Nakala

سم الله الرحمن الرحیم


MAELEZO KWA UFUPI


KUHUSU UISLAMU


Kila sifa njema ni zake Mwenyezi


Mungu Mola wa viumbe vyote, sala na


amani ziwe juu ya Imamu wa Mitume,


Nabii wetu Muhammad, na jamaa zake,


na Masahaba wake wote.


Ama baada:_


UISLAMU:_ ni kushuhudia kuwa


hapana Mola apasae kuabudiwa kwa


haki ila Mwenyezi Mungu mmoja, na


Muhammad (rehema na amani za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) ni


mjumbe wa Mwenyezi Mungu,


(kushuhudia) kwa moyo, na kwa ulimi,


na kwa viungo.


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٣


Na (huo Uislamu) unajumuisha


kuamini nguzo sita za Imani kwa


kutekeleza nguzo tano za Uislamu, na


nguzo mbili za Ihsani.


Na (huo Uislamu) ni risala ya mwisho


miongoni mwa risala za Mwenyezi


Mungu, ambayo ameiteremsha


Mwenyewe Allah kwa mwisho wa


manabii wake na mitume wake, Mtume


Muhammad bin Abdillah (rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu


yake).


Na (huo Uislamu) ndiyo dini ya haki


ambayo Mwenyezi Mungu hatakubali


dini nyingine isiyokuwa uislamu, na


hakika ameifanya Mwenyezi Mungu dini


ya uislamu kuwa nyepesi na rahisi,


hakuna ugumu au uzito ndani yake, wala


tabu, hakuwalazimisha (Allah) wenye


kuingia ndani ya dini hiyo mambo


wasiyo yaweza, na wala hakuwakalifisha


kwa yale wasiyoweza.


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٤


Na ni dini ambayo msingi wake ni


TAUHID (kumpwekesha Mwenyezi


Mungu katika ibada), na alama yake ni


ukweli, na imezungukwa na uadilifu, na


ndiyo usimamizi wa haki, na roho yake


(dini hii) ni huruma, na ni dini tukufu


ambayo huwaongoza waja (watu)


kwenye kila jambo lenye manufaa katika


dini yao na dunia yao, na


huwatahadharisha kutokana na kila lenye


madhara katika dini yao na maisha yao,


Na ni dini ambayo Mwenyezi Mungu


amerekebisha kwayo itikadi na tabia, na


akarekebisha kwayo maisha ya duniani


na Akhera, na akaziunganisha kwayo


nyoyo zilizo tafautiana, na matamanio


mbali mbali, akazisafisha kutokana na


sifa za upotofu, na akazielekeza kwenye


haki, na akaziongoza kwenye njia iliyo


nyooka.


Na ni dini iliyo sawa iliyo kamilika


isiyokuwa na kasoro katika habari zake


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٥


zote, na hukumu zake zote, haikuelezea


ila ukweli na haki, na wala haikuhukumu


ila kwa kheri na uadilifu, miongoni mwa


itikadi sahihi, na vitendo vilivyo sawa,


na tabia bora, na desturi za hali ya juu.


Na ujumbe wa Uislamu unalengo la


kutimiza mambo yafuatayo:


~ Kuwajulisha watu mola wao na


muumba wao kwa majina yake mazuri


ambayo hakuna mwenye majina hayo


isipokuwa yeye tu, na sifa zake za hali


ya juu ambazo hakuna mwenye


kufanana nae katika sifa hizo, na


vitendo vyake vya hekima ambavyo


hana mshirika kwenye vitendo hivyo,


na kustahiki kwake (majina hayo, na


sifa hzo, na vitendo hivyo) ambako


hana mshirika ndani yake.


~ Kuwalingania waja (watu) ili


wamuabudu Mwenyezi Mungu


pekeyake hana mshirika, kwa kufuata


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٦


mambo aliyo wawekea sheria katika


kitabu chake (Qurani) na Sunna za


mtume wake (Muhammad rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu


yake) miongoni mwa maamrisho, na


makatazo ambayo ndani yake mna


kutengenea kwao katika dini yao, na


akhera yao.


~ Kuwakumbusha hali yao na


marejeo yao baada ya kufa na mambo


watakayo kutana nayo ndani ya


makaburi yao, na wakati wa kufufuliwa


kwao , na kuhesabiwa kwao, na


mwisho wao ima peponi au motoni.


Mwenyezi Mungu atawalipa kulingana


na matendo yao, aliye tenda wema


atalipwa wema, na aliye tenda uovu


atalipwa uovu.


Na tunaweza kufupisha misingi muhimu


ya Uislamu kwenye nukta zifuatazo:-


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٧


NUKTA YA KWANZA:


NGUZO ZA IMANI


NGUZO YA KWANZA:- NI


KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU


MMOJA.


Nayo inajumuisha mambo yafuatayo:-


A-Kuamini kuumba kwake Mwenyezi


Mungu mtukufu, yaani kuamini kuwa


Mwenyezi Mungu ndiye Mola Muumba


mwenye kumiliki kila kitu, mwenye


kuendesha mambo yote ya viumbe


vyake, mwenye uwezo wa utendaji kazi


kwao.


B-Kuamini kuwa ibada ni kuabudiwa


Mwenyezi Mungu mtukufu, yaani


kuamini kuwa yeye Mwenyezi Mungu


ndiye Muabudiwa wa haki, na kila


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٨


kiabudiwacho asiyekua Mwenyezi


Mungu ni batili.


C-Kuyaamini majina yake, na sifa zake


Mwenyezi Mungu, yaani kuamini kuwa


yeye Mwenyezi Mungu ana majina


mazuri, na sifa zilizokamilika za hali ya


juu, kwa namna yalivyokuja katika


kitabu chake, na Sunna za Mtume wake


(rehema na amani za Mwenyezi Mungu


ziwe juu yake)


NGUZO YA PILI:- KUAMINI


MALAIKA


MALAIKA: ni viumbe na waja walio


tukuzwa, aliwaumba Mwenyezi Mungu


mtukufu, wana muabudu, na wanamtii,


na akawapa kazi tafauti tafauti.


Miongoni mwa hao ni: Jibril ambae


alipewa kazi ya kuteremsha Wahyi


kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa


amtakae katika manabii wake, na


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٩


mitume wake. na miongoni mwa hao ni:


Mikael aliyepewa kazi ya mvua, na


mimea. na miongoni mwa hao ni: Israfil


aliyepewa kazi ya kupuliza Baragumu


wakati wa kutolewa viumbe vyote roho


zao (mwisho wa dunia) na wakati wa


kufufuliwa. na miongoni mwa hao


Malaika ni Malaika wa mauti aliyepewa


kazi ya kutowa roho wakati wa kufa.


NGUZO YA TATU:-KUAMINI


VITABU


Mwenyezi Mungu mwenye nguvu na


aliyetukuka aliteremsha vitabu kwa


Mitume wake, ndani ya hivyo vitabu


mna uongofu na kheri na utengenefu. Na


tunavyovijuwa miongoni mwa vitabu


hivyo ni:-


A-TAURATI:


Aliiteremsha Mwenyezi Mungu kwa


Mtume Musa (rehema na amani ziwe


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٠


juu yake). Na ni kitabu kitukufu cha


Wana wa Israili.


B- INJILI:


Ambayo aliiteremsha Mwenyezi


Mungu (Aliyetukuka) kwa Mtume Issa


(sala na amani za Mwenyezi Mungu


ziwe juu yake).


C- ZABURI:


Ambayo Mwenyezi Mungu


(Aliyetukuka) alimpa Mtume Daudi


(rehema na amani za Mwenyezi Mungu


ziwe juu yake).


D- NYARAKA:


Alizopewa Nabii Ibrahimu, na


Mtume Musa, (rehema na amani za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yao).


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١١


E- QURANI TUKUFU:-


Ambayo Mwenyezi Mungu


(Aliyetukuka) aliiteremsha kwa Nabii


wake Muhammad (rehema na amani za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake),


mwisho wa Manabii wote, Mwenyezi


Mungu akafuta kwayo (hiyo Qurani)


Vitabu vyote vilivyo tangulia, na


akachukuwa jukumu la kuihifadhi (hiyo


Qurani) kwasabu itabaki kuwa hoja juu


ya viumbe vyote hadi siku ya kiyama.


NGUZO YA NNE:-KUWAAMINI


MITUME.


Mwenyezi Mungu aliyetukuka


aliwatuma Mitume kwa viumbe vyake,


na wa kwanza wao (hao mitume) ni


Nuhu, na wa mwisho wao ni


Muhammad (rehema na amani za


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٢


Mwenyezi Mungu ziwe juu yao. Na


Mitume wote wakiwemo Issa mwana


wa Mariyamu, na Uzeir (rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu


yao) na Salama, ni wanadamu


walioumbwa, hawana sifa zozote za


uungu. Wao ni waja miongoni mwa


waja wa Mwenyezi Mungu,


aliwatukuza (mwenyewe) Mwenyezi


Mungu aliyetukuka kwa (kuwapa)


ujumbe (kwa viumbe wake) na


amekamilisha Mwenyezi Mungu


wajumbe wote kwa ujumbe aliokuja


nao Mtume Muhammad (rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu


yake), na akamtuma kwa watu wote.


Hakuna (Mtume wala) Nabii


mwingine baada yake (Mtume


Muhammad rehema na amani za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake).


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٣


NGUZO YA TANO:KUAMINI SIKU


YA MWISHO.


Nayo ni siku ya Qiyama, ambayo


hakuna siku nyingine baada yake,


wakati Mwenyezi Mungu atawafufuwa


watu wawe hai ili wabaki ima katika


nyumba ya neema (peponi), na ima


katika nyumba ya adhabu iumizayo


(motoni). Na kuiamini siku ya mwisho


ni kuamini kila jambo litakalokuwa


baada ya kufa.


Miongoni mwa mitihani ya kaburini


na starehe zake na adhabu zake, na


yatakayotokea baada ya hapo kama


kufufuliwa, na kutawanyika, na hesabu,


kisha iwe pepo au moto.


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٤


NGUZO YA SITA:KUAMINI


KADARI


Kadari ni kuamini kwamba Mwenyezi


Mungu alikadiria kila kitu, na akaumba


viumbe kulingana na elimu yake


iliyotangulia, na namna alivyotaka kuwa


kutokana na hekima yake. Mambo yote


Mwenyezi Mungu (Aliyetukuka)


ayajuwa kwa elimu yake ya hapo awali,


na yameandikwa kwenye Lauhil


Mahfudh (Ubao ulio hifadhiwa), na


Mwenyezi Mungu aliyataka na


akayaumba yote, hakuna jambo lolote


lenye kutokea ila kwa kutaka kwake, na


kutengeneza kwake, na kuumba kwake.


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٥


NUKTA YA PILI: NGUZO ZA


UISLAMU


Uislamu umejengwa juu ya nguzo


tano. Na mtu hawi Muislamu wa sawa


sawa mpaka aziamini, na azitekeleze,


nazo ni:-


NGUZO YA KWANZA: SHAHADA


MBILI.


Ni kushuhudia kwamba hakuna Mola


apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa


Mwenyezi Mungu, na Muhammad ni


mtume wa Mwenyezi Mungu, na huku


kushuhudia ndiwo Ufunguo wa Uislamu,


na Msingi wake ambao hujengwa juu


yake.


Na maana ya LA ILAHA ILLA LAHU


yaani hakuna apasae kuabudiwa kwa


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٦


haki isipokua Mwenyezi Mungu peke


yake, yeye ndie Muabudiwa wa haki, na


kila chenye kuabudiwa asiye kuwa


Mwenyezi Mungu ni batili. Na ILAHU


maana yake ni:-mwenye kuabudiwa.


Na maana ya kushuhudia kwamba


Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi


Mungu:- Ni kukubali yale aliyoeleza, na


kumtii katika yale aliyoamrisha, na


kujiepusha na yale aliyoyakataza na


akayakemea na asiabudiwe Mwenyezi


Mungu ila kwa namna alivyo weka


sheria.


NGUZO YA PILI: SALA


Nazo ni Sala tano katika nyakati tano


usiku na mchana, Aliziwekea sheria


Mwenyezi Mungu ili ziwe ni utekelezaji


wa haki yake Mwenyezi Mungu ambayo


inawalazimu waja wake, na ziwe ni


kushukuru neema zake Mwenyezi


Mungu, na mfungamano baina ya


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٧


Muislamu na Mola wake


anamnong’oneza ndani yake na


anamuomba, na ili ziwe ni zenye


kumzuia Muislamu kutokana na mambo


machafu na maovu, na akazifanya kuwa


ni dini bora, na kutengenea kwa imani,


na Thawabu za papo hapo na za baadae.


Mja hupata kwa hizo Sala raha ya nafsi,


na ya mwili, ambayo humfanya kufaulu


duniani na akhera.


NGUZO YA TATU: ZAKA


Nayo ni sadaka ambayo huitowa yule


inaye mlazimu, kila mwaka kwa


wanaostahiki kupewa, miongoni mwa


Mafukara na wengineo miongoni mwa


wale wanao faa kupewa Zaka, na hiyo


Zaka si lazima kwa fukara ambae hana


kiwango cha Zaka, lakini nilazima kwa


matajiri, ili kutimiza dini yao, na


Uislamu wao, na kuziendeleza hali zao,


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٨


na tabia zao, na kuwaondoshea maafa


wao na mali yao, na kuwatakaza


kutokana na makosa, na kuwahurumia


wenye kuhitaji, na mafukara, na


kusimamia maslahi yao yote, na hiyo


Zaka pamoja na hilo, ni fungu dogo sana


ukilinganisha na kile alicho wapa


Mwenyezi Mungu miongoni mwa mali


na riziki.


NGUZO YA NNE:SAUMU


Nayo ni kufunga mwezi mtukufu wa


Ramadhani, mwezi wa tisa miongoni


mwa miezi inayokwenda kwa hesabu za


kimwezi kwa kalenda ya kiislamu.


Katika mwezi huo wa Ramadhani


Waislamu huwacha kila kitu chenye


kutamanisha, au kusababisha


kufunguwa, kama vile kuwaingilia wake


zao mchana wa ramadhani, kunywa,


kula, na kadhalika, kutoka kuchomoza


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


١٩


alfajiri mpaka kuzama kwa jua, na


huwalipa Mwenyezi Mungu kutokana na


hilo miongoni mwa fadhila zake, na


hisani yake, kukamilika dini yao, na


imani yao, na kuwasamehe maovu yao,


na kuwapandisha daraja zao, na


mengineyo miongoni mwa yale aliyo


yaweka kwenye Saumu miongoni


mwa kheri kubwa katika dunia na


akhera.


NGUZO YA TANO:-HIJA


Nayo ni kuitembelea Nyumba tukufu


ya Mwenyezi Mungu (Al-Kaaba) kwa


ajili ya kutekeleza ibada makhsusi katika


wakati makhsusi kama inavyo eleweka


katika sheria ya kiislamu, ameifanya


Mwenyezi Mungu (Hija) kuwa lazima


kwa anae weza, katika umri mara moja,


na katika hiyo Hija hukusanyika


Waisilamu katika eneo bora (Makka)


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٢٠


kutoka kila sehemu, wanamuabudu Mola


mmoja, wanavaa nguo aina moja, hakuna


tofauti baina ya kiongozi na raiya, na


tajiri na fukara, na mweupe na mweusi,


wanatekeleza ibada maalum.


Miongoni mwa hizo ibada tukufu ni:-


A-Kusimama kwenye uwanja wa


Arafat.


B-Kuizunguka Al-Kaaba Tukufu


(Kibla cha Waislamu).


C-Kutembea baina ya Safa na Marwa.


Na ndani ya hiyo Hija mna manufaa


mengi ya kidini, na ya kidunia ambayo


hayahesabiki.


NUKTA YA TATU:IHSAN


Ni kumuabudu Mwenyezi Mungu


aliyetukuka kwa imani na kujisalimisha


(kwake) kama kwamba unamuona na


ukiwa haumuoni basi yeye anakuona,


yaani uhisi hivyo, na uifanye kwa namna


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٢١


Sunna ya mtume wake Muhammad


(rehema na amani za MwenyeziMungu


ziwe juu yake) inavyoeleza na bila ya


kuikhalifu.


Na yote yaliyotangulia yanakusanya


maana ya Dini ya Kiislamu. Na ina


eleweka ya kwamba Uislamu


umekwisha panga maisha ya watu wake


wakiwa mmoja mmoja, na wakiwa


makundi makundi, kwa mambo ambayo


yanawapa ufanisi katika dunia na akhera.


Ukawahalalishia kuowa na


ukawahimiza, na ukawaharamishia zinaa


na liwati na mambo yote mabaya. Na


ukawalazimisha kuunga jamaa na


kuwasikitikia mafukara na maskini, na


kuwatumikia, kama ulivyolazimisha na


kuhimiza katika kila tabia iliyo njema, na


ukaharamisha na kutahadharisha


kutokana na kila tabia mbaya, na


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٢٢


ukawahalalishia pato zuri (halali) kwa


kupitia biashara na ukodishaji, na mfano


wa hayo. Na ukaharamisha riba, na kila


biashara iliyo haramishwa, na kila jambo


lenye ulaghai na udanganyifu.


Kama ulivyotambuwa Uislamu tafauti


ya watu kutengenea (kunyoka) katika


njia yake, na kuchunga haki za wengine.


Ukaweka sheria za adhabu zenye


kukemea baadhi ya uvukaji mipaka


inayofungamana na haki zake


(Mwenyezi Mungu aliyetakasika), kama


kutoka kwenye Uislamu na zinaa, na


kunywa pombe, na makosa mengine


kama hayo.


Kama ulivyoweka sheria za adhabu


zenye kukemea uvamizi wa aina yoyote


wa haki za watu katika nafsi zao na mali


yao na heshima zao kama: kuuwa, au


kuiba, au kumsingizia mtu (kuwa


amezini bila ya kuwa na mashahidi) au


uvamizi kwa kupiga na kuudhi na


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٢٣


kuchukuwa mali za watu pasina haki. Na


ni adhabu zenye kulingana na kosa bila


ya kuongeza wala kupunguza,


Kama ulivyopanga na ukaweka mipaka


na uhusiano baina ya raiya na viongzi.


Na ukawalazimisha raiya kuwatii


(viongozi), katika mambo yasiyopelekea


kumuasi Mwenyezi Mungu. Na


ukaharamisha kutoka katika amri zao


hali itakayo pelekea ufisadi kwa watu


wote kwa jumla na kwa watu binafsi.


Na mwisho tunaweza kusema kuwa


Uislamu umefungamana na kujenga na


kuweka uhusiano sahihi, na matendo


sahihi baina ya mja na Mola wake, na


baina ya mwanadamu na jamii yake


katika mambo yake yote, hakuna kheri


yoyote miongoni mwa tabia na


utendajikazi isipokuwa Uislamu


umekwisha uongoza Umma wake, na


ukawahimiza kwayo, na hakuna shari


yoyote katika tabia na utendaji kazi ila


PDF created with pdfFactory trial version www.pdffactory.com


٢٤


Uislamu umekwisha utahadharisha


Umma wake, na ukawakataza, jambo


ambalo lina bainisha ukamilifu wa dini


hii, na uzuri wake katika pande zote.


Na kila sifa njema ni za Mwenyezi


Mungu


Mola wa viumbe vyote.






 



Machapisho ya hivi karibuni

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI

KWANINI UISLAMU? UZU ...

KWANINI UISLAMU? UZURI NA FAIDA ZA UISLAMU