Nakala

1


بسم الله الرحمن الرحيم


KINGA YA KILA SIKU DHIDI YA SHETANI, UCHAWI, HUSDA NA KILA UBAYA. Imeandaliwa na :Yunus Kanuni Ngenda. Imepitiwa na :Abubakari Shabani Rukonkwa. Uislam ni dini iliyokamilika katika kila idara miongoni mwa mambo ambayo pia yanapatikana ndani ya uislam ni kinga ya kisheria dhidi ya kila shari kama vile shetani,uchawi, husda, kijicho n.k. Kinga hii ndiyo mujarrab na hupaswi kujikinga kwa hirizi wala chale kama wafanyiwavyo wengi miongoni mwa jamii ya wanaadamu na la kusikitisha zaidi katika kundi la wanaoamini na kufanya ushirikina huu ni waislam! Ndugu zangu shirki ni jambo baya sana na ni miongoni mwa dhambi kubwa ambayo ALLAH amemuambia mtume wake kuwa وَلَقَدۡ أُوحِىَ إِلَيۡكَ وَإِلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكَ لَ ٮِنۡ أَشۡرَكۡتَ لَيَحۡبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ





Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa walio kuwa kabla yako: Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na lazima utakuwa


2


miongoni mwa wenye kukhasiri


Surat Zumar: 65


Huyo ni mtume wa allaah vipi mimi na wewe?


Kwa kuzingatia hilo nimeona ni kheri leo nikawaletea


taratibu sahihi za kujikinga ambazo unatakiwa udumu nazo


kila siku asubuhi na jioni.


Ni matarajio yangu kwamba tutaendelea kuwa pamoja ili


tuweze kufaidika na elimu hii ya bure kabisa kwa ajili ya


kutafuta radhi za ALLAH.





Laa Ilaaha Illa llaahu wahdahuu laa shariika lahu


lahulmulku walahul hamdu wahuwa alaa kulli shai-in


qadiir


mara 100 asubuhi na jioni


 Allaahu laa ilaaha illaa huwalhayyul qayyuum laa taakhudhuhuu


sinatun walaa nauum lahuu maa fis


samaawaati wamaafil-ardhwi yashfa'u 'in-dahuu illaa biidhnihii


ya'alamu maa baina aidiihim wamaa khalfahum


walaa yhiitwuuna bishai-in min 'ilmihii illaa bimaa shaa-a


wasi'a kursiyyuhus samaawaati wal-ardhwa walaa yauuduhuu


hifdhuhumaa wahuwal'aliyyul'adhwiim.


mara 1 kila baada ya swala ya fardhi.


3





Qul huwa llaahu ahadu.1) Allaahus Swamadu. 2) Lam yalid


wa lam yuulad. 3) Wa lam yakunlahuu kufuwan ahad. 4)


Mara 3 kila baada ya swala ya fardhi.





Qul a'uudhu birabbil falaq. 1) Minsharri maa khalaq. 2) Wa


minsharri ghaasiqin idhaa waqaba. 3) Wa minsharrin n


affaathaati fil'uqad. 4) Wa minsharri haasidin idhaa


hasada.5)





Qul-a'uudhu birabbin naas.1) Malikin naas. 2) ILaahin


naas.3) Minsharril was-waasil khannaas. 4) Alladhii


yuwas’wisu fii swuduurin naas. 5) Minaljinnati wan naas.6)


Sura hizo tatu za unatakiwa kuzisoma kila baada ya swala


ya fardhi mara 3, na wakati wa kulala.


Isipokua wakati wa kulala ukishazisoma hizo sura mara 3


unapulizia kwenye viganja vyako vya mikono kisha


unajifuta mwili mzima.





4


A'uudhu bikalimaati LLaahi taammaati minsharri maa


khalaqa. mara 3 baada ya Maghribi





Bismi llaahi lladhiy laa yadhurru ma'asmihi shay-un filardhwi


walaa fis samaa-i wahuwas samii'ul-'aliim. mara 3


asubuhi na jioni.


Hizo ni baadhi ya nyiradi za Asubuhi, Mchana, Jioni na


Usiku ambazo kwa nwenye kudum nazo basi mtu huyo


atakua na kinga ya Allah! Kutokana na mambo


tuliyozungumza hapo juu.


Tunamuomba Allah atulinde na kila shari, na atujaalie


mwisho mwema. Ameen!!



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI