Nakala




Lengo la kuumbwa Mwanadamu


Sheikh: Binadamu ameumbwa kwa malengo gani?.


JAWABU: Kwajina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma Mwenye


kurehemu, Namshukuru Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu mzima, na


Rehma na Amani zimshukie Nabii Muhammad (s.a.w), pamoja na Familia yake


na Maswahaba zake, Baada ya hayo.


Kwa hakika kabla ya kujibu swali hilo napenda kutoa zinduo kuhusu kanuni


muhimu sana katika mambo anayo yaumba Mwenyezi Mungu Mtukufu na yale


aliyo yapanga.


Na kanuni hiyo imechukuliwa kutoka katika kauli yake Mwenyezi Mungu


Mtukufu: (Na Yeye ni Mwenye kujua, Mwenye hikima). Tahrim (2).


Na kauli yake: (Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima).


Ahzab (1).


Na aya nyingi tofauti na hizo zinazo onyesha na kuthibitisha hikma ya uumbaji


wa Mwenyezi Mungu na yale aliyo yapanga.


Maana yake: katika mambo ya kidunia na yakisheria, kwa sababu hakuna jambo


lolote analo liumba Mwenyezi Mungu Mtukufu isipokuwa ndani yake kuna


hikma, sawa sawa katika kuwepo jambo hilo au katika kuliondoa, na hakuna


jambo analo lipanga Mwenyezi Mungu Mtukufu isipokuwa kwa hikma vile vile,


sawa sawa iwe katika ulazima au katika kuharamisha au kuhalalisha.


Lakini hikma zinazo fungamana na mambo ya kidunia au ya kisheria,


yawezekana tukayajuwa na yawezekana tusiyajuwi, na yawezekana baadhi ya


watu wakayajua na wengine wasiyajue, hii nikutokana na elimu na ufahamu


anao wapa Allah waja wake.


Ikiwa ndivyo hivyo tunasema ya kwamba: Hakika Mwenyezi Mungu


Mtukufu kaumba Majini na Binadamu kutokana na hikma kubwa na malengo


mazuri nayo ni kumuabudu Mwenyezi Mungu Mtukufu.


Lengo la kuumbwa Mwanadamu


2


Kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu:(Nami sikuwaumba majini na


watu ila waniabudu Mimi). Adhariyati: (56).


Na kauli yake: ( Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba


nyinyi kwetu hamtarudishwa). Al-Muminun: (115). Na akasema: (Ati anadhani


binaadamu kuwa ataachwa bure). Al-Qiyama: (36).


Na aya nyingine tofauti na hizo zinazo julisha ya kwamba Mwenyezi Mungu


anayo malengo maalum katika kuumba binadamu na majini, nako ni kufanya


ibada.


Na ibada ni kudhalilika kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kupenda na


kutukuza kwa kufanya amri zake na kujiepusha na makatazo yake katika njia


iliyo elekezwa na sheria zake, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Nao


hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini,


wawe waongofu). Al-Bayyina: (5).


Hii ndio hikma ya kuumbwa majini na binadamu.


Kwa maana hiyo yeyote atakae fanya jeuri na kiburi kwa Mwenyezi Mungu kwa


kuacha kufanya ibada, kwa hakika atakuwa ni mwenye kupuuza hikma ambayo


viumbe wameumbwa kwa sababu hiyo.


Na kitendo chake hicho kinaonyesha ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu


kaumba viumbe kwa mchezona bila ya majukumu yoyote, na yeye japo


hajatamka lakini vitendo vyake vina ashiria hivyo kutokana na jeuri yake na


kupinga kwake ibada ya Mola wake.





Nini maana ya Ibada? Je, ina maana ya ujumla na maana maalumu?.


JAWABU: Ibaada ina maana mbili:


A.Maana ya ujumla.


B.Maana maalumu.


Maana yake kwa ujumla nikama tulivyo eleza katika swali la kwanza ya


kwamba: ni kudhalilika kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kupenda


na kutukuza kwa kufanya amri zake na kujiepusha na makatazo yake katika njia


iliyo elekezwa na sheria zake.


Hii ndio maana yake kwa ujumla.


Maana yake maalum - nakusudia kwa urefu- Amesema Sheikhul-Islam Ibnu


Taimiyya (r.h): Ni jina lililo kusanya kila anacho kipenda Mwenyezi Mungu na


kukiridhia kutokana na maneno na vitendo vya siri na dhahiri,


Mfano: Khofu, Unyenyekevu, Kutegemea, Swala, Zaka, Funga, na ibada


nyinginezo tofauti na hizo zilizopo katika sheria ya Uislamu.


Na ukiwa unakusudia maana ya ibada kwa ujumla au kwa maana maalum kama


walivyo taja badhi ya wanachuoni ya kwamba Ibada yawezekana ikawa ya


kidunia au ya kisheria.


Kwa maana ya kwamba yawezekana binadamu akadhalilika kwa ajili ya


Mwenyezi Mungu Mtukufu lakini ikawa kwa sababu ya dunia, na yawezekana


ikawa kudhalilika kwa sababu ya kisheria.


Ibada za kidunia ni kwawote, Muislamu, Kafiri, Mwema, Muovu. Kwa kauli


yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hapana yeyote aliomo


mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni


mtumwa wake). (Maryam: 93).


Maana ya Ibada


2


Vyote vilivyopo mbinguni na duniani ni vyenye kunyenyekea kwa ajili ya


Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa yale aliyo ya panga, haiwezekana kiumbe


akaenda kinyume na matakwa ya Allah katika mambo aliyo ya kadiria.


Lakini Ibada maalum nazo ni ibada za kisheria ni kudhalilika kwa ajili ya


Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kisheria, ibada hizi ni maalumu kwa waumini


wenye kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu, wenye kusimama katika amri


zake.


Kisha miongoni mwa ibada kuna ibada maalum zaidi. Zile ibada maalumu nizile


za Mitume (s.a.w), mfano kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Ametukuka


aliye teremsha Furqani kwa mja wake). (Al-Furqan: 1).


Na kauli yake: (Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo mteremshia mja wetu).


(Al-Baqara: 23.)


Na kauli yake: (Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu).


)Swad: 45.)


Na dalili nyingine tofauti na hizo zinazo wasifia Mitume (s.a.w), kuonyesha


kama na wao ni waja wake.


Je, wanalipwa thawabu wale wanao dai kufanya ibada kwa kuamini


matendo ya Mwenyezi Mungu kama kuumba na kufisha na kuhuyisha, bila


kufanya ibada alizo zifaradhisha Mwenyezi Mungu kama kutoa shahada na


kuswali na kufunga …nk. ?


JAWABU: Hao hawalipwi, kwasababu wanadamu wote wameubwa na


Mwenyezi Mungu wakiwa katika maumbile ya kukiri ukubwa wa Mwenyezi


Mungu na vitendo vyake katika ulimwengu na hilo nilazima kwa watu wote,


mwanadamu anauguwa na anakuwa masikini, na anampoteza kipenzi chake bila


yeye kupenda, bali halipendi jambo hilo, lakini ni lazima iwe hivyo kwa sababu


nimatashi ya Mwenyezi Mungu.



Machapisho ya hivi karibuni

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI

KWANINI UISLAMU? UZU ...

KWANINI UISLAMU? UZURI NA FAIDA ZA UISLAMU