Nakala

1


بسم الله الرحمن الرحيم


Fadhila Za Tawhiyd. Imeandaliwa na alhidaaya.com Imepitiwa na Yunus Kanuni Ngenda. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa):





Basi elewa kwamba laa ilaaha illa-Allaah (hapana mungu anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Allaah)[Muhammad: 19] Maana ya Tawhiyd kama alivyosema ‘Allaamah ‘Abdir-Rahmaan Naaswir As-Sa’dy katika “Al-Qawlus-Sadiyd Fiy Maqaaswidit-Tawhiyd - Sharh Kitaab At-Tawhiyd” “Tambua kwamba maana ya Tawhiyd haina mipaka. Ni maarifa na kukiri kumpwekesha Ar-Rabb (Mola) kwa Swifa za ukamilifu, na kuthibitisha kwamba Anapwekeshwa katika Sifa Zake Adhimu na Tukufu, na kumpwekesha katika ‘ibaadah zote”. Kinyume cha Tawhiyd ni ‘Shirk’ ambayo ni kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) katika hayo yaliyotajwa yote yanayomuhusu Yeye Pekee. ‘Ulamaa wameigawanywa Tawhiyd katika sehemu tatu: 1 – Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah


2


Nayo ni kumpwekesha Allaah katika Uumbaji,


Uendeshaji wa mambo yote katika Ulimwengu, Utoaji


rizki, Uletaji uhai na Ufishaji, kwa kuamini kwamba


Yeye Ndiye Aliyeumba kila kitu, Anayeruzuku na


kuendesha mambo yote ni Allaah (Subhaanahu wa


Ta’alaa). Hana mshirika, na kuamini kwamba Ufalme


wote ni wake:


Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) Anasema:


 Sema: "Ni nani Mola wa mbingu na ardhi?" Sema: "Ni


Allaah" [Ar-Ra’d:16]


Na Anasema:





Sema: “Nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na


ardhini. Au nani anayemiliki kusikia na kuona; na nani


anayemtoa (aliye) hai kutoka mfu, na anayemtoa mfu


kutoka (aliye) uhai; na nani anayedabiri mambo (yote)?


Watasema: “Ni Allaah”; basi sema: “Je basi hamuwi na


taqwa?” (Hamumkhofu Allaah?) [Yunus: 31]


2-Tawhiyd Al-Uluwhiyyah


Maana yake ni kumwepekesha Allaah katika 'ibaadah


na kuzielekeza ‘ibaadah zote kwa Allaah (Subhaanahu


wa Ta’alaa).


3


Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) Anasema:





Sema: “Hakika Swalaah yangu, na nusukiy (kuchinja


kafaara na ‘ibaadah zangu) na uhai wangu na kufa


kwangu ni kwa ajili ya Allaah (Pekee) Mola wa


walimwengu.” Hana mshirika, na kwa hayo ndio


nimeamrishwa, nami ni Muislamu wa kwanza


(waliojisilimisha kwa Allaah). [Al-An’aam: 162-163]


3-Tawhiyd Asmaa wasw-Swifaat


Kumpwekesha Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) kwa


Sifa Zake Tukufu, na Majina Yake mazuri, bila


kuzigeuza Sifa hizo maana zake, au kuzipinga, au


kuzifananisha na viumbe au kuzipa unamna. Yeye


Amejipa Majina mazuri mazuri na Sifa nzuri nzuri na


Akawataka waja Wake wamuombe na kumtukuza kwa


Majina na Sifa hizo.


Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) Anasema:





Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni


kwayo. Na waacheni wale wanaopotoa (kwa kuharibu


utukufu, kukanusha, kugeuza maana, kushabihisha)


katika Majina Yake, watalipwa yale waliyokuwa


wakiyatenda. [Al-A’raaf: 180]


4


Qur-aan nzima imedhihirisha Tawhiyd ya Allaah


(Subhaanahu wa Ta’ala); mfano Suwratul-Faatihah


ambayo tunaisoma kila siku mara kumi na saba katika


Swalaah zetu za fardhi na pia katika Swalaah zote


nyinginezo, imejumuisha aina tatu zote za Tawhiyd.





Kwa Jina la Allaah Ar-Rahmaanir-Rahiym (Mwingi wa


Rahmah - Mwenye kurehemu). AlhamduliLLaahi (Sifa


njema zote ni za Allaah) Mola wa walimwengu. Ar-


Rahmaanir-Rahiym (Mwingi wa Rahmah-Mwenye


kurehemu). Maalik (Mfalme) wa siku ya malipo. Wewe


Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba


msaada [Al-Faatihah: 1-5]


Na pia kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):





Mola wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake; basi


mwabudu Yeye tu na dumisha subira katika ‘ibaadah


Yake. Je, unamjua (mwengine) mwenye Jina Lake? (Bila


shaka hakuna aliyefanana Naye kwa lolote, vyovyote, na


wala hana mshirika!). [Maryam: 65]



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI