Nakala

SHIA ITHNA ASHARIA NI WATU GANI?





Maswahaba zake na wote waliyo ongoka kupitia


Muongozo wa Mtume amma baad.


Kitabu hiki ni miongoni mwa mfululizo wa vitabu


Ambavyo ni Muhtasari vyenye malengo ya


kuwabainishia Waislamu na kuwawekea wazi Itikadi za


Mapote [Makundi] yaliyo potea ili wawe na Tahadhari


na Makundi hayo hasa ukizingatia kuwa baadhi ya


Makundi hayo sasa yameanza kuwa na Sauti na


yamekuwa na Harakati za waziwazi katika kueneza


Upotovu wao na Tumeanza mfululizo huu kwa kundi la


[SHIA ITHNA ASHARIA] Hasa miongoni mwa


Makundi mengi ya Kishia kwa sababu Kundi hili ndilo


lenye kudhihiri zaidi.


Pia sababu nyingine iliyo pelekea kuanza na kundi hili ni kwa kuwa kundi hili Mara nyingi hunadi kuwa Madhehebu yao hayatofautiani na Madhehebu ya Ahlus-sunnah na wanadai kuwa wamedhulumiwa tu na kuzuliwa mambo ambayo sii kweli pia kundi hili linafanya Juhudi kubwa sana katika kutetea Itikadi yake na kusambaza Vitabu na Risala mbali mbali ili kueneza Madai yao pia kundi hili limekuwa likifuatilia Vitabu mbalimbali vya Wanachuoni wa Ahlus-sunnah na Kuvirudi wakati Juhudi hizi hatuzioni katika Makundi Mengine, Na kwakuwa Vitabu vya Kishia sasa vime'enea Ueneaji ambao Hatukuuzoea huko Nyuma na wamekuwa wakivieneza kwa njia mbali mbali kila Mahala, kutokana na sababu hizi zimetupelekea kuona Ulazima kuviweka Bayana na kubainisha Itikadi Potovu zilizomo ndani


صفحة 4


yake, Ambazo walijitahidi sana kuzificha Lakini


Tunasema kama Alivyosema Msemaji Mmoja:


(Tutakusimamishieni Hoja kupitia Vinywa Vyenu)!


Tunamuomba Allah Ainyanyue Bendera ya Sunnah na watu wake na Aidhalilishe Batwili na watu wake Allah peke yake ndie anayajua makusudio na ndie Mwenye kuongoza njia iliyo sawa. NB: Kuna baadhi ya Maneno Ambayo nimeongeza yanaumuhimu kwa Msomaji.


Yameandikwa na: ABDULLAHI BIN MUHAMMADI AS-SALAFY


Yame Tafsiriwa na:


YASSINI TWAHA HASSANI


(KONGOLO)


ASILI YA MADHEHEBU YAO


صفحة 5


Miongoni mwa itikadi za Shia ithna asharia: ni


kwamba wanakiri na kukubali kwamba Ushia Asiliyake


ni Uyahudi uliotokana na myahudi anaitwa Ibnu sabai


pia wanakiri kwamba Aly bin abi Twalib -Radhi za Allah


zimwendee- aliwachoma moto pindi walipomfanya


kuwa Mungu na akatangaza wazi wazi kuwa yuko mbali


nao kabisa na yuko mbali na itikadi hiyo.


Rejea kitabu: (Firaqu shia).


cha An-nubukhty. ukurasa. (22).


pia rejea kitabu: (Ikhtiyaaru marifatir-rijaal).


cha Atwuusy. ukurasa wa. (107).


Nao wanasema vilevile na kukiri bali kujifakharisha kwa kuitwa jina la Raafidhwa. Rejea kitabu: (Biharul- anwaar). cha almajlisy. (65/97).


ITIKADI YAO JUU YA ALLAH


Wanasema: Hakika sisi (Mashia) Hatuungani nao (yaani hawaungani na Ahlus-sunnah) katika itikadi ya Mungu wala Mtume wala Imamu kwa sababu wao wanasema kwamba: Mungu wao ni Yule ambaye Muhammadi alikuwa ndio Mtume wake na Khalifa wa Mtume wake alikuwa ni Abubakari. Na sisi (Mashia) Hatumuitakidi Mungu huyo wala Mtume huyo bali sisi Tunaitakidi kwamba Mungu ambaye khalifa wa Mtume wake alikuwa ni Abubakari huyo sio Mungu wetu na wala huyo sio Mtume wetu.


صفحة 6


Rejea kitabu: (Al-anwaarun-nuumaaniyya).


cha Niimatullahi Aljazaairy. (2/278).


Na katika itikadi zao wanasema kuwa: Allah


hataonekana siku ya Qiyama na kwamba Allah hasifiwi


kwa mahala wala kwa zama wala haashiriwi na kwamba


yeyote atakaye sema kuwa Allah hushuka katika Mbingu


ya dunia na kwamba ataonekana kwa watu wa peponi


wamuone wazi wazi kama wanavyo uona Mwezi basi


Mtu huyo anakuwa ni sawa na Kafiri.


Rejea kitabu:


(Aqaaidul- Imaamiyyah).


cha Muhammad Ridhwaa Midhfar.


ukurasa (58).


Na wanasema vilevile: hakika Mwenyezi Mungu


atakapo msemesha mja wake siku ya Qiyama atakuwa


Amejishika Kiunoni na mja nae Atasimama mbele ya


Mola wake hali kajishika nae kiunoni huku akitajiwa


Madhambi yake. Pakaulizwa: nini makusudio ya


kujishika kiunoni? Akasema mpokeaji wa habari hii:


Yule msemaji akajishika kiunoni kisha akasema:


yaani hivi kama vile Mtu anavyoongea na ndugu yake


katika jambo la siri kati yao.


Tazama kitabu: (Al-usuulus-sitata ashara). kilicho


hakikiwa na: Dhwiyaud-diin alhamuudy. ukurasa (203).


Na wanasema vilevile: Hakika Allah huteremka siku ya Arafa pindi Jua linapo pinduka Akaja Ardhini akiwa juu ya Ngamia akiwa kawaenea Watu wa Arafa Kuliani na


صفحة 7


Kushotoni.


Angalia kitabu: (Al-usuulus-sitata ashara).


Kilicho Hakikiwa na: Dhwiyaud-diin Alhamuudy.


ukurasa (204).


Na wanasema: Kulielekea Kaburi ni Jambo la Lazima


hata kama litakuwa haliko upande wa Qibla pia


kulielekea kaburi la Mtume kwa Mwenye kulizuru ni


sawa na kuelekea Qibla na huo ndio (Muelekeo wa


Mwenyezi Mungu) yaani alio waamrisha watu kuuelekea


katika hali hiyo.


Angalia kitabu: (Biharul- Anwaar).


cha Almajlisy. (101/369).


Na wanasema kuwa: (Aaah) ni jina miongoni Mwa


Majina ya Allah yaliyo mazuri hivyo Mwenye kusema


neno hilo anakuwa kamwita Allah kwa namna ya


kuomba msaada.


Angalia kitabu: (Mustadrakul-wasaail).


cha Annuury at-twabrasy. (2/148).


Pia wanasema kuwa: Mwenyezi Mungu huwa


anamzuru (kumtembelea) Husein bin Ally na kupeana


naye mkono na Anakaa naye juu ya Kiti.


Rejea kitabu: (Swahiifatul-Abraar).


cha Mirza Muhammad taqy. (2/140).


ITIKADI YAO KUHUSU KUBADILISHWA QUR-ANI


صفحة 8


Wanasema: Qur-an imebadilishwa na kwamba ni


Pungufu na Qur-an ambayo ni sahihi anayo Almahdi wao


anayesubiriwa kuja kwake. Miongoni mwa Wanachuoni


wa Kishia walio weka wazi Itikadi hii ni: Ally bin


Ibrahim Alqummy Pamoja na Niimatullahi Aljazaairy na


Alfaidhul Kaashaany na Ahmad Attwabrasy na


Muhammad Baaqir Almajlisy na Muhammad bin


Nuumaan wanaye muita Almufiid na Abulhasan al-


Aamily na Adnaan Albahraany na Yusuf Albahraany na


Annuury Attwabrasy na Wengineo wengi. Tazama


kitabu: (Ash-shia al-ithnaa asharia wa tahriiful-quran).


cha Muhammad Sayf. Na


kitabu: (Mauqifur-raafidhwa Minal-Quran)


cha Mamadoo kaaraambiiry.


Na wanasema kuwa tamko: (Aali Muhammadi na Aali


Ally) liliondolewa katika Qur-an.


Tazama kitabu: (Minhaajul-baraati sharhu nahjul balaaghah).


cha Habibullah alkhuui. (2/216).


Na wanasema kwamba: hakuna aliye ikusanya Qur-an


yote ispokuwa Maimamu.


(yaani maimamu wa shia ithna asharia)


na kwamba wao ndio wanajuwa Elimu yake yote.


Tazama kitabu: (Usuulul-kaafy). cha Alkulayny.


(1/228).


Na wanasema: Qur-an haiwezi kuwa ni hoja mpaka


atakapo kuja Alqayyim wao. (Mahdy).


Angalia kitabu: (Usuulul-kaafy). cha Alkulainy. (1/169).


صفحة 9


Na wanasema: katika Qur-an kuna sura inaitwa:


Suuratul-wilaaya ambayo inaanza hivi:


(Enyi mlio amini ziaminini nuru mbili…)


kwamba Othman bin Afani aliifuta sura hii kama


wanavyo dai.


Angalia kitabu:


(Faslul-khitwaab fiitahriif kitaab rabbul-arbaab).


cha An-nuur attwabrasy. ukurasa (18).


Na wanasema kwamba: kuna Msahafu unaitwa Mushaf


Faatwimah na kwamba Msahafu huyo ukubwa wake


ni mfano wa Qur-an yetu mara tatu.


Angalia kitabu: (Usuulul-kaafy). cha Alkulainy. (1/239).


Na wanasema: kauli ya Mwenyezi Mungu iliyopo katika


suratil-Maida aya ya (67) Isemayo:


(Ewe Mtume yafikishe yale yaliyo teremshwa kwako


kutoka kwa Mola wako na kama hukufanya hivyo basi


hujafikisha Ujumbe wake).


Mashia wanasema: aya hii ilikuwa hivi:


(Ewe Mtume yafikishe yale yaliyo teremshwa kwako -


Kuhusu Ally- na kama hukufanya hivyo basi hujafikisha


ujumbe wake) wakaongeza katika aya neno:


(kuhusu Ally). Yaani kwamba Mtume -rehma na amani


za Allah ziwe juu yake- Aliliacha huenda kwa


kuwaogopa Wanafiki kama walivyo eleza katika vitabu


vyao vingi tu.


Angalia kitabu:


(Faslul-khitwaab fiitahriif kitaab rabbul-arbaab).


cha An-Nuur attwabrasy. ukurasa (182).


صفحة 10


Na wanasema: Hawamkemei mwenye kusema kuwa


Qur-an imebadilishwa bali mtu kama huyo


wanamzingatia ni miongoni mwa Wanachuoni ambao ni


Mujtahid ama mwenye kukanusha (Wilaya -Utawala


baada ya mtume-) ya ally kwa mashia huyo anazingatiwa


ni Kafiri tena ukafiri usio na shaka ndani yake.


Tazama kitabu: (Al-iitiqaadaat).


cha Ibnu Baabawayhi Alqummy. ukurasa (103).


Na wanasema: kuwa wamewaamrisha wafuasi wao


kuisoma Qur-an hii tuliyo nayo katika Swala zao na


Sehemu nyingine pamoja na kuzifanyia kazi hukumu


zake mpaka atakapo kuja: (Maulaana Swahibuz-zamaan)


yaani Mahdi ndipo Qur-an hii itaondoshwa na


kunyanyuliwa Mbinguni na hapo itakuja Quran aliyo


itunga Amiril-muuminina iwe ndio yenye kusomwa na


kufuatwa hukumu zake.


Tazama kitabu: (Al-an war Annuumaaniyyah).


cha Niimatullahi Aljazaairy (2/363).


Na wanasema kuwa: Msiwafundishe wanawake Surati


Yusuf wala msiwasomeshe sura hiyo maana ndani yake


kuna Fitna lakini wafundisheni Suratin-nuur maana ndani


yake mna Mawaidha.


Rejea kitabu:


(Al-furuu minal kafy) cha Alkulayny (5/516).


AL-IMAAMAH (MRITHI) KWAO NI NGUZO NA ASIYE AMINI NGUZO HII NI KAFIRI


صفحة 11


Wanasema: Hakika asiye amini Al-imaamah basi Imani


yake haikamiliki ispokuwa kwa kuitakidi na kuamini


hivyo.


Angalia kitabu: (Aqaaidul-imaamiyyah).


cha Muhammad Ridhwaa midhfar. ukurasa (78).


Na wanasema: Hakika al-imaamah ni muendelezo wa


Utume na nidalili inayo wajibisha kutumwa Mitume na


kuwatuma Manabii jambo hili pia linawajibisha kuwepo


na Imamu baada ya Mtume.


Angalia kitabu: (Aqaaidul-imaamiyyah).


cha Muhammad Ridhwaa midhfar. ukurasa (88).


Na wanasema: Makusudio yao kuhusu swala la Alimaama


ni kuwa hiki ni cheo cha KiMungu Allah


anamchagua atakaye mpa cheo hiki miongoni mwa waja


wake kutokana na Elimu yake ya tangu kama vile anavyo


Mteua Mtume wake kuufahamisha umati wake juu ya


huyo Imamu na kuwaamuru wamfuate.


Angalia kitabu: (Aslush-shia wa Usuulihaa). cha


Muhammad Hussein kaashiful-ghitwaa. ukurasa (102).


Bali itikadi hii ni katika mambo ya msingi katika dini na


Haitimii Imani ya Mtu ispokuwa kwa itikadi hii. Na kwa


Ibara nyingine wanasema: Hakika Imama ni kuendelea


kwa Utume.


Na wanasema: Hakika Mwenye kupinga Uimamu wa Amiril-muuminina Ally bin Abi Twaalib Radhi za Allah ziwe juu yake na Maimamu wengine baada yake ni kama Mtu aliye pinga Unabii wa Manabii wa Allah na kwamba


صفحة 12


Mwenye kukiri Uimamu wa Ally lakini akampinga hata


Mmoja miongoni mwa Maimamu baada yake ni sawa na


Mtu aliye wakubali Mitume wote lakini akakanusha


Utume wa Muhammadi -rehma na amani za Allah ziwe


juu yake-.


pia wanasema: Mwenye kupinga Uimamu wa yeyote


miongoni mwa Maimamu kumi na mbili ni sawa na


Mwenye kuwapinga Mitume wote.


Angalia kitabu: (Minhaajun-najaat).


cha Alfaidhul-kaashy. ukurasa (48).


*Majina kumi na mbili ya maimamu wa kishia:


1/Ally bin Abi Twalib. (Al-mur-tadhwa)


2/Hassan bin Ally. (Azzakii – al-mujtabaa)


3/Hussein bin Ally. (Shahiid)


4/Ally bin Hussein. (Zainul-aabidiyna)


5/Muhammad bin Ally. (Al-baaqir)


6/Jaafar bin Muhammad. (Aswaadiq)


7/Mussa bin Jaafar.(Al-kaadhwim)


8/Ally bin Mussa. (Arridhwah)


9/Muhammad bin Ally. (Al-jawaadu)


10/Ally bin Muhammad. (Al-haady)


11/ Hassan bin Ally. (Al-askary)


12/Muhammad bin Hassan. (Al-mahdy)


Na wanasema: kwa Mujibu wa makubaliano ya Imaamiyyah wote ni kwamba yeyote Mwenye kupinga Uimamu wa yeyote miongoni mwa Maimamu wao na akakanusha kutekeleza Utiifu ambao Allah kawajibisha juu yao basi mtu huyo ni Kafiri na nimpotevu na


صفحة 13


anastahiki kudumu Motoni Milele.


Angalia kitabu: (Haqqul-yaqiin Fii Maarifat Usuulid diin)


cha Abdallah bishri (2/189).


Na wanasema: Hakika tamko la Shirki au Kufru kwa


kila asiye itakidi Uimamu wa Amiril-muuminina na


Maimamu wengine miongoni mwa watoto wake na


akawafadhilisha Wengine juu yao Matamko haya


yanamaanisha kuwa watu hao ni wenye Kudumu Motoni


milele.


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar).


cha Almajlisy. (23/390).


KUMKOSEA KWAO ADABU MTUME MUHAMMADI-REHMA NA AMANI ZA ALLAH ZIWE JUU YAKE- NA MABINTI ZAKE NA WATU WA NYUMBANI KWAKE.


Wanadai kuwa: Pindi Mtume -rehma na amani za Allah


ziwe juu yake- Alipo zaliwa alikaa Masiku kadhaa hana


Maziwa ya kunyonya basi Abuu Twaalib Akamuweka


katika Maziwa yake Allah akateremsha ndani yake


maziwa hivyo Akanyonya kwa siku kadhaa mpaka


Abuu Twalib Alipo mpata Halimatu Saadia na


kumkabidhi ili Amnyonyeshe.


Angalia kitabu: (Usuulul-kaafy).


cha Alkulayny. (1/448).


Na wanasema kwamba: Ally -radhi za Allah ziwe juu yake- Alikuwa ni Shujaa kuliko Mtume -rehma na amani za Allah ziwe juu yake- Bali Mtume hakupewa Ushujaa


صفحة 14


asilani.


Angalia kitabu: (Al-an war annuumaaniyyah).


cha Niimatullahi Aljazaairy. (1/17).


Na wanasema: Mtume -rehma na amani za Allah ziwe


juu yake- Alikuwa hawezi kulala Mpaka Abusu Paji la


Uso wa Faatwima (Binti yake) au kifua chake Kunyonya


Maziwa!!!.


Angalia kitabu: (Bihaarul-Anwaar).


cha Al-majlisy. (42/43).


Na wanasema: Mtume -rehma na amani za Allah ziwe


juu yake- Hakuwa na Mabinti ispokuwa Faatwima ama


Ruqayyah na Ummu kulthum na Zainabu hawa ni watoto


walio lelewa kwake tu.


Angalia:


(Daairatul-maariful-islaamiyyatu ash-shiiyyah) (1/27).


*Mtume wetu Muhammad-rehma na amani za Allah


ziwe juu yake- Alikuwa na watoto saba wakiume wa


tatu na wakike wa nne:


1/Qasim. 2/Abdullahi.


3/Ibrahim. 4/Zainabu.


5/Ruqayyah. 6/Ummu kulthum. 7/Faatwima.


Na wanasema kwamba: Hassan bin Ally-radhi za Allah


ziwe juu yao- yeye ndie Aliwadhalilisha Waumini kwa


sababu Alimbaayii (Alimpa kiapo cha utiifu)


Muawiya-radhi za Allah ziwaendee.


Angalia kitabu: (Rijaalul-kashy).


cha Alkashy. ukurasa (103).


صفحة 15


KUWAKUFURISHA KWAO MAMA WA WAUMINI: BI AISHA NA BI HAFSWA


Mashia wanasema: Hakika Mke wa Mtume anaweza


akawa ni Kafiri kama alivyokuwa Mke wa Nabii Nuhu


na Mke wa Nabii Lutwi. Wanamkusudia katika kusema


hivyo Mke wa Mtume-rehma na amani za Allah ziwe juu


yake- Bibi Aisha Allah amuwie radhi.


Angalia kitabu: (Hadiithul-ifki)


cha Jaafar Murtadhwa. Ukurasa (17).


Na wanasema kwamba: Bibi Aisha Allah amuwie radhi


Aliritadi Baada ya kufa Mtume-rehma na amani za Allah


ziwe juu yake- kama walivyo ritadi wengi miongoni


mwa Maswahaba.


Angalia kitabu:


(Ash-shihaabuthaaqib Fii bayaani maanan-naaswib).


cha Yusuf al-bahraany ukurasa (236).


Na wanasema kwamba: Bibi Aisha-radhi za Allah ziwe


juu yake- Alikusanya Dinari (40) kutokana na khiyana na


Akazigawa kwa watu wenye kumchukia Ally -radhi za


Allah ziwe juu yake-!.


Angalia kitabu: (Mashaariqu anwaaril-yaqiin).


cha Rajab Albisry. ukurasa (86).


Na wanasema kuwa: Bibi Aisha-radhi za Allah ziwe juu yake- Alifanya Faahisha (Zina) na kwamba kauli ya Allah katika suratin-nuur aya (26) Aliposema: {Hao ni wenye kutakaswa na hayo wayasemayo} wakasema: aya


صفحة 16


hii Imekuja kumtakasa Mtume-rehma na amani za Allah


ziwe juu yake- kutokana na Zina na sio Bibi Aisha.


Angalia kitabu: (Aswiraatul-mustaqiim).


cha Zainud-diin An-nabatwi Albayaadhwi. (3/165).


Na wanasema kwamba: Bibi Hafsa-radhi za Allah ziwe juu yake- Alikufuru kwa kauli yake alipo Muuliza Mtume: {Nani kakupa habarihizi}?. Kama ilivyo kuja katika suratu Tahrim aya (3). Na ndipo Allah Akateremsha kuhusu yeye pamoja na Bibi Aisha kauli yake: {Ikiwa Mtatubia kwa Allah bila shaka nyoyo zenu zimekwisha elekea huko}. suratu Tahrim aya (4).


Wanasema: Neno: (Zaaghat) lina maana ya Ukafiri. Na wanadai kuwa Bibi Aisha pamoja na Hafsa walikubaliana kumnywesha Sumu Mtume -rehma na amani za Allah ziwe juu yake- na pindi Allah alipo Mueleza Mtume wake njama zao akataka kuwauwa ndipo wakamuapia kuwa Hawakufanya hivyo na ndipo Allah akateremsha ayah ii: {Enyi mlio Kufuru Msitake Udhuru leo hii… } suratu Tahrim aya (7). Angalia kitabu: (Aswiraatul-mustaqiim). cha Zainud-diin An-nabatwi Albayaadhwi (3/168).


KUCHUPA KWAO MIPAKA KWA ALLY-RADHI ZA ALLAH ZIWE JUU YAKE.


Wanasema: Hakika Allah Alimsemesha Mtume wake -rehma na amani za Allah ziwe juu yake- Usiku wa Miiraji kwa Lugha ya Ally bin Abi Twalib.


صفحة 17


Angalia kitabu:


(kashful-yaqiin Fii Fadhwaaili Amiiril-muuminiin). cha


Hasan bin Yusuf bin Al-mut-har Alhuly. ukurasa (229).


Na wanasema kuwa: Allah Alimsemesha Ally bin abi


Twalib katika Mji wa Twaifu Akiwa pamoja na Jibril.


Angalia kitabu: (Baswaairud-darajaat).


cha Swaffaar. (8/230).


Na wanasema: Hakika Ally bin abi Twalib -radhi za


Allah ziwe juu yake- Ndiye Mwenye kugawa Pepo na


Moto!! Atawaingiza watu wa Peponi Peponi na watu wa


Motoni Motoni!!!.


Angalia kitabu: (Baswaairud-darajaat).


cha Swaffaar). (8/235).


Na wanasema: Hakika Allah Atamuingiza Peponi


Mwenye kumtii Ally hatakama atamuasi Allah! Na Allah


atamuingiza Motoni Mwenye kumuasi Ally hatakama


atamtii Allah!.


Angalia kitabu:


(Kashful-yaqiin Fii Fadhwaaili Amiiril-muuminina).


Cha Hasan bin Yusuf Al-mut-har al-huly. Ukurasa (8).


Na wanasema: Hakika Ally bin Abi Twalib -radhi za


Allah ziwe juu yake- Ndie siri ya Manabii na kwamba


Allah Alimwambia Mtume wake: {Ewe Muhammadi


hakika nilimtuma Ally pamoja na Mitume wengine kwa


siri na nimemtuma pamoja Nawe kwa Dhahiri".


Angalia kitabu: (Al-asraarul-alawiyya).


Cha Muhammad Al-mas-uudy. Ukurasa (181).


صفحة 18


Na wanasema kwamba: Ally -radhi za Allah ziwe juu


yake- ni Alama na Dalili ya Muhammadi na


Muhammadi-rehma na amini za Allah ziwe juu yake-


Alilingania juu ya Utawala wa Ally.


