Nakala




WASIA KWA WENYE KUFUNGA


RAMADHAN


Imeandaliwa na Raudhwah Islamic


Group


Imepitiwa na Ust.Abubakari Shabani


Rukonkwa.


Ilipokaribia kuingia Ramadhan Mtume swalla Allahu alayhi


wasalam aliwausia maswahaba zake kuhusu Ramadhan,


wasia tutakaouona katika mada zijazo Inshaa Allah. Na sisi


tukiwa tumeuanza mwezi huu mtukufu ni muhimu


kukumbushana yafuatayo ili uwe wasia wetu kwa ajili ya


kufaidika na Ramadhan.


1-Kumshukuru Allah subhanahu wataala kwa


kutuwafikisha kuidiriki Ramdhan. Hakika kushukuru ni


miongoni mwa ibada azipendazo Allah, na akaahidi kwa


waja wake wakimshukuru basi atawaongeza neema


alizowapa. Amesema Allah subhanahu wataala“Na


alipotangaza Mola wenu : Kama mtanishukuru


nitakuzidishieni, na mkikufuru hakika adhabu yangu ni kali


sana” (Suratu Ibrahim: 7) na akasema tena katika Suratul


Baqarah aya ya 152 “….na nishukuruni wala msinikufuru”.


Uhakika hatuwezi kufikia upeo wa kushukuru neema za


Allah, kwani neema zake hazihesabiki wala hazipimiki.


Amesema Ibnul Qayyim rahimahullah: “Kuwafikishwa


kushkuru neema za Allah, nayo ni neema inayohitaji


shukrani, na kuwafikishwa kushkuru neema ya shukrani, ni


neema nyengine inayohitaji shukrani, na hivyo hivyo


inaendelea kua muislamu aendelee kumshkuru Allah


mpaka mwisho wa pumzi zake”. Miongoni mwa neema hizo


ni kuwafikishwa kuidiriki ramadhan, alau siku moja na usiku


wake, kwani wangapi walitamani alau waweze kufunga


lakini maradhi yamewaweka vitandani, hawawezi kufunga,


na kula yao mpaka watumie mirija? Wangapi walitamani


waidiriki ramadhan na family zao, lakini sasa wako kaburini


ima katika viwanaja vya pepo au mashimo ya moto?


Hatutojua neema mpaka ikiondoka. Tumepewa nafasi ya


kujirekebisha matendo yetu ,kwa kuitumia vizuri


Ramadhan,ili siku ya Qiyama tupate ujira mkubwa apatao


mfungaji, ujira ambao mimi na weye wakati huu


tumewafikishwa na Allah kuupata,na tuukimbilieni huku


tukiomuomba Allah atuwafikishe tuimalize Ramadhan kwa


salama, asitunyime ujira wake wote, na atuwafikishe


tuidiriki Ramadhan inayokuja. Tumshukuruni Allah si kwa


maneno tu, bali na kwa matendo kwa kuonesha kuithamini


Ramadhan.


2-Kufunga kwa Imani na kutarajia malipo


Amesema Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam)katika


hadith sahihi, iliyopokelewa na Bukhari,Muslim na Nasai


rahimahumullah na kusimuliwa na Abu-Hurayra radhiallahu


anhu :“Yoyote atakaefunga Ramadhan, kwa imani na kwa


kutarajia malipo atasamehewa dhambi zake zilotangulia”.


Kufunga kwa Imani ni kukiri kua funga ni amri ya Allah, na


ni miongoni mwa nguzo za kiislamu, atakaesimamisha basi


atakua ameusimamisha uislamu wake, na atakaevunja basi


atakua kaubomoa uislamu wake. Allah hataki kula yetu na


wala hana haja ya kukaa na njaa kwetu lakini anachotaka ni


ibada na kama anavyosema katika lengo la funga ni kuwa


anataka watu wawe wacha-Mungu yani wamuogope yeye


Subhanah.


Kutarajia malipo ni kutaraji kuwa kutokana na funga


tunayofunga basi kuna malipo mazuri yaliyoandaliwa kwa


wafungaji,na malipo ya mwanzo ni kusamehewa dhambi na


mengine yanafuatia Akhera. Ni madhambi mangapi


tumeyafanya ya dhahiri na siri,makubwa na madogo yote


hayo yatasamehewa kwa atakaefunga kwa imani na kutaraji


malipo. Amesema Mtume wa Allah (swalla Allahu alayhi


wasallam) katika Hadith inayosimuliwa na Anas(radhia


Allahu anhu) :“Hakuna amali kwa asiekua na nia na hakuna


na malipo kwa asiyeyatarajia” .


Na tumkumbukeni Allah na ukubwa wake na kwamba


akatayarisha malipo mazuri kwa wafungaji na papo hapo


tuyatarajie malipo hayo.


3-Kuchunga ulimi na mambo ya kipuuzi.


Anasimulia kwamba amesema Mtume swalla Allahu alayhi


wassalam katika hadithi iliyopokewa na Bukhari na Abu-


Daud na kusimuliwa na Abu-Hurayra:“Yoyote asiewacha


maneno ya upuuzi, na kuyafanyia kazi,basi Allah hana haja


ya kuacha chakula chake na kinywaji chake”. Je


tumeizingatia hadithi hii tukafumba midomo yetu?


Amesema Mtume wa Allah (swalla Allahu alayhi wasallam)


kuwa “Yoyote anaemuamini Allah, na siku ya mwisho basi


na aseme la kheri au anyamaze” .(Muttafaqun alayhi). La


kusikitisha Ramadhan ndio imekua mwezi wa


porojo,Ramadhan imekua ndio mwezi wa kusengenyana,


Ramadhan ndio mwezi wa watu kukaa barazani na kuanza


kutaja sifa za wapita njia,na wengine kukaa maskani na


kuhadithiana uongo. Tumejiweka wapi na hadithi hii?


Tokea hapo mwanzo Allah hahitaji chakula chetu wala


kukaa kwetu na njaa lakini analolitaka ni ucha-mungu,na


haupatikani kwa kuzungumza ovyo,na kwa mwenye kusema


uongo na kufanya upuuzi mwengine basi ni bora kwake kula


kwani Allah hahitaji kulifungia tumbo akauwachia


ulimi,kama kufunga basi na viungo vyote vifungwe.


Hatopata hasara anaenyamaza kimya lakini hasara kwa


asiweza kuumiliku ulimi wake.


Kumiliki ulimi ni jambo alousiwa Muadh bin Jabal na


kaambiwa kuumiliki ulimi ndio itakua sababu ya kutengenea


matendo yote iwe sala,swaumu,hajj na hata Jihad. Aliulizwa


Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam):” Ni kipi


kitachowaingiza wengi motoni ? Akajibu kua ulimi na utupu


ndivyo vitakaowaingiza wengi motoni. Na akasema


atakaenidhamini viungo hivyo basi na yeye amemdhamini


Jannah,(Hadith imepokewa na Bukhari). Basi na tuanze


kumdhamini Mtume wa Allah viungo hivi ndani ya


Ramadhan hii kwa kutosema uongo,kutosengenya,kutukana


na porojo nyenginezo.


4-Kutia nia ya kuzidisha kheri, na kushindana katika


mazuri.


Muumini wa kweli hatasheki na kufunga tu ndio ikawa


basi,wala hatosheki na kusali sala zake tano, kisha ikawa


ndio kishamuabudu Allah. Kumuabudu Allah hakutoshi kwa


dakika 25 kwa sala zote tano, ndani ya masaa 24. Allah


hahitaji kupangiwa au kutengewa muda kwani muda wote ni


wake na anastahiki muda wote kuabudiwa. Alipotaja pepo


na starehe zake akamalizia kwa kusema na washindane


wenye kushindana(Muttafifin :26) na kwengine akasema


Kwa mfano wa haya nawatende watendao. (swaaffaat :61).


Pepo inahitaji kushindaniwa kwani kama anavyosema


Rasuul (swalla Allahu alayhi wasallam) kuwa “….Hakika


bidhaa ya Allah ni ghali na bidhaaa ya Allah ni


pepo.(Tirmidhy). Ikiwa kushindana kwenyewe sisi ndio


tutaenda na sala tano tu ambazo hazina khushui ndani yake,


na haikutimizwa rukuu wala sijdah, mbele ya wale ambao


wanaswali mpaka kuvimba miguu yao, na kuroa ndevu zao


kwa kulia na kukesha usiku mzima, kwa kumuabudu Allah


hivi tutakua sawasawa? Au ndo sisi tunashindana kwa aina


za vyakula na nani kapika vingi na vizurii?


Wengi wetu kabla ya Ramadhan tulitia nia ya kuzidisha


kufanya kheri, na wengine baada ya kufanya vibaya


Ramadhan zilopita, tukajiapiza Ramadhan