Nakala

بسم الله الرحمن الرحيم


MAMBO 10 YATAKAYOKUFANYA UWE MUME BORA Imeandikwa na Kabuga Kanyegeri Imepitiwa na Abubakari Shabani Rukonkwa. Utangulizi: Kila sifa kamilifu nizake Allah mtukufu alie fanya maisha yasiwe mazuri mpaka mtakapo kuwa wawili mke na mume kasha akamfanya mume ndie msimamizi wa mambo yoote katika nyumba,kasha akawaumba wanawake ili wawe pomziko na starehe kwa waume zao,anasema Allah Mtukufu: {Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri }Ar-Rum 21. Sala na amani zimuendee Mtume Rehma na amani za Allah ziwe juuyake mtume ambae alikuwa nimfano mwema kwa waume bora na alikuwa nimwalimu wa waalimu, na ziwe juu ya maswahaba zake na woote watakao mfuata kwa wema mpaka siku ya Qiyama. Mada hii inazungumzia sababu ya kuwa mume bora nimada muhimu sana hasa katika zama hizi za utanda wazi na zama za


fitna ambazo watu wameifanya halali kuwa haramu mabaya


kuwa nimazuri ,NK


Leo tunakuletea mambo haya ili uwe mume bora kwa familia


yako,sababu hizi niningi sana ila tuta kuelimisha haya mambo


kumi tulio kuchagulia.


1. Vaa vizuri kwa ajili ya mkeo, uonekane nadhifu na mwenye


kunukia vizuri. Kama ambavyo mume anapenda mke wake


aonekane maridadi kwa ajili yake, naye pia anapenda mume


wake avae vizuri kwa ajili yake. Kumbuka kwamba Mtukufu


Mtume (s.a.w) daima alikuwa akianza kupiga mswaki pindi


anaporudi nyumbani na daima alikuwa akipenda harufu nzuri.


2. Muite mkeo kwa majina mazuri. Mtukufu Mtume (s.a.w)


alikuwa akiwaita wakeze kwa majina mazuri ambayo hata wao


wenyewe walikuwa wakipenda kuyasikia. Muite mkeo kwa jina


zuri analolipenda zaidi kulisikia, na epuka kutumia majina


yatakayoumiza hisia zake.


3. Usiamiliane na mkeo kama nzi. Mara zote katika maisha yetu


ya kila siku huwa hatukumbuki kuwa kuna nzi mpaka pale


wanapotuudhi. Angalia, mkeo hukufanyia mambo mengi mema


kwa siku nzima ambayo huwa huyaangalii, ila pale


anapokufanyia kosa kidogo unamtazama. Usiishi naye kwa


namna hii; yatambue mambo mema yote anayokufanyia.


4. Ukiona kosa kutoka kwa mkeo, jaribu kutohamaki au


kumkaripia, muongoze kwa hekma na busara, atakuelewa! Hivi


ndivyo Mtukufu Mtume (s.a.w) alivyokuwa pale anapoona


jambo lisilokuwa muafaka kutoka kwa wakeze. Ni njia ambayo


ni wanaume wachache wa Kiislamu wameimudu.


5. Onyesha tabasamu kwa mkeo pindi unapomuona na daima


zidisha kumkumbatia. Kutabasamu ni sadaqah na mkeo naye


anastahili hiyo sadaka kwa namna ya kipekee. Fikiria maisha


yatakavyokuwa pale mkeo anapokuona unatabasamu kwa ajili


yake! Kumbuka pia zile hadith zinazosema kuwa Mtukufu


Mtume (s.a.w) alikuwa akimbusu mkewe kabla ya kwenda


kuswali, hata kama akiwa amefunga.


6. Mshukuru kwa kila analokufanyia. Kisha mshukuru tena na


tena! Angalia, mkeo anakuandalia chakula, anasafisha nyumba


na anafanya kazi nyingine nyingi mno. Wakati mwingine hata


kumpongeza hufanyi! Usiwe hivyo, mshukuru na useme:


“Ahsante mke wangu!”


7. Muombe akuandikie mambo kumi uliyomfanyia na


yakamfurahisha. Kisha mfanyie mambo hayo tena. Mara nyingi


huwa ni vigumu kujua mambo yanayomfurahisha mkeo. Huna


haja ya kubahatisha, muombe akwambie na kisha uyafanye hayo


na mengine pia katika kipindi chote cha maisha yenu.


8. Usiyapuuze na kuyabeza matakwa yake. Mfariji. Wakati


mwingine wanaume huyadharau maombi ya wake zao. Mtukufu


Mtume (s.a.w) hakuwa hivyo.


9. Uwe mwenye kunyumbulika na fanya michezo na mkeo.


Mtukufu Mtume (s.a.w) alikuwa akishindana na mkewe bibi


Aisha katika mchezo wa kukimbia. Mara ya mwisho


umemfanyia lini mkeo jambo kama hilo?


10.Daima kumbuka maneno ya Mtukufu Mtume (s.a.w): “Mbora


wenu ni yule anayeitendea mambo bora familia yake. Nami ni


mbora wenu kwa familia yangu.” Jaribu kuwa bora!


Usisahau kumuomba Mwenyezi Mungu aifanye ndoa yako


kuwa bora.


Mwisho:Ninaamini kuwa umefaidika vyakutosha na utayafanyia


kazi kwa idhini ya Allah.


Ninamuomba Allah azijaze nyumba na nyoyo zetu utulivu,


upendo na kuhurumiana sasa na hata milele!!!.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI