Nakala

UHARAMU WA NYAMA YA NGURUWE NI


BAYANA YA KISAYANSI


Mwenyezi Mungu Amesema : “ Sema; “ Sioni katika yale niliyofunuliwa mimi kitu


kilichoharamishwa kwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni mzoga au damu inayomwagika au


nyama ya nguruwe, kwani hiyo ni uchafu; au kile ambacho kwa kuhalifiwa amri ya Mwenyezi


Mungu kimechinjwa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Lakini aliyelazimika kula


pasipo kupenda wala kuchupa mipaka, basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe na


Mwingi wa k urehemu.” Aya ya 145, Suratul An-aam.


UHAKIKA WA KISAYANSI


Imekuja elimu kudiriki baadhi ya mambo yaliyokatazwa na sheria ya Kiislamu


iliyohifadhiwa na wafuasi wake karne kwa karne kabla ya kugunduliwa kwa darubini na kwa


mpangilio huo huo : Mzoga ambao bakteria hukua ndani yake, damu ambayo bakteria hukua


ndani yake kwa kasi kubwa zaidi, hasa ikiwa ni nyingi, na mwisho nguruwe ambapo katika


mwili wake hukusanyika jumla ya vijiumbe maradhi visivyoondoka kwa kuoshwa. Mwenyezi


Mungu Amesema : “ Sema; “ Sioni katika yale niliyofunuliwa mimi kitu kilichoharamishwa


kwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni mzoga au damu inayomwagika au nyama ya nguruwe,


kwani hiyo ni uchafu; au kile ambacho kwa kuhalifiwa amri ya Mwenyezi Mungu


kimechinjwa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Lakini aliyelazimika kula pasipo


kupenda wala kuchupa mipaka, basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe na Mwingi


wa kurehemu.” Aya ya 145, Suratul An-aam.


UHAKIKA WA KISAYANSI


Imekuja elimu kudiriki baadhi ya mambo yaliyokatazwa na sheria ya Kiislamu


iliyohifadhiwa na wafuasi wake karne kwa karne kabla ya kugunduliwa kwa darubini na kwa


mpangilio huo huo : Mzoga ambao bakteria hukua ndani yake, damu ambayo bakteria hukua


ndani yake kwa kasi kubwa zaidi, hasa ikiwa ni nyingi, na mwisho nguruwe ambapo katika


mwili wake hukusanyika jumla ya vijiumbe maradhi visivyoondoka kwa kuoshwa. Mdomo ni


maficho ya vijidudu, bakteria na virusi vinavyokwenda kwa binadamu na wanyama. Baadhi


yake vinamhusu nguruwe, mfano wa kidudu kiitwacho Trchinella, nywelenywele ziitwazo


Balantidium Dysentery, wadudu wa tumbo (Taenia Solium) na mchango wa nguruwe


(Spiralis). Baadhi yake huingizwa kwenye maradhi mengi ya pamoja baina ya binadamu (


Cysticercosis & Influenza) na wanyama. Minyoo (Ascaris na Fasciolopsis Buski) hupatikana


kwa wingi nchini China. Maradhi ya Balantidiasis hupatikana kwa wachunga nguruwe na


wenye kuchanganyika nao, na yanaweza kuenea kwa sura ya mlipuko kama ilivyotokea


katika moja ya visiwa vya bahari ya Pacific baada ya kimbunga. Maradhi yanakuwepo


panapokuwepo nguruwe katika nchi zilizoendelea kiviwanda kinyume na madai ya


uwezekano wa kuushinda uchafu wake kwa kutumia teknolojia mpya zinazoharamisha kula


nyama bila ya kibali, hasa nchini Ujerumani, Ufaransa, Philippines na Venezuela. Kwa kula


minofu ya nyama ya nguruwe, (Trichinellosis) hupatwa na ugonjwa wa Balantidium


Dysentery. Kwani mke hubungua kuta za matumbo kwa ajili ya kuweka mayai ambayo


yanafikia kiasi cha 10,000. Mayai hayo huingia kwenye misuli kupitia damu na kugeuka


kuwa ni vijiyai vyenye kuambukiza. Ama kupata maradhi kupitia mchango wa nguruwe, ni


kuwa hiyo hupatikana baada ya kula minofu ya nguruwe mwenye ugonjwa. Minyoo hukua


kwenye mchango wa binadamu na urefu wake unaweza kufikia meta saba, na unakuwa na


kichwa chenye miba inayosababisha kukwaruzika kwa kuta za michango na mchupo mkubwa


wa damu, na ana mirija minne na shingo. Aina za mke huzaliwa kama kwamba ni wanyama


pekee na hufikia maelfu. Na katika kila mmoja kati ya mnyama, huzaliwa zaidi ya mayai elfu


moja iwapo utakula Cysticercosis. Kupatwa na ugonjwa wa minyoo ya tumbo la binadamu,


hutokana na kula chakula kilichoingia mayai na kutoa lava, na huingia katika damu kupitia


kiungo chochote. Na hatari yake hukisiwa kwa mujibu wa umuhimu wake. Maradhi haya


hayatokei kabisa kutokana na kupatwa na mchango usio na miba katika kichwa na wenye


madhara madogo kabisa Taenia Saginata ya ng’ombe.


UPANDE WA MIUJIZA :


Nguruwe ni mwenye tabia mbaya. Kuchukiwa na wasio na dini kumepelekea


kumhesabu kuwa ni muuaji wa alama za kheri. Visa vya kale vimehadithia kuwa nguruwe


alimuua Houras kwa Wamisri wa kale na Adun kwa Wakanaan na Adonis kwa Wagiriki na


Atis katika Asia ndogo. Wafuga nguruwe katika Misri ya kale, walihesabiwa kuwa ni watu


walioijua vyema kazi yao. Mchunga nguruwe haingii kwenye mfumo na wala haoi isipokuwa


wanawake mfano wake. Na mwenye kumgusa nguruwe ni juu yake kuoga. Nguruwe ni


haramu kwa watu wa kitabu ingawa wamekwenda kinyume. Lakini Qurani imetoa sababu ya


kukatazwa kula nyama yake kwa kauli yake Mwenyezi Mungu “ Kwani hiyo (nyama) ni


uchafu”. Neno uchafu ni neno lenye kukusanya maana nyingi ikiwemo uchafu, najisi, yenye


maudhi, na yenye madhara. Ukatazo wa kula nyama ya nguruwe japo kidogo kama ni


chakula, umekuja katika sehemu tatu nyengine. Kwanza kauli yake Mwenyezi Mungu


“Amekuharamishieni mzoga tu na damu na nyama ya nguruwe na kilichotajiwa katika


kuchinjwa kwake jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu”. Lakini aliyefikwa na dharura (ya kula


vitu hivi) bila kutamani wala kupita kiasi, basi yeye hana dhambi. Hakika Mwenyezi Mungu ni


Mwingi wa kusamehe na Mwingi wa kurehemu.” Suratul Al Bakarah aya ya 173. Pili kauli


yake Mwenyezi Mungu katika aya ya 115 ya Suratul Nahl, “ Amekuharamishieni nyamafu tu


(mzoga) na damu na nyama ya nguruwe na (mnyama) achinjwae kwa jina lisilokuwa la


Mwenyezi Mungu. Lakini anayekosa budi (anayeshurutishwa) bila kuasi wala kuruka mpaka,


basi (Mwenyezi Mungu atamsamehe); hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe na


Mwingi wa kurehemu.” Tatu ni kauli yake Mwenyezi Mungu katika aya ya 3 ya Suratul


Maidah, “ Mmeharamishiwa nyamafu na damu na nyama ya nguruwe, na kinyama


kilichochinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na kilichokufa kwa kusongeka koo, na


kilichokufa kwa kupigwa, na kilichokufa kwa kuanguka, na kilichokufa kwa kupigwa pembe


(na mwengine) na alichokila mnyama (kikafa), ila mkiwahi kukichinja (kabla hakijafa). Na (pia


mmeharamishiwa) kilichochinjwa panapofanyiwa ibada isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu


(kama mizimuni). Na ni (haramu kwenu) kutaka kujua siri kwa kuagua kwa maboa (na yaliyo


kama hayo). Hayo yote ni maasiya.” Uharamu umekusanya vyote vinavyoliwa kama mafuta.


Kuharamishwa peke yake kwa Mayahudi kunathibitisha kwamba asili ni kuingia kwake


katika nyama kama chakula. Mwenyezi Mungu Anasema, “Na kwa wale walio Mayahudi,


Tuliharamisha kila (mnyama) mwenye kucha. Na katika ng’ombe na kondoo na mbuzi,


Tukawaharamishia shahamu (mafuta) yao isipokuwa ile iliyobeba migongo yake (wanyama


hao) au (iliyobeba) matumbo au ile iliyogandamana na mifupa. Tuliwalipa hivyo kwa sababu


ya uasi wao. Na bila shaka sisi ndio Wakweli.” Kuharamishwa kwa nyama kunaharamisha


mafuta hata kama ni chakula cha mnyama anayeliwa na binadamu. Siku ilipoteremka


Qurani, hakuna mtu aliyekuwa akijua madhara ya nguruwe. Kwa hiyo inatoka wapi kinga


hiyo iliyokuja kwa sheria ikiwa haikuteremshwa kwa ujuzi wa Mjuzi na Mwenye hekima!


Mwenyezi Mungu Mweza Anasema, “ Na watu wako wameikadhibisha chini Qurani hali hiyo


ni haki. Sema: “Mimi si mlinzi juu yenu”. Kila khabari (iliyotajwa hapa) ina wakati wake


(maalumu wa kufika). Na hivi karibuni mtajua (haya).”



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI