Nakala

1


بسم الله الرحمن الرحيم


FAIDA YA KUTOA SADAKA


Imeandaliwa na Yunus Kanuni Ngenda


Imepitiwa na Yasin Twaha Hassani


Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote, na rehma na amani zimwendee Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na watu wake na Maswahaba wake wote. Amma baad: Hakika Mwenyezi Mungu anawalipa malipo makubwa wale wanaotoa sadaka kwa kutafuta radhi zake. Laiti mtoa sadaka angejua kwa yakini kwamba sadaka yake inapitia kwenye (mkono) wa Mwenyezi Mungu kabla ya kuingia mkononi mwa masikini, ingekuwa ladha ya mtoaji. ni kubwa kuliko ladha ya mpokeaji.. Ibun Alqayyim.


2


Je unajua faida ya kutoa sadaka?


Sikilizeni enyi watoa sadaka, wenye kutoa na ambao


wanasaidia kufikisha sadaka.


1- Sadaka ni mlango miongoni mwa milango ya pepo


2-Sadaka ni bora ya matendo mema, na sadaka bora ni kulisha


chakula


3- Sadaka inamfunika kivuli mtoaji na inamuondosha kwenye


moto


4-Sadaka inazima ghadhabu za Mola na joto la kaburi


5- Sadaka ni jambo bora la kumzawadia maiti na inamfaa


zaidi, na Mola anaitunza


6-Sadaka ni usafisho, na utakaso wa nafsi na huongeza mema


7- Sadaka ni sababu ya furaha kwa mtoa, na ni sababu ya


kung'ara uso wake siku ya kiama


8- Sadaka inaleta amani kutokana na hofu siku ya fazaa


kubwa, na humfanya mtoa sadaka asipatwe na huzuni


9- Sadaka ni sababu ya kughufiriwa dhambi na kusamehewa


makosa


10- Sadaka ni miongoni mwa bishara za mwisho mwema na


sababu ya dua ya Malaika


11- Mtoa sadaka ni mbora wa watu, na sadaka thawabu zake


ni kwa kila aliyeshiriki


12- Mwenye kutoa sadaka ameahidiwa kheri nyingi na ujira


mkubwa


13- Kutoa ni miongoni mwa sifa za wacha Mungu, na sadaka


ni sababu ya mapenzi ya waja wa Mola kwa mtoa sadaka


14- Sadaka ni ishara miongoni mwa ishara za ukarimu na


alama miongoni mwa alama za ukarimu na wema


3


15- Sadaka ni sababu ya kukubaliwa dua na kuondoshewa


matatizo


16- Sadaka inaondoa balaa na inaziba milango sabini ya


mabaya ya dunia


17- Sadaka inazidisha umri na mali, na ni sababu ya riziki na


nusra


18- Sadaka ni ponya, dawa, na shifaa


19- Sadaka inazuia moto, gharika, wizi, na inazuia kifo kibaya


20- Sadaka ujira wake ni ule ule japo ukitoa kwa wanyama au


ndege.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI