Nakala




 MASWALI SITINI KATIKA HUKUMU ZA HEDHI NA


 NIFASI


 


 Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.


 UTANGULIZI:


 Sifa zote njema anastahiki Mwenyezi Mungu, na rehema na amani zimuendee Mtume wa Allah,


 Muhammad bin Abdillah na wafuasi wake na maswahaba wake na kila atakayepita katika njia yake


 mpaka siku ya malipo, baada ya hayo:


 Dada yangu Muislam!


 Tukitazama maswali mengi ambayo wanaulizwa wanachuoni kuhusiana na hukumu za hedhi katika


 ibada, tukaona tuyakusanye maswali yote yanayojirudia mara nyingi, na mara nyingi yanatokea bila


 kurefusha, na hilo ni katika kutaka kufupisha.


 Dada yangu Muislamu!


 Jitihada zetu za kuyakusanya maswali haya, ni ili yawe mikononi mwako daima, hilo linatokana na


 umuhimu wa utambuzi wa sheria ya Allah, ili uweze kumuabudu Allah kwa ujuzi na maarifa.


 Angalizo: Inaweza kuonekana kuwa baadhi ya maswali yemejirudia kwa yule atakayekipitia kitabu hiki


 kwa mara ya kwanza, lakini baada ya mazingatio ataona katika maswali hayo kuna ziada ya elimu katika


 jibu moja ziada ambayo haipatiani katika jibu lingine, tukaona tusiyaache maswali hayo.


 Kwa utangulizi huu: Tunaomba-Rehema na amani ziwe juu- ya Muhammad na wafuasi wake wote na


 Maswahaba wake wote.


 *


 MIONGONI MWAHUKUMUZAHEDHIKATIKASWALANA


 SWAUMU:


 Swali la 1:Akitwaharika mwanamke baada ya swala ya Alfajiri, je ajizuie na afunge swaumu siku hiyo?, na


 je siku hiyo itahesabika kwake kuwa kafunga au atatakiwa kuilipa siku hiyo?


 Jawabu la 1:Akitwaharika mwanamke baada ya kuchomoza Alfajiri, wanachuoni wana kauli mbili juu ya


 mwanamke huyu katika kujizuia kula na kunywa na tendo la ndoa mchana wa siku hiyo.


 Kauli ya kwanza: Atalazimika kujizuia kula, kunywa, na tendo la ndoa katika masaa yaliyobakia kwa siku


 hiyo, lakini haitohesabika kwake siku hiyo, bali atawajibika kuilipa, na hii ndio kauli ya wanachuoni wengi


 katika madhehebu ya Imam Ahmad-Allah amrehemu


Kauli ya pili: Hatolazimika kujizuia kula, kunywa, na tendo la ndoa mchana wa siku hiyo, kwa sababu


 haikubaliki funga kwa siku hiyo, kwa sababu mwanzo wa siku alikuwa kwenye hedhi, na aliye katika hedhi


 hafai kufunga, na kwakuwa swaumu yake si sahihi, basi hakuna faida ya kujizuia kula, kunywa, na tendo


 la ndoa, na wakati wa siku hiyo si wakati wa kuheshimiwa kwa upande wake, kwa sababu ameamrishwa


 kula mwanzo wa mchana, bali ni haramu kwake kufunga mwanzo wa mchana,Na swaumu ya kisheria: Ni


 kujizuia na vyote vyenye kufunguza kwa lengo la kumwabudu Allah toka kuchomoza alfajiri mpaka


 kuzama kwa jua.


 Na kauli hii-kama unavyoiona- ina nguvu zaidi kuliko kauli ya kwanza ya kujizuia, lakini kwa kauli zote


 hizi mbili itamlazimu kulipa siku hii.


 Swali la 2:Atakapotwaharika aliyekuwa na hedhi, na akaoga josho kubwa baada ya swala ya Alfajiri, na


 akaswali, na akaikamilisha swaumu ya siku yake ile, je anawajibika kulipa siku hiyo?


 Jawabu la 2:Atakapo twaharika Mwanamke aliyekuwa katika hedhi kabla ya kuchomoza Alfajiri hata kwa


 dakika moja, lakini akapata yakini kuwa ametwaharika, ikiwa ni katika Ramadhani basi atalazimika


 kufunga, na inakuwa funga yake siku hiyo ni sahihi, na wala halazimiki kuilipa siku hiyo, kwa sababu


 amefunga akiwa ametwaharika, hata kama hakuoga josho kubwa ila baada ya Alfajiri basi hakuna


 tatizo.Kama vile Mwanaume akiwa katika janaba lililotokana na tendo la ndoa au kujiotea, na akala daku


 na wala hakuoga janaba ila baada ya Alfajiri, funga yake itakuwa sahihi.


 kwa uhusiano huu, napenda kutoa angalizo la jambo lingine kwa wanawake, pindi mwanamke atakapo


 ijiwa na hedhi, na alikuwa kafunga siku hiyo, baadhi ya wanawake hudhania kwamba hedhi itakapowajia


 baada ya kufungua kabla ya kuswali swala ya Ishaa funga yao ya siku hiyo inakuwa imeharibika,Jambo


 hilo halina dalili katika sheria, bali hedhi itakapo muijia mwanamke baada ya magharibi walau kwa muda


 mchache basi funga yake inakuwa imetimia na ni sahihi.


Swali la 3:Je ni lazima kwa wanawake wenye Nifasi kuswali na kufunga wakitwaharika kabla ya siku


 arobaini?


 Jawabu la 3:Naam, muda wowote atakapo twaharika mwanamke mwenye nifasi kabla ya siku Arobaini


 basi ni lazima juu yake kufunga ikiwa ni ndani ya Ramadhani, ni lazima juu yake kuswali, na inafaa kwa


 mume wake kumuingilia; Kwa sababu yuko twahara, hakuna kitu kinachomzuia kufunga na hakuna


 kinachomzuia kuswali wala kufanya tendo la ndoa.


 Swali la 4:Ikiwa mzunguko wa mwezi wa mwanamke ni siku nane au siku saba, kisha mzunguko wake


 ukaendelea mara moja na mara nyingine zaidi ya siku hizo, ni ipi hukumu yake?


 Jawabu la 4:Ikiwa mzunguko wa mwanamke huyu ni siku sita au saba, kisha muda wa kuwa na damu


 ukarefuka, ukawa siku nane, au saba, au kumi, au kumi na moja, basi hatoswali mwanamke huyu mpaka


 atwaharike,Na hilo ni kwa sababu Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake- hakuweka ukomo maalumu


 wa siku za mzunguko wa hedhi.





 ]، Na amesema Allah


 Mtukufu: "Na wanakuuliza kuhusu hedhi, sema: Huo ni uchafu" [Al-baqara: 222],Muda wowote damu hii


 ikiwepo basi mwanamke atabaki katika hali hiyo mpaka atwaharike, na aoge josho kubwa, kisha aswali,


 na ukija mwezi wa pili siku zimepungua ukilinganisha na mwezi wa kwanza, basi akitwaharika ataoga


 hata kama mwezi huu haukuwa kama ule uliopita.


 Na jambo la msingi nikuwa; Muda wowote mwanamke akiwa katika mzunguko wa hedhi basi hatoswali,


 uwe mzunguko huo una siku kama mzunguko uliopita, au zimezidi au zimepungua, atakapotwaharika


 ataswali.


 Swali la 5:Je mwanamke mwenye nifasi anakaa siku arobaini haswali na hafungi, au kinachozingatiwa ni


 kukatika ile damu, muda wowote ikikatika anakuwa katwaharika na ataswali, na ni upi muda mchache wa


 kutwaharika?


 Jawabu la 5:Damu ya uzazi haina wakati maalumu, muda wowote damu ikiwepo atakaa, hatoswali,


 hatofunga, na hatoingiliwa na mumewe.


 Na pindi akiona katwaharika-hata kabla ya siku arobaini, hata kama hakukaa isipokuwa siku kumi au


 tano- basi ataswali, atafunga, na ataingiliwa na mumewe, wala hakuna tatizo katika hilo.


 Na jambo la msingi nikuwa; Nifasi ni jambo linahisika, linafungamana na hukumu za kisheria kwa kuwepo


 kwake na kutokuwepo kwake, muda wowote ikiwepo basi zinathibiti hukumu zake, na muda wowote


 akitwaharika basi hukumu za nifasi hatohusika nazo.


 Lakini lau zikizidi zaidi ya siku sitini basi damu hiyo itakuwa ni damu ya ugonjwa, atakaa muda ule ambao


 unawafikiana na muda wake wa hedhi pekee, kisha ataoga, na ataswali.


