Nakala




DINI YA KWELI YA MWENYEZI MUNGU NI IPI?


ila mtu huzaliwa katika mazingira au hali ambayo si chaguo


lake mwenyewe. Hupachikwa dini ya familia yake au


mtazamo wa taifa lake toka mwanzoni mwa kuwepo kwake


katika dunia hii. Wakati anapofikia ujana wa (miaka 13 – 20), kwa


kawaida hulazimika kuamini kwamba imani ya jamii yake ndiyo


imani sahihi ambayo kila mtu anapaswa kuwa nayo. Ingawa wakati


fulani baadhi ya watu wanapokuwa wakubwa na wakaona imani


nyingine huanza kuuliza na kuhoji ukweli wa imani yao. Wale


wanaotafuta ukweli mara kwa mara hufikia mahali


wakachanganyikiwa wanapogundua kwamba kila dini, dhehebu, au


falsafa hudai ndio njia pekee iliyo sahihi kwa mwanadamu, kwani


makundi yote hayo yanahamasisha watu kufanya matendo mema.


Sasa ni ipi imani sahihi? Zote haziwezi kuwa sahihi, kwani kila moja


hudai kuwa nyingine zote si sahihi. Sasa katika hali hiyo, yule


anayetafuta ukweli vipi ataweza kuchagua njia iliyosahihi?


Mwenyezi Mungu ametupa sote akili na uwezo wa kutuwezesha


kufanya maamuzi sahihi na ya maana. Nayo ni maamuzi muhimu sana


katika maisha ya mwanadamu. Mustakabali wake unautegemea uamuzi huo,


kufuatana na hilo, kila mmoja wetu lazima achunguze ushahidi


uliotolewa bila kupendelea ndipo achague kile kinachoonekana kuwa


ni sahihi mpaka pale ushahidi mwingine utakapotokea.


Kama ilivyo kwa kila dini au falsafa, Uislamu nao unadai kuwa huo


ndio njia ya pekee iliyo sahihi kuelekea kwa Mwenyezi Mungu.


Katika hali hiyo ya Uislamu kudai kuwa ni njia sahihi si tofauti na


mifumo mingine. Kijitabu hiki kinakusudia kukupa ushahidi juu ya


ukweli wa dai hilo. Hata hivyo, mara zote ni lazima izingatiwe


kwamba, mtu anaweza kuipata njia ya kweli kwa kuweka kando hisia


na chuki, vitu ambavyo mara kwa mara hutupofua tusiuone ukweli.


Kisha, baada ya kufanya hivyo tu, ndipo tutakapoweza kutumia akili


zetu tulizopewa na Mwenyezi Mungu kufanya maamuzi ya kiakili na


yaliyo sahihi?


Kuna hoja mbali mbali ambazo zinaweza kutolewa ili kulipa nguvu


dai la Kiislamu kuwa ndio dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu.


K


3


Zifuatazo ni hoja tatu zilizo wazi sana. Ya kwanza inaegemea juu ya


ukweli wa asili ya majina ya dini na upana wa maana zake. Hoja ya


pili inahusiana na mafundisho ya kipekee na yasiyotatanisha


yanayoonyesha uhusiano kati ya Mwenyezi Mungu, mwanadamu na


uumbaji. Hoja ya tatu inatokana na ukweli kwamba Uislamu ni dini ya


dunia nzima kwa watu wote na kwa nyakati zote. Hizi ndizo hoja tatu


za msingi ambazo kimantiki na kiakili zinalazimu ziwepo kwa dini


yeyote ile ili izingatiwe kuwa ni dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu.


Kurasa zifuatazo zitaufafanua ufahamu huo kikamilifu.


4


JINA LA DINI


itu cha kwanza kabisa ambacho mtu anapaswa kukijua na


kukifahamu kwa kina kuhusu Uislamu ni juu ya maana ya


neno lenyewe “Uislamu.” Neno hilo ni la asili ya Kiarabu


lenye maana ya kutii au kusalimisha matakwa ya mtu kwa Mwenyezi


Mungu wa kweli wa pekee, ajulikanaye kwa Kiarabu kama “Allah”.


Mtu ambaye amesalimisha matakwa yake kwa Mwenyezi Mungu


(Allah) huuitwa “Mwislamu”. Dini ya Kiislamu haikupewa jina


kutokana na jina mtu au watu, wala halikuamuliwa na kizazi chochote


cha wanadamu kama vile Ukristo ambao ulipewa jina kutokana na


“Yesu Kristo”, Ubudha unatokana na jina la Gautama Buddha,


Kunfushian, unatokana na Confucius, Umaksi ulipewa jina la Karl


Marx; Uyahudi unatokana na jina la kabila la Yuda na Ubaniani


(Uhindu) unatokana na jina la Hindu. Uislamu (kutii amri za Mwenyezi


Mungu) ni dini aliyopewa Adam, mtu wa kwanza na mtume wa


kwanza wa Mwenyezi Mungu, na Uislamu ndio dini ya mitume wote


waliotumwa na Mwenyezi Mungu kwa wanadamu. Kwa kuongezea,


jina la Uislamu lilichaguliwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe na


limetajwa wazi wazi katika kitabu cha mwisho cha Allah (Quran).


Allah alimfunulia mwanadamu katika kitabu cha mwisho


alichomfunulia Mwanadamu. Katika ufunuo wa mwisho, uitwao kwa


Kiarabu Al-Quran Allah ameeleza yafuatayo:-


“… Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na kukutimizieni neema


Yangu, na Nimekupendeleeni Uislamu uwe Dini yenu…” [Quran 5:3]


“Na anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa


kwake…” [Quran 3:83]


Kwa hiyo, Uislamu haudai kuwa ni dini mpya iliyoletwa Arabuni na


Mtume Muhammad katika karne ya saba, lakini Uislamu ni


mwendelezo wa sehemu ya mwisho ya dini ya Allah, kama


ilivyofunuliwa toka mwanzo kwa Adam na mitume waliomfuatia.


Hadi kufikia hapa tutatoa maoni kwa ufupi kuhusu dini nyingine mbili


zinazodai kwamba ndizo njia sahihi. Hakuna sehemu yoyote katika


Biblia ambayo utakuta kwamba Mwenyezi Mungu amewafunulia


K


5


watu wa Mtume Musa au vizazi vyao kwamba dini yao inaitwa


Uyahudi, au kwa wafuasi wa Kristo kuwa dini yao inaitwa Ukristo.


Kwa maneno mengine, majina “Uyahudi" na "Ukristo” hayakutokana


na asili ya Mwenyezi Mungu wala hayani idhini yake. Jina Ukristo


halikuwepo hadi muda mrefu baada ya kuondoka Yesu ndipo jina hilo


lilipotolewa kwa dini ya Yesu.


Sasa nini lililokuwa jina la kweli hasa, la dini ya Yesu, ambalo


linajipambanua na jina lake? (Majina yote mawili Yesu na Kristo


yanatokana na maneno ya Kiebrania, kupitia Kigiriki na Kilatini.


Jesus ni Kingereza na kwa Kilatini cha Kigiriki ni Iesous, ambalo kwa


Kiebrania ni Yeshua au Yehoshua' (Joshua). Neno la Kigiriki Christos


ni tafsiri ya Kiebrania kwa neno “Messiah”, jina la heshima


linalomaanisha “Mpakwa mafuta.” Dini yake inaakisi mafundisho


yake, ambayo aliwaamrisha wafuasi wake kuyakubali kama misingi


ya kuwaongoza katika uhusiano wao na Mwenyezi Mungu. Katika


Uislamu, Yesu ni mtume aliyeletwa na Allah na jina lake la Kiarabu


ni Issa. Kama ilivyo kwa mitume ya kabla yake, yeye naye


aliwalingania watu wasalimishe matakwa yao kwa matakwa ya


Mwenyezi Mungu (jambo ambalo ndilo linalosimamiwa na Uislamu).


Kwa mfano katika Agano Jipya inasemekana kwamba Yesu


aliwafundisha wafuasi wake kusali kwa Mwenyezi Mungu kama


ifuatavyo:-


“Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje,


[Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.] (Luka


11:2/Mathayo 6:9).


Wazo hili lilisisitizwa sana na Yesu katika maelezo yake mengi


yaliyoandikwa katika Biblia. Kwa mfano, amefundisha kuwa,


waliojisalimisha kwa Mwenyezi Mungu, hao peke yao ndio


watakaopata uzima wa milele. (Peponi).


Yesu pia alifafanua kwamba yeye mwenyewe amejisalimisha kwa


matakwa ya Mwenyezi Mungu.


6


“Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme


wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye


mbinguni.” (Mathayo 7:21).


“Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo


nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti


mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.” (Yohana


5:30).


Kuna maelezo mengi katika Biblia yanayoonesha kwamba Yesu


aliweka wazi kwa wafuasi wake kwamba yeye siye Mungu.


Kwa mfano, aliposema kuhusu saa ya mwisho alisema:


“Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika


walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba. (Marko 13:-32).


Kwa hiyo, Yesu kama walivyokuwa Mitume waliopita kabla yake na


yule aliyekuja baada yake, alifundisha dini ya Kiislamu:


kujisalimisha kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu mmoja aliye wa


kweli.


7


MWENYEZI MUNGU NA UUMBAJI


wa vile jambo la mtu kujisalimisha kikamilifu kwa Mwenyezi


Mungu linamaanisha kiini cha kuabudu, ujumbe wa msingi


wa dini ya Mwenyezi Mungu, Uislamu ni kumwabudu


Mwenyezi Mungu peke yake. Vilevile Uislamu unawataka watu


waachane na kuabudu binadamu, eneo au kitu zaidi ya Mwenyezi


Mungu. Kwa vile vitu vyote ukimtoa Mwenyezi Mungu muumbaji wa


vitu vyote, ni uumbaji wa Mwenyezi Mungu; inawezekana kusemwa


kwamba Uislamu kimsingi unamlingania mtu aache kuabudu viumbe


na kumwita amwabudu muumbaji wake pekee. Yeye ndiye pekee


anayestahiki kuabudiwa na watu, kwa sababu ni kwa matakwa yake


yeye tu ndipo maombi yote hujibiwa.


Kutokana na hilo, endapo mwanadamu atauomba mti na maombi yake


kujibiwa, basi akumbuke kwamba si mti uliojibu maombi yake bali ni


Mwenyezi Mungu, ndiye aliyeruhusu maombi hayo yawe kama


alivyoomba. Mtu anaweza kusema, “jambo hilo lipowazi”. Hata


hivyo, kwa wale wanaoabudu miti, inawezekana isiwe hivyo. Vivyo


hivyo, wale wanaomwabudu Yesu, Budha, au Krishna au mtakatifu


Kristofa, au mtakatifu Jude au hata Muhammad, maombi yao


hayajibiwi na hao, bali yanajibiwa na Mwenyezi Mungu. Yesu


hakuwaambia wafuasi wake wamwabudu yeye bali aliwaambia


wamwabudu Mwenyezi Mungu, kama inavyoeleza Quran:


"Na (kumbukeni) Mwenyezi Mungu atakaposema: "Ewe Isa bin


Maryamu! Je, wewe uliwaambia watu: 'Nifanyeni mimi na mama


yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu'?" Aseme (Nabii


Isa): "Wewe umetakasika na kuwa na mshirika. Hainijuzii mimi


kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uwongo).


(Quran 5:116)


Yesu hajajiabudu yeye mwenyewe alipokuwa anaabudu, lakini


alimwabudu Mwenyezi Mungu. Yesu amenukuliwa ndani ya Biblia


akisema,


“…Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye


peke yake.” (Luka 4:8).


K


8


Kanuni hii ya msingi ipo katika sura ya kwanza katika Quran


ijulikanayo kama Suratul-Fatiha, aya ya nne


“Wewe tu ndiye tunayekuabudu, na Wewe tu ndiye tunayekuomba


msaada.” (Quran 1:5)


Na katika sehemu nyingine ndani ya Kitabu cha ufunuo wa mwisho,


ambacho ni Quran, pia Mwenyezi Mungu amesema:


“Na Mola wenu Anasema: “Niombeni Nitakujibuni.” (Quran 4:60)


Ni muhimu mno kusisitiza kwamba msingi wa ujumbe wa Uislamu


(umetaja kumwabudu Mwenyezi Mungu peke yake) pia umetangaza


kwamba Mwenyezi Mungu na viumbe vyake ni tofauti kabisa.


Mwenyezi Mungu hayuko sawa na viumbe vyake wala si sehemu ya


viumbe vyake, na wala viumbe vyake si sawa Naye na wala si sehemu


ya Uungu.


Hili lawezekana kuonekana ni jambo lililowazi, lakini kitendo cha


mwanadamu kuabudu viumbe, badala ya Muumba kwa kiasi kikubwa


Kinatokana na ujinga au kupuuza, ufahamu huu. Ni imani ya baadhi


ya watu kwamba kuwepo kwa Mwenyezi Mungu kupo kila mahala


katika viumbe vyake au kuwepo kwa uungu wake kupo au


kulikuwepo katika baadhi ya sehemu za viumbe vyake, jambo


lilowahalalishia waabudu viumbe vya Mwenyezi Mungu na kusema


kuwa wanamwabudu Mungu. Hata hivyo, ujumbe wa Uislamu kama


ulivyoletwa na Mitume ya Mwenyezi Mungu, ni kumwabudu


Mwenyezi Mungu peke yake na kuacha kuabudu viumbe vyake kwa


moja kwa moja au kwa kutumia njia yoyote ile.


Katika Quran Mwenyezi Mungu amesema wazi wazi:


“Na bila shaka Tulimpeleka Mtume katika kila umma ya kwamba:


“Muabuduni Mwenyezi Mungu na mwepukeni (Iblisi) muovu.”


(Quran 16:36)


Wakati wale wanaoabudia masanamu wanapoulizwa; kwa nini


wanaabudu masanamu yaliyotengeneza na Wanadamu? Jibu la siku


9


zote ni kuwa; kwa hakika wao hawaiabudu ile picha ya jiwe bali


wanaabudia Mwenyezi Mungu aliyopo katika masanamu hayo.


Wanadai kwamba masanamu hayo ni sehemu za kumuelekea


Mwenyezi Mungu tu na si Mwenyezi Mungu mwenyewe! Mtu


aliyekubali wazo la kuwa Mwenyezi Mungu kwa namna yoyote ile


yupo ndani ya viumbe vyake atalazimika kukubali hoja hii ya kuabudu


masanamu. Wakati, mtu aliyeufahamu vizuri msingi wa ujumbe wa


Uislamu na utekelezwaji wake kamwe hawezi kukubali kuabudia


masanamu hata kama kutajengewa hoja za kimantiki.


Wale waliodai ungu tangu zamani mara kwa mara wameelekeza


madai yao katika imani potofu ya kwamba Mwenyezi Mungu yu


katika mwanadamu. Tukienda hatua moja mbele, wanadai kuwa


Mwenyezi Mungu yu pamoja nao kuliko alivyo kwetu sisi tuliobakia,


kwa hiyo, wanadamu wanapaswa kunyenyekea kwao na kuwaabudu


wao kama vile Mwenyezi Mungu aliye katika mwanadamu au


Mwenyezi Mungu aliejiingiza kwa wanadamu. Vilevile wale


wanaotangaza uungu wa watu wengine baada ya kufa kwao wamepata


ardhi yenye rutba miongoni mwa wale wanaoamini imani potofu ya


kuwa Mwenyezi Mungu yupo ndani ya mwanadamu.


Hadi sasa hivi, lazima iwe wazi kabisa kwamba mtu aliyeelewa


msingi wa ujumbe wa Uislamu na vidokezo vyake kamwe hawezi


kukubali kumwabudu mwadamu mwenzake katika hali yoyote ile.


Dini ya Mwenyezi Mungu, kwa asili, ni wito uliowazi wa kumwabudu


Muumba na kukataa kuabudu viumbe kwa namna yoyote ile. Na hii


ndio maana ya wito wa Uislamu.


"Laa Ilaha Ill Allah" (Hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila


Allah).


Kutamka kwa dhati ibara hii na kumkubali Mtume, moja kwa moja


kunampelekea mtu kuwa katika Uislamu, na imani ya dhati kwa


tamko hilo humuhakikishia mtu kuingia Peponi. Kwa hiyo, Mtume wa


mwisho wa Uislamu (S.A.W) amenukuliwa akisema kuwa, “Yeyote


asemaye: Hakuna Mungu wa haki ispokuwa Allah, na akafa akiwa na


imani hiyo ataingia Peponi.”


10


Imani juu ya tamko hili la kiitikadi inamtaka mtu kusalimisha


matakwa yake kwa Mwenyezi Mungu kwa namna zilizofundishwa na


Mitume ya Mwenyezi Mungu. Vilevile tamko hilo linamtaka muumini


aache kuabudu miungu ya uongo.


11


UJUMBE WA DINI ZA UWONGO


una madhehebu, makundi ya kidini, dini, falsafa, na harakati


nyingi duniani, yote hayo yanadai kuwa ndio njia sahihi au


ndio njia ya pekee ya Mwenyezi Mungu. Sasa vipi mtu


ataweza kugundua ni kundi lipi lililosahihi au kama yote ni sahihi?


Njia moja ya kupata jibu la swali hilo ni kuondoa tofauti za kijuu juu,


katika mafundisho ya wadai mbali mbali ili kuufikia ukweli, na


kutambua kitu kikuu kinachoabudiwa na kitu hicho ndicho hasa


wanachokilingania, moja kwa moja au sio moja kwa moja. Dini za


uongo zote, kikawaida, zina hoja moja maarufu iliyo ya msingi juu ya


Mwenyezi Mungu, aidha wanadai wanaume wote ni miungu, au


wanaume fulani tu ndiyo miungu au maumbile (nature) ndiyo


Mwenyezi Mungu au Mwenyezi Mungu ni kitu kilichopo tu katika


dhana za watu.


Kwa hiyo, kuna uwezekano wa kusema kwamba, msingi wa ujumbe


wa dini za uongo ni kwamba Mwenyezi Mungu anaweza kuabudiwa


kwa mfumo wa umbaji wake. Dini za uongo huwaita watu waabudu


viumbe vya Mwenyezi Mungu kwa kuviita viumbe hivyo au sehemu


ya viumbe hivyo ni Mwenyezi Mungu. Kwa mfano, Nabii Issa (Yesu)


aliwaita, wafuasi wake wamwabudu Mwenyezi Mungu, lakini wale


wanaodai kuwa wao ni wafuasi wa Yesu leo hii wanawalingania watu


wamwabudu Issa (Yesu), wakidai kwamba yeye ni Mwenyezi Mungu.


Budha alikuwa mrekebishaji ambaye alianzisha kanuni mbali mbali za


kibinadamu katika dini ya Kihindu. Hakudai kuwa yeye ndiye Mungu


mwenyewe, wala hakupendekeza kwa wafuasi wake kwamba yeye


awe wa kuabudiwa. Leo hii, Mabudha wengi mno walio nje ya India


wanamfanya yeye (Budha) kuwa ni Mwenyezi Mungu na wanasujudia


masanamu yaliyotengenezwa kwa sura yake.


Kwa kutumia msingi wa kutambua kitu kinachoabudiwa, tunaweza


kuzigundua kwa urahisi dini za uongo na asili ya vyanzo vyake.


Kama Mwenyezi Mungu alivyosema katika Quran:


K


12


“Hamuabudu badala yake (Mwenyezi Mungu ila majina (matupu)


mliyoyapanga nyinyi wenyewe na baba zenu (mkayaita hayo


masanamu). Mwenyezi Mungu hakuteremsha dalili kwa hayo.


Haikuwa hukumu ila hii ya Mwenyezi Mungu tu; Ameamrisha


msimuabudu yoyote ispokuwa Yeye tu. Hiyo ni Dini madhubuti,


lakini watu wengi hawajui”. (Quran 12:40)


Watu wanaweza kutoa hoja kwamba dini zote zinafundisha mema,


kwa hiyo, kuna haja gani ya kujali kuifuata dini mojawapo? Jibu ni


kwamba dini za uwongo zote zinafundisha dhambi kubwa sana ya


kuabudu viumbe. Kuabudu viumbe ni dhambi kubwa kabisa awezayo


kuifanya mwanadamu kwa sababu tendo hilo linapingana na lengo la


kuumbwa kwake.


Mwanadamu ameumbwa ili kumwabudu Mwenyezi Mungu tu kama


Allah alivyosema katika Quran:


“Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu”. (Quran 51:56)


Matokeo yake, kuabudu viumbe; jambo ambalo ni asili ya kuabudu


masanamu ni dhambi pekee isiyosameheka. Mtu atakayekufa katika


hali hiyo ya kuabudu masanamu, ameshaangamiza majaaliwa yake ya


ahera. Hii si rai ya mtu, bali ni ufunuo wa kweli ulioelezwa na


Mwenyezi Mungu katika ufunuo wake wa mwisho kwa wanadamu:


“Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe kushirikishwa; na Husamehe


yasiyokuwa haya kwa amtakaye. (4:48 na 116)


13


DINI YA MWENYEZI MUNGU NI YA ULIMWENGU MZIMA


wa vile matokeo ya kufuata dini ya uwongo ni hatari sana,


dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu ni lazima ifahamike dunia


nzima, iwe imepatikana dunia nzima wakati uliopita na


lazima idumu milele na iwe inafahamika milele na ipatikane dunia


zima. Kwa maneno mengine, dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu


haiwezi kuwa na mipaka kwa watu fulani tu, eneo, au kipindi fulani


tu. Wala si jambo la kimantiki kwamba dini kama hiyo iamuru


mazingira yasiyo na maana yoyote katika uhusiano kati ya


mwanadamu na Mwenyezi Mungu kama vile, kubatiza, au imani


kwamba mwanadamu ni mwokozi, au ni mpatanishi. Katika kanuni


kuu ya Uislamu na ambayo maana yake ni (kusalimisha matakwa ya


mtu kwa Mwenyezi Mungu) ndipo inapopatikana mizizi ya Uislamu


kuwa wa dunia nzima. Wakati wowote mwanadamu anapotambua


kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja na ametofautiana na viumbe vyake,


na mtu huyo akajisalimisha kwa Mwenyezi Mungu, Mtu huyo


anakuwa Mwislamu kimwili na kiroho na anastahiki Pepo.


Kwa hiyo, mtu yoyote katika muda wowote hata yule aishiye maeneo


ya mbali anaweza kuwa Mwislamu, mfuasi wa dini ya Mwenyezi


Mungu, Uislamu, kwa kukataa moja kwa moja kuabudu viumbe na


kuamua kumgeukia Mwenyezi Mungu peke yake.


Ni lazima ikumbukwe, hata hivyo, ili kujisalimisha kwa matakwa ya


Mwenyezi Mungu kikweli kweli, mtu ni lazima achague baina ya haki


na batili. Kwa hakika, binadamu amejaaliwa uwezo na Mwenyezi


Mungu sio tu wa kutofautisha kati ya wema na uwovu bali vilevile


kuchagua kati ya vitu viwili hivyo.


Huu uwezo wa kupewa na Mwenyezi Mungu unabeba majukumu


muhimu sana, nayo ni kuwa, mwanadamu atajibu kwa Mwenyezi


Mungu juu ya chaguo alilolichagua. Kinachofuata mwanadamu


anapaswa ajaribu kwa kutumia uwezo wake wote afanye mema na


aache maovu.


Ufahamu huu umeelezwa katika ufunuo wa mwisho kama ifuatavyo:


K


14


“Katika walioamini (Mitume ya zamani huko) na Mayahudi na


Wakristo na Wasabai; yoyote (miongoni mwao) atakayemwamini


Mwenyezi Mungu (sasa kama anavyosema Nabii Muhammad) na


akaamini Siku ya Mwisho na akafanya vitendo vizuri, basi watapata


thawabu zao kwa Mola wao, wala haitakuwa khofu juu yao, wala


hawatahuzunika. (Quran 2:62)


Ikiwa kwa sababu yoyote ile, wanadamu watashindwa kuukubali


ujumbe wa mwisho baada ya kuelezwa bayana, watakuwa katika


hatari kubwa mno. Mtume wa mwisho amesema:


"Yoyote miongoni mwa Wakristo na Wayahudi atakayesikia habari


zangu na akaendelea na imani ya kukakanusha kile nilichokuja nacho


na akafa katika hali hiyo atakuwa ni miongoni mwa wakazi wa


Motoni."


(Sahih Muslim [English Translation], Vol.1 p.91 N0, 284)


15


KUMTAMBUA MWENYEZI MUNGU.


wali linalojitokeza hapa ni: vipi itarajiwe kuwa watu wote


watamwamini Mwenyezi Mungu mmoja wa kweli, ukizingatia


watu hao wana asili za jamii na tamaduni tofauti tofauti? Ili


watu wawajibike kwa kumwabudu Mwenyezi Mungu mmoja wa


kweli, wanahitaji wapate elimu ya kumtambua Mwenyezi Mungu.


Ufunuo wa mwisho unafundisha kwamba wanadamu wote wana athari


ya kumtambua Mungu mmoja wa kweli athari ambayo iliwekwa


katika nafsi zao ikiwa ni kama sehemu ya asili yao waliyoumbiwa


nayo.


Katika sura ya saba ya Quran (Al-Aaraf, aya ya 172 – 173), Mwenyezi


Mungu ameeleza kwamba wakati alipomuumba Adam alijaalia kizazi


cha Adam kuwepo ulimwenguni na Mwenyezi Mungu akuchukua


ahadi toka kwao na kuwaambia: “Je, Mimi siye Mola wenu?"


Wakasema: “Ndiye; tunashuhudia (kuwa Wewe ndiye Mola wetu)."


Kisha Allah akaeleza sabababu za kuwalazimisha wanadamu wote


wakiri kwamba yeye ndiyo muumba wao na ndiye Mwenyezi Mungu


wa kweli wa pekee anayestahiki kuabudiwa. Amesema:


“Msije mkasema Siku ya Kiyama kuwa sisi tulikuwa tumeghafilika na


hayo (hatuyajui). (Quran 7:172)


Hii inamaanisha kwamba, hatuwezi kudai katika siku hiyo kwamba


tulikuwa hatujui kuwa Allah ndiye Mungu wetu na kwamba hakuna


mtu aliyetwambia kwamba tulipaswa kumwabudu Allah peke yake.


Allah akaendelea kuelezea kuwa:


“Au mkasema, Baba zetu ndio walioshirikisha zamani, nasi tulikuwa


kizazi nyuma yao, basi Utatuangamiza kwa sababu ya yale


waliyoyafanya waovu?” (Hamuwezi kusema haya kwani nyote


Tumekufahamisheni, nyinyi na wao). (Quran 7:173).


S


16


Kwa hiyo, kila mtoto huzaliwa na imani ya kumtambua Mwenyezi


Mungu na mwelekeo wa kumwabudu Mwenyezi Mungu pekee. Imani


hii ya kuzaliwa nayo na mwelekeo huo huitwa kwa Kiarabu “Fitrah”.


Mtume Muhammad (S.A.W) ameeleza kwamba Allah amesema,


“Niliwaumba waja wangu katika dini sahihi, lakini shetani


aliwapoteza.” Vilevile Mtume amesema, “Kila mtoto huzaliwa katika


Fitrah. Kisha wazazi wake wanamfanya aidha awe Myahudi, Mkristo


au Mmajusi (waabudio moto).’’ Ikiwa mtoto ataachwa peke yake,


atamwabudu Mwenyezi Mungu kwa namna yake mwenyewe, lakini


watoto wote huathiriwa na mazingira. Kwa hiyo, ni kama vile mtoto


anatii sheria za kimaumbile, ambazo Allah ameziamrisha kimaumbile,


katika hali hiyo hiyo nafsi yake pia inatii maumbile ya kuwa Allah ni


Mola na Muumba wake. Lakini, ikiwa wazazi wake watajaribu


kumfanya afuate njia tofauti, mtoto anakuwa hana nguvu za kutosha,


hasa hasa katika hatua zake za mwanzo za maisha yake, za kuzuia na


kupinga matakwa ya wazazi wake.


Katka hali kama hizo, dini ambayo mtoto anaifuata, ni tamaduni na


malezi, na Mwenyezi Mungu hamuhesabu wala hamuadhibu kwa dini


hiyo mpaka atakapofikia umri fulani maishani mwake. (baleghe).


17


DALILI ZA MWENYEZI MUNGU.


atika hatua zote za maisha ya wanadamu, kutoka utoto hadi


kufikia kufariki, dalili za Mwenyezi Mungu mmoja wa kweli


zinaonyeshwa kwao katika pande zote za dunia na katika


nafsi zao mpaka inapowabainikia kwamba kuna Mwenyezi Mungu


mmoja tu wa kweli (Allah). Mwenyezi Mungu amesema katika


Quran:


“Tutawaonyesha (ukweli wa) Maneno Yetu haya katika nchi za mbali


na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni


kweli…” (Quran: 41:53)


Ufuatao ni mfano wa ufunuo wa Mwenyezi Mungu kwa dalili ya kosa


la mtu mmoja la kuabudu sanamu. Katika maeneo ya kusini mashariki


mwa msitu wa Amazoni huko Brazili, Amerika ya Kusini watu wa


kabila la wasiostaarabika walijenga kibanda kipya ili kuhifadhi


sanamu la mtu liitwalo Skwatch, likiwa ni Mungu mkuu wa viumbe


vyote.


Siku iliyofuatia kijana mmoja aliingia kibandani kutoa heshima kwa


Mungu huyo, na alipokuwa ameinama (kukisujudia) kile alichofunzwa


kuwa ndicho Muumba na Mpaji wake, ghafla mbwa mkondefu


mwenye viroboto na mafunza aliingia pole pole mule kibandani. Yule


kijana aliinua kichwa chake kwa kitambo kidogo akamtazama yule


mbwa, akiinua mguu wake wa nyuma na kulikojolea lile sanamu.


Yule kijana alimfukuza yule mbwa nje ya kile kibanda kikatili, lakini


mara tu ghadhabu zake zilipoisha alitambua kwamba lile sanamu


kamwe haliwezi kuwa Mola wa Ulimwengu wote. Mwenyezi Mungu,


lazima atakuwa yupo sehemu nyingine, alihitimisha. Ni jambo la


kushangaza kama linavyoweza kuonekana, mbwa kulikojolea lile


sanamu ilikuwa ni alama kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa kijana


huyo. Alama hii imebeba ujumbe mtakatifu kwa kuwa kile


alichokuwa akikiabudu kilikuwa cha uwongo. Huo ni ukombozi


kutoka utumwa wa kufuata mafundisho ya utamaduni wa kuabudu


mungu wa uongo. Matokeo yake, mtu huyu amehiyarishwa: aidha


K


18


amtafute Mwenyezi Mungu wa kweli au aendelee katika njia yake ya


makosa.


Allah (S.W) anataja utafutaji wa kumtafuta Mwenyezi Mungu


unaomuhusu Mtume Ibrahimu kuwa ni mfano wa jinsi ya wale wote


wanaofuata dalili zake wataongozwa katika njia sahihi.


“Na namna hivi Tulimwonyesha Ibrahimu ufalme wa mbingu na ardhi


(kuwa ni wa Mungu), na ili awe miongoni mwa wenye yakini. Na


usiku ulipomwingilia (Ibrahimu na hali kakaa na makafiri), akaona


nyota, alinena (makusudi kutaka kuwavuta watumie fikra zao):


“(Nyota) hii ni Mola wangu.” Ilipotua (ikapotea), alisema (kuwaambia


wale makafiri kama kwamba yu pamoja nao katika ibada ile):


“Sipendi waola wanaopotea (hawawepo ila wakati makhsusi tu).” Na


(usiku wa pili) alipouona mwezi unachomoza alisema (kuwaambia


wale marafiki zake wa kikafiri): “Huu (mwezi) ndio Mola wangu.”


Ulipotua alisema: “Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa


miongoni mwa watu wapotofu. (Na mola huyu hawezi kuniongoza


kwani anakuwa hayupo wakati mwengine).” Na (siku ya tatu)


alipoliona jua linachomoza alisema (kuwaambia): “Hili (jua) ndilo


Mola wangu. Huyu (mola) mkubwa kabisa,” lilipotua alisema: “Enyi


watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha (na Mungu)


“Mimi nimeuelekeza uso wangu kwa Yule aliyeziumba mbingu na


ardhi. Hali ya kuwa nimewacha dini za upotevu. Mimi (ni Mwislamu)


wala si miongoni mwa washirikina.” (Quran 6:75-79)


Kama tulivyosema hapo mwanzoni, Mitume wametumwa kwa kila


taifa na kila kabila ili kuiwezesha imani ya kimaumbile ya


mwanadamu juu ya Mwenyezi Mungu na ule mwelekeo wa


kumwabudu Yeye, pia kuutia nguvu ukweli mtatakatifu kwa dalili na


alama za kila siku zinazooneshwa na Mwenyezi Mungu. Ingawa


mafundisho mengi ya Mitume hao yamebadilishwa, baadhi ya sehemu


zinazofunua ujumbe wa zimebakia bila kuvurugwa na zinahudumia


katika kuwaongoza watu katika kuchagua kati ya haki na batili.


Athari za ujumbe uliofunuliwa na Mwenyezi Mungu kwa muda mrefu


zinaweza kuonekana katika "Amri Kumi" za Torati ya Wayahudi


ambazo baadaye ziligeuzwa na kuwa katika mafundisho ya Kikristo,


19


vilevile, kuwepo kwa sheri dhidi ya uuaji, wizi na uzinzi katika jamii


nyingi kote kote katika zama za kale na za sasa za ulimwengu.


Matokeo ya alama za Mwenyezi Mungu kwa wanadamu wa zama zote


zikiwa na ufunuo wake kupitia Mitume yake, wanadamu wote


wamepewa nafasi ya kumtambua mungu wa kweli wa pekee.


Matokeo yake, kila nafsi itahesabiwa kwa imani yake juu ya


Mwenyezi Mungu na kwa kukubali kwake dini ya kweli ya Mwenyezi


Mungu, iitwayo Uislamu, ambayo inamaanisha utiifu mkamilifu kwa


matakwa ya Allah.


20


HITIMISHO


aelezo yaliyotangulia yamefafanua kwamba jina la dini ya


Kiislamu linaeleza wazo kuu na la msingi la Uislamu, ni


kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu, na kwamba jina


"Uislamu" halikuchaguliwa na mwanadamu, bali lilichaguliwa na


Mwenyezi Mungu, kwa mujibu wa vitabu vitakatifu vya Uislamu.


Vilevile imeoneshwa kwamba ni Uislamu pekee unaofundisha


kwamba Mwenyezi Mungu ni mmoja na Sifa zake na unaamrisha


kumwabudu Mwenyezi Mungu tu bila ya mshirika. Mwisho, kutokana


na utakatifu wa mwelekeo ulioingizwa pole pole kwa mwanadamu ili


amwabudu Mwenyezi Mungu na dalili zilizooneshwa na Mwenyezi


Mungu kwa miaka mingi kwa kila mtu, Uislamu unaweza kufikiwa na


watu wote kwa nyakati zote.


Kwa ufupi, maana ya neno Uislamu (kujisalimisha kwa Allah),


Uislamu kikamilifu unakiri upweke wa Mwenyezi Mungu na ufikiwaji


wa Uislamu kwa watu wote katika nyakati zote kukinaisha watu


kuunga mkono dai la Uislamu la kwamba toka mwanzoni mwa


Ulimwengu katika lugha zote imeelezwa kwamba, Uislamu pekee


ndio uliokuwa na utakaoendelea kuwa dini pekee ya kweli ya


Mwenyezi Mungu.


Tunahitimisha kwa kumuomba Allah, Mtukufu, atuweke katika njia


iliyosahihi ambayo ametuongoza kwayo, na atupatie baraka na rehema


zake, kwani yeye ni Mwingi wa msamaha. Shukrani ziende kwa


Allah, Mola wa ulimwengu wote, na rehema na amani ziende kwa


Mtume Muhammad (S.A.W) na kwa Mitume ya Allah yote na kwa


wafuasi wao waliowema.


M



Machapisho ya hivi karibuni

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI

KWANINI UISLAMU? UZU ...

KWANINI UISLAMU? UZURI NA FAIDA ZA UISLAMU