Nakala




Adabu za safari na hukumu zake


2


Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu


wote, na rehema na amani ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad, na aali


zake na Maswahaba zake wote.


Ama baada ya hayo:


Hii ni makala fupi kuhusu adabu za safari na hukumu zake. Tumepupia


ndani yake kuweka wazi mambo ambayo aghalabu anayahitajia msafiri.


Tunamuomba Mwenyezi Mungu aifanye iwe kwa ajili ya uso wake


mtukufu, na anufaishe kwayo Waislamu wote.


Jumuiya ya Masomo mbalimbali ya Kiislamu katika lugha mbalimbali


Adabu za safari na hukumu zake


Kwanza: Adabu za safari


Mwenye kusafiri kwenda Hija au safari nyingine ya kiibada anafaa


kuzingatia yafuatayo:


Amuombe Mwenyezi Mungu Mtukufu amchagulie muda sahihi wa


safari, kipando, rafiki wa kuendana naye, na muelekeo wa njia ikiwa njia


zitakuwa nyingi. Na awatake ushauri kuhusu safari hiyo watu wenye


uzoefu na wale walio wema. Ama Hija na Umra, ibada hizo ni za heri na


hakuna shaka katika hilo. Na namna ya kumuomba Mwenyezi Mungu


amchagulie jambo ni: Aswali rakaa mbili kisha aombe dua iliyopokelewa


kutoka kwa Mtume - remema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.


Ni wajibu kwa mwenye kufanya ibada ya Hija na Umra akusudie katika


Hija yake na Umra yake uso wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kujiweka


karibu naye, na ajihadhari na kukusudia starehe za kidunia au


kujifaharisha au kupata umaarufu au kujionyesha au kutaka kusikiwa;


kwani kufanya hivyo kunasababisha kuharibika kwa matendo na


kutokubaliwa kwake. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:ْ


ُلﻗ)ﺎَﻣﱠﻧِإﺎَﻧَأ ٌَرﺷَﺑ ُْمﻛُﻠْﺛﱢﻣﻰَﺣُوﯾﱠﻲَﻟإِﺎَﻣﱠﻧَأ ُْمﻛُﮭَﻟإِ ٌﮫَﻟإِ ٌِدﺣوَاَنﻣَﻓ َنﺎَﻛُوﺟَْرﯾ َءﺎَﻘِ ﻟ ِﮫﱢﺑَر َْلﻣْﻌَﯾْﻠَﻓ ًﻼَﻣَﻋﺎًﺣِﻟﺎَﺻ


ﻻَ و ْْرِكﺷُﯾ ِدَةﺎَ ﺑِﻌِﺑ ِﮫﱢﺑَر(َدًاﺣَأ


"Sema: 'Mimi ni mwanadamu tu kama nyinyi. Ninaletewa Wahyi kwamba Mungu


wenu ni Mungu Mmoja tu. Kwa hivyo, mwenye kutaraji kukutana na Mola wake Mlezi,


basi naatende vitendo vyema, wala asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake


3


Mlezi.'" Na katika Hadithi takatifu: "Mimi ndiye niliyejitosheleza zaidi


kuhitaji mshirika. Atakayefanya jambo lolote akamshirikisha pamoja


nami mwingine, nitamuacha yeye na shirki yake (au na mshirika


wake)."


Ni wajibu kwa mwenye kufanya ibada ya Hija na Umra kujifunza


hukumu za Umra na Hija, na kujifunza hukumu za safari kabla ya kuanza


safari; ili asijekuwacha jambo la wajibu au akafanya jambo la haramu.


Amesema Mtume -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake:


"Yule ambaye Mwenyezi Mungu amemtakia heri, humpa ufahamu wa


dini."


Ni wajibu kwa mwenye kukusudia kufanya Hija au Umra achaguwe


mali halali kwa ajili ya ibada yake ya Hija na Umra; kwa sababu Mwenyezi


Mungu ni mzuri na hakubali isipokuwa kilicho kizuri; na kwa sababu mali


haramu husababisha kutojibiwa maombi.


Kutubia madhambi yote na maasi, na ikiwa aliwadhulumu watu,


atarudisha alichokidhulumu na kuwataka wamwachilie. Ni sawa dhuluma


hiyo iwe ni kuhusiana na heshima, mali au haki nyingine.


Inapendekezwa kwa msafiri aandike wasia wake, na kuandika


anachodai na anachodaiwa. Amesema Mtume - rehema na amani za


Mwenyezi Mungu, ziwe juu yake: "Sio haki ya mtu Muislamu mwenye


jambo analotaka kulitolea wasia alale siku mbili, isipokuwa


ahakikishe kwamba anao wasia wake pamoja naye tayari


umeshaandikwa." Na auwekee wasia huo mashahidi, na alipe madeni


anayodaiwa, na arudishe amana kwa wenyewe au awatake idhini


ziendelee kubakia kwake.


Inapendekezwa kwa msafiri ajitahidi kuchaguwa rafiki mwema na


apupie kwamba yule amchaguaye ni miongoni mwa wanafunzi wenye


kujifunza elimu ya sheria; kwani kufanya hivyo ni sababu ya kufanikiwa na


kuepuka kuingia kwenye makosa katika safari yake na katika ibada yake


ya Hija na Umra. Haya ni kwa ushahidi wa maneno ya Mtume, rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Mtu huwa katika mwenendo


wa mwendani wake. Basi na aangalie mmoja wenu ni nani


anayemfanya kuwa mwendani wake." Na kwa maneno yake Mtume,


rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Usifuatane katika


safari zako isipokuwa na Muumini na asile chakula chako isipokuwa


mchamungu."


4


Inapendekezwa kwa msafiri kuwaaga watu wake, jamaa zake wa


karibu, majirani zake na marafiki zake. Amesema Mtume, rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Yeyote anayetaka kusafiri,


basi na awaambie wale anaowaacha: Astaudiukumullahu alladhiy laa


tadhwiiu wadaa'iuhu (Ninawaacha katika amana ya Mwenyezi


Mungu ambaye amana zake hazipotei)." Na alikua Mtume - rehema na


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - akiwaaga maswahaba zake


anapotaka mmoja wao kusafiri. Alikuwa akisema: "Astaudiullaaha


diinaka, wa amaanataka, wa khawaatiima a'malika (Ninamkabidhi


Mwenyezi Mungu dini yako, na amana yako na mwisho wa matendo


yako)." Na alikuwa Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe


juu yake - akimwambia msafiri mwenye kumtaka Mtume ampe wasia:


"Zawwadaka llaahut taqwa, waghafara dhambaka, wayassara lakal


khaira haithu ma kunta (Mwenyezi Mungu akupe uchamungu, na


akusamehe dhambi zako na aifanye kheri kuwa nyepesi kwako


mahala popote utakapokuwa)." Na alikuja mtu mmoja kwa Mtume -


rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - akitaka kusafiri na


akasema: 'Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, nipe wasia.' Akasema:


"Ninakuusia kumcha Mwenyezi Mungu, na kuleta Takbiira kila


unapofika sehemu ya muinuko." Alipoondoka, Mtume, rehema na


amani ziwe juu yake, akamuombea kwa kusema: "Ewe Mwenyezi


Mungu, mkunjie ardhi na umfanyie safari yake kuwa nyepesi."


Asiandamane na kengele wala gitaa wala mbwa katika safari; kwa


ushahidi wa Hadithi ya Abuu Huraira - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu


yake - kwamba Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu


yake, alisema: "Malaika hawaandamani na msafara ambao ndani yao


kuna mbwa au kengele."


Na akitaka kusafiri na mmoja kati ya wake zake, ikiwa ni mwenye mke


zaidi ya mmoja ,atawapigia kura ,na mke yeyote atakeyeangukiwa na kura


ndiye atakaye safiri naye, kwa ushahidi wa hadithi ya Aisha - radhi za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwamba alisema: "Alikuwa Mtume -


rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - akitaka


kusafiri, anapiga kura kati ya wake zake, na yeyote ambaye utatoka


mshale wenye jina lake, basi huyo ndiye aliyekuwa akisafiri pamoja


naye."


Inapendekezwa kwa msafiri asafiri siku ya Alhamisi mwanzo wa


mchana ikiwa ni wepesi kwake; kwa sababu Mtume -rehema na amani za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake -alikuwa akifanya hivyo. Amesema Kaab


ibnu Maalik - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Ni mara chache


5


sana alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani ziwe juu


yake, akitoka kwenda safarini isipokuwa angetoka siku ya Alhamisi."


Inapendekezwa kwa msafiri aombe dua ya kutoka nyumbani wakati


wa kusafiri na wakati mwingine usiokuwa wa safari. Atasema wakati wa


kutoka: "Bismillahi. Tawakkaltu ala llahi walaa haula walaa quwwata illa


billah. Allahumma inniy auudhubika an- adhwilla au udhwalla, au azilla au


uzalla, au adh-lima au udh-lama, au aj-hala au yuj-hala alaiyya (Kwa jina la


Mwenyezi Mungu. (Ninatoka) nimetegemea kwa Mwenyezi Mungu na


hapana uwezo wala nguvu ila vyote vinatokana na Mwenyezi Mungu. Ewe


Mola wangu wa haki, ninajilinda kwako kutokana na kupotea au


kupotezwa, au kuteleza au kutelezeshwa, au kudhulumu au kudhulumiwa,


au kuwa mjinga au kufanywa mjinga)."


Inapendekezwa kwa msafiri aombe dua ya safari anapopanda


mnyama wake, au gari lake, au ndege, au kipando kingine chochote. Hivyo


atasema: "Allahu Akbar, Allahu Akbar, sub-hanalladhii sakhara lana


haadha, wamaakunna lahuu muqriniina, wainna ilaa rabbina


lamunqalibuuna. Allahumma inna nas-aluka fii safarina haadha al-birra


wat-taqwaa, waminal amali maa tar-dhwaa. Allahumma hawwin 'alaina


safarana haadha, wat-wi 'anna bu'udahu. Allahumma antas-swaahibu


fis-safar, wal-khaliifatu fil-ahli. Allahumma inniy a'udhubika min


wa'athaais-safar, waka-aabatil man-dhwar, wasuu-il munqalabi fil maali


wal-ahli (Mwenyezi Mungu ni mkubwa, Mwenyezi Mungu ni mkubwa,


Mweyezi Mungu ni mkubwa. Utakasifu ni wa Mwenyezi Mungu ambaye


ametutiishia haya na tusengeliweza kuyadhibiti, na kwa hakika kwa Mola


wetu Mlezi bila shaka tutarejea. Ewe Mola wetu wa haki, tunakuomba


katika safari yetu hii wema na uchamungu, na tufanye matendo


unayoyaridhia. Ewe Mola wetu wa haki, tufanyie wepesi safari yetu hii, na


ufupishe umbali wake. Ewe Mola wetu wa haki, hakika Wewe ndiye


mwenza katika safari hii, na mchungaji wa familia yangu. Ewe Mola wetu


wa haki, hakika mimi ninajikinga kwako kutokana na ugumu wa safari, na


ubaya wa mtizamo na kurudi kubaya kwenye mali na familia)."123


Inapendekezwa kwa msafiri asisafiri peke yake pasina kuwa na mtu


wa kufuatana naye; kwa maneno ya Mtume - rehema na amani za


3 Maana ya neno "Wa'athaais-safar" ni ugumu wa safari. Maana hii inapatikana kwenye


kitabu kiitwacho Al-ifswaahu 'an Ma'aani As-swihaah (4/284).


2 Neno hili linamaanisha muonekano mbaya na mtu kuwa katika hali ya kuvunjika


kunakotokana na huzuni. Al-ifswaahu 'an Ma'aani As-swihaah (4/284).


1 Neno "Al-munqalab" ni kurudi. Maana hii inapatikana katika kitabu kiitwacho


Al-ifswaahu 'an Ma'aani As-swihaah (4/284).


6


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Lau wangetambuwa watu yaliyopo


kwenye upweke ninavyotambuwa mimi, asingesafiri msafiri wakati


wa usiku akiwa peke yake."


Wasafiri wanafaa kumchagua moja wao kuwa kiongozi; ili iwe rahisi


zaidi kukusanya jambo lao pamoja, na kuwafanya kukubaliana zaidi, na


lenye nguvu zaidi katika kupata malengo yao. Amesema Mtume - rehema


na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Watakapotoka watu


watatu katika safari yoyote, basi wamfanye mmoja wao kuwa


kiongozi."


Awe na pupa ya kufanya yale ambayo Mwenyezi Mungu


amemuwajibishia miongoni mwa ibada, na kujiepusha na


yaliyoharamishwa, na ajipambe kwa tabia njema, na amsaidie mwenye


kuhitajia msaada, na atoe elimu kwa mwenye kuitafuta na kuihitajia, na


awe mkarimu kwa mali yake, kwa kuitoa katika masilahi yake mwenyewe


na katika masilahi ya ndugu zake na kuwatekelezea mahitaji yao.


Inafaa aongeze matumizi na vinavyohitajika safarini, kwa kuwa shida


inaweza kumtokea na mambo yakaenda tofauti.


Inafaa awe katika safari ni mwenye uso wa bashasha, roho safi,


akijitahidi kuingiza furaha kwa anayesafiri pamoja naye, ili awazoee


wengine na azoeleke.


Anafaa kuwa na subira kwa kila kinachomkuta miongoni mwa


muamala mgumu wa wenye kusafiri pamoja naye, na wanapokwenda


tofauti na maoni yake, na aamiliane nao kwa namna iliyo nzuri, ili awe ni


mwenye kuheshimiwa baina yao na mwenye kupewa taadhima nyoyoni


mwao.


Inapendekezwa kwa wasafiri wanapofika mahala pa kushukia, wakae


pamoja. Kwa maana, baadhi ya Maswahaba wa Mtume - rehema na amani


za Mweyezi Mungu ziwe juu yake - walikuwa wanapofika sehemu ya


kushukia, wanatawanyika kwenye njia za milimani na mabonde. Akasema


Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Hakika


kutawanyika kwenu na kwenda kwenye njia hizi za milimani na


mabonde kunatokana na Shetani." Kwa hivyo, baada ya hapo wakawa


wanakusanyika pamoja kiasi kwamba ingekunjuliwa nguo juu yao


ingewatosheleza wote.


Inapendekezwa kwa msafiri atakapofika mahala pa kushukia akiwa


katika safari yake au akafika sehemu ya kushukia akiwa hayuko safarini,


aombe dua iliyothibiti kutoka kwake Mtume -rehema na amani za


7


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Ninajikinga kwa maneno ya


Mwenyezi Mungu yaliyotimia kutokana na shari ya alichokiumba."


Kwani hakika akiyasema maneno hayo, hatodhuriwa na kitu chochote


mpaka atakapoondoka mahala pale.


Inapendekezwa amtukuze Mwenyezi Mungu (kwa kusema: Allahu


Akbar) katika sehemu zenye miinuko, na kumtakasa (kwa kusema:


subhanallah) anaposhuka kwenye sehemu na mteremko na mabonde.


Amesema Jaabir - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Tulikuwa


tunapopanda miinuko, tunamtukuza Mwenyezi Mungu (kwa kusema:


Allahu Akbar), na tunapoteremka, tunamtakasa (kwa kusema:


subhanallah)." Na wala wasipaze sauti zao kwa kuleta Takbira. Amesema


Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Enyi watu


zioneeni huruma nafsi zenu. Kwani nyinyi hamumuombi kiziwi wala


aliye mbali. Hakika Yeye yu pamoja nanyi. Hakika Yeye ni Msikivu,


aliye karibu."


Inapendekezwa kwenda safari wakati wa usiku na haswa mwanzo wa


usiku, kwa maneno ya Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu


ziwe juu yake: "Shikamaneni na kusafiri wakati wa usiku, kwani


hakika ardhi hukunjwa wakati wa usiku."


Inapendekezwa kwake azidishe Dua awapo safarini; kwa maneno ya


Mtume - rehema na amani ziwe juu yake: "Dua za aina tatu ni zenye


kukubaliwa bila shaka. Katika dua hizo ni dua ya aliyedhulimiwa,


dua ya msafiri na dua ya mzazi kwa mtoto wake."


***


Pili: Twahara (usafi) katika safari


Ni wajibu kwa msafiri atilie umuhimu usafi wake. Kwa hivyo,


atachukuwa udhu kutokana na hadathi ndogo na ataoga kutokana na


Janaba.


Na ikiwa hakupata maji, au ikiwa ana maji machache anayoyahitajia


kwa ajili ya kupikia na kunywa, basi atafanya Tayammam.


Na namna ya kutayammamu ni: Aipige ardhi kwa mikono (kwa ndani


ya mikono) yake miwili, na aupake uso wake na viganja vyake kwayo.


Twahara ya kutayammam ni twahara ya muda tu. Kwa hivyo, wakati


wowote akipata maji, tayammamu yake inaharibika, na itamlazimu


kuyatumia maji. Na ikiwa alifanya tayammamu kwa sababu ya kupata


Janaba kisha akapata maji, basi itamlazimu kuoga. Na kama akitayammam


8


kwa sababu ya kukidhi haja kubwa kisha akapata maji, basi itamlazimu


atawadhe. Imekuja katika hadithi kwamba: "Udongo safi ni udhu wa


Muislamu hata kama atakosa maji miaka kumi. Akiyapata maji, basi


amche Mwenyezi Mungu na ayagusishe kwenye mwili wake."


Kupangusa juu ya khofu mbili ni jambo la kisheria katika Qur'ani na


Sunnah na ni makubaliano ya Ahlussunnah.


Kuna masharti kadhaa kwa ajili ya kupangusa juu ya khofu mbili na


chenye kufanana na nazo:


1. Khofu mbili hizo au soksi mbili hizi zinapaswa kuwa zinaruhusika


na ni safi.


2. Azifae akiwa na twahara.


3. Ziwe ni zenye kufunika sehemu za faradhi.


4. Iwe kupangusa ni katika kupatwa na hadathi ndogo. Hairuhusiki


kupangusa kwa kupatwa na Janaba wala kwa jambo ambalo linalazimisha


kuoga.


5. Iwe kupangusa ni ndani ya wakati uliowekwa kisheria, nao ni


mchana na usiku kwa mkazi, na michana mitatu na masaa yake ya usiku


kwa msafiri. Muda huu kulingana na kauli sahihi huanzia pale mtu


alipangusa kwa mara ya kwanza ya baada ya kuharibika kwa udhu, na


huisha kwa kutimia masaa 24 kwa mkazi, na kwa masaa 72 kwa msafiri.


Na kupangusaji juu ya khofu hubatilika kwa moja kati ya mambo haya


matatu:


1. Likitokea jambo lenye kuwajibisha kuoga kama vile janaba, basi


kunaharibika kupangusa juu ya khofu na inamlazimu mtu huyo kuoga.


2. Ikiwa atazivua khofu baada ya kuwa amekwishapangusa juu yake.


3. Ikiwa muda unaozingatiwa kisheria utaisha, basi upangusaji


utakuwa batili.


***


Tatu: Hukumu za kupunguza swala safarini


Kupunguza swala katika safari ni bora kuliko kuswali swala kamili;


lakini kama msafiri atakamilisha swala rakaa nne, basi swala yake itakuwa


ni sahihi lakini atakuwa amekwenda kinyume na kilicho bora.


9


Anapunguza swala msafiri atakapokuwa ametoka na kuziwacha kabisa


nyumba zote za kijiji chake au mji wake, na huu ndio msimamo wa


madhebu ya wengi wa maulamaa.


Ikiwa atasafiri baada ya kuingia wakati wa swala, ana haki ya


kupunguza swala kwa sababu amesafiri kabla ya muda wake kwisha.


Ama kukusanya swala kati ya Adhuhuri na Alaasiri na kati ya


Magharibi na Isha, hilo ni Sunna kwa msafiri anapohitajia kufanya hivyo.


Itakapokuwa safari imeshika kasi na imeshaendelea, basi afanye


litakalokuwa rahisi kwake kama vile kutanguliza au kuchelewesha.


Ama ikiwa msafiri hana hitajio la kukusanya, basi asikusanye, mfano


awe ameshuka na kukaa mahala ambapo hataki kuondoka hapo mpaka


ifike saa ya swala inayofuata, basi lililo bora kwake ni kutokusanya. Kwa


sababu hahitaji kufanya hivyo. Na ndiyo maana Mtume - rehema na amani


za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - hakukusanya alipokuwa ameshuka na


kukaa Mina katika Hija ya Kuaga kwa sababu hakuhitaji kufanya hivyo.


Ama swala za sunnah, ataziswali msafiri kwa namna anavyoziswali


mkazi. Kwa hivyo ataswali swala ya Dhuha, Tahajjud, Witiri na zinginezo


miongoni mwa swala za sunna isipokuwa sunna za kabla na baada ya


swala ya Adhuhuri, Maghari na Isha. Sunnah katika hizo ni kuwacha


kuziswali.


Ni sahihi kuswalia swala za sunnah juu ya kipando kama vike ndege,


gari, meli na vyombo vinginevyo vya usafiri. Ama swala za Faradhi, hizo ni


lazima kuteremka kwa ajili ya kuziswalia chini isipouwa


itakaposhindikana.


Swala ya msafiri anayeswali nyuma ya mkazi ni sahihi, na atakamilisha


msafiri kama swala ya imamu wake. Ni sawa ameikuta swala yote au


amekuta rakaa moja au chini ya hivyo. Hata kama ataingia pamoja naye


katika Tashahhud ya mwisho kabla ya kutoa salamu, basi atakamilisha


swala hiyo bila kufupisha. Hivi ndiyo sahihi kutoka katika kauli za


wanazuoni.


***


Nne: Adabu za kurudi kutoka katika ibada ya Hija, Umra au safari


Anapaswa afanye haraka kurudi na wala asikae muda mrefu katika


safari pasina kuwa na haja ya kukaa muda mrefu; kwa maneno ya Mtume


-rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Safari ni kipande


cha adhabu. Inamzuia mmoja wenu kula na kunywa na kulala kwake.


10


Kwa hivyo, akimaliza mmoja wenu hitajio lake, basi na afanye haraka


arudi kwa watu wake."


Na akitaka kurudi kwenye mji wake, atasoma dua ya safari wakati wa


kupanda kwake kipando chake na atazidisha kwa kusema: "Aaibuuna


taaibuuna aabiduuna lirabbina haamiduuna (Tunarejea, tunatubia,


tunafanya ibada na tunamsifu Mola wetu Mlezi)."


Inapendekezwa kwa msafiri wakati wa kurudi kutoka safari yake


aseme kilichothibiti kutoka kwa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake -


alipokuwa akirudi kutoka vitani au Hija au Umra. Alikuwa akipiga takbira


katika kila muinuko wa ardhi mara tatu kisha anasema: "Laailaha illa llahu


wahdahuu laashariikalah, lahul mulku walahul hamdu wahuwa 'alaa kulli


shay-in qadiir. Aayibuuna, taaibuuna, saajiduuna, lirabbina haamiduuna.


Swadaqallahu waa'dahu, wanaswara 'ab-dahu, wahazamal ahzaaba


wah-dahu (Hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi


Mungu mmoja peke yake, asiye na mshirika. Ni wake ufalme na sifa njema


ni zake, naye ni Muweza wa kila kitu. Tunarejea, tunabatubia makosa yetu,


tu naabudu, tunasujudia na tunamsifu Mola wetu Mlezi. Alitimiza


Mwenyezi Mungu ahadi yake, na alimnusuru mja wake, na aliyashinda


makundi ya maadui peke yake)."


Inapendekezwa kwa msafiri atakapouona mji wake, aseme hivi:


"Aayibuuna, taaibuuna, 'aabiduuna, lirabbinaa haamiduuna (Tunarudi,


tunatubia, tunaabudu, na tunamuabudu Mola wetu Mlezi)" na


ayarudirudie maneno hayo mpaka auingie mji wake. Hii ni kwa sababu


Mtume - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake alifanya


hivyo.


Asije kwa mke wake usiku ikiwa alika mbali kwa muda mrefu pasina


kuwa na haja ya kuja usiku isipokuwa ikiwa aliwafikishia kuwa anakuja, na


akawapa habari kwamba atafika usiku. Hii ni kwa sababu Mtume - rehema


na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - alikataza hilo. Amesema


Jaabir ibnu Abdillah - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao: "Mtume -


rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikataza


kwamba mwanamume asiwapigie hodi familia yake usiku." Na


miongoni mwa hekima ya kutofanya hivyo, ni vile riwaya nyingine


ilivyotafsiri: "Ili mwanamke mwenye nywele zilizotimka achane nywele


zake, na mwanamke ambaye mumewe hayuko anyoe nywele za sehemu za


siri." (4) Na katika riwaya nyingine:4 "Alikataza Mtume -rehema na


4 Neno "Ash-shaa'tha" linamaanisha mwanamke mwenye nywele matimtimu ambazo


hazijapakwa mafuta kwa muda mrefu. Na "Al-istihdaad" ni kutumia alaa iliyotengenezwa


11


amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - mwanamume kuwagongea


watu wa familia yake usiku ili kuchunguza kama wanamfanyia


khiyana au kutafuta makosa yao."


Inapendekezwa kwa mwenye kutoka safarini aanzie msikiti ambao


upo jirani naye na aswali humo rakaa mbili; kwa sababu Mtume -rehema


na amani ya Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa akifanya hivyo


Inapendekezwa kwa msafiri atakapofika kutoka safarini, awaonyeshe


huruma watoto wa nyumbani kwake na majirani zake na awafanyie wema


watakapompokea. Imepokelewa kutoka kwa Ibnu Abbas - radhi za


Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kwamba alisema: Alipofika Mtume,


rehema na amani ziwe juu yake, katika mji wa Makkah, walimpokea


watoto wadogo wa Banii Abdul Mutwalib. Basi akambeba mtoto mmoja


mbele yake na mwingine mgongoni kwake." Naye Abdullahi ibnu Jaafar -


radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - alisema: "Alikuwa Mtume


-rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - anaporudi


kutoka safarini, analakiwa pamoja nasi. Basi siku moja alilakiwa


pamoja nami na Hassan au Hussein na akambeba mmoja wetu mbela


yake na mwingine nyuma yake mpaka tunaingia Madinah."


Inapendekezwa kutoa zawadi, kwa kuwa kutoa zawadi kuna furahisha


nyoyo na kuondoa chuki. Na inapendekezwa kuikubali zawadi na kulipa


juu yake. Na inachukiza kuikataa pasina kuwepo kizuizi cha kisheria.


Ndiyo maana amesema Mtume -rehema na amani za Mwenyezi Mungu


ziwe juu yake: "Peaneni zawadi, mtapendana." Na zawadi ni sababu


miongoni mwa sababu za kuleta upendo baina ya Waislamu.


Akifika msafiri katika mji wake, imependekezwa kukumbatiana, kwa


sababu ya yale yaliyothibiti kutoka kwa Maswahaba wa Mtume - rehema


na amani za Mwenyezi mungu ziwe juu yake - kama alivyosema Anas -


radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Walikuwa wanapokutana,


wanasalimiana mikononi, na wanaporudi kutoka safarini,


wanakumbatiana."


***


kwa chuma kama vile wembe katika kunyoa sehemu za siri. Nalo neno "Al- maghiiba" ni


mwanamke ambaye mume wake amekaa mbali na yeye kwa muda mrefu. Tazama


At-Tahriir fii sharh Swahih Muslim, cha Al-Asbahaaniy (292)


12


Yaliyomo


Adabu za safari na hukumu zake 3


Kwanza: Adabu za safari 3


Pili: Twahara (usafi) katika safari 8


Tatu: Hukumu za kupunguza swala safarini 9


Nne: Adabu za kurudi kutoka katika ibada ya Hija, Umra au safari 10


13



Machapisho ya hivi karibuni

Mafungamani ya Shahad ...

Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.

Namna ya swala ya mtu ...

Namna ya swala ya mtume (s.a.w). na Namna ya kutawadha

FADHILA YA SUNNA ZA M ...

FADHILA YA SUNNA ZA MTUME (S.A.W)

MAZUNGUMZO KATIKA PEP ...

MAZUNGUMZO KATIKA PEPO NA JAHANNAMU (SEHEMU YA 3 KATI YA 3): NA SITAWAHI WAKASIRIKIA TENA.