 Swali la 6:Litakapo dondoka tone dogo la damu ya hedhi mchana wa Ramadhani, na ikaendelea damu hii


 kumtoka mwanamke ndani ya mwezi wa Ramadhani naye anafunga, je funga yake ni sahihi?


 Jawabu la 6:Ndio, swaumu yake ni sahihi, ama haya matone si chochote, yanatokana na mishipa ya


 damu, imepokewa kutoka kwa Ally bin Abi twalib-Allah amridhie- amesema: "Hakika matone haya


 ambayo yanakuwa mithili ya damu inayotoka puani si hedhi" hivyo ndivyo alivyosema radhi za Allah ziwe


 juu yake.


 Swali la 7:Mwanamke mwenye hedhi au nifasi akitwaharika kabla ya Al fajiri, je swaumu yake iko sahihi


 au la?


 Jawabu la 7:Naam, iko sahihi swaumu ya Mwanamke mwenye hedhi atakapo twaharika kabla ya Al fajiri,


 na hakuoga josho kubwa la kujitwaharisha isipokuwa baada ya Al fajiri, na hukumu hii ni pamoja na


 wanawake walio katika nifasi, kwa sababu kwa wakati huo ni katika watu wanaotakiwa kufunga, na huu ni


 mfano wa aliyepatwa na janaba, na ikachomoza Alfajiri akiwa na janaba, swaumu yake ni sahihi;





 ]، Kutokana na


 kauli yake Allah-Mtukufu-: "Na sasa hivi waingilieni na tafuteni yale aliyowaandikieni Allah kwa ajili yenu,


 na kuleni na kunyweni mpaka ibainike kwenu nyinyi weupe wa alfajiri ya kweli itokanayo na giza la usiku"


 (Al baqara: 187)Na akiruhusu Allah kumuingilia mwanamke mpaka ibainike Alfajiri ya kweli basi


 inamlazimu katika hilo kusiwe na kuoga josho kubwa isipokuwa baada ya kuchomoza Alfajiri, kutokana na


 hadithi ya Aisha-Radhi za Allah ziwe juu yake- kwamba Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake


alikuwa akiamka asubuhi akiwa na janaba kutokana na kumuingilia mkewe naye akiwa katika


 swaumu.Yaani: Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake- haogi janaba isipokuwa baada ya kuchomoza


 Alfajiri.


 Swali la 8:Mwanamke akihisi damu ya hedhi,na Damu hiyo haikutoka kabla ya magharibi, au akahisi


 maumivu ya mzunguko wake, je inafaa swaumu yake siku hiyo, au ni wajibu kwake kuilipa?


 Jawabu la 8:Pindi akihisi mwanamke aliyotwaharika kuja kwa damu ya hedhi akiwa amefunga, lakini


 haikutoka mpaka baada ya kuzama kwa jua, au alihisi maumivu kwa sababu ya hedhi, lakini haikutoka


isipokuwa baada ya kuzama kwa jua, basi swaumu yake hiyo siku ni sahihi, hatoirudia swaumu ile ikiwa


 ni swaumu ya lazima, na wala haziharibiki thawabu zake kwa hilo ikiwa ni swaumu ya sunna.


 Swali la 9:Pindi mwanamke atakapoona damu, na hakuwa na uhakika kama ni damu ya hedhi, je ni ipi


 hukumu ya swaumu yake siku hiyo?


 Jawabu la 9:Swaumu yake siku hiyo ni sahihi; Kwa sababu asili ni kutokuwa na hedhi mpaka ibainike


 kwake kwamba ile ni hedhi.


 Swali la 10:Baadhi ya wakati, mwanamke anaona athari ya damu chache ikiwa katika hali ya matone


 yakimtoka katika nyakati tofauti tofauti ndani ya siku moja, baadhi ya wakati anaziona wakati wa


 mzunguko wake wa kisheria na mzunguko ukiwa bado haujamtoka, na mara nyingine anaziona wakati


 ambao sio wa mzunguko wake, ni ipi hukumu ya swaumu yake katika hizo hali mbili.


 Jawabu la 10:Limetangulia jawabu linalofanana na swali hili muda si mrefu lakini kilichobaki ikiwa haya


 matone yanatokea katika siku za mzunguko, ikiwa hivyo yatazingatiwa kama ni hedhi ambayo unaijua,


 inakuwa ni hedhi.


 Swali la 11:Je mwanamke aliye katika mzunguko wa hedhi na nifasi anakula na kunywa mchana wa


 Ramadhani?


 Jawabu la 11:Ndio, wanakula na kunywa katika mchana wa Ramadhani, lakini bora ikawa kula huko ni


 kwa siri akiwa ana watoto ndani ya nyumba kwa sababu jambo hilo huleta tatizo kwa watoto wakiona mtu


 anakula mchana wa ramadhani.


 Swali la 12:Akitwaharika mwenye hedhi au nifasi muda wa Alasiri, je analazimika kuswali swala ya


 Adhuhuri na Alasiri, au je halazimiki kuswali isipokuwa Alasiri peke yake?


 Jawabu la 12:Kauli yenye kutegemewa katika swala hili nikuwa: Analazimika kuswali swala ya Alasiri


 pekee kwa sababu hakuna dalili juu ya ulazima kwake kuswali Adhuhuri, na asili ni kutokuwa na dhima ya


 jambo na Nabii-Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:"Atakaye upata wakati wa swala ya Alasiri


 kwa kiwango cha rakaa moja kabla jua halijazama basi ameipata Lasiri",Na hakutaja kwamba amediriki


 Adhuhuri, ingekuwa swala ya Adhuhuri ni lazima kwa mtu huyu basi angebainisha Nabii-Rehema na


 amani ziwe juu yake- na mwanamke akitokwa na damu ya hedhi, baada ya kuingia wakati wa Adhuhuri


 basi haimlazimu akitwaharika kulipa isipokuwa swala ya Adhuhuri pekee na hatolipa Alasiri pamoja na


 kwamba swala ya Adhuhuri hujumuishwa na swala ya Alasiri na wala hakuna tofauti kati yake na sura


 iliyoulizwa katika swali.


 Na kuhusu suala hili, kauli ya kutegemewa nikwamba halazimiki isipokuwa swala ya Alasiri pekee


 kutokana na dalili ya kisheria na kiyasi (Kuoanisha mambo), na hivyo hivyo ikiwa ametoharika kabla ya


 kutoka wakati swala ya Ishaa, basi halazimiki isipokuwa kuswali swala ya ishaa peke yake, wala


 halazimiki kuswali swala ya Magharibi.


 Swali la 13:Baadhi ya wanawake ambao zinatoka mimba zao, haiwi hali zao isipokuwa: Ujauzito ukitoka


 kabla mtoto hajaumbwa tumboni, au mimba ikatoka baada ya kuumbwa kiumbe na ukadhihiri muundo wa


 umbile lake, ni ipi hukumu ya swaumu siku hiyo ambayo katokwa na mimba ile, na swaumu za siku


 ambazo ataiona damu inatoka?


 Jawabu la 13:Ikiwa mtoto hajaumbwa tumboni basi damu itakayomtoka si damu ya uzazi, na juu ya hili


 basi atafunga na kuswali na swaumu yake ni sahihi.


 Na ikiwa mtoto ameumbwa basi damu itakayomtoka ni damu ya nifasi, haifai kwake kuswali katika hali


 hiyo, wala haruhusiwi kufunga swaumu.


 Na kanuni na kigezo katika swala hili ni kuwa; Ikiwa mtoto ameumbwa basi damu itakayomtoka ni damu


 ya uzazi (nifasi), na ikiwa hajaumbwa basi damu itakayomtoka siyo damu ya nifasi, na ikiwa damu


 itakayomtoka ni damu ya uzazi (nifasi) haitofaa kwake yote yale yasiyofaa kwa wanawake wanaotokwa


 na damu ya uzazi (nifasi) na ikiwa si damu ya uzazi (nifasi) basi hatoharamishiwa juu yake


 anayoharamishiwa mwanamke mwenye nifasi.


 Swali la 14:Mwanamke mjamzito akitokwa na damu mchana wa Ramadhani, je jambo hili lita athiri


 swaumu yake?


 Jawabu la 14:Itakapotoka damu ya hedhi na mwanamke akiwa amefunga basi funga yake itaharibika,


 kutokana na kauli ya Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake-"Hivi haikuwa wakati alipokuwa katika


 mzunguko wake wa hedhi haswali wala hafungi?"Na kwa ajili hii tunazingatia hili ni katika mambo


 yanayofunguza swaumu, na damu ya uzazi ni mfano wake, na kutoka damu ya hedhi na nifasi vinaharibu


 funga ya mtu.


 Na mwanamke mjamzito akitokwa na damu mchana wa ramadhani basi ikiwa ni hedhi basi hiyo ni hedhi


 kama ilivyo hedhi ya mwanamke asiye mjamzito, na inaathiri swaumu yake, na ikiwa siyo hedhi basi


 haiathiri funga yake.


Na damu ya hedhi ambayo inaweza mtokea mwanamke mwenye mimba ni damu ya hedhi ambayo


 haikatiki kwake tangu kubeba ujauzito huo, bali inamjia katika zile nyakati zake alizozizoea kuwa damu ya


 hedhi humuijia, basi hedhi hii kwa kauli yenye kutegemewa inathibiti kwake na inachukua hukumu za


 hedhi ya kawaida.


 ama ikikatika damu hiyo ya hedhi naye bado mjamzito, kisha ikawa baada ya hapo anaona damu katika


 wakati ambao siyo wa mzunguko wake wa kisheria, hili haliathiri funga yake, kwa sababu hii si hedhi.


 Swali la 15:ikiwa mwanamke anaona damu siku moja akiwa katika mzunguko wake, na siku inayofuata


 haoni damu mchana kutwa, ni kipi juu yake anatakiwa kufanya?


 Jawabu la 15:Linalo onekana ni kwamba, hii twhara au ukavu (katika sehemu za siri) uliopatikana wakati


 wa siku zake za hedhi, utafuata (hukumu za) hedhi, hautohesabika kama ni twhara, pamoja na hilo


 ataendelea kujizuia kwa yale anayojizuia kwayo mwanamke aliye katika hedhi.


 Na wamesema baadhi ya wanachuoni: Mwanamke mwenye kuona damu siku moja, na siku nyingine


 akaona yuko twahara, basi ile damu (aliyoiona) ni hedhi, na ule usafi (aliouona) ni twahara mpaka zifike


 siku kumi na tano.Na ikifika siku ya kumi na tano, inakuwa damu itokayo baada ya hapo ni damu ya


 ugonjwa (Istihadhwa). Na hili ndilo limetajwa kuwa ni sahihi na wanachuoni wengi katika madhehebu ya


 Imam Ahmad ibn Hanbali (Allah amrehemu).


 Swali la 16:Katika siku za mwisho za hedhi au kabla ya kutwaharika, mwanamke ikiwa haoni athari ya


 damu ya hedhi, je anaruhusiwa kufunga siku hiyo? ikiwa haoni maji maji meupe yakitoka katika tupu


 yake, au afanye nini?


 Jawabu la 16:Ikiwa ni kawaida ya mwanamke, haoni maji maji meupe kama ilivyo kwa baadhi ya


 wanawake basi mwanamke huyu atafunga swaumu yake, na ikiwa kawaida yake anaona maji maji


 meupe, basi hatofunga mpaka aone maji maji hayo yamekatika.


 Swali la 17:Ni ipi hukumu ya mwanamke mwenye hedhi na anaetokwa damu ya uzazi (Nifasi) kusoma


 Qur'ani akiwa anatizama au kile alichohifadhi katika hali ya dharura, mfano yeye ni mwanafunzi au ni


 mwalimu?.


 Jawabu la 17:Hakuna tatizo kwa mwanamke aliye katika hedhi au damu ya uzazi (Nifasi) kusoma Qur'ani


 ikiwa ni kwa hitajio, kama vile mwalimu wa kike, au mwanafunzi wa kike ambaye anasoma uradi wake


 (kiwango anachohitaji kusoma katika Qur'ani) usiku au mchana.


 Ama kisomo-Namaanisha: Kusoma Qur'ani kwa ajili ya kutafuta ujira na thawabu za kisomo-jambo bora


 asisome; kwa sababu wanawachuoni wengi au wengi wao wanaona kwamba mwanamke aliye katika


 hedhi haifai kwake kusoma Qur'ani.


 Swali la 18:Je analazimika mwanamke aliye katika hedhi kubadili nguo zake baada ya kutwaharika,


 pamoja na kuwa nguo hizo hazikudondokewa na damu yoyote wala uchafu wowote?.


 Jawabu la 18:Haimlazimu yeye kufanya hivyo, kwa sababu hedhi haichafui (hainajisi) mwili, bali damu ya


 hedhi inachafua inacho kutana nacho pekee na kwa hili Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake


aliamrisha wanawake pindi zinapogusa damu za hedhi nguo zao wasafishe pale palipopatwa na damu


 kisha waswalie nguo zao.


 Swali la 19:Mwanamke amefungua katika Ramadhani siku saba, alikuwa akitokwa damu ya uzazi, na


 hakulipa siku hizi mpaka akajiwa na Ramadhani ya pili, na akazungukiwa katika Ramadhani ya pili na


 siku saba ambazo alikuwa ananyonyesha (hakufunga) kwa hoja alikuwa na maradhi, na imekaribia


 kuingia Ramdhani ya tatu, tupeni faida, Allah awalipeni thawabu.


 Jawabu la 19:Ama akiwa mwanamke huyu kama alivyojieleza-kuwa yeye ni mgonjwa na wala hawezi


 kulipa-, basi wakati wowote akiweza kulipa basi na afunge; kwa sababu yeye ana udhuru hata kama ikija


 Ramadhani ya pili.


 Ama ikiwa mwanamke huyu hana udhuru wowote ule, alikuwa akijifanya mgonjwa na anafanya uzembe,


 huyu hairuhusiwi kwake kuchelewesha kulipa Ramadhani mpaka Ramadhani ya pili.Amesema Aisha


 (Radhi za mwenyezi mungu ziwe juu yake na amani): "alikuwa nikidaiwa swaumu ambayo natakiwa


 kulipa, basi siwezi kuzilipa isipokuwa katika mwezi wa Shaaban".


 Na kwa namna hiyo, ni juu ya mwanamke huyu aitizame nafsi yake, ikiwa hana udhuru basi anapata


 dhambi, na juu yake kutubia kwa Allah, na apupie kulipa swaumu zilizo juu yake, ikiwa ana udhuru


 hakuna shida juu yake, hata kama ikichelewa mwaka au miaka miwili.


 Swali la 20:Baadhi ya wanawake wanaingiwa na Ramadhani ya pili na wao hawajafunga baadhi ya siku


 katika Ramadhani iliyopita, ni lipi jambo la lazima juu yao kufanya?.


 Jawabu la 20:Jambo la lazima juu yao: Kutubia kwa Allah juu ya jambo hili; kwa sababu haifai kwa


 mwenye deni la swaumu za Ramadhani akachelewesha mpaka Ramadhani ya pili bila udhuru; kutokana


 na kauli ya Aisha-Radhi za Allah ziwe juu yake- "Ilikuwa ninaokuwa na deni la swaumu natakiwa kulipa,


 basi siwezi kuzilipa isipokuwa katika mwezi wa Shaaban".


Na hii inaonyesha ya kwamba haiwezekani kuchelewesha kulipa mpaka ramadhani ya pili, ni juu yake


 atubie kwa Allah-mshindi aliyetukuka- kwa yale aliyoyafanya, na alipe siku alizoziacha baada ya


 ramadhani ya pili.


 Swali la 21:Mwanamke atakapo tokwa na damu ya hedhi adhuhuri, akiwa hajaswali swala ya adhuhuri, je


 analazimika kuilipa swala ile baada ya kutwaharika?


 Jawabu la 21:Katika hili kuna tofauti baina ya wanachuoni, wapo wanaosema haimlazimu mwanamke


 huyu kuilipa swala hii, kwa sababu hakufanya uzembe na wala hatopata dhambi; na kwakuwa


 anaruhusiwa kuichelewesha swala mpaka ukikaribia mwisho wa wakati wa swala.


 Wengine wanasema: Analazimika kuilipa, namaanisha kuilipa swala ile iliyompita kabla ya hedhi kutoka,


 kutokana na ujumla wa maneno ya Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake-"Atakaye idiriki rakaa katika


 swala basi amediriki swala"


 Na kwa kujiepusha kuingia katika madhambi: Bora ailipe, maana ni swala moja, hakuna ugumu katika


 kuilipa.


 Swala la 22:Atakapo ona mjamzito damu kabla ya kujifungua kwa siku moja au siku mbili, je ataacha


 kufunga na kuswali kwa ajili ya damu hiyo au lipi afanye?


 Jawabu la 22:Mjamzito atakapoiona damu siku moja au siku mbili kabla ya kujifungua, huku akiwa na


 uchungu wa kujifungua, basi damu hiyo ni damu ya uzazi (Nifasi), kwa ajili ya damu hiyo hatoswali na


 wala hatofunga, isipoambatana damu hiyo na uchungu wa kujifungua, basi damu hiyo iliyoharibika


 haizingatiwi, na wala haimzuii mwanamke kufunga wala kuswali.


 Swali la 23:Ni yapi maoni yako kuhusu kumeza vidonge vya kuzuia mzunguko wa mwezi wa damu ya


 hedhi kwa ajili ya Kufunga pamoja na watu?


 Jawabu la 23:Mimi ninatahadharisha kuhusu hilo, na hilo ni kwa sababu vidonge hivi vina madhara


 makubwa, limethibiti hilo kwangu kupitia matabibu, na anaambiwa mwanamke: Hilo jambo ameliandika


 Allah kwa mabinti wa Adam, basi tosheka kwa lile alilokuandikia Allah Mtukufu, na ufunge siku ambazo


 hakuna kizuizi, kitakapo patikana kizuizi basi fungua kwa kuridhia yale ambayo Allah Mtukufu amekadiria.


 Swali la 24:Mwanamke baada ya miezi miwili tangu kukatika kwa damu ya uzazi (Nifasi), akaanza kuona


 vitone vidogo vya damu, je atafungua, na wala hatoswali? au ni kipi atafanya?.


 Jawabu la 24:Matatizo ya wanawake katika damu ya hedhi na damu ya uzazi (Nifasi) ni bahari isiyo na


 ufukwe, na katika sababu za matatizo hayo: Matumizi ya vidonge vya kuzuia mimba au kuzuia damu ya


 hedhi, na watu hawakuwa wakijua matatizo haya mengi,Sahihi, haya matatizo yalikuwepo tangu


 alipopewa Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake- Utume, bali yalikuwepo tangu alipopatikana


 mwanamke, lakini kwa wingi wake katika sura hii ambayo anafikia mwanadamu haelewi namna ya


 kutatua matatizo haya, hili ni jambo la kuhuzunisha sana.


 Lakini kanuni ya ujumla: Mwanamke akitwaharika, akaona kutwaharika baada ya damu ya hedhi na damu


 ya uzazi: Yakatoka maji maji meupe wanayajua wanawake- basi baada ya mwanamke kutwaharika


 ukitoka uchafu, unjano, au tone, au unyevu, hivi vyote si hedhi, na havimzuii vitu hivyo kuswali, kufunga


 na wala havizuii tendo la ndoa baina ya mwanaume na mwanamke kwa sababu vitu hivyo si damu ya


 hedhi.Alisema Ummu Atwiyah: "Tulikuwa hatuoni unjano na uchafu kuwa ni kitu"amesimulia Al Bukhari na


 akazidisha Abu Daud: (wakiona vitu hivyo) Baada ya kutwaharika.Mtiririko wa wapokezi wake ni sahihi.


 Na kuhusu hili tunasema: Kila kitakachotokea katika vitu hivyo baada ya kutwaharika kwa uhakika, vitu


 hivyo havimdhuru mwanamke na wala havimzuii kuswali swala zake, na kufunga swaumu zake, na


 havimzuii kuingiliwa na mume wake lakini ni lazima kwa mwanamke huyu asifanye haraka asubiri mpaka


 aone kuwa katwaharika.Kwa sababu baadhi ya wanawake damu ikikauka, hufanya haraka na


 hujitoharisha kwa kuoga kabla hajaona kule kutwaharika kunakotakiwa.Na kwa hivyo, walikuwa


 wanawake walioishi kipindi cha Mtume wakiagiza Kursuf yaani; pamba yenye damu, iende kwa mama wa


 waumini Aisha radhi za Allah ziwe juu yake, alikuwa akiwaambia; Msifanye haraka mpaka muone maji


 maji meupe ambayo hutoka baada ya hedhi kumalizika.


 Swali la 25:Baadhi ya wanawake damu inaendelea, na wakati mwingine inakatika siku moja au siku mbili


 kisha inarejea, je ni ipi hukumu katika hali hii kuhusu swaumu yake na swala yake na ibada zingine.


 Jawabu la 25:Linalofahamika kwa wanachuoni walio wengi ni kwamba: Mwanamke anapokuwa katika


 siku zake, zikiisha siku zake, basi anajitwaharisha kwa kuoga, na ataswali na kufunga na atakacho kiona


 baada ya hapo siku moja au siku mbili si hedhi kwa sababu siku chache za kutoharika baina ya hedhi


 mbili kwa wanachuoni hawa ni siku kumi na tatu.


 Na wamesema wanachuoni wengine kwamba: Bali kwa mwanamke huyu atakapo ona damu basi hiyo ni


 hedhi, na wakati wowote akitwaharika basi ametwaharika, hata kukiwa hakuna baina ya hedhi ya kwanza


 na ya pili siku kumi na tatu.


Swali la 26:Lipi bora kwa mwanamke: Akaswali usiku ndani ya mwezi wa Ramadhani nyumbani kwake,


 au msikitini, hasa hasa msikitini kukiwa na mawaidha na ukumbusho? Ni upi muongozo wako kwa


 wanawake ambao wanaswali msiktini?.


 Jawabu la 26:Bora akaswali katika nyumba yake, kutokana na ujumla wa kauli ya Mtume-Sala na salama


 ziwe juu yake-"Na Nyumba zao ni bora kwao wao"Na ni kwa sababu mwanamke kutoka nyumbani kwake


 hakujasalimika na fitna katika nyakati nyingi, na kuwa mwanamke kubakia nyumbani kwake ni bora


 kwake, kuliko kutoka kwenda msikitini, ama mawaidha na mazungumzo ya kheri inawezekana akayapata


 kupitia kanda.


 Na muongozo wangu kwa wanawake ambao wanaswalia msikitini: Watoke katika nyumba zao wakiwa


 hawaja jipamba kwa mapambo, wala kujipulizia manukato.


 Swali la 27:Ni ipi hukumu ya mwanamke kuonja chakula mchana wa Ramadhani akiwa amefunga.


 Jawabu la 27.Hukumu yake: Hakuna shida juu ya jambo hilo, akiwa na haja ya jambo hilo, lakini akiteme


 kile alichokionja (asimeze).


 Swali la 28:Mwanamke kapata ajali, na alikuwa mwanzo wa mimba yake, mimba ikatoka baada ya


 kutokwa na damu nyingi, je inajuzu kwake kufungua, au anaendelea kufunga? Akifungua je atapata


 dhambi?


 Jawabu la 28:Tunasema: Hakika mjamzito hatokwi na damu ya hedhi, kama anavyosema Imam Ahmad:


 Wanawake wengi hujua ujauzito kwa kukatika hedhi,na hedhi kama walivyosema Wanawachuoni,


 ameiumba Allah-Mtukufu- kwa hekima ya kuwa ni chakula cha mtoto aliye tumboni, mimba itakapo anza


 hedhi hukatika.


 Lakini baadhi ya wanawake inaweza ikaendelea kwake damu ya hedhi kama kawaida kama ilivyokuwa


 kabla ya mimba, huyu atahukumiwa kuwa hedhi yake ni hedhi ya kawaida, kwa sababu hedhi kwake


 iliendelea na wala haikuathirika na mimba, hedhi hii itamzuia na yale yote ambayo yanayozuiwa na hedhi


 ya siku zote ya mwanamke asiyemjamzito, hivyo, itawajibisha yale ambayo yanawajibika kwa mwenye


 hedhi, na itadondosha yale yote ambayo yanadondoshwa na hedhi ya kawaida (ikiwemo swala n.k)


 Na kwa ufupi ni kwamba: Damu inayomtoka mjamzito iko katika aina mbili:


 Aina moja wapo inahukumiwa kuwa ni hedhi, nayo ni ile ambayo inaendelea kutoka kwake kama


 ilivyokuwa ikitoka kabla ya mimba, basi maana ya jambo hili ni; Mimba haijamuathiri, hii itakua ni hedhi ya


 kawaida.


 Na aina ya pili, ni damu inayotoka wakati wa mimba, ima kwa sababu ya ajali, au alibeba kitu, au


 kudondoka toka juu ya kitu fulani na mfano wake, damu hii si hedhi, bali ni damu ya ugonjwa.kwa hiyo,


 haimzuii damu hii kuswali, wala kufunga, bali anakuwa katika hukumu ya wanawake waliotoharika.


 Lakini ajali ikisababisha mtoto kushuka au mimba ambayo iliyokuwa tumboni, atakuwa kama


 walivyosema Wanawachuoni: Mimba ikitoka na imebainika kwake umbile la mwanadamu, basi damu


 itakayotoka baada ya kutoka mtoto itahesabika kuwa ni damu ya uzazi, ataacha kuswali, na kufunga, na


 mumewe atajitenga naye mpaka atwaharike.


 Na akitoka mtoto ambaye hajakamilika basi haizingatiwi kuwa ni damu ya uzazi, bali ni damu iliyoharibika,


 haimzuii mwanamke kuswali, wala kufunga, wala kingine chochote.


 wamesema Wanachuoni: Muda mchache ambao kinabainika kiumbe: Ni siku themanini na moja; kwa


 sababu mtoto yupo tumboni kwa mama yake.Kama alivyosema Abdullah bin Masoud-Radhi za Allah


 ziwe juu yake- Ametuhadithia mkweli mwenye kusadikishwa, akisema: "Hakika mmoja wenu hukusanywa


 umbile lake katika tumbo la mama yake siku arobaini, kisha linakuwa pande la damu mfano wa siku hizo,


 kisha linakuwa pande la nyama mfano wa siku hizo, kisha hutumwa Malaika na anaamrishwa kuandika


 mambo manne; kuandika riziki yake, kifo chake, muovu au mwema".Na wala haiwezekani kuumbwa


 kabla ya hizo siku, mara nyingi kiumbe hakibainiki kabla ya siku tisini, kama walivyosema baadhi ya


 Wanachuoni.


 Swali la 29:Mimi ni mwanamke ilitoka mimba ikiwa katika mwezi wa tatu, mwaka umepita sasa, na


 sikuswali mpaka nilivyotwaharika, waliniambia, ulikuwa unatakiwa kuswali, basi kipi natakiwa kufanya, na


 mimi sifahamu idadi ya siku maalumu?.


 Jawabu la 29.Jambo linalofahamika kwa wanawachuoni ni kwamba: Mwanamke pindi itakapotoka mimba


 yake ikiwa imetimiza miezi mitatu basi yeye hatoswali, kwa sababu aliyetoka ni mtoto aliyebainika umbile


 lake na damu inayotoka inakuwa ni damu ya uzazi hivyo hatoswali ikiwa inatoka damu hiyo.


 wanasema wanachuoni: Inawezekana kubainika umbile la mtoto tumboni zikitimia siku 81 na hizi ni chini


 ya miezi mitatu, akiwa na yakini kwamba mimba imetoka ikiwa na miezi mitatu, damu itakayomtoka


 inakuwa damu iliyoharibika, haachi swala kwa sababu hiyo.


Na jambo hili ni juu ya mwanamke kukumbuka, ikiwa mtoto aliyetoka ilikuwa kabla ya siku 80 basi


 atazilipa swala zile, ikiwa hajui ni swala ngapi kaziacha?Basi akadirie, na ajitahidi kujua idadi, kisha


 dhana yake kubwa ikiwa katika idadi fulani ya swala zilizompita, basi azilipe kwa idadi hiyo.


 Swali la 30:Muulizaji wa kike anauliza:Yeye tangu awajibikiwe na swaumu anafunga Ramadhani, lakini


 halipi siku zake alizofungua kwa sababu ya mzunguko wa damu ya hedhi, na kwa sababu ya kutokujua


 idadi ya siku alizofungua, kwa hiyo, yeye hivi sasa, anaomba muongozo lile la lazima juu yake kulifanya.


 Jawabu la 30:Inasikitisha kutokea hili baina ya wanawake wa waumini, hakika huko kuacha- namaanisha:


 Kuacha kulipa siku ambazo ni lazima kwao kufunga-ima ni kwa sababu ya kutokujua, na ima ni kwa


 sababu ya uzembe, yote mawili ni msiba, kwa sababu ujinga dawa yake ni kusoma na kuuliza,Ama


 kuzembea, dawa yake ni kumcha Allah mshindi aliyetukuka, na kujichunga kujua Allah anakuona, na


 kuogopa mwisho wa mambo, na kupupia yale ambayo Allah anayaridhia.


 Juu ya mwanamke huyu, atubie kwa Allah kwa yale aliyoyafanya, na aombe msamaha, ajitahidi kuzijua


 siku alizoacha kadiri ya uwezo wake kisha atazilipa, na kwa kufanya hili hatolaumiwa, natarajia Allah


 atakubali toba yake.


 Swali la 31:Ni ipi hukumu ya mwanamke kafikiwa na mzunguko wa hedhi baada ya kuingia wakati wa


 swala? Je inawajibika kwake yeye kulipa akitwaharika? Na hivyo hivyo pindi akitwaharika kabla ya kutoka


 muda wa swala?


 Jawabu la 31:Kwanza: Mwanamke akiingia katika mzunguko wa damu ya hedhi baada ya kuingia wakati


 wa swala basi inawajibika kwake akitoharika alipe swala ambazo alipatwa na mzunguko katika wakati


 wake, ikiwa hajaswali kabla ya kuingiwa na hedhi.Na hali hiyo ni kwa mujibu wa neno lake Mtume rehema


 na amani za Allah zimfikie:"Mwenye kuipata rakaa moja ya swala basi kwa hakika atakuwa ameipata


 swala".Ikiwa mwanamke ataupata muda wa swala kiasi cha rakaa moja, kisha akaingia katika hedhi kabla


 hajaswali, itamlazimu kukidhi (kulipa) swala hiyo pindi atakapo twaharika.


 103


 :ءﺎﺳﻧﻟا]


 Pili: Ikiwa mwanamke atatwaharika kutokana na hedhi kabla muda wa swala haujatoka, basi


 itamuwajibikia kulipa swala hiyo. Na lau atatwaharika kabla ya jua kuchomoza kwa kiasi cha rakaa moja


 itamuwajibikia kulipa swala ya alfajiri,Na lau atatwaharika kabla ya jua kuzama kwa kiasi cha rakaa moja


 itamuwajibikia kuswali swala ya Alasiri,Na lau atatwaharika kabla ya usiku kufikia katikati itamuwajibikia


 kulipa swala ya Ishaa,Na ikiwa atatwaharika baada ya nusu ya usiku, haitamuwajibikia swala ya Ishaa,لﺎﻗ





 ]، Allah Mtukufu anasema:


 "...Na mtakapopata amani mkawa katika salama, hapana vita, basi simamisheni swala, kwa hakika swala


 kwa waumini ni faradhi iliyopangiwa wakati maalumu" [Annisai: 103],Yaani: Ni faradhi iliyopangiwa wakati


 maalumu, haifai kwa mtu kuitowa swala nje ya wakati wake (akaswali baada ya kutoka muda wake), wala


 kuiswali kabla ya kuingia wakati wake.


 swali la 32:Iwapo imeingia kwangu desturi ya mwezi (hedhi) na hali nikiwa katikati ya swala, nitatakiwa


 kufanya nini ? na je, nitawajibika kulipa swala hiyo baada ya muda wa hedhi?


 103


 jawabu la 32:Ikiwa mwanamke itamtokea hedhi baada ya kuingia wakati wa swala; kwa mfano


 mwanamke akafikwa na hedhi baada ya kupinduka jua kwa nusu saa, basi bila shaka baada ya


 kutwaharika kutokana na hedhi yake atailipa swala hii ambayo uliingia muda wake na hali akiwa na


 twahara.





 ]. Na hiyo ni kwa mujibu wa kauli ya Allah


 Mtukufu: "..Kwa hakika swala imekuwa juu ya waumini ni faradhi iliyopangiwa wakati maalumu" [An-Nisai:


 103]


 Na wala mwanamke hatolipa swala zilizomkuta akiwa ndani ya hedhi; kwa mujibu wa kauli ya Mtume


 rehema na amani za Allah zimfikie- katika hadithi ndefu:"je, si pale mwanamke anapoingia katika hedhi


 haswali na wala hafungi?"Na wanachuoni wamekubaliana kuwa mwanamke halipi swala ambayo ilimpita


 akiwa katika hedhi.


 Ama ikiwa atatwaharika, na hali ilikuwa imebaki katika muda wa swala kiasi cha rakaa moja na zaidi, basi


 ataswali swala hiyo ambayo ni ya wakati aliotwaharika ndani yake. Na hii ni kwa mujibu wa kauli yake


 Mtume rehema na amani za Allah zimfikie:"Mwenye kupata rakaa moja katika swala ya Alasiri kabla jua


 halijazama, basi kwa hakika atakuwa ameipata swala ya Alasiri".Na ikiwa mwanamke atatwaharika ndani


 ya wakati wa Alasiri, au kabla ya kuchomoza jua, na ikawa imebaki kabla ya kuzama jua au kuchomoza


 jua kwa kiasi cha rakaa moja, basi ataswali Alasiri kwa mnasaba wa swala la kwanza, na ataswali Alfajiri


 kwa mnasaba wa swala la pili.


 swali la 33:Mimi nina mama mzazi ambaye anafikia umri wa miaka sitini na tano, na yeye katika kipindi


 cha miaka kumi na tisa hajapata mtoto. Na hivi sasa ana kipindi cha miaka mitatu akiwa na ugonjwa wa


 kutokwa na damu,-na inavyoonekana nikuwa-maradhi hayo yaliimpata katika wakati huo vile vile


 atakabiliwa na ibada ya swaumu. Je ni nini nasaha zenu kwake? Na je, nini atakachotakiwa kufanya ?


Jawabu la 33:Hukumu ya mfano wa mwanamke kama huyu aliyefikwa na ugonjwa wa kutokwa na damu:


 anatakiwa aache kuswali na kufunga katika kipindi cha desturi yake iliyotangulia kabla ya kufikwa na


 ugonjwa huu. Hivyo basi iwapo ilikuwa kawaida yake anapata hedhi katika mwanzo wa kila mwezi kwa


 muda wa siku sita kwa mfano, basi atakaa katika mwanzo wa kila mwezi kwa muda wa siku sita na hali


 ya kuwa haswali wala hafungi, na zitakapoisha siku hizo basi ataoga na ataswali na atafunga.


 Na namna ya swala ya mwanamke kama huyu na mfano wake: ataosha tupu yake kwa ukamilifu, halafu


 ataifunga na atatawadha, na atakuwa akifanya hivyo baada ya kuingia wakati wa kila swala ya faradhi, na


 atafanya hivyo hivyo atakapokuwa anataka kuswali swala za suna zisizokuwa faradhi.


 Na katika hali kama hii, na kutokana na tabu anazopitia, itakuwa inajuzu kwake kukusanya swala ya


 Adhuhuri na Laasiri, na swala ya Magharibi na Ishaa: kwa kufanya kwake hivi ataswali swala mbili kwa


 mara moja; Yaani swala ya Adhuhuri na Alasiri.Na twahara moja pia kwa ajili ya swala mbili: Yaani swala


 ya Magharibi na Ishaa, na Alfajiri itakuwa pekee. Hivyo basi badala ya kuswali mara tano ataswali mara


 tatu tu.


 Na hapa nitarudia maelezo mara ya pili, ninasema: Pindi atakapotaka kujitwaharisha ataosha tupu yake,


 na ataifunga kwa kitambaa au mfano wa kitambaa, ili ipungue ile hali ya kutoka damu. Kisha atatawadha,


 na ataswali Adhuhuri rakaa nne na Alasiri rakaa nne. Na Magharibi rakaa tatu na Ishaa rakaa nne, na


 Alfajiri rakaa mbili. Kwa maana kwamba asipunguze rakaa hizo. Kama wanavyodhania baadhi ya watu


 wasiokuwa na elimu na maarifa.Lakini inajuzu kwake kukusanya kati ya swala ya Adhuhuri na Alasiri, na


 kati ya swala ya Magharibi na Ishaa, ima kwa kutanguliza au kwa kuchelewesha, na ikiwa atataka kuswali


 swala ya sunna kwa udhu huo huo aliyoswalia swala hizo za faradhi, hapana ubaya wa kufanya hivyo.


 swali la 34:Nini hukumu ya mwanamke kukaa katika msikiti mtukufu wa Makka au msikiti wa Madina, na


 hali akiwa na hedhi; kwa nia ya kusikiliza mafunzo ya hadithi za Mtume rehema na amani za Allah


 zimfikie, na kusikiliza hotuba?


 Jawabu la swali la 34:Haijuzu kwa mwanamke mwenye hedhi kukaa ndani ya msikiti wa Makka au msikiti


 mwingine wowote. Lakini inajuzu kwake kupita na kukatisha ndani ya msikiti kwa nia ya kutimiza haja


 yake humo, na mfano wa hilo;Kama alivyosema Mtume rehema na amani za Allah zimfikie,


 alipomuamrisha mama Aisha alete Msala, mama Aisha akasema: Msala uko msikitini na mimi nina hedhi.


 Mtume wa Allah rehema na amani zimfikie akasema "Hedhi yako haiko mkononi mwako",Na ikiwa


 mwanamke mwenye hedhi atakatisha msikitini, na hali ya kuwa damu yake haichuruziki ndani ya msikiti,


 basi hapana ubaya wowote juu yake.1


 Ama ikiwa mwanamke huyo anataka tu kukaa msikitini hilo halitajuzu kisheria.


 Na dalili ya hilo: Ni kuwa Mtume rehema na amani za Allah zimfikie aliwaamrisha wanawake kutoka


 katika swala ya iddi ili kuhudhuria mahala pa tukio la swala ya iddi (wanawake walioachwa huru kutokana


 na utumwa na mabinti wanaotawa na wanawake wenye hedhi) isipokuwa tu ameamrisha wenye hedhi


 wajitenge na mahala pa kuswalia.Hivyo hilo linajulisha kuwa mwanamke mwenye hedhi haijuzu kwake


 kukaa msikitini kwa nia ya kusikiliza hotuba au kusikiliza darasa na hadithi.


 *


 MIONGONI MWAHUKUMUZATWAHARAKATIKASWALA:


 Swali la 35:Je kinachotoka kwa kuchuruzika toka kwa mwanamke (katika sehemu zake za siri)- kikiwa ni


 rangi nyeupe au ya njano- ni najisi au tohara? je unawajibika udhuu kwa hicho kinachotoka? pamoja na


 kujuwa na kutambua kwamba kinaendelea kutoka bila kukatika, na ipi hukumu ikiwa kitaacha kutoka?


 hususani ni kwamba wengi katika wanawake wasomi wanazingatia kile kinachotoka ni unyevunyevu wa


 kawaida na wa asili, hailazimiki kuchukua Udhu?


 Jawabu la swali la 35:Kinachodhihiri kwangu baada ya utafiti ni kuwa: Kinachochuruzika kutoka kwa


 mwanamke ikiwa hakitoki kwenye kibofu basi kinatoka katika mfuko wa uzazi na kitakuwa ni twahara.


 Lakini kinatengua udhu pamoja na kuwa ni twahara: Kwa sababu kitu kinachotengua udhu si sharti kiwe


 najisi, kwani huoni upepo unaotoka sehemu ya nyuma hauna umbo, lakini pamoja na hivyo unatengua


 udhu.


 Na kwa ajili hiyo tu, ikiwa damu hiyo itamtoka mwanamke na hali akiwa na udhu basi damu hiyo itatengua


 udhu wake, na itamuwajibikia kutawadha udhu mpya.


 Na ikiwa damu hiyo inaendelea kutoka haitatengua udhu wake, lakini atatawadha kwa ajili ya swala pindi


 utakapoingia muda wake. Na kwa udhu huo huo ataswali swala ya sunna na atasoma Qur'ani, na


 atafanya lolote katika mambo ya halali kwake.Na hivi ni kama walivyosema wasomi kuhusu mtu mwenye


 1 Neno "Khumra" lililotumika katika hadithi: Ni Mswala unaotumika kuswalia. Na Mswala huo umeitwa


 hivyo kwa sababu unafunika uso.


ugonjwa wa kutokwa na mkojo mfululizo, hii ndiyo hukumu ya mwenye kutokwa na damu katika kadhia ya


 twahara, anakuwa twahara, na katika swala la kutenguka udhu wake, mkojo huo unatengua udhu ila tu


 ikiwa unatoka mfululizo wakati huo hautatengua udhu. Lakini mwanamke hatatawadha kwa ajili ya swala


 ila baada ya kuingia muda, na awe muangalifu.


 Ama ikiwa damu hiyo inakatika, na ikawa desturi yake ni kukatika katika nyakati za swala, basi


 ataahirisha swala mpaka wakati ambao damu inakatika, madhali tu hahofii kupitwa na kipindi cha swala.


 Ikiwa atahofia kupitwa na kipindi cha swala basi itambidi atawadhe na atajifunga na kujihifadhi na kuswali.


 Na hapana tofauti kati ya damu ndogo na damu nyingi; Kwa sababu zote hizo zinatokea katika njia moja;


 hivyo basi ikiwa ni nyingi au kidogo zote hizo zinatengua udhu. Hii ni tofauti na damu inayotoka katika


 maeneo mengine ya mwili kama damu au matapishi, vitu hivyo havitengui udhu vikiwa kidogo au vikiwa


 vingi.


 Ama itikadi ya baadhi ya wanawake kuhusu damu hiyo kwamba haitengui udhu hili mimi sijui linatokana


 na asili ipi, isipokuwa kauli ya Ibn Hazmi Allah amrehemu yeye anasema: Damu hii haitengui udhu, lakini


 hakuleta dalili yoyote juu ya kauli yake hii na lau angetaja dalili yoyote kutoka katika kitabu na sunna na


 kauli za Maswahaba hiyo ingelikuwa ni hoja.


 Na ni juu ya mwanamke kumcha Allah na apupie kujitwaharisha; kwa sababu swala haikubaliwi bila ya


 twahara, japo ataswali mara mia. Kwani baadhi ya wanachuoni wanasema: Mtu anayeswali bila ya


 twahara anafanya kufuru; kwa sababu kufanya hivyo ni kuzifanyia kejeli aya za Allah-Aliyetakasika na


 Kutukuka.


 Swali la 36:Atakapo tawadha mwanamke ambaye anatokwa na kinachomtoka katika sehemu zake za siri


 bila kukatika kwa ajili ya swala ya lazima, je ni sahihi kwake yeye akaswali swala za sunna anazotaka na


 kusoma Qur'ani kwa ule udhu aliouchukua kwa ajili ya ile swala ya lazima mpaka swala ya lazima


 nyingine inayofuata?


 Jawabu la 36:Atakapo chukua udhu mwanamke kwa ajili ya swala ya lazima katika mwanzo wa wakati


 wake basi ni juu yake akaswali swala za sunna anazotaka na kusoma Qur'ani mpaka utakapo ingia


 wakati wa swala nyingine.


 Swali la 37:Je ni sahihi kwa huyo mwanamke kuswali swala ya dhuha kwa udhu wa swala ya Al fajiri?


 Jawabu la 37:Hilo si sahihi, kwa sababu swala ya dhuha ni swala ya wakati maalumu, ni lazima kuchukua


 udhu kwa ajili ya swala ya dhuha ukiingia wakati wake, kwa sababu huyu mwanamke ni mfano wa yule


 mwanamke anayetokwa na damu ya ugonjwa, na alimuamrisha Nabii-rehema na amani ziwe juu yake


mwanamke anayetokwa na damu ya ugonjwa achukue Udhu kwa kila swala (anayotaka kuswali).


 Na wakati wa swala ya Adhuhuri: Ni toka kupinduka kwa jua (kuelekea Magharibi) mpaka wakati wa


 swala ya Alasiri.


 Na wakati wa swala ya Alasiri: Ni toka wakati wa kutoka swala ya Adhuhuri mpaka jua likiwa la njano, (na


 wakati wa) dharura(kwa ajili ya swala ya Lasiri) ni mpaka kuzama kwa jua.


 Na wakati wa Magharibi: Ni toka kuzama kwa jua mpaka kupotea kwa wekundu unaotokea angani wakati


 wa kuzama kwa jua.


 Na wakati wa swala ya Ishaa: Ni kutoka wakati umepotea ule wekundu unaotokea angani wakati wa


 kuzama kwa jua mpaka nusu ya usiku.


 Swali la 38:Je ni sahihi kwa huyu mwanamke kuswali kisimamo cha usiku itakapopita nusu ya usiku kwa


 udhu ule wa Ishaa?


 Jawabu la 38:Hapana, itakapopita nusu ya usiku inawajibika kwa mwanamke huyu kuchukua Udhu tena,


 na pamesemwa kuwa: Sio lazima kuchukua udhu mpya na hii ndio kauli yenye nguvu yenye kufanyiwa


 kazi.


 Swali la 39:Ni upi muda wa mwisho wa swala ya Ishaa, na vipi utautambua?.


 Jawabu la 39:Wakati wa mwisho wa swala ya Ishaa ni nusu ya usiku, na hilo hutambuliwa kwa kugawa


 baina ya kuzama kwa jua na kuchomoza alfajiri mara mbili, nusu ya kwanza inaisha muda wa mwisho wa


 swala ya Ishaa, na inabakia nusu ya mwisho haina wakati bali ni kizuizi baina ya Ishaa na Alfajiri.


 Swali la 40:Atakapo chukua udhu mwanamke anayetokwa na chenye kutoka kwa kukatikakatika (hakitoki


 mfululizo sehemu za siri) na baada ya kumaliza kuchukua udhu na kabla ya swala yake, kikatoka mara


 nyingine, nini afanye mwanamke huyu?


 Jawabu la 40:Ikiwa kile kinachotoka kiliacha kutoka basi asubiri mpaka ule muda ambao kinaacha kutoka,


 ama ikiwa hana hali inayofahamika, muda wa kutoka na muda wa kuacha kutoka, basi atachukua udhu


 baada ya kuingia wakati wa swala, ataswali, na halazimiki juu yake chochote.


 Swali la 41:Kipi kinalazimu pindi hicho kinachotoka (sehemu za siri) kikigusa mwili au nguo?


 Jawabu la 41:Ikiwa kile kinachotoka ni tohara (kisafi) basi hakuna kinachomlazimu, na kikiwa ni


 najisi-nacho ni kile kinachotoka katika kibofu- basi inawajibika juu yake akoshe (mwili au nguo hizo)


Swali la 42:kuhusu udhu kutokana na kile chenye kutoka, je inatosha akaosha vile viungo vya udhu peke


 yake?


 Jawabu la 42:Ndio, inatosha hilo, ikiwa kinachotoka ni tohara, nacho ni kile kinachotoka katika mfuko wa


 uzazi na sio kinachotoka katika kibofu.


 Swali la 43:Ni ipi sababu ya kutonukuliwa kutoka kwa Mtume- Rehema na amani ziwe juu yake- hadithi


 yoyote yenye kuonyesha juu ya kutenguka kwa udhu kwa kile kinachotoka, pamoja na kwamba


 Maswahaba wa kike walikuwa wakipupia juu ya kutaka kujua mambo katika dini yao?


 Jawabu la 43:Kwa sababu kinachotoka hakimjii kila mwanamke.


 Swali la 44:Yule mwanamke ambaye alikuwa hachukui udhu kwa kutokujua hukumu yake, anawajibika


 nini juu yake mwanamke huyo?


 Jawabu la 44:Juu yake mwanamke huyo ni kutubu kwa Allah (Mshindi aliyetukuka) na awaulize


 wanazuoni juu ya hilo.


 Swali la 45:kuna wanao nasibisha kwako kauli ya kutochukua udhu kwa kutoka kile chenye kutoka


 (sehemu za siri)?


 Swali la 45:Mwenye kuninasibishia kauli hii sio mkweli, jambo linalodhihiri ni kwamba yeye kafahamu


 kutoka katika kauli yangu: Kwamba hakitengui Udhu.


 Swali la 46:Ni ipi hukumu ya uchafu unaomtoka mwanamke kabla ya hedhi kwa siku moja au zaidi au


 chini ya hapo, na kinaweza kuwa chenye kutoka kikawa mfano wa uzi laini mweusi au kahawia au mfano


 wa hiyo? Ni ipi hukumu lau ikiwa baada ya hedhi?


 Jawabu la 46:Hiyo ikiwa ni mwanzo wa hedhi basi hiyo ni hedhi, na hutambuliwa hilo kwa maumivu


 ambayo yanamkuta aliye na hedhi kwa kawaida.


 Ama uchafu baada ya hedhi, atasubiri mpaka uondoke; kwa sababu uchafu unaoungana na hedhi nao ni


 hedhi; kutokana na kauli ya Aisha- Radhi za Allah ziwe juu yake: Msifanye haraka mpaka muone tohara


 baada ya hedhi. Na Allah ndiye Mjuzi zaidi.


 *


 MIONGONI MWAHUKUMUZAHEDHIKATIKAHIJANA


 UMRA:


 Swali la 47:Vipi anaswali mwanamke anayetokwa na damu ya hedhi rakaa mbili za baada ya kuhirimia?


 Na je inafaa kwa mwanamke mwenye hedhi kusoma na kurudia rudia Adhkari katika nafsi yake? au


 haifai?


 Jawabu la 47Jambo la kwanza: Tunapaswa kujua kwamba Ihram (Nia ya kuanza Hija au Umra) haina


 swala yoyote; kwa sababu haikuja kutoka kwa Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake- kwamba


 ameweka sheria kwa umma wake kuwe na swala maalum kwa ajili ya Ihram, si kwa kauli yake, au


 kitendo chake, au kufanyika kitu mbele yake akakipitisha.


 Jambo la pili: Mwanamke huyu mwenye hedhi ambaye ameingia katika hedhi kabla hajahirimia, anaweza


 kuhirimia akiwa katika hedhi.Kwa sababu Mtume- Rehema na amani ziwe juu yake-alimuamrisha Asmaa


 bint Umeysi, mke wa Abubakari-Radhi za Allah ziwe juu yao- pindi alipopata damu ya nifasi katika eneo


 la Dhul Hulayfah, akamuamrisha akoge na aweke nguo sehemu inayotoka damu, na ahirimie, na hivi pia


 anafanya mwanamke mwenye hedhi, anabakia katika ibada yake aliyohirimia mpaka atoharike, kisha


 azunguke nyumba ya Allah na azunguke Swafah na Marwah.


 Na ama kauli yake katika swali: Je anaweza kusoma Qur'ani? Basi jawabu ni ndio, na mwanamke


 mwenye hedhi anaruhusiwa kusoma Qur'ani akiwa na haja au akiona kuna masilahi juu ya hilo, ama


 kama hakuna haja wala masilahi, bali anasoma tu kama ibada na kujikurubisha kwa Allah, lililo bora


 asisome.


 Swali la 48:Amesafiri mwanamke kwenda katika Hijja, na akajiwa na mzunguko wa mwezi (Hedhi), toka


 siku tano kabla ya safari yake, lakini baada ya kufika katika sehemu ya kuhirimia, akaoga na akaingia


 katika ibada ya Hijja kwa kuhirimia, lakini yeye hajatoharika na mzunguko wake wa hedhi, alipofika katika


 mji wa Makka akabakia nje ya eneo tukufu, hakufanya chochote katika metendo matukufu ya Hijja na


 Umra, na akakaa siku mbili katika mji wa Minah, kisha akatoharika, akajitoharisha kwa kukoga, na


 akatekeleza matendo yote ya Umrah akiwa ametoharika, kisha ikamrudia damu akiwa katika Twawaf ya


 Hijja (kuzunguka Al-Kaaba kwa ajili ya Hijja) isipokuwa aliona haya na akakamilisha matendo ya Hija,


 hakumwambia msimamizi wake mpaka baada ya kufika katika mji wake, ni ipi hukumu ya hilo?


 Jawabu la 48:Hukumu ya hilo: Damu iliyompata wakati anazunguka Al-Kaaba wakati wa Hijja, ikiwa ni


 damu ya hedhi ambayo anaijua kwa ile kawaida yake na ugonjwa wake basi hakika kule kuzunguka


 kwake Kaaba kwa ajili ya Hija (Twawaful ifadha) hakuko sahihi, inamlazimu arudi katika mji wa Makka; ili


 aweze kutufu twawaful Ifadha (kuzinguka Kaaba kwa ajili ya Hijja), ahirimie kufanya ibada ya Umra katika


maeneo ya kuhirimia kisha atekeleze ibada ya Umrah kwa kutufu (Kuzunguka Kaaba) na kuzunguka


 swafah na Marwah na apunguze nywele kisha ndio atufu twawaful Ifadha (kuzunguka Kaaba kwa ajili ya


 Hijja)


 Ama ikiwa hii damu sio damu ya hedhi, ni damu ya kawaida inayojulikana, bali imetokana na


 msongamano mkubwa au hofu na yanayofanana na hayo, basi kuzunguka kwake kuko sahihi kwa wale


 wanaoshurutisha twahara (katika wanazuoni) mtu akiwa anazunguka Kaaba.


 Ikiwa ameshindwa kurudi, katika swala la mwanzo, kiasi kwamba yuko katika miji ya mbali, basi Hijja


 yake ni sahihi, kwa sababu hana uwezo wa kufanya zaidi ya vile alivyofanya.


 Swali la 49:Amefika mwanamke amehirimia kwa ajili ya Umra, na alipofika katika mji wa Makka akapata


 hedhi, na msimaizi wake analazimika kusafiri kwa haraka, na hana msimamizi mwingine katika mji wa


 Makka, ni ipi hukumu yake?


 Jawabu la 49:Atasafiri pamoja naye, na atabakia katika ibada yake akiwa amehirimia, kisha atarejea


 akitoharika, na hili ikiwa atakuwa Saudia; kwa sababu kurejea akiwa hapo ni jambo jepesi, na wala halina


 tabu ndani yake jambo hilo, hahitaji hati za kusafiria na mengineyo.


 Ama akiwa anatoka nje ya Saudia, na ni tabu kwake kurudi, basi atajihifadhi, atazunguka Al-Kaaba,


 atazunguka Swafah na Marwah na amalize ibada yake ya Umrah katika safari hiyo hiyo, kwa sababu


 kuzunguka kwake Kaaba wakati huo ni dharura, na dharura huruhusu mambo yaliyokatazwa.


 Swali la 50:Ni ipi hukumu ya mwanamke wa kiislamu ambaye amepatwa na damu ya hedhi katika siku za


 Hijja, je ile Hijja itamtosheleza (Itakubalika)?


 Jawabu la 59:Hili haliwezekani kulijibu mpaka ijulikane ni muda gani huyu mwanamke kapatwa na damu


 ya hedhi, na hilo ni kwa sababu baadhi ya matendo ya Hijja hayazuiliwi na hedhi kufanyika, na mengine


 yanazuiliwa, mfano: Kuzunguka Kaaba, hawezi kuzunguka mpaka awe na udhu (Tohara), na mengine


 katika matendo ya Hijja anaweza kuyafanya akiwa na hedhi.


 Swali la 51:Nilikuja kufanya Hija yangu ya lazima mwaka jana, nilifanya matukio yote ya Hija isipokuwa


 Twawaful Ifadha (kuzunguka Kaaba kwa ajili ya Hijja) na Twawaful wadaa (Kuzunguka kaaba kwa ajili ya


 kuaga), nilizuiwa na udhuru wa kisheria, nikarudi nyumbani kwangu katika mji wa Madina nikiazimia


 kurudi siku katika masiku ili nizunguke Kaaba mizunguko niliyoiacha, kutokana na mimi kutojuwa mambo


 ya dini, nimehalalika na kila kitu, nimefanya mambo yote ambayo nakatazwa katika ihraam, nikaulizia


 kurudi ili nizunguke Kaaba nikaambiwa: Hauwezi tena kurudi, kwani tayari umeharibu ibada yako,


 inakulazimu kurudia Hija mara nyingine mwaka unaokuja, pamoja na kuchinja Ngamia au Ng'ombe, je


 fatwa hii ni sahihi? Je kuna njia nyingine, ni ipi hiyo, na je Hija yangu imeharibika? Na je natakiwa


 kurudia? Nipe faida kwa yale ninayotakiwa kuyafanya, Allah awabariki.


 Jawabu la 51:Na hili pia ni katika balaa, kutolewe Fatwa bila ya elimu, na wewe katika hali hiyo


 unawajibika kurudi katika mji wa Makka, na ukatufu Twawaful ifadha pekee (Kuzunguka Kaaba kwa ajili


 ya Hijja).


 Ama kuzunguka Al-Kaaba kwa lengo la kuaga (Twawaful Wadaa) hulazimiki kufanya hivyo madamu


 ulikuwa na hedhi wakati unatoka katika mji wa Makka, kwa sababu mwenye hedhi halazimiki kufanya


 mzunguko huo;kutokana na hadithi ya bin Abbas-Radhi za Allah ziwe juu yao- Aliwaamrisha watu jambo


 lao la mwisho katika ibada ya Hija liwe ni kuzunguka Kaaba, isipokuwa aliwafanyia wepesi waliopatwa na


 hedhi.Na katika Riwaya ya Abu Daudi: Jambo lao la mwisho katika ibada ya Hija liwe ni kuzunguka


 Kaaba.Na ni kwa sababu Mtume-Rehema na amani ziwe juu yake- alipo ambiwa kwamba Swafiya


 ametufu (amezunguka Kaaba kwa mzunguko wa Hijja) basi akasema: (Na arudi basi).Imeonesha hadithi


 hiyo kwamba mzunguko wa Kaaba kwa kuiaga Kaaba unadondoka kwa mwanamke mwenye hedhi.


 286


 :ةرﻘﺑﻟا]


 Ama mzunguko wa Kaaba kwa ajili Hijja huo ni lazima, na kwa kuwa amehalalika na kila kitu kwa kutojua,


 hilo halimdhuru kitu, kwa sababu asiyejua anapofanya katazo katika makatazo ya Ihiramu, hana


 dhambi.


 



Machapisho ya hivi karibuni

MASWALI SITINI KATIKA ...

MASWALI SITINI KATIKA HUKUMU ZA HEDHI NA NIFASI

Muhutasari wenye fai ...

Muhutasari wenye faida kwa muislamu mpya