Nakala




 


NDOTO NJEMA


Sifa za ukamilifu zote ni za Allah, tunamhimidi, tunamuomba 


msaada, tunamuomba msamaha, na tunajilinda na Allah kutokana 


na shari za nafsi zetu, na kutokana na amali zetu mbovu, yule 


ataongozwa na Allah, basi hakuna wa kumpoteza, na 


atakayempoteza hakuna wa kumuongoza, nashuhudia ya kwamba 


hapana apasaye kuabudiwa ila Allah peke yake, hana mshirika, na 


nashuhudia kuwa Nabii wetu Muhammad ni mja wake na mtume 


wake, swala na salamu za Allah nyingi zimshukie yeye, watu wake, 


na masahaba wake. 


(Ammaa ba'd) Ama baada ya himdi hii: 


Mcheni Allah - enyi waja wa Allah - kama ipasavyo kumcha, 


na mchungeni [chungeni amri zake na makatazo yake] katika siri 


na minong'ono. 


[Ayyuhal muslimuun] Enyi Waislamu: 


Allah amewatimizia waja wake neema za dhahiri na za batini, 


kaika hali ya kuwa macho kwao na kulala kwao, Naye aliyetakasika 


anapelekesha mambo usiku na mchana; na Allah kwa hekima yake 


ameficha elimu ya ghaibu kwa viumbe, na hakuna njia ya kujua 


ghaibu isipokuwa kile ambacho Allah anawajulisha Mitume wake 


(yaani isipokuwa kile ambacho Allah aliwaambia Mitume wake), 


[Allah] aliyetakasika amesema: 





{Yeye ndiye mjuzi wa ghaibu, wala hamdhihirishii yeyote 


 


  )1( [Hotuba hii] imetolewa siku ya ijumaa, tarehe kumi na sita  ya mwezi wa Safar, mwaka wa elfu moja mia 


nne na arobaini na tano hijria, katika Masjid An-Nabawi.  


NDOTO NJEMA   2 


alqasim.com-a 


ghaibu yake * isipokuwa Mtume aliyemridhia, basi hakika 


humwekea huyo walinzi mbele yake na nyuma yake} [Al-Jinn: 27] 


Na miongoni mwa neema za ndani za Allah na maajabu ya 


uumbaji wake mzuri; ni kwamba amewaachia sehemu ya Unabii ili 


kupata kujua baadhi ya ghaibu, [Allah] huwajulisha anaowataka 


katika waja wake ndani ya usingizi wao, amesema Nabii swala na 


salamu za Allah zimshukie: (Hakuna kilichobakia katika Unabii 


isipokuwa yenye kubashiria. Waliuliza: Na yenye kubashiria ni 


nini? Akasema: Ndoto nzuri.) [Imepokelewa na Bukhari], kwa 


hivyo, katika ndoto nzuri kuna maarifa ya ajabu ya Allah na fadhila 


zake ambazo humfanya muumini azidi katika imani yake, kwani 


inamjulisha yaliopita, ya wakati ulio na mustakabali, jambo lenye 


kumkomboa kutokana na uoga wa waganga na mfano wao, na mnao 


ndani yake [ndoto njema] msisitizo (yaani motisha) wa kufanya 


mema, kuonya dhidi ya uovu, na habari njema na onyo. 


Inayo ndoto cheo adhimu katika sheria ya Kiislamu, kwani 


ipamoja na Manabii katika mitihani na matukio magumu mno, nayo 


ni ufunuo [wahyi] kwao peke yao, Ibrahim alimwambia Ismail, 


Amani iwe juu yao: 





{Ewe mwanangu, hakika mimi naona usingizini kuwa 


nakuchinja} [As-Saffat:102]. 


Allah aliinua hadhi ya Ibrahim kwa kuisadikisha ndoto na kutii 


amri ya Mola wake, akamwachia sifa ya kweli kizazi baada ya 


kizazi, Allah Mtukufu amesema: 





{Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye * salamu 


kwa Ibrahim (kutoka kwa mola wake) * hivyo ndivyo 


tunavyowalipa wafanyao mema} [As-Saffat:108-110]. 


Maisha ya Yusuf salamu zimshukie yalianza na ndoto: 


NDOTO NJEMA   3 


a-alqasim.com 


 


{Ewe babangu! Hakika mimi nimeota nyota kumi na moja, jua na 


mwezi, nimeota zinanisujudia} [Yusuf:4], Ikatimia ndoto yake kwa 


kupata izza kwake na cheo. 


 


{Na akawapandisha wazazi wake juu ya kiti cha enzi, na wote 


wakaporomoka kumsujudia} [Yusuf:100]. 


Heri ya kwanza na nuru ya umma huu ilikuwa kupitia ndoto; 


Aisha, Allah amridhie, alisema: (Ilikuwa mwanzo wa ufunuo kwa 


Mtume wa Allah swala na salamu za Allah zimshukie ni: ndoto ya 


kweli katika usingizi, na hakuona ndoto isipokuwa ilikuja kama 


mwanzo wa alfajiri) [wameafikiana Bukhari na Muslim kuipokea]. 


Katika vita vya Badr, Allah alimuonyesha Nabii wake ushindi 


katika ndoto, [Mtume] akawahadithia Masahaba zake ndoto hiyo, 


basi nyoyo zao zikazidi nduvu, na wakawa wajasiri katika kupigana 


na adui wao Pamoja na uchache wao: 





{Kumbuka (ewe Nabii) pindi Allah alipokuonyesha uchache wa 


maadui zako ukiwa usingizini, na kama angelikuonyesha wingi wa 


maadui zako mngeliingiwa na uoga, na mngelizozana kuhusu 


kupigana, lakini Allah aliepusha (jambo hilo)} [Al-Anfal:43]. 


Allah alimuonyesha Nabii wake ndotoni ushindi wa Makkah 


akiwa Madina, basi ikawa habari njema kwao: 





{Hakika Allah alimtimizia Mtume wake ndoto kwa haki, bila 


4


 NDOTO NJEMA


 shaka mutaingia Msikiti mtakatifu in shaa Allah mkiwa na amani, 


hali mmenyoa vichwa vyenu na mmepunguza. Hamtakuwa na 


hofu} [Al-Fath:27], basi Allah akawafutahia [Makkah] baada yam 


waka mmoja. 


Na Nabii swala na salamu za Allah zimshukie akiona ndoto 


huwasimulia Masahaba zake; bali alikuwa anapomaliza kuswali 


alfajiri huwakabili masahaba zake kwa uso wake na kuwauliza: (Je, 


kuna yeyote kati yenu aliyeona ndoto jana usiku?) [wameafikiana 


Bukhari na Muslim kuipokea]. 


Asili ya kuekwa adhana ni Nabii kuikiri kwa Nabii swala na 


salamu za Allah zimshukie ndoto aliyoiona sahaba Abdullah ibnu 


Zaid Allah amridhie, alisema: "Nilipoingiliwa na asubuhi 


nilimwendea Mtume wa Allah swala na salamu za Allah zimshukie 


na nikamhadithia nilichoona. Basi akasema: (Hakika hiyo ni ndoto 


ya haki in shaa Allah. Nenda na Bilal, umhadithie kile ulichoona, 


ili aadhini [kwa maneno hayo]) [imepokewa na Ahmad]. Ibn 


Abdul-Barr alisema: "Imamu wa waongofu, katika masahaba, 


tabi'ina, na waliokuja baada yao miongoni mwa wanazuoni wa 


waislamu wa madhehebu ya Ahlu Ssunnah wal Jama'a 


wamekubaliana juu ya kuiamini [ndoto hii]". 


Na ndoto zimegawanyika vigawanyo vitatu; moja yazo ni haki 


hapana budi itokee, na mbili [zilizosalia] ima zinatoka kwa Shetani, 


ima ni mchangamaniko wa ndoto zisizo na uhakika. Nabii swala na 


salamu za Allah zimshukie amesema: (Ndoto ni aina tatu: Ndoto 


nzuri ni bishara kutoka kwa Allah, ndoto ya huzuni ni kutoka kwa 


Shetani, na ndoto ya kutokana na yale mtu anayojihadithia nafsi 


yake) [imepokewa na Muslim]. 


Ndoto njema humfurahisha muumini wala haimghuri, nayo ni 


sehemu katika Unabii. [Mtume] swala na salamu za Allah 


zimshukie amesema: (Ndoto ya muumini ni sehemu katika sehemu 


arobaini na sita za Unabii) [wameafikiana Bukhari na Musllim 


kuipokea], nayo ni mojawapo wa yenye kubashiria yaliosalia baada 


ya Unabii. Nabii swala na salamu za Allah zimshukie aliulizwa 


a


alqasim.com


NDOTO NJEMA   





kuhusu kauli yake Allah aliyetukuka: 





 {wanao bishara katika Maisha ya duniani na Akhera} [Yunus: 64] 


Akasema: (Hiyo ni ndoto njema muislamu huiona au ionekane 


na wengine) [imepokewa na Ahmad]. 


Na ndoto ya kweli ni sehemu katika Unabii, na Unabii ni ufunuo 


[Wahyi], na mwenye kusema uongo katika usingizi wake huwa 


amemsemea uongo Allah kwamba amemwonyesha kile ambacho 


hakuona. [Mtume] swala na salamu za Allah zimshukie alisema: 


(Hakika katika uongo mkubwa ni kuyaonyesha macho yake kile 


ambacho hayakukiona) [imepokewa na Bukhari], na siku ya 


Kiyama ataamrishwa kitu ambacho hana uwezo wa kukifanya ili 


kuzidisha adhabu, Nabii swala na salamu za Allah zimshukie 


alisema: (Atakayedai ndoto ambayo hakuiona; ataamrishwa azipige 


fundo tembe mbili za ngano, na hataweza kufanya hilo), 


[imepokewa na Bukhari]. 


Nayo [ndoto njema] ingawa aghalabu ni mahususi kwa watu 


wema, ila inaweza kutokea kwa wengineo; kwani Yusuf salamu 


zimshukie alifasiri ndoto ya wenzake wa gerezani ikatokea kama 


alivyoifasiri, na akafasiri ndoto ya mfalme kafiri ya ng’ombe saba 


na ikawa kweli. Bukhari amesema katika kitabu chake cha 'swahih': 


“[Huu ni] Mlango wa ndoto za wafungwa, waovu na washirikina”, 


na Ibn Hazm Allah amrehemu amesema: “Na ndoto ya kafiri 


inaweza kuwa kweli, na wakati huo haitakuwa sehemu katika 


Unabii, wala si miongoni mwa yenye kubashiria, lakini ni onyo 


kwake na kwa wengine na ni mawaidha”. 


Na ndoto ya mchana ni ya haki kama ndoto ya usiku. 


Nabii swala na salamu za Allah zimshukie alimtembelea Ummu 


Haraam binti Milhaan Allah amridhie akalala kwake wakati wa 


mchana, basi akaona ndoto, na akamsimulia [wameafikiana 


Bukhari na Muslim kuipokea].  


a-alqasim.com 


NDOTO NJEMA   6 


alqasim.com-a 


Inapendekezwa kwa mwenye kuona ndoto anayoipenda 


kumhimidi Allah kwa ndoto hiyo, aifurahikie, na amsimulie mtu 


anayempenda, ama hasidi na mwenye vitimbi basi asimsimulie, 


kama alivyosema Yakub salamu zimshukie: 





{Akasema: ewe mwanangu! Usiwasimulie ndugu zako ndoto 


yako, wasije wakapanga njama dhidi yako} [Yusuf: 5] 


Na atakayeona ndoto anayoichukia ni sunnah kwake kujikinga 


na Allah kutokana na shari yake, na shari ya shetani, ateme 


kushotoni mwake mara tatu, ageuke kutoka upande aliokuwa 


amelala, asimsimulie ndoto hiyo yeyote, na asimame aswali, An


Nawawiy Allah amrehemu amesema: "na akitosheka kufanya 


baadhi yake [haya yaliotangulia], yatamtosheleza kukinga shari 


yake [ndoto hiyo] kwa idhini ya Allah aliyetukuka kama hadithi 


zilivyoweka wazi hilo." 


Kutafsiri ndoto ni mojawapo ya elimu za Manabii na watu wa 


imani, nayo ni elimu adimu inayochanganya baina ya kipawa na 


ujuzi unaochumwa, na ni neema ambayo Allah humpa amtakaye. 


[Allah] anasema akielezea kuhusu Yusuf salamu zimshukie: 





{Na ili tumfundishe kufasiri ndoto} [Yusuf: 21] 


Tafsiri ya ndoto ni fatwa, nayo haijuzu kwa mtu yeyote 


kujiingiza ndani yake bila elimu, Yusuf salamu zimshukie 


aliwaambia wale vijana wawili: 





{limekwisha amuliwa jambo ambalo mnataka fatwa kulihusu}, 


na Mfalme alisema: 





NDOTO NJEMA   





{Nipeni fatwa katika ndoto yangu} [Yusuf: 43]. 


na yule Kijana alimwambia Yusufu: 





 {Nipe fatwa katika [ndoto ya] ng'ombe saba} [Yusuf: 46].  


Nayo [tafsiri ya ndoto] inategemea kiasi na kufananisha, na 


kuzingatia mambo ya kiakili kwa kutegemea yale ya kihisia. Ibnul 


Qayyim Allah amrehemu amesema: "Mifano yote ya Qur'ani ni 


misingi na kanuni za elimu ya kutafsiri ndoto kwa yule anayeielewa 


vizuri kuitolea hoja. Vivyo hivyo, yule anayeelewa Qur'ani ana 


uwezo wa kutafsiri ndoto kwa njia bora zaidi, na misingi sahihi ya 


tafsiri ya ndoto imechukuliwa katika shubaka la Qur'ani". 


Mtu yeyote anayetaka kutafsiri ndoto yake asiitafsiri isipokuwa 


kwa mtaalamu wa kufasiri ndoto, kwani si kila anayejitokeza 


anaweza kutafsiri vizuri, wala aliyetosheka na vitabu vya ndoto, ni 


mfasiri, kwani inayo [ndoto] hali tofauti kulingana tofauti za watu, 


wakati na sehemu; [imamu] Malik Allah amrehemu aliulizwa: "Je, 


kila mtu anaweza kutafsiri ndoto?" Akajibu: "Je, Unabii 


huchezewa?!" 


Yule aliyepewa na Allah uzuri wa kutafsiri ndoto inamlazimu 


kuwa na uchaji Allah, ajiepushe na riya na kupenda kutangaa, 


amuombe Mola wake msaada na kusibu, ajihadhari na majivuno 


kwani yanapoteza neema, na amshukuru Allah kwa neema hii. 


Yusuf salamu zimshukie alishukuru neema za Allah kwa kusema: 





 {Ewe Mola wangu! Hakika umenipa ufalme na umenifunza 


tafsiri ya ndoto} [Yusuf: 101] 


Mufti, mfasiri ndoto, na daktari huona siri na aibu za watu 


ambazo wengine hawaoni. Kwa hivyo, ni lazima wawe ni wenye 


kusitiri yale yasiopendeza kudhihirishwa. 


Hapana budi ndoto ya kweli kutokea, iwe imetafsiriwa au la, 


a-alqasim.com 


8


 NDOTO NJEMA


 kwani Yakub alimwambia Yusuf salamu ziwashukie: 





 {Usisimulie ndoto yako} [Yusuf: 5], wala hakuitafsiri, lakini 


bado ilitokea.  


Hakika mfasiri anafichua uhakika wa maana ya ndoto, lakini 


anaweza kusibu na anaweza kukosea, Nabii swala na salamu za 


Allah zimshukie alimwambia Abu Bakr Allah amridhie baada ya 


kutafsiri kwake ndoto: (Umepata baadhi na umekosea baadhi) 


[wameafikiana Bukhari na Muslim kuipokea].  


Ama wakati wa kutokea kwake [ndoto] basi inaweza kutokea 


papo hapo, au inaweza kuchelewa kidogo au sana, Abdullah ibn 


Shaddaad Allah amrehemu amesema: "Ndoto ya Yusuf salamu 


zimshukie ilitokea baada ya miaka arobaini, na kufikia mda huo 


ndio upeo wa ndoto", na kila Muislamu anapaswa kujua ya kwamba 


kile ambacho Allah amemkadiria ni kheri kwake, sawa itokee kwa 


haraka au katika siku zijazo. 


[Wa ba'du, Ayyuhl muslimuun] Baada ya hayo, enyi 


Waislamu: 


Basi pindi zama za Unabii na athari zake zilipoisha; Allah 


aliwapa waislamu badala yake ndoto. Nabii swala na salamu za 


Allah zimshukie amesema: (Pindi Kiyama kitakapokurubia, ndoto 


ya muumini haitokosea) [wameafikiana Bukhari na Muslim 


kuipokea].  


Ama katika zama za nguvu ya nuru ya Unabii; basi mna katika 


kudhihiri kwa nuru yake na nguvu yake yenye kutosheleza kuhitajia 


ndoto. Mtu mwenye ndoto ya kweli zaidi ni aliye mkweli zaidi 


katika kuzungumza wakati yu macho, Nabii swala na salamu za 


Allah zimshukie amesama: (Mkweli wenu zaidi katika ndoto ni 


mkweli wenu zaidi katika kuzungumza) [imepokewa na Muslim]. 


Ibnu Hajar Allah amrehemu amesema: "Yule ambaye mara nyingi 


husema kweli wakati yumacho, atakuwa hivyo pia katika usingizi 


a


alqasim.com


NDOTO NJEMA   





wake, basi hataona isipokuwa ukweli, na hili ni kinyume na 


mwongo na mwenye kuchanganya; kwani moyo wake unaharibika 


na kuwa na giza, basi haoni [ndotoni] isipokuwa kuchanganyikiwa 


na ndoto za ovyo". 


Basi Jilazimishe ukweli katika mazungumzo, na shikamana na 


uchaji Allah; utafanikiwa kupata kheri za duniani na Akhera. 


[Audhu billahi mina sh-shaitwani rrwajiim] Najilinda na 


Allah kutokana na shetani aliyelaaniwa 





 {Na akawapandisha wazazi wake kwenye kiti cha enzi. Na wote 


wakaporomoka kumsujudia. Na akasema: Ewe baba yangu! Hii 


ndiyo tafsiri ya ile ndoto yangu ya zamani, Allah ameijaalia kuwa 


kweli} [Yūsuf: 100] 


Allah anibarikie mimi na nyinyi katika Qur-ani tukufu... 


a-alqasim.com 


10


 NDOTO NJEMA


 HOTUBA YA PILI 


Sifa njema zote astahili Allah kwa wema Wake [kwetu], na 


shukrani zote astahili Yeye kwa kutuafikia na kutuneemesha, na 


nashuhudia ya kwamba hakuna apasaye kuabudiwa ila Allah peke 


yake hana mshirika; ili kuadhimisha shani yake, na nashuhudia ya 


kwamba Nabii wetu Muhammad ni mja Wake [Allah] na Mtume 


wake, swala na salamu nyingi za Allah zimshukie yeye, watu wa 


nyumba yake na Masahaba wake. 


[Ayyuhal muslimuun] Enyi Waislamu! 


Dini imekamilika kwa kifo cha Nabii swala na salamu za Allah 


zimshukie, na ndoto njema haithibitishi chochote katika hukumu 


[za sheria], Ash-Shatibi Allah amrehemu amesema: "Faida yake - 


yaani: ndoto – ni kutoa tu habari njema au onyo, ama kutoa 


hukumu, basi hapana".  


Allah amemlinda Nabii wetu Muhammad swala na salamu za 


Allah zimshukie kutokamana na Shetani kujifananisha naye, basi 


aliyemuona katika ndoto, atakua amemuona kweli. Nabii swala na 


salamu za Allah zimshukie amesema: (Anayeniona katika ndoto, 


basi ameniona [kweli]. Kwani Shetani hawezi kujifananisha na sura 


yangu) [wameafikiana Bukhari na Muslim kuipokea], na 


atakayemuona Nabii katika ndoto haimaanishi kuwa ni mtu mwema 


kuliko wengine, na atakayemuona katika ndoto kwa sura 


isiyolingana na ile iliyotajwa katika Sunnah na Seera yake, au 


akamuona akimuamrisha batili, basi hizo ni ndoto za ovyo 


[zinazotokana na Shetani au mawazo ya mtu mwenyewe]. Na heri 


ipo katika kumfuata Nabii swala na salamu za Allah zimshukie. 


Kisha jueni kuwa Allah amewaamrisha kumswalia na 


kumsalimu Mtume wake... 


a


alqasim.com


NDOTO NJEMA   





a-alqasim.com 



Machapisho ya hivi karibuni

MASWALI SITINI KATIKA ...

MASWALI SITINI KATIKA HUKUMU ZA HEDHI NA NIFASI

Muhutasari wenye fai ...

Muhutasari wenye faida kwa muislamu mpya