Angalia kitabu: (Baswaairud-darajaat).


cha Swaffaar. Ukurasa (91).


Na wanasema kwamba: Allah hakuwahi kumtuma


Mtume yeyote Ispokuwa Alimtaka kuutambua Utawala


wa Ally kwa kupenda au kwa kukarahishwa.


Angalia kitabu: (Al-asraarul-alawiyya).


Cha Muhammad Al-mas-uud. Ukurasa (190).


Na wanasema kuwa: Hakika Dini ya Mtu haikamiliki


ispokuwa kwa kuutambua Utawala wa Amirilmuuminina


Ally bin Abi Twalib.


Angalia kitabu: (Al-ihtijaaj). Cha Attwabrasy. (1/57).


Na wanasema: Hakika Mtume -rehma na amani za


Allah ziwe juu yake- Alisema: "Sikilizeni Jibril Alinijia


akanambia: {Ewe Muhammadi Mola wako anakuamrisha


Umpende Ally bin Abi Twalib na Anakuamrisha


Kuutambua Utawala wake}.


Angalia kitabu: (Baswaairud-darajaat).


cha Swaffaar. Ukurasa (92).


Na wanasema: Ally bin Abi Twalib Ataingia Peponi


kabla ya Muhammadi -rehma na amani za Allah ziwe juu


yake-Angalia kitabu: (Ilalush-sharaai).


Cha Ibnu Baabawayhi Alqummy. Ukurasa (205).


صفحة 19


Na wanasema kuwa: Radi ni katika Amri ya kipenzi


chenu alipo ulizwa Msemaji nani kipenzi chetu?


Akasema: Amiril muuminina Ally bin abi Twalib.


Angalia kitabu: (Al-ikhtiswaas).


Cha Almufiid. Ukurasa (327).


Wanasema kuwa: Ally bin abi Twalib -radhi za Allah


ziwe juu yake- Anauwezo wa Kufufua na Kuondoa


Matatizo kwa wenye Matatizo.


Angalia kitabu: (Uyuunul-muujizaati).


Cha Husein Abdul-wahaab. Ukurasa (150).


Na Risala (Halaalul-mashaakil).


Na wanasema: Hatoingia Peponi yeyote ispokuwa kwa


Idhni ya Ally bin abi Twalib.


Angalia kitabu: (Manaaqibu Amiril-muuminina).


Cha ally bin Maghaazily. Ukurasa (93).


Na wanasema kuwa: kila Mwenye kum-khaalifu Ally


basi huyo ni Kafiri na kila Mwenye kumfadhilisha


Yeyote juu yake basi huyo anakuwa Karitadi.


Angalia kitabu:


(Bishaaratul- mustwafaa lishiiatil- murtadhwaa). (2/79).


Na wanasema kuwa: Mwenyezi Mungu Alijifakharisha


Mbele ya Malaika wake kwa ajili ya Ally bin abi Twalib.


Angalia kitabu:


(Bishaaratul- mustwafaa lishiiatil- murtadhwaa). (1/66).


Wanasema: Manabii wote na Mitume walitumwa hali yakuwa wameamrishwa kukiri Utawala wa Ally bin abi Twalib.


صفحة 20


Angalia kitabu: (Al-maalimuz-zulfaa).


Cha Shekh wao Haashimul-bahraany. Ukurasa (303).


Na wanasema: Ally bin abi Twaalib -radhi za Allah


ziwe juu yake- Aliashiria kwa mkono wake Angani mara


likatanda Wingu na Mawingu yakapandana kisha


yakamtolea Salamu kisha Ally Akamwambia Ammar:


Panda Pamoja nami na Useme:


"Bismillahi Majreeha wamursaahaa".


Kama ilivyo kuja katika suurat Huud aya (41).


Ammar Akapanda kisha wakatoweka machoni kwetu.


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar). Cha Almajlisy.


Na wanasema kuwa: Mbwa Aliwang`ata Maswahaba


wawili kwa ajili ya kumlipizia kisasi Ally bin abi


Twaalib na kwamba Punda Alishuhudia kuwa Ally ni


Walii wa Allah na ndie aliepewa wasia wa utawala baada


ya Mtume - rehma na amani za Allah ziwe juu yake-.


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar).


Cha Almajlisy. (41/247). Na (17/306).


KUCHUPA KWAO MIPAKA KWA FAATWIMA RADHI ZA ALLAH ZIWE JUU YAKE


Wanasema kama: Fatwima na Hassan na Husein na wengine miongoni mwa kizazi cha Husein, ni maasuumin (Hawakosei).


صفحة 21


Angalia kitabu:


(Aqaaidul-imaamiyya).


Cha Muhammad ridhwaa. Ukurasa (89) na (98).


Na wanasema: Lau kama sio Ally basi Muhammadrehma


na amani za Allah ziwe juu yake- asingeumbwa,


na lau kama sio Fatwima basi nisingelikuumbeni.


Angalia kitabu:


(Al-asraarul-faatwimiyya).


Cha Muhammad almas-uudy. Ukurasa (98).


Na wanasema: Hakika Faatwima ni sehemu ya Uungu!


Utukufu wangu nimeudhihirisha katika umbile la


Mwanamke.


Angalia kitabu:


(Al-asraarul-faatwimiyya).


Cha Muhammad Almas-uudy. Ukurasa (355).


Na wanasema kuwa: Faatwima alikuwa akiongea na


Mama yake huku akiwa tumboni mwake.


Angalia kitabu:


(faatwimatu zahraa minal-mahdi ilal-lahdi).


Cha Muhammad alqaz-wiiny. Ukurasa (38).


KUWAFADHILISHA KWAO MAIMAMU WAO JUU YA MANABII PAMOJA NA KUCHUPA KWAO MIPAKA


Mashia wanasemakuwa: Hakika Maimamu wa Shia ithna asharia ni bora kuliko Manabii na Mitume -rehma


صفحة 22


na amani za Allah ziwe juu yao-.


Angalia kitabu: (Al-anwaarun-nuumaaniyya).


Cha Niimatullahi aljazaairy. (3/308).


Na wanasema: Hakika Maimamu wa Shia wana Elimu


ya yaliyo kuwepo na yatakayo kuwepo na kwamba


hakifichikani kwao kitu chochote (yaani wanajua ghaibu)


na kwamba wao hawafi ispokuwa kwa kutaka kwao.


Angalia kitabu: (Usuulul-kaafy).


Cha Alkulayny. (1/258-260).


Na wanasema: Hakika Imamu katika Maimamu wao


anayo Daraja yenye kusifiwa mbele ya Allah na anao


utawala ambao unanyenyekewa na kila kitu hapa


Ulimwenguni.


Angalia kitabu: (Tahrirul-wasiila).


Cha Al-khumainiy. Ukurasa (52).


Na wanasema: Hakika Maimamu wao Kumi na mbili


wanao Utawala usio kuwa kwa viumbe wote na kwamba


utawala huo ni sawa na utawala wa Allah kwa viumbe


wake.


Angalia kitabu: (Misbaahul-fuqaaha). -


Cha Abul-qaasim al-khuui. (5/33).


Na wanasema: Hakika sisi kwa Allah tunazo hali (yaani


Maimamu wao kumi na mbili) hali ambazo hazipati


yeyote si Malaika alie karibu wala Mtume alie tumwa.


Angalia kitabu: (Tahrirul-wasiila).


Cha Al-khumainiy. Ukurasa (94).


صفحة 23


Na wanasema: Hakika Maimamu kumi na mbili Hakuna


Pingamizi kabisa kuwa Mambo ya Ulimwengu yanaenda


kwa Idhini yao na kuwa wanaipitisha lailatul-qadri na


mengineyo na Hakuna Pingamizi kabisa kuwa jambo hili


limethibiti.


Angalia kitabu: (Al-burhaanul-qaatwii).


Ambacho ni mkusanyiko wa majibu na mambo ya


kiitikadi na sheria.


cha shekh wao: Muhammad taqiyyul-bahjat.


Ukurasa (41).


Na wanasema: Hakika mawaswii (Yaani Maimamu


kumi na mbili wa kishia) Wanabebwa tumboni na


wanatoka kwenye mapaja lakini hawaguswi na Uchafu


(wakati wa kuzaliwa).


Angalia kitabu: (Madiinatul-maajiz).


cha Haashimul-bahrany. (8/22).


Na wanasema: Hakika Allah na Malaika wake na


Mitume wake pamoja na Waumini huwa wana zuru


kaburi la Ally bin Abi Twalib.


Angalia kitabu: (Alfuruu minal-kaafy).


Cha Alkulayny. (4/580).


Na wanasema: Imamu ni kama Nabii ni lazima awe kaepushwa na mambo yote machafu ya dhahiri na ya siri tangu utotoni mwake mpaka kufa kwake ya kufanya kwa kukusudia au hata kwa kusahau kwa kuwa Maimamu ndio wenye kuihifadhi sheria na wenye kuisimamia halizao katika hili ni kama hali ya Mitume. Angalia kitabu:


صفحة 24


(Aqaaidul-imaamiyya).


Cha shekh wao: Ibrahim zanjaany. (3/179).


Na wanasema: Malaika wameumbwa ili kuwa


watumishi wa Ahlul-baiti.


Angalia kitabu:


(Bihaarul-anwaar).


Cha Almajlisy. (26/335).


KUWAKUFURISHA KWAO MASWAHABA WOTE ISPOKUWA WATATU TU MIONGONI MWAO


Mashia wanasema: Maswahaba wote watukufu


Wamekufuru na Kuritadi kiongozi wa kuritadi alikuwa ni


Abubakari na Omari na Othman na Khalid bin waliid na


Muawiya bin Abi Sufyaan na Mughiirat bin Shuubah -


radhi za Allah ziwe juu yao-


Ispokuwa watatu tu katika Maswahaba.


Angalia kitabu:


(Ar-raudhwatu minal-kaafy).


Cha Alkulayny. (8/245).


CHUKI ZAO JUU YA ABUBAKARI NA OMARI NA OTHMANI –RADHI ZA ALLAH ZIWE JUU YAO


Mashia wanasema: Na imani yetu katika kuwatenga nikwamba tunajitenga mbali na Masanamu wanne: Abubakri na Omari na Othmani na Muawiya pamoja na


صفحة 25


wanawake wanne: Aisha na Hafswa na Hindu na


Ummul-hakam (Dada yake na Muawiya) na tunajitenga


mbali kabisa na wafuasi wao wote na tunaitakidi kuwa


wao ni viumbe waovu kabisa miongoni mwa viumbe wa


Allah juu yamgongo wa Ardhi na tunaamini kwamba


haiwezi kutimia imani ya mtu kumuamini Allah na


Mtume wake na Maimamu ispokuwa kwa kujiweka


mbali kabisa na maadui zao.


Angalia kitabu:


(Haqqul-yaqiin).


Cha Almajlisy. Ukurasa (519).


Na wanasema: Hakika Abubakari na Omari ni Makafiri,


na kila Mwenye kuwapenda naye ni Kafiri.


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar).


Cha Almajlisy. (69/137-138).


Na wanasema: Abubakari na Omari wamelaaniwa na


wamekufa wakiwa ni makafiri, nani wenye


kumshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu.


Angalia kitabu: (Baswaairud-darajaat).


Cha As-swaffaar. (8/245).


Na wanasema: Sababu iliyompelekea Mtume -rehma na


amani za Allah ziwe juu yake- kwenda na Abubakari


Pangoni ilikuwa ni kuchelea asije kuwafahamisha


Makafiri wa Kikuraishi Mahala alipo.


Angalia kitabu: (Tafsiirul-burhaani).


Cha Haashimul-bahraany. (2/127).


صفحة 26


Na wanasema kwamba: Abubakari alikuwa akiswali


nyuma ya Mtume -rehma na amani za Allah ziwe juu


yake- hali yakuwa Kaning'iniza Sanamu Shingoni


mwake kisha analisujudia.


Angalia kitabu: (Al-anwaarun-nuumaaniyyah).


Cha Niimatullahil-jazaairy. (1/53).


Na wanasema: Omari alikuwa na Maradhi ambayo tiba


yake ni Maji ya Wanamume (Yaani Mpaka Aingiliwe


nyuma)! Na kwamba Bibi yake ni Motto wa zinaa.


Angalia kitabu: (Al-anwaarun-nuumaaniyyah).


Cha Niimatullahil-jazaairy). (1/63).


Na kitabu: (Aswiraatul-mustaqiim).


Cha Zainud-din annabatwy albayadhwy. (3/28).


Na wanasema: Tunaitukuza siku ya Tairuuz nisiku


ambayo Majusi huitukuza (Baniani) na kuisheherekea


siku aliyo uwawa Omari bin Khatwaab -radhi za Allah


ziwe juu yake- na wana Mwita alie Muuwa Omari kuwa


ni (Baba shujaa wa dini) na wanahimiza kulizuru kaburi


lake kutokana na kazi kubwa aliyo ifanya ya kumuuwa


Omari -radhi za Allah ziwe juu yake.


Angalia kitabu: (Aqdu durar Fii Baqri Batnu Omar).


Cha Yaasin As-swawaaf. Ukurasa (120).


Na wanasema: Kusoma dua ya kuwalaani Masanamu wawili wa Kiquraishi (Abubakari na Omari) ni katika Ibada tukufu za kujikurubisha nazo kwa Allah, na wamemwita abubakari na omari kuwa ni Aljibti na Twaaghuuti (Jibti ni Uchawi Twaaghuti ni Shetani).


صفحة 27


Angalia kitabu: (Ihqaaqul-haqq).


Cha Al-mar-ashy. (1/337).


Na wanasema kwamba: Mahdi wao wauongo


atamfufua Abubakari na Omari, Awasulubu na kisha


kuwachoma Moto kisha Amfufue Bibi Aisha -radhi za


Allah ziwe juu yake- na Amsimamishie Hadd.


(Adhabu kwa Sababu ya zinaa).


Angalia kitabu: (Ar-raj-a).


cha Ahmad al-ahsaani. Ukurasa (1116) na (161).


Na wanasema: Hakika Othmani -radhi za Allah ziwe juu


yake- Alikuwa ni Mzinifu na Khanithi na alikuwa ni


Mpiga Dufu.


Angalia kitabu: (As-siraatul-mustaqiim).


Cha Zainud-diin annabtwy albyaadhwy. (3/30).


KUHUSU MAHDI WAO WA KUZUA NA KAULI ZAO JUU YA KUREJEA KWAKE


Na Wanasema kuwa: Jibril na Miikaail na Kursy na


Lauhil-mahfuudh na Kalamu vyote hivi ni vyenye


kudhalilika na kumnyenyekea Mahdi wa kishia, sababu


sifayake ni Saffah (M-mwagaji damu).


Angalia kitabu: (Aqaaidul-imaamiyya).


Cha Muhammad ridhwaa midhfar. Ukurasa (102).


Na wanasema Kuwa: kiwiliwili cha Mahdi wa kishia ni kiwiliwili cha Israaili. (Chaguo la Mungu). Angalia kitabu:


صفحة 28


(Al-imaamul-mahdy minal wilaadati iladh-dhuhuur).


Cha Muhammad qazwiiny. Ukurasa (53).


Na wanasema kuwa: Mahdi wa Mashia atakuja na Amri


Mpya na Kitabu Kipya na Hukumu Mpya na Atakuwa ni


Mkali sana kwa Waarabu hatokuwa na uamuzi juu yao


zaidi ya Upanga tu Hatampa Nafasi yeyote ya kutubia


wala hato'ogopa lawama ya mwenye kulaumu kwaajili ya


Allah.


Angalia kitabu:


(Al-ghaibah).


Cha Muhammad an-nuuman. Ukurasa (154).


Na wanasema: Pindi atakapo kuja Mahdi hakutakuwa


kitu kati yake na Waarabu na Maquraishi, ispokuwa


Upanga tu.


Angalia kitabu:


(Al-ghaibah).


Cha Muhammad an-nuuman. Ukurasa (154).


Na wanasema: Haikubakia baina yetu na Waarabu


ispokuwa Kuchinjana kisha msemaji akaashiria Shingoni


mwake.


Angalia kitabu: (Al-ghaibah).


Cha Muhammad an-nuuman. Ukurasa (155).


Na wanasema kwamba: Mahdi wao atakapo kuja Atauvunja Muskiti wa Makkah na Muskiti wa Madina na Atahukumu kwa Sheria ya watu wa Daawud na Atamsemesha Allah kwa jina lake la Kiebrania sihivyo tu bali Atauwa Theluthi mbili ya watu wa Ardhini.


صفحة 29


Angalia kitabu:


(Biharul-anwaar). Cha Al-majlisy.(52/338).


Na kitabu: (Uswuulul-kaafy). Cha Al-kulainy. (1/397).


Na kitabu: (Alghaibah).


Cha Annuumaany. Ukurasa (326).


Na kitabu: (Arraj'a).


cha Ahmad al-ahsaai. Ukurasa (51).


Na wanasema: Jihadi haifai wala hairuhusiwi mpaka atakapo kuja Mahdi wao wakudai kutoka katika Pango lake. Angalia kitabu: (Wasaailush-shia). Cha Al-hurr al-aamily. (11/37).


KUCHUPA KWAO MIPAKA KULIKO KUBAYA KATIKA IBADA ZA MAKABURI


Mashia wanasema kuwa: Kulizuru kaburi la husein bin


Ally ni bora kuliko kwenda Kuhiji Makkah si hivyo tu


bali wanasema kuwa wanao kwenda kumzuru Husein ni


watakasifu ama wanao kuwa katika Mauqifu (Arafa)


katika Hijja ni Watoto wa Zinaa.


Angalia kitabu:


(Biharul-anwaar). Cha Al-majlisy. (98/85).


Na wanasema: Hakika kulizuru kaburi la Husein bin Ally-radhi za Allah ziwe juu yake- Nisawa na kufanya Hijja Milioni mbili (2,000,000) na Umra Milioni mbili (2,000,000) na kupigana Jihadi Milioni mbili (2,000,000) na Thawabu za kila Hijja na Umra na Jihadi ni sawa na Thawabu za Aliye Hijji na akafanya Umra na akapigana


صفحة 30


Jihadi Pamoja na Mtume -rehma na amani za Allah ziwe


juu yake- Pamoja na Maimamu waongofu.


Angalia kitabu:


(Nuurul-ayni fil-mashyi ilaa ziyaarati qabril-husaini).


Cha Muhammad al-istwihbaanaaty.


Ukurasa (265).


Na wanasema kwamba: Karbalaa (Alipo zikwa


Husaini) ni Ardhi takatifu katika Uislamu na ina Utukufu


kushinda Makkah na Madina na kuliko hata Baitulmaqdis.


(Muskiti wa palestina).


Angalia kitabu:


(Misbaahul-jinaani).


Cha shekh wao Abbaas al-kaashaany.


Ukurasa (360).


Na wanasema kuwa: Kula Udongo ulipo katika Kaburi


la Husein -radhi za Allah ziwe juu yake- ni Shifaa


(Dawa) ya kila Ugonjwa.


Angalia kitabu:


(Almizaar)


cha Shekh wao Almufiid.


Ukurasa (125).


Pia wanasema kwa uongo na uzushi kuwa: Abu abdillahi (Jaafar As-swaadiq) -rehma na amani za Allah ziwe juu yake- Amesema: Wallahi laiti kama ninge kusimulieni juu ya Fadhila za kulizuru kaburi la Husein na juu ya ubora wa kaburi lake basi mgeliacha kufanya Hijja moja kwa moja na hakuna yeyote miongoni Mwenu ambaye ange fanya Hijja, olewako! Hivi hujuwi kama


صفحة 31


Allah kaifanya Ardhi ya Karbalaa (Aliko zikwa Husein)


kuwa ni Haram (Sehemu takatifu) yenye amani na yenye


kubarikiwa kabla ya kuifanya Makkah kuwa ni


Haramu?!.


Angalia kitabu: (Kaamiluz-ziyaaraat).


Cha shekh wao Ibnu quuluwayhil-qummy.


Ukurasa (449).


Na wanasema: Hakika kuswali katika Mashaahid zao


(Makaburi) ni bora kuliko kuswali Miskitini bali


wanasema: swala katika Msikiti wa Ally bin Abi Twalib


malipo yake ni makubwa kuliko kuswali katika Msikiti


Mtakatifu wa Makkah.!!


Angalia kitabu: (Manhajus-swaalihiina).


Cha Shekh wao Ally as-sistaany. (1/187).


Na wanasema kuwa: Hakika Sikukuu kubwa katika Uislamu sio Eidul-fitri wala Eidul-adhwhaa bali ni Eidi ya (Ghadiir) Eidi ya kizushi wala haina asili katika Uislamu. Angalia kitabu: (Eidul-ghadiir). Cha Shekh wao Muhammad ash-shiiraazy. Ukurasa (11). *Ghadiir: Ni sehemu Baina ya Makkah na Madina sehemu ambayo Mtume alimsifu Ally…


KUWAPENDA KWAO MAKAFIRI NA KHIYANA ZAO NA UDANGANYIFU WAO


Mashia wanasema: Na miongoli mwa makosa waliyo yafanya watu wa Kuufa, nikwamba wao walimchoma choma Visu Hassan bin Ally na wakamuuwa Husein -


صفحة 32


radhi za Allah ziwe juu yao- Baada ya kuwa walimwita.


Angalia kitabu: (Taariikhul-kuufa). Ukurasa (113).


Na wanasema: Hakika Husein Alisema: Ewe Mwenyezi


Mungu nakuomba Uhukumu Baina yetu na baina ya


watu walio Tuita ili watunusuru waka Tuuwa.


Angalia kitabu: (Muntahal-aamaal). (1/535).


Na wanasema: Husein alisema: Hakika watu hawa


wamenihofisha (Yaani mashia wa kuufa -iraqi) Nahizi


hapa Barua za watu wa kuufa nao ni wenye Kuniuwa.


Angalia kitabu: (Maqtalul-husaini).


Cha Abdurrazzaaq almuqrim. Ukurasa (175).


Na wanasema kwamba: Ally bin Husein -rehma na


amani za Allah ziwe juu yake- Aliwaona watu wa Kuufa


Wakiomboleza na Kulia, Akawaambia: Mnaomboleza na


Kulia kwa Ajili Yetu! Ni nani Aliye Tuuwa??(Bila kua


nyinyi).Angalia kitabu: (Nafsul-mahmuum).


Cha Abasi al-qummy. Ukurasa (357).


Na wanasema: kisha wakampa Husein Baia (Utawala)


katika watu wa Iraq, watu elfu ishirini (20,000) kisha


wakamtelekeza na wakamtokea pamoja na viapo vyao,


vya utiifu wakamuuwa. Angalia kitabu:


(Aa'yanush-shia). Cha Muhsinul-amiin. (1/32).


Na wanasema: Niwaajibu kuwanusuru Maaduwi wanao Shambulia Dola (Nchi) ya Kiislamu nakuto waziwiya Makafiri wanao Washambulia Waislamu. Angalia: Fat'wa Aliyoitowa kiongozi wao Mkubwa: As-sistaany.


صفحة 33


Tarehe: (4/3/2003). Baada ya Marekani kuishambulia


Iraq. Na kutilia Mkazo jambo hilo Anasema shekh wao


Swaadiq Ash-shiirazy, Anaye ishi Irani:


Nilazima kusaidiana Na Marekani katika kuangusha


Utawala wa Iraq.


Angalia: (Jariidatul-watwaniyya al-kuwaitiyya-al jumua)


(27/9/2002).


Na wanasema: Hakika Muislamu yeyote Mwenye


kupigana Jihadi dhidi ya Makafiri basi Anahesabiwa ni


Muuwaji Hapa Duniani na Akhera.


Hakuna anaekufa Shahidi Ispokuwa Shia Imaamiyya,


Hata akifia kitandani kwake.


Angalia kitabu: (Tahdhiibul-ahkaam).


Cha Atwuusy. (6/98).


KUICHUKIA KWAO MAKKAH NA MADINA


Mashia wanasema: Hakika watu wa Makkah wanamkufuru Mwenyezi Mungu wazi wazi, na watu wa Madina niwaovu kuliko watu wa Makkah, niwaovu zaidi yao mara sabini (70). Angalia kitabu: (Usuulul-kaafy). Cha Alkulainy. (2/410).


CHUKI ZAO KWA MISRI NA SHAM


Wanasema kuwa: Watu wa Misri wamelaaniwa kwa Ulimi wa Daaud, na miongoni mwao wamegeuzwa kuwa


صفحة 34


Manyani na Nguruwe.


Na wanasema kuwa: Allah hakupata kuwakasirikia


wana wa Izraail ispokuwa aliwaingiza (Misri) na pindi


alipokuwa Radhi nao basi aliwatoa humo.


Na wanasema kwamba: Abu Jaafar Imamu wao


ambaye wanasema ni Maasuumu (Hafanyi dhambi)


Alisema: Hakika Mimi nachukia kula kitu chochote


kilicho pikwa katika vyungu vya Misri, wala sipendi


kuosha kichwa changu kutokana na Udongo wake, usije


kuniambukiza Udhalili na kuniondolea Ghera (wivu)


wangu, Jitengeni na Misri wala msitamani kuishi humo.


Pia nadhani alisema: kuishi katika nchi hiyo


kunamrithisha mtu tabia ya Udayuthi (kuridhia maasi).


Angalia kitabu: (Tafsiirul-qummy). Cha Alqummy.


(2/241). Na kitabu: (Tafsiirul-bur-haan).


Cha Hashimul-bahraany. (1/456).


Na kitabu: (Furuu minal-kaafy). Cha Alkulainy. (6/501)


Na kitabu: (Bihaarul-anwaar). Cha Almajlisy. (60/211).


Na wanasema: Bora ya Ardhi ni ardhi ya Sham, na watu wa baya ni watu wa Sham. na watu wa Roma walikufuru lakini hawakutufanyia Uaduwi, lakini watu wa Sham walikufuru na wakatufanyia Uaduwi, na wala msiseme: sisi niwatu wa Sham lakini semeni sisi niwatu wa sehemu mbaya. Angalia kitabu: (Tafsiirul-bur-haan). Cha Hashimul-bahraany. (1/456). Na kitabu: (Usuulul-kaafy). Cha Alkulainy. (2/410). Na kitabu: (Tafsiirul-qummy). Cha Alqummy. (2/241).


صفحة 35


ULAJI WAO WA KHUMUS (MOJA YA TANO) KWA VIGOGO WAO WAVAAJI WA VIREMBA VIKUBWA


Mashia wanasema kuwa: Mali ya Khumus,


(mali ikigawiwa mafungo matano fungo moja ndio


linaitwa khumus) Ambayo ni maalumu kwa watu wa


Mtume -rehma na amani za Allah ziwe juu yaowanapaswa


kuichukuwa watu wa Viremba (vigogo wao)


kwa hoja kwamba wao wanasimamia nafasi ya Imamu


wao aliye jificha kwenye Pango.


Angalia kitabu: (Wasaailush-shia).


Cha Alhurrul-aamily. (6/383).


WANADAI KUJIPIGA MAKOFI NA KUJICHOMA VISU NI MIONGONI MWA MAMBO YA KUJIKURUBISHA


Mashia wanadai kuwa: Kujipiga piga Makofi na Kujichoma visu na kuvaa mavazi Meusi siku ya Ashura na kuomboleza ni miongoni mwa mambo Makubwa ya kujikurubisha kwa ajili ya Husain -radhi za Allah ziwe juu yake- na kwamba matendo hayo ni katika matendo mazuri. Angalia fataawa za Muhammad kaashif Alghitwaa, na Ar-rauhany, na At-tabrizy. na rejea nyingi miongoni mwa rejea za al-imaamiyyah.


KUHIMIZA KWAO MUT'A NA KUSTAREHE NA WANAWAKE MAKAHABA


صفحة 36


Mashia wanasema: Mtu anaweza kuowa (kwa ndoa ya


Mut'a) mpaka mara Elfu moja, (1000) kwa sababu


Mwanamke wa Mut'a hapewi Talaka wala hana Mirathi,


bali anahesabiwa ni Mwenye kukodiwa tu.


Angalia kitabu: (Al-istibswaar).


Cha Abii Jaafari atwuusy. (3/155).


Na wanasema: Hakika Mtoto aliye zaliwa katika Mut'a


ni bora kuliko aliye zaliwa katika Ndoa ya kudumu.


Angalia kitabu: (Manhajus-swaadiqiin).


Cha Almulla fat-hullah al-kaashaany. Ukurasa (356).


Na wanasema kuwa: Inajuzu kufanya Mut'a na


Wanawake wazinifu na ambao ni maarufu kwa


(Uchangudoa-Ukahaba) bali wanadai kuwa


kumepokelewa Mahimizo juu ya jambo hilo.!


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar).


Cha Almajlisy. (100/319-320).


Na wanasema kwamba: Mwanamke wa kufanya nae


Mut'a Haesabiwi katika Ile idadi ya Wanawake Wanne,


kwa sababu yeye Haachwi kwa kupewa Talaka wala


hana haki ya Mirathi, bali yeye ni Mwenye kukodiwa tu.


Angalia kitabu: (Alfuruu minal-kaafy).


Cha Alkulainy. (5/415).


Na wanasema: Inajuzu kufanya Mut'a na Wanawake Warembo hata kama watakuwa Wameolewa, au hatakama ni Wazinifu. Angalia kitabu:


صفحة 37


(Alfuruu minal-kaafy).


Cha Alkulainy. (5/462).


Na wanasema kuwa: Uchache wa muda wa Mut'a ni


kustarehe na Mwanamke mara moja tu.


Angalia kitabu: (Alfuruu minal-kaafy).


Cha Alkulainy. (5/460).


Na wanasema kwamba: Inajuzu kufanya Mut'a na


Mwanamke Mzinifu hata kwa Kumlazimisha hasa akiwa


ni miongoni mwa Wanawake Maarufu kwa Ukahaba.


Angalia kitabu: (Tahriirul-wasiilah).


Cha Khumainy. (2/256).


TAQIYYA NA KUSEMA UONGO NI KATIKA ASILI YA MADHEHEBU YAO


Mashia wanasema: Inajuzu kutumia Taqiyya na maana


yake ni: (Mtu kudhihirisha mambo ambayo ni kinyume


na vile anavyo itakidi moyoni) au kama alivyo eleza


mmoja wa wanachuoni wao kwamba taqiyya nikusema


au kufanya kinyume na unavyo itakidi kwa lengo la


kujiondolea madhara au kulinda heshima yako.


Angalia kitabu: (Ash-shiatu fil-miizaan).


Cha Muhammad Jawaadu Maghniyah. Ukurasa (48).


Na wanasemakuwa: Sehemu kubwa ya Dini ni Taqiyya,


wala hana Dini asie kuwa na Taqiyya.


Angalia kitabu:


(Uswuulul-kaafy).


Cha Alkulainy. (2/217).


صفحة 38


Na wanasema: Hakika Nyinyi mko katika Dini ambayo


Mwenye kuificha basi atampa utukufu na Mwenye


kuiweka wazi basi Mwenyezi Mungu Atamdhalilisha.


Angalia kitabu:


(Uswuulul-kaafy).


Cha Alkulainy. (2/222).


Na wanasema: Hakika Husein Alikuwa akinyonya kidole cha Mtume -rehma na amani za Allah ziwe juu yake- kiasi cha kumtosha siku mbili mpaka tatu. Angalia kitabu: (Uswuulul-kaafy). Cha Alkulainy. (1/465).


KUWAKUFURISHA KWAO WAISLAMU PAMOJA NA CHUKI ZAO KUBWA JUU YA WAISLAMU


Mashia wanasema kuwa: Hakuna yeyote aliyopo katika


Mila ya Kiislamu zaidi yetu (Yaani Maimamu wa Ithna


Ashariyya Pamoja na Wafuasi wao miongoni mwa Shia


Imaamiyya).


Angalia kitabu: (Uswuulul-kaafy).


Cha Alkulainy. (1/223-224).


Na wanasema kwamba: Mahdi wao Atarejea ili aje


kuwalipizia kisasi Mashia kutoka kwa Maaduwi zao


ambao ni Waislamu, ama Mayahudi na Wakristo wao


Atafanya nao Suluhu na kuwasalimisha.


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar).


Cha Almajlisy. (52/376).


صفحة 39


Na wanasema kuwa: Mwenye kuturudi Sisi ni sawa na


Mwenye kumrudi Allah, na anakuwa ni sawa na aliye


mshirikisha Allah.


Angalia kitabu: (Uswuulul-kaafy).


Cha Alkulainy. (1/67).


Na wanasema kuwa: Watu wote ni Watoto wa Zinaa


Ispokuwa Mashia tu.


Angalia kitabu: (Arraudhwatu minal-kaafy).


Cha Alkulainy. (8/285).


Na wanasema: Hakika Mtoto yeyote anapo zaliwa Ibilisi


miongoni mwa Maibilisi huwa anahudhuria kuzaliwa


kwake, Pindi anapojuwa kuwa Mwenye kuzaliwa ni


Miongoni Mwetu, Basi huwa anamkinga kutokana na


Shetani, na kama atakuwa mwenye kuzaliwa sio katika


sisi basi Shetani humuingiza kidole Matakoni mwake


akiwa ni kijana. na kwa ajili hiyo anakuwa ni Mwenye


kuziniwa!!!, Na akiwa ni wakike basi hutia kidole chake


katika Utupu wake (Sehemu ya siri ya mbele)!!! Na kwa


ajili hiyo anakuwa ni Muovu.


Angalia kitabu: (Tafsiirul-ayaashy).


Cha Muhammad al-ayaashy. (2/218).


Na wanasema kwamba: Hakika yeyote ambaye sio


katika Shia ithna asharia, au asiye muamini hata mmoja


miongoni mwa Maimamu kumi na mbili, au


akamkanusha hata mmoja wao, basi huyo ni Kafiri, na


Akhera mafikio yake ni Motoni.


Angalia kitabu: (Jaamiu ahaadiithi shia).


Cha Alburuujirdy. (1/429).


صفحة 40


Na wanasema: Hakika habari zinafidisha juu ya hukumu ya Ukafiri na Ushirikina huko Akhera kwa kila ambaye sio katika Shia ithna asharia. Angalia kitabu: (Tanqiihul-maqaal). Cha Abdallah Almaamaqany. (1/208).


CHUKI ZAO KWA AHLUS-SUNNA ZIMEPITA KIWANGO


Mashia wanasema: Hakika Naaswib (yaani Muislamu)


damu yake ni halali, lakini mimi nakuepushia shari,


ikiwa utaweza kumuangushia Ukuta, au Kumzamisha


kwenye Maji, ili asije kukutolea ushahidi basi fanya


hivyo, akauliza muulizaji: na vipi Mali yake? Akasema:


Ichukuwe, ikiwa kama kuna uwezekano.!


Angalia kitabu: (Wasaailu sh-shia).


Cha Alhurrul-Aamaly. (18/463).


Na wanasema: Hakika Diya ya Sunni (yaani pindi


Akiuliwa) ni sawa na Diya ya Beberu, na Beberu nibora


kuliko Yeye. na Diya yao hailingani na Diya ya ndugu


yao Mdogo ambaye ni Mbwa wa kuwinda, wala


hailingani na ya ndugu yao Mkubwa ambaye ni


Myahudi.


Angalia kitabu: (Al-anwaarun-nuumaaniyyah).


Cha Niimatullahi Aljazaairy. (3/308).


Na wanasema: Chukuwa mali ya Naaswib (Muislamu) Popote utakapo ipata na utupatie sisi Khumusi tu. (Moja ya tano).


صفحة 41


Angalia kitabu: (Wasaailu sh-shia).


Cha Alhurrul-Aamaly. (6/340).


Na wanasema: Hakika siku ya Qiyama, mema waliyo


yafanya Ahlus-sunnah watapewa Shia, na makosa waliyo


yafanya Shia watapewa Ahlus-sunnah, kisha watupwe


Motoni.


Angalia kitabu: (Bihaarul-anwaar).


Cha Almajlisy. (5/247-248).


Na wanasema: Ahlus-sunnah ni najsi (Wachafu) na


Damu zao ni halali na Mali zao piya, na kwamba wao ni


watu wa Motoni, na wala hawatatoka ndani ya Moto.


Angalia kitabu: (Al-anwaarun-nuumaaniyyah).


Cha Niimatullahi aljazaairy. (2/306).


Na kitabu: (Haqqul-yaqiin Fii Maarifati Uswuulud-diin).


Cha Abdallah Bishri. (2/188).


Na wanasema: Shia akimwita Mshia mwenzake (Ewe


sunni) basi ana adhibiwa, na imethibiti juu yake kisheria


kupewa adhabu itakayo mpa fundisho.


Angalia kitabu:


(hayaatul-muhaqiq alkarkry wa aatharuhu). (6/237).


UZUSHI WA MASHIA


Mashia wanadai kuwa: Eti kundi miongoni mwa Malaika walizozana kuhusu jambo Fulani, kisha wakamtaka mwanaadamu awe muamuzi baina yao, Allah akawateremshia wahyi, kuwa chaguweni kati ya


صفحة 42


Wanaadamu, wakamchaguwa Ally bin Abiitwalib.


Angalia kitabu: (Musnad faatwima).


Cha Husein Attuwaisir kaany. Ukurasa (296).


Na wanasema kwamba: Punda aitwae (Ghufair)


alimsemesha Mtume -rehma na amani za Allah ziwe zuu


yake- Akamwambia: Namtowa Fidia Baba yangu na


Mama yangu, hakika Baba yangu Alinisimulia kutoka


kwa Baba yake, kutoka kwa Babu yake, kutoka kwa


Baba wa Babu yake, kwamba: Alikuwa na Nabii Nuhu


katika Safina (Jahazi) Nabii Nuhu akasimama kisha


Akampakusa katika Matako yake, kisha Akasema:


Atatoka katika Mgongo wa Punda huyu, Punda ambaye


atapandwa na Bwana wa Mitume wote na wa Mwisho


wao, hivyo namshukuru Allah aliye nijaalia kuwa Mimi


ndiye Yule Punda.!!!


Angalia kitabu: (Uswuulul-kaafy)


Cha Alkulainy. (2/237).


Na wanasema kuwa: Imamu wao Albaaqir


Alitengeneza Tembo wa Udongo kisha Akampanda Yule


Tembo, akaruka naye mpaka Makkah.!!! Angalia kitabu:


(Madiinatul-maajiz). Cha Haashimul-bahraany. (5/10).


Na wanasema: Mikojo na Mavi ya Maimamu wao hamna Uchafu wowote wala Harufu mbaya, bali ni kama Miski (Mafuta uzuri namba moja) na Mwenye Kunywa Mikojo ya Maimamu wao na Mavi yao na Damu zao Allah Atamziwiya kuingia Motoni, na ata Muingiza Peponi. Angalia kitabu: (Anwaarul-wilaaya).


صفحة 43


Cha A'ayatullah Al-aakhundi Mulaa zainul-Aabidiina


alkalbaaikaany. Ukurasa (440).


Na wanasema: Hakika Ushuzi na Mavi ya Maimamu


zao vina harufu kama ya Miski.!!!


Angalia kitabu: (Uswuulul-kaafy).


Cha Alkulainy. (1/319).


Na wanasema: Kuvaa Viatu vyeusi kunasababisha


mambo matatu, Nikasema: Nimambo gani hayo?


Akasema: kunasababisha: Kudhoofika kwa nuru ya


Macho, na kurefusha dhakari (Sehemu ya siri inakuwa


ndefu) na kunamjengea Mtu kuwa na Huzuni.


Angalia kitabu: (Uswuulul-kaafy).


Cha Alkulainy. (6/465).


Na wanasema: Kuvaa Viatu vya njano kunasababisha


mambo matatu: kunaleta nuru ya Macho, na kuikomaza


Dhakari, na kuondowa Huzuni.


Angalia kitabu:


(Alfuruu minal-kaafy).


Cha Alkulainy. (6/465).


Na wanasema: Kula Karoti kunachemsha Bandama, na


kusimamisha Dhakari (sehemu ya siri) na kunaongeza


Nguvu za tendo la ndoa.


Angalia kitabu: (Alfuruu minal-kaafy).


Cha Alkulainy. (6/372).


Na wanasema: Hakika Sheitwani huwa anakuja na kumkalia Mwanamke kama vile Mwanamume anavyo mkalia, na yanatokea kama yale yanayo tokea kwa



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI