Nakala




NYUMBA KATIKA PEPO





MTUNZI SHEKH: YASINI TWAHA


KIMEREJEWA NA SHEKH: ABUBAKARI SHABANI RUKONKWA


2


بسم الله الرحمن الرحيم


Ndugu yangu Duniani kuna Nyumba nyingi za kila aina Lakini Nyumba


zote hizo zimejengwa na Miti au Udongo au Tofari au Mawe au Mchanga


au Simenti……Nk.


Nyumba zote hizo zina Vyoo vya ndani na vya nje Wenye kuishi ndani


ya Nyumba hizo hakupiti Siku wala Mwezi au Mwaka ila Utasikia


Matatizo ndani ya Nyumbahizo, Utasikia Mtu Kaumwa, Mwengine


Mnyonge, Mwengine Ana huzuni, au Nyumba ime Bomoka,Wengine


Wana fukuzwa kwenye Nyumba za kupanga kwa Ajili ya kodi,Wengine


Chakulatabu,Wengine Mpaka Waseme Uongo ndio wapate Kula! Yaani


Matatizo Juu ya Matatizo, Hii ndio Hali ya Nyumba za Duniani na watu


Wake.


Lakini Ndugu Yangu Waweza kujenga Nyumba katika Pepo Ukiwa Hapa


Hapa Duniani, Nyumba Ya ajabu kabisa, Nyumba Ambayo Tofari zake


za Dhahabu na Fedha, Simenti ni Miski, ndani ya Nyumba hiyo kuna


Wanawake wanaitwa Hurul-aini, Laiti Mwanamke wa Peponi


Akichungulia kwenye Mbingu ya Dunia basi Dunia yote itajaa Nuuru na


Harufu nzuri!!, Ndani ya Nyumba hiyo Pamejaa Neema zisizo katika, za


kila Aina, Neema Ambazo Macho hayajawahi kuona, wala Masikio


hayajawahi kusikia, sihivyo tu Hata Moyo kuwaza Namna ya Neema hizo


zilivyo bado!, Watu Wanyumba hiyo Watakula na Kunywa Wataishi


hawatokufa.


3


Ndugu yangu Ukitaka Kuipata Nyumba hiyo Fanya Hili jambo:





Kapokea Imam Muslim Mungu Amrehemu katika Swahihi yake:


(Mlango unaoelezea Ubora wakuswali Sala za Sunna zilizo pangiliwa


kabla ya Faradhi na baada yake).


Kanihadithia Muhammad bin Abdullahi bin Numairi, Kanihadithia Baba


yake na Khalid ambae ni Suleiman bin Hayyan' kutoka kwa Daaud bin


Abiihindi, kutoka kwa Nuuman bin Saalim, kutoka kwa Amru bin Ausi,


Amesema: Amenihadithia Ambasa bin Abii Sufyan katika Maradhi


alioFishwa nayo, Mazungumzo Ambayo Ukiyasikia yanafurahisha,


Amesema: Nilimsikia Mama Habiba Akisema: Nilimsikia Mtume wa


Mwenyezi Mungu (Rehma na Amani za Allah ziwe juu yake) Akisema:


{Yeyoto Atakae Swali Rakaa kumi na mbili kwa Usiku na Mchana


Hujengewa Nyumba Katika Pepo kutokana na Rakaa hizo}.!!!


Akasema Ummu Habiba: Sikuacha kuswali Rakaa hizo toka nilipo


Msikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Rehma na Amani za Allah ziwe


juu yake).


4


Na Akasema Ambasa: Sikuacha kuswali Rakaa hizo toka nilipo msikia


Mama Habiba.


Na Akasema Amru bin Ausi: Sikuacha kuswali Rakaa hizo toka nilipo


msikia Ambasa.


Na Akasema Nuuman bin Saalim:Sikuacha kuswali Rakaa hizo toka


nilipo msikia Amru bin Ausi.


Ndugu zangu tukimbilieni kheri hizi na tujitahidini katika hali hii na


tuwaamrishe tunaowamiliki akiwemo mke, motto, nawengineo.


Ndugu yangu Jaribu kuiuliza Nafsi yako Maswali machache:


1/ Miaka mingapi imepita katika Umri wangu Sijaswali Rakaa hizi?.


2/ Thawabu ngapi zimenipita kwa sababu ya Mambo ya Kipuuzi?.


3/ Mambo gani Mema Ambayo Nimekwisha yatanguliza mbele ya


Mwenyezi Mungu?.


4/ Lini nitaacha Kumuasi Mwenyezi Mungu?.


5/ Nitaanza lini Kufanya Ibada?.


6/ Kwa nini Nafsi yangu ni nzito Katika Mambo ya Kheri?.


7/ Kwa nini Nafsi yangu ni nyepesi Katika Mambo ya Shari?.


Mwisho kabisa:


Ndugu yangu Muislam kuwa na pupa katika kutekeleza Sunna tulizo


zitaja, Faida yake Utaikuta Mbele ya Allah pia Usisahau Kufanya Mambo


ya Kheri kwa wingi kama vile: Kuswali Swala tano kwa Jamaa Muskitini,


Funga za Sunna: J/tatu na Al-khamis na zile ayyaamulbiidh (Masiku


meupe) Tarehe (13-14-15) Kila Mwezi ,na Funga ya Ashuraa, na Funga


ya Arafaa, na Nyenginezo. Pia Katika Mambo ya Kheri kutoa Zaka na


kutoa Sadaka kufanya Ibada ya Hija naUmra. Ndugu yangu Milango ya


Kheri ni Mingi sanaTushindane Katika hilo, Mungu Atufanyie Wepesi.


5


NَAMNA YA KUTEKELEZA IBADA ZA SUNNA TULIZO ZITAJA:


َ


Ishaaَ Maghrebَ Laasiriَ Adhuhuriَ Al-fajri


BَAADIAَ KABLIAَ BAADIAَ KABLIAَ BAADIAَ KABLIAَ BAADIAَ KABLIAَ BAADIA KABLIA


2 2 2 4 2


Kuna Swala za Sunna Nyingine Tofauti na Tulizo zitaja:


1/ Rakaa 2 Wakati Wa kuingia Mskitini.


2/ Rakaa 4 Kabla ya Swala ya Laasiri 2unatoa Salam 2 unatoa Salam.


3/ Rakaa 2 Kabla ya Maghreb kwa Mwenye Kutaka.


4/ Rakaa 2 Baada ya Kumaliza Kutawadha. Nk….


Tuna Muomba Mwenyezi Mungu Atupe Kila la Kheri, na Atuepushe


na Kila la Shari, Atupe Mwisho Mwema Wakati Wa kufa kwetu,


Atuepushe na Adhabu za Kaburini, Atufufue Siku ya MwishoTukiwa


Nyuma ya Mtume wetu Muhammad (Rehma na Amani za Allah ziwe


juu yake) ,Atupe Kitabu chetu Kwa Mkono wa Kulia.


Rehma na Amani za Allah zimuendee Nabii Muhammad Pamoja na


Watu wa Nyumbani kwake na Maswahaba zake na Waislamu wote


watakao Fuata Mwenendo wake Mpaka Siku ya Mwisho, Mwenyezi


Mungu Atujaalie Tue Miongoni Mwa watu wema. Ameen!!


AMIN.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI