Nakala

 





Mafungamano ya shahada na


Aina za Tawhiidi.


1


Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.


Swali: Je shahada inakusanya vigawanyo vya Tawhid?


Jawabu: ndio shahada inakusanya aina za tawhiid zote, ima kwa kuambatana na


shahada au kulazimiana.


Kwa mfano: mtu anaposema : (Ash’hadu an laa ILLaha ila Allah), mtu


anafahamu kuwa makusudio yake ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika


ibada, na kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika ibada kunaitwa (Tawhid Al


Uluhiya) ambayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika ibada za


wanadamu, tawhidi hii inalazimiana na kuambatana na tawhidiya (Al-


Rububiyyah) ambayo maana yake ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika


vitendo vyake Mwenyezi Mungu kama kuumba na kuhuisha na kufisha na kutoa


rizki nk.


Kwasababu kila mwenye kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake hakika


hatamuabudu mpaka awe ni mwenye kukiri Uungu wa Mwenyezi Mungu katika


vitendo vyake, na hii inakusanya kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika majina


yake na sifa zake, kwasababu hii alisema Nabii Ibrahim kumwambia Baba yake:


} Ewe baba yangu! Kwa yakini imenifikia elimu isiyokufikia wewe. Basi nifuate


mimi, name nitakuongoza Njia iliyo Sawa{. (Maryam 43).


Basi tawhid ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika ibada ndio tawhid Al


Uluhiyyah ambayo imekusanya tauhidi ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu


katika vitendo vyake (Tawhid al-rububiyyah) na kumpwekesha Mwenyezi


Mungu katika majina yake na sifa zake (Tawhidi Al As’mai wa swifati).



Machapisho ya hivi karibuni

Mafungamani ya Shahad ...

Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.

Namna ya swala ya mtu ...

Namna ya swala ya mtume (s.a.w). na Namna ya kutawadha

FADHILA YA SUNNA ZA M ...

FADHILA YA SUNNA ZA MTUME (S.A.W)

MAZUNGUMZO KATIKA PEP ...

MAZUNGUMZO KATIKA PEPO NA JAHANNAMU (SEHEMU YA 3 KATI YA 3): NA SITAWAHI WAKASIRIKIA TENA.