Nakala

Swali : Nilipi jambo la kwanza la wajibu kwa kiumbe?


Jawabu: Jambo la wajibu la kwanza kwa viumbe ni lile ambalo viumbe


wanalinganiwa kwalo, na amelibainisha Mtume (s.a.w) kwa Muadhi bin Jabal


(r.a) wakati alipomtuma kwenda Yemen, alimwambia: "Hakika unawaendea


watu ambao ni mayahudi na manaswara, basi liwe jambo la kwanza utakalo


walingania ni kutoa shahada ya Laa Ilaha ila Allah Muhamada rasulu Allah".


Imepokelewa na Imamu Bukhari (1496) na Imamu Muslim (19).


Hili ndilo jambo la kwanza ambalo ni wajibu kwa kila mja ashahidilie kuwa


hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haqi ila ni Mwenyezi Mungu na Mtume


(s.a.w) ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni wajibu kwa waja wampwekeshe


Mwenyezi Mungu, na waukubali na kukiri utume wa Muhamad (s.a.w), kwa


kufanya hivyo ndio inapatikana Ikhlas na kufuata mambo hayo mawili ndio


sharti ya kukubaliwa ibada.


Haya ndiyo mambo ya kwanza ambayo ni wajibu kwa kila mja kuyafanya,


ampwekeshe Mwenyezi Mungu na akiri Utume wa Muhamad (s.a.w) na


kutamka shahada ya (La ILLaha ila Allah Muhamada rasulu Allah) ndani yake


ndiyo kunaTawhiidi yote.c



Machapisho ya hivi karibuni

Mafungamani ya Shahad ...

Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.

Namna ya swala ya mtu ...

Namna ya swala ya mtume (s.a.w). na Namna ya kutawadha

FADHILA YA SUNNA ZA M ...

FADHILA YA SUNNA ZA MTUME (S.A.W)

MAZUNGUMZO KATIKA PEP ...

MAZUNGUMZO KATIKA PEPO NA JAHANNAMU (SEHEMU YA 3 KATI YA 3): NA SITAWAHI WAKASIRIKIA TENA.