleza hivyo, na akasema kwenye Kauli yake


Taala:{Na wenye ujamaa} [Al Hashr:7] "Yaani jamaa wa Nabii


(s.a.w) nao ni aal -jamaa wa - Ali , aal-jamaa wa - "Abbas, aal-jamaa


19 Angalia Aalil Bait wa (Hukuukuhum Shariyyah ) cha Qadhi Swalih


Darwiish (uk . 9-12 ).


20 (Manaaqib Amiiril Muuminiin (a.s) (116/2) na akaashiria hivi pia arbili


kwenye Kashfil Ghummah na …. )


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


19


wa Jaafar na aal-jamaa wa- 'Aqiil (r.a), na kamwe hakushirikiana na


yeyote mwengineo, na wajhu huu ni sahihi kwani unawafikiana na


madhehebu ya Muhammad (s.a.w) "unajulisha wale waliotajwa kwao


wao"21


Amesimulia Assidiq kwamba Ali (r a) amesema "Ewe Mtume wa


Allah hakika wewe unampenda Aqiil: Akasema "Naam Wallahi,


hakika mimi ninampenda mapenzi mawili: mapenzi kwa ajili yake na


mapenzi kwa ajili ya Abi Twalib kwake, na kwamba mwanawe


atauliwa kwa sababu ya kumpenda mwanao.. mpake pale aliposema:


"Nashitakia kwa Allah kwa yatakayowakuta jamaa zangu baada


yangu"22


Hivyo akamuingiza Uqail na wanawe wawili kwenye wanaoitwa -


jamaa waliotoharika (al ataratit taahirah)-.


Jambo la Sita:


Nyingi ni kauli baina ya kurasa za vitabu vyenye shubuha ambavyo


vinadai kwamba Aalil Bait ( r.a) wamedhulumiwa na kukandamizwa


miaka kadha tokea kifo cha Nabii (s.a.w) na kupitia kwenye zama


Makhalifa waongofu mpaka kwenye Dola ya Umawiyyah na


Abbaasiyyah na hakuna yeyote yule miongoni mwa Aalil Bait ( r.a) ila


ameteseka kwa kufungwa, kuuawa, kuhamishwa, kutiliwa sumu au


madai zaidi ya hayo .


Haya hujibiwa kwa njia mbili :


Wajhi wa mwanzo :


Kwamba msingi wa ahli Sunna wal Jamaa na jambo ambalo halina


khitilafu katika hilo na kuwa makubaliano baina yao ni kuwaheshimu


Aalil Bait ( r.a) kujuwa fadhila na ujamaa wao kwa Nabii (s.a.w) na


wasia wake kwao amesema: Nabii (s.a.w) ''Na watu wa nyumba yangu


nakukumbusheni Allah kwenye watu wa nyumba" "nakukumbusheni


21 ()'Umdatu'uyuunSahhahil Akhbaar)cha Hully(6-7).


22( Amaalit Tuusy ) uk. (191 ) na Bihaarul Anwaar cha Al Majlisy


(288/22,44/287)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


20


Allah kwenye watu wa nyumba yangu","nakukumbusheni Allah


kwenye watu wa nyumba yangu "23 Hivyo Aqida ya Ahli Sunnah wal


Jamaa imo kwenye vitabu vyao; vitabu vya Hadithi vitabu Aqidah,


vitabu vya Fiqhi, vitabu vya Tarajum na Sirah ambamo kila mwenye


kitabu hutaja kwenye sehemu iliyo na mnasaba na habari hiyo. Hivyo


kwenye vitabu vya Hadithi utaona milango kuhusiana fadhila zao,,


kwenye vitabu vya Aqida utaona ubainishaji wa itikadi kuhusiana na


wao, kwenye vitabu vya Fiqhi utaona milango kuhusiana na


yanayohusina nao katika ahkami, kama vile kuharamishwa sadaka juu


yao, na vitabu vya Tarajum na Sirah vinataja utajo wao, maelezo


kuhusiana na wao na taarifa zao.


Huu ndio msingi kwa Ahli Sunnah, msingi huu kamwe hauwezi


kuporomoka ila kwa dalili iliyo ya wazi, na tunaposoma Historia na


tutaona kwamba hayo yanayodaiwa na baadhi yao kuhusiana na


ukandamizaji wa Ahli Sunnah na viongozi wao kwa aal beit ni batili


yasiyosihi wala kuthibiti ila pale panapokuwa na kinyang'nganyiro juu


ya uongozi na madaraka kama ilivyotokea kwenye mapinduzi ya


Imam Zaid, Allah amrehemu yeye na wengine.


Amesema Sheikhul Islaam Ibni Taymiyah (  !""    #$) "Ama yule


aliyemuuwa Hussein, au kusaidia basi huyo amethibitikiwa na laana "


ya Allah. Malaika na watu wote"24


Hivyo haisihi kabisa muislamu kupaka matope historia ya Aalil Bait


(r.a) iliyosafi na mapenzi ya waislamu kwao kwa kisa cha batili au


riwaya ya uongo kama vile anavyofanya Al Asfahaany kwenye kitabu


chake (Muqaatilut Twalibiin), kitabu cha Al Asfahaany kilichopewa


anwani ya (Muqaatilut Twalibiin) ni kitabu kilichojaa batili na uongo


wa kihistoria ambao mwandishi yeyote anashindwa kuyathibitisha


kabla hajawarembea ahli Sunna wal Jamaa uongo huu ulio mkubwa .


23 Swahihu muslim(Hadithi nam.2424)


24 Majmuu Fataawa )(487/4).


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


21


Vitabu vya kihistoria vimesheheni habari za kuheshimiwa kwa Aalil


Bait (r.a) na Makhalifa, kuwapenda na kuwapa kwao hadhi :


Amesema Abu Bakri (r.a) "Mchungieni Muhammad watu wa nyumba


yake"25 Na akasema (r.a) "Naapa na yule ambaye nafsi yangu iko


kwenye mikono yake hakika ujamaa wa Mtume wa Allah (s.a.w)


kwangu mimi ni bora zaidi kuliko asili ya jamaa wangu "26 Nae (r.a)


akasema vile vile akiwa anazungumza na Fatma na Ali "Wallahi


kamwe sikuwacha nyumba wala mali, na jamaa na watu wa


nyumbani, ila kwa kutafuta ridhaa ya Allah, ridhaa ya Mtume wake na


ridhaa ya jamaa zake"27


Abu Bakri (r.a) alipeleka mmoja wa wake zake nae ni Asmaa bint


Umeish kwenye nyumba ya Ali kwa lengo la kumuhudumia kwa tiba


Fatma (r.a) wakati wa ugonjwa wake bali pia akashiriki kwenye


kumkosha Fatma Az Zahraa na kumvisha sanda (r.a)28


Amesema Umar Ibn Al khatab (r.a) kumwambia Fatma (r.a) "Ewe


binti wa Mtume wa Allah hakuna yeyote kipenzi zaidi kwetu katika


viumbe kuliko baba yako na hakuna yeyote kipenzi zaidi kwetu katika


viumbe baada ya baba yako kwetu kuliko wewe.29 Inatosheleza


kwamba Omar alimteua Ali (r.a) kuwa katika jumla ya kundi ambalo


ndani yake muwe na khalifa wa waislamu baada yake"


Na Omar Alimuoa binti ya Ali -Ummu Kulthuum- (r.a)


Hivyo hivyo hali pamoja na Khalifatir Rashid Othman bin Affaan,


historia yake ni yenye kumeremeta kwa wingi kutokana na misimamo


25 Akasema pia (r.a)


26 Imesimuliwa na Bukhary (3713) mlango wa sifa za Hassan na Hussein .


27 Angalia (As Sunanil Kubra) cha Bayhaqy 301/6,na (Bidaaya wan Nihaaya)


cha Ibni Kathiir253/5.


Akasema Ibni Kathiir :"Hii sanad yake ni sahihi ,yenye nguvu"


28 Angalia Al Istiiaab cha Ibni 'Abdil Barri 387/4 na (Asmaal Matwaalib )


cha As Swalaaby 160.


29 (Muswannaf Ibni Abii Shaibah ) 567/14, na isnadi yake ni sahihi.


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


22


ya kushirikiana baina yake na baina ya Aalil Bait ( r.a) na namna


alivyokuwa akishauriana na Ali kwenye kadhia kadha, bali uhakika


wa uhusiano huu wa kidugu unatudhihirikia namna Ali


alipowasimamia wanawe kwenye kumlinda Othman bin Affaan siku


alipostashhadi kwenye nyumba yake (r.a) na hivyo ni kwa ajili ya


mapenzi kwake na mapenzi ya Othman bin Affaan kwake kwani


msimamo wao ni kujizuwia na vita.30 Imeelezewa kwamba Harun


Rashid alikwenda kwenye kaburi la Nabii (s.a.w) akijifakharisha kwa


watu, akasema Assalamu Alaikum Ewe Mtoto wa ami-yangu – kwani


yeye ni katika kizazi cha Al Abbas bin Abdil Muttalib, akaja Musa bin


Jaafar kamwambia; Assalamu 'alaika ewe baba yangu, Harun Rashid


anaangalia, akasema Wallahi huku ni kujifaharisha.


Harun Rashid akasema "Nimepata habari kwamba wengi


wananidhania mimi namchukia Ali bin Abi Talib, na Wallahi mimi


kamwe simpendi yeyote kama ninavyompemnda yeye."31


Khalifa Muadilifu Umar bin Abdilaziz alimwabia Fatmah bint Ali bin


Abi Talib (r.a) "Ewe bint Ali Wallahi kwenye uso wa ardhi hii hakuna


Aalil Bait ( r.a) vipenzi kwangu kuliko nyie na nyie ni vipenzi zaidi


kwangu kuliko jamaa zangu"32


Watu walijikumbusha Zuhudi na Mazuhadi basi kundi moja likasema


fulani na jengine likasema fulani Umar bin Abdilaziz akasema: zahid


kuliko yeyote yule ni Ali bin Abi Talib (r.a)"33


30 Tarekhe Dimashq cha Ibnl 'Asaakir 402/1 na Twabaqaat Ibn Saad 128/8.


31 Tarekheul Khulafaa cha as Suyuuty uk. 293.


32 Angalia Twabaqatil Kubraa cha Ibni Saad 388/5


33 Siya'Umar cha Ibnil Jawzy 292.akiwa amenakili tokakwenye(Ad Dawlwtul


Umawiyyah cha Daktari As Swallaaby .)


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


23


Wajhi wa Pili


Hakika jambo kubwa na lenye hadhi kubwa toka kwa watu na hasa


hasa akiwa ni katika wema wa umma na maulamaa wake Allah (S .W)


analomfanyia mtihani ili amnyanyulie hadhi na daraja yake kwenye


Pepo zenye neema, hivyo mwenye kupata mtihani mkubwa au kuuawa


miongoni mwa ahlil Bait kama ilivyotokea kwa Hussein (r.a) -Shahidi


mwenye kufanikiwa, basi huwa ni namna ile (Allah anapompenda mja


humfanyia mthani), na jambo hili sio maalum wala kukusudiwa ahlil


Beit (r.a) tu bali dhuluma imetokea juu ya maulamaa wengi wa Sunna


na wakuu wao kama vile Said bin Jubeir, Imam Abu Hanifa, Imam


Malik na, Imam Ahmad na wengi wengineo miongoni mwa wema wa


umma wa Muhammad (s.a.w).


Dhuluma, ukandamizaji na mabalaa yamewatokea Manabii wa Allah


(a.s) na wema waliokuja baada yao, huyu Daniel (a.s) aliekutana na


mabalaa ya aina ya mwisho ya ukandamizaji aliyofanyiwa na mfalme


mwenye kiburi "Bakhtanasir" kwa kumfunga na akamuingizia simba


wawili lakini Allah akamuhifadhi na kumlinda dhidi yao.34


Hivyo hivyo kisa cha Nabii wa Allah Yaqoub (a.s) kwa kupotelewa na


mwanawe, Nabii wa Allah Zakariyyah, Nabii wa Allah Mussa (a.s)


mbele ya mwenye kiburi Firaun, Nabii wa Allah Issa (a.s) pamoja na


mayahudi, Nabii wa Allah Muhammad (s.a.w) akiwa na Makureshi na


makafiri wa Makka, na visa vyao ni mashuhuri vyenye kujulikana.


Na baada yao ni Masahaba wa Nabii (s.a.w) waliohama toka kwenye


nchi zao, mali na jamaa zao, waliadhibiwa kwa aina za adhabu na


kuendelea mpaka baada kufariki kwake Nabii (s.a.w) yalitokea


yaliyotokea kwa waliokuwa kabla yao miongoni mwa watukufu,


Omar al Faruq (r,a) aliuawa kwa khanjari ya khiyana na chuki, akiwa


anasalisha kwenye mihirabu, hivyo hivyo Shahidudaar Othman bin


Affaan (r.a) aliyeuawa kwenye nyumba yake akiwa anasoma Quran,


hivyo hivyo ndivyo alivyouawa amiiril Muuminiin Ali (r.a) akiwa


anatangaza :"Enyi watu sala! Sala!, na wengineo katika Masahaba


34 "Al Bidaaya wa An Nihaaya " cha Ibni Kathiir 428/1


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


24


wema, na kadhalika balaa na ukandamizwaji yamewapitia maulamaa


wengi na wakuu.


Huyu hapa Imamu Al Awaza'iy –Allah amrehemu –alifikwa na balaa


kubwa mbele ya mmoja wa wenye jeuri na kukaribia kumuawa,


Habari za Imam wa Ahli Sunna Imam Ahmad–Allah amrehemu –


pamoja na Khalifa Muutaswim ni mashuhuri na zenye kujulikana,


hakika alimuadhibu na kumpiga viboko mpaka mgongo wake


ukachanika na kuchunika ngozi, akamfunga gerezani na kumbana 35


Pale Fatimiyina walipotawala Misri waliwakandamiza maulamaa na


miongoni mwao alikuwa Imam Abi Bakri An Naablisy, wakaamrisha


kupigwa kwenye siku ya mwanzo kisha siku ya pili kutundikwa mbele


ya watu, kisha siku ya tatu yake kuchunwa na kutolewa ngozi toka


kwenye nyama yake, kwa kisu cha kiyahudi .36


Imam Nuaim bin Hamad aliekufa akiwa amefungwa kwa minyororo


gerezani na kumuondowa akiwa maiti wakamrembea shimoni bila ya


kuoshwa .37


Imam al Harawyil Answaary anasema:"Nilionyeshwa upanga mara


tano, siambiwi rudi kwenye madhehebu yako, ila naambiwa nyamazia


waliokutangulia, huku nasema sinyamazi ."38


Mifano ni mingi mno, na lengo ni ukandamizaji na dhuluma juu ya


Ahli Sunna na maulamaa wake, kama ilivyotokea kwa wenginewe, na


mtukufu hufanyiwa mitihani, na kamwe hawatowachwa kufanyiwa


mitihani. .


35 Sira ya Imama Ahmad cha Ibnil Jawzy.


36 " Hashia ya Al Bidaaya wa An Nihaaya " 284/11, na "Al 'Ibar fii Akhbaaril


Ghubar " cha Ad Dhahaby 33/2


37 Angalia (As Siyari a'alaamin Nubalaa) cha Adh Dhahaby 610/10


38 (As Siyari a'alaamin Nubalaa) cha Adh Dhahaby 509 /18


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


25


MLANGO WA NNE


Miongoni Mwa Vitabu Muhimu vyenye Kutegemewa kwenye


Historia


Mwenye lengo la kujuwa vianzio vya Tarekhe vyenye kukubalika,


anaweza kupata kwenye vitabu vya tarekhe na Hadithi zenye


kuwekewa sanad maalum kwa maelezo ya historia za watu na watu


maalum na historia zao, ni sawa iwe watunzi wake wamejiwekea


sharti atika maulamaa wenye kukubalika usahihi kwenye kuzitaja


kwao, au kwa kutolea maelezo juu ya riwaya kuhusiana na usahihi na


udhaifu wake, hivyo vitabu vimemtoshelezea msomaji wake tabu za


kutafiti na uhakiki, ama vile vitabu ambavyo wasimulizi wake


wanasimulia kwa sanadi bila ya kubainisha hali zake basi ni wajibu


juu ya msomaji wake kuhakikisha usahihi wake.


• Na hivi hapa ni baadhi ya vianzio vya Kihistoria ambavyo


inawezekana kutegemewa katika usomaji na kuandika


Historia ya kiislamu ,tunavitaja minogoni mwao:


1. Kitabu" Tabaqatil Kubraa" cha Ibni Saad aliyefariki


mwaka 230 H:


Nacho ni kitabu muhimu katika mlango huu ; kwani yeye –Allah


amrehemu –anataja riwaya kwa sanadi zake, hivyo msomaji hana kazi


yoyote ile isipokuwa kufanyia utafiti sanadi hizo ikiwa ni mwenye


uwezo wakufanya hivyo, na katika sifa zenye kutofautisha kitabu


hichi na chengine ni kwamba ni katika vitabu vilivyotangulia na


vianzio vya Sira ya Nabii (s.a.w), Tarajumi na habari, mtunzi wake


aliwahi karne ya pili hijriyya pamoja na kuchukulia tahadhari riwaya


za Waaqidiy, na madhaifu na matrukina (wenye kuwachwa riwaya


zao) na wenginewe, au kama haelewi basi aulize wanaolewa kama


alivyoamrisha Allah Azza wa Jalla kwenye Kitabu chake kitukufu.


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


26


2. Taariikh Khaliifati bin Khayyaat ":


Nacho hata kikiwa ni kidogo zaidi kuliko kitabu 'Tabaqatil kubra"


ila ni kwamba kinayo sifa ya ziada ya usalama wa matini zake


katika udhihirishaji wa fitina ,na mara nyingi yaliyotokea kwenye


zama za Masahaba (r.a).


3-(Tarekheil Umam wal Muluuk) maarufu (kwa Tarekhet


Twabary)


Nayo ni Tarekhe iliyojaza habari, athari na riwaya, lakini


imechanganya yaliyokonda na yaliyonona, na hakuna lawama


kwa Twabariy, kwani yeye ameweka sanadi kwenye riwaya hizi,


na mwenye kuwekea sanad basi huyo ameshajiondoshea dhima na


lawama, na tumeshabainisha kwa uwazi kwenye utangulizi wa


kitabu .


4-Al Bidaaya Wan Nihaaya Cha Imam Ibni Kathiir:


Mtunzi wa kitabu cha “Tafsiiril Quran al Karim “,kitabu hichi


hata pamoja na kwamba ananukuu riwaya zake toka kwenye


baadhi na vianzio vilivyotangulia ila tu ni kwamba kinayo


maelezo juu ya riwaya nyingi za kihistoria kuhusiana na usahihi


na udhaifu, kutokana na kuwa kwake Imamu kwenye hadithi na


elimu zake, na chapa bora zaidi ni chapa ya Daaril Hijra chini ya


usimamizi wa ‘Abdillahi Turky.


5-“Taariikh Dimashq “ cha Ibn ‘Asaakir:


Nayo ni historia iliyojaza ni makhsusi kwa walioingia Damascus


miongoni mwa maulamaa katika masahaba na wengineo mpaka


kwenye kipindi cha mtunzi, nacho kinatofautiana na vyengine


kwa kuwa na sanadi kwa kila tukio’


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


27


6-“Tarekheul Islaam” cha Shamsid Diin Adhdhahaby


Nacho ni kitabu kikubwa chenye manufaa makubwa, husimulia


kisa kamili cha historia ya kiislamu, na vielelezo vyake na


matukio yake muhimu, kina sifa ya ziada inayotokana na maelezo


ya imam juu ya taarifa za matukio ya kihistoria, matukio na athari.


Nae imam Dhahaby ni bahari kwenye elimu ya Jarhu na Taadiil


ni katika maimamu wakubwa katika fani hii, na Daktari Bishar


Awaadh Maaruuf amefanya kazi kubwa ya kufanyia uhakiki,


kitabu hichi kinahesabiwa kuwa ni katika chapa bora zaidi.


7-“Siyaru ’Alaam Nubalaa” cha Hafidh Adhdhahaby (  !    #$)


Nacho ni kitabu chenye manufaa vilevile, kinatowa sira na habari


za nyota na muhimu katika maulamaa zilizojulikana katika


historia ya kiislamu tokea mwanzo wa kipindi cha Masahaba (r.a)


mpaka karibu ya kifo cha mwandishi (  !    #$), nae


ameambatanisha na kitengo maalum kwa Sira ya Nabii (s.a.w) na


historia za Makhalifa wanne waongofu na chapa bora zaidi ni ile


chapa ya Muasasat Risaalah.


8.”Taariikhul Madiinah cha Ibn Abii Shaibah


Ni kitabu kilichojaa faida, Ibn Abi Shaibah ametilia umhimu


mkubwa utajaji sanadi kwenye hadithi na habari zilizo nyingi, na


ndani yake zimo riwaya muhimu kuhusiana na fitina na mauaji ya


Shahidi Othman bin Affaan (r.a), na kitabu kina kosoro ya baadhi


ya maudhui zake kutokana na kupotea kwa baadhi ya miswada,


kwa mfano ukhalifa wa Abi Bakr haumo kwenye kitabu.39.


9- “Tarekhe Ibn Khulduun”


10-“Al Muntadham fiy Att arikh “ cha Ibnil Jawzy .


39 Angalia Mpango wa uandishi wa historia ya Kiislamu cha Muhammad


Swamil as Salmy.


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


28


11-“Awaaswim minal Qawaasim” cha Abi Bakr bin Al ‘Araby


Kimehakikiwa na kutolewa maelezo na sheikh Muhibbudini al


Khatib (r.a), na kitabu hichi kimechapishwa mara nyingi, na


kukubalika kwa wasomi wakuu na wengineo kutokana na nafasi


na hadhi ya mtunzi wake ambaye ni katika maimamu. wa


Kiislamu Abi Bakr bin Al ‘Araby na kutokana na hoja zilizowazi


na majibu yanayotosheleza kwa masuala mengi muhimu, hivyo


kitabu ni cha aina yake kwenye uwanja wake, anakuja na


(Qasima) shubuha, anaifuatanisha na uchambuzi na kuweka wazi


shubuha (‘Aswima ), na kuijibu kwa hoja, dalili sahihi.


Hivi ndivyo vitabu muhimu vilivyotolea umuhimu uelezaji wa tarekhe


na matukio ya kiislamu , na vyenginevyo vipo vingi katika uwanja


huu ,ni sawa viwe vya zamani au vya kisasa .


Kamwe haituondekei kwenye kiini chake kuashiria kwamba vipo


vitabu sio makhsusi kwa Tarekhe, na humo mumewekwa matukio


muhimu, na habari za kimsingi kwenye Tarekhe ya kiislamu, na hasa


kwenye zama za mwanzoni, mfano kama vile vitabu vya hadithi,


Masanidi Maajim, na muhimu vyao :


1-“Asahihi “ ya Imam Bukhariy .


2-“Asahihi “ ya Imam Muslim .


3-“Sunanul Arb’a” ya Abi Daud, Annasai, At Tirmidhy, na Ibn


Maajah .


4- “Al Musnad “ cha Imam Ahmad bin ‘Hanbal.


5- Al Muswannaf cha Ibni Abi Shaibah .


6-“ Mustadrak “ ya Haakim Nisapury.


• Ama vitabu vya tarajumi za Masahaba –wakiwemo Aalil


Beit- (r.a) vya kimsingi n amuhimu ni kama :-


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


29


1-Al Istii’aab fiil Ashaab cha Ibni ‘Abdil Barr .


2-“Usudul Ghaabah fii tamyiiz Sahaabah “ cha Ibni;l Athiir .


3- Al iswabah fi Tamyiiz Sahabah cha Ibn ‘Hajaril ‘Asqalany


Vitabu hivi ni vyenye habari na athari, na tunakumbusha kwamba


habari na athari hizi vinalazimikiwa na mizani ya uhakiki na utafiti


hasa katika kufahamu sanadi na kuhusiana na Jarh na Taadiil; ili


kujuwa sahihi kutokana na dhaifu .


• Ama vitabu vy kisasa :Wapo watafiti waliosafisha na


kudadisi riwaya, wakabainisha sahihi toka kwenye dhaifu


zake, hapa tunaashiria baadhi ya vitabu muhimu katika


vitabu hivi, mfano, Mtungo wa vitabu vya Daktari Ali bin


Muhammad As Swallaaby Allah amuhifadhi na ambariki


katika kuwepo kwake :


I -Al Inshiraah fii raf -i dhiiq siirati Abii Bakr.


2-Faswlil Khitaabi fii siirati Amiiril Mu-u- miniin Omar ibn Khatab


shakhsiyyatuhu wa Asruhu .”


3- Taysiiril Kariim fii sirati ‘Uthman bin ‘Affaan ‘’


4- Asmal Matwaalib fii siiratilAmiiril Muuniin Alibin Abi Talib “


5- Amiiril Muuniinal ‘Hussein bin Ali–Shakhsiyyatuhu wa ‘asrih I”


6-“Muawiya bin Abi Sufyaan “


7-“Omarbin ‘Abdil ‘Aziiz “


8-“Ad Dawalatul Umawiyyahtu ‘Awaamilil Idizdihaar wa


Tadaa’iyaatil anhiyaar”


Kadhalika vipo baadhi ya vitabu muhimu, mfano :


1- “Mausuatu Taariikhil Islaamy “ cha Muhammad Shaakir


2-Silsilatu KutubulMahmuud Muhammad Shaakir kuhusiana na


shakhsiyati40 za kiislamu .


40 Watu muhuhimu


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?


30


3-Siiratiu ‘Aaisha bint Ummul Mu-u –miniin “ cha Annadawy .


“Ahdathi wa ahadithi fitina".cha Daktari Abdil ‘Aziiz ad


Dakhkhaan :


Nacho ni kitabu chenye umuhimu wa kiwango cha juu katika kufanyia


uhakiki msimamo wa Masahaba kuhusiana na fitina zilizotokea, na


utafiti wa udadisi kwa wingi wa riwaya zilizokuja kuhusiana na jambo


hili, pamoja na maana ya fitina, msimamo wa Masahaba kuhusiana na


fitina hiyo, kubainisha sababu na athari zake, msimamo wa muislamu


kuhusiana na fitina hiyo na kitabu ni kutokana na risala ya udaktariri


na kimechapishwa na Maktabati Swahaabah Sharjah chapa ya


Mwanzo.


5- ‘Hiqbatun minat Tarekhe “ cha Sheikh ‘Uthayman Khamis :


Kitabu hichi kinahesabiwa kuwa ni vitabu muhimu vya wakati huu


mtunzi ametolea umuhimu kutaja miongoni mwa habari zilizosihi


katika habari na athari zilizokuja baada ya kifo cha Nabii (s.a.w),


mpaka kipindi cha kuuawa kwa Al Hussein (r.a) pamoja na kuweka


rai wa usahihishaji baina ya rai hizo


Viwanda vingi vya kupiga chapa vimekipiga chapa, na chapa yake


bora ni ile chapa ya Maktabatil Imamil Bukhaary -Ismailiya Misri-.


6-“Tahqiiq Mawqifis Swahaabati minal Fitan" cha Daktari


Muhammad Amhazuun.:


Nayo ni kazi ya risala udaktari, mtafiti ameshughulikia ndani ya


kitabu hicho riwaya na athari muhimu zilizokuja kwenye Ukhalifa wa


Makhalifa wane kisiasa (r.a).


Kimepigwa chapa na Dar twayyibah, na Maktabatil Kawthar Riyadh


chapa ya tatu .


7-‘Asrul Khilaafaashidah” cha Daktari Akrau Dhiyaail ‘Umary


Nacho ni kitabu chenye kudadisi riwaya za kihistoria kilicho mbali na


kushadidia au kufanyia wepesi .Kimepigwa chapa na Maktabatil


‘Abiikaan chapa ya nne. :


Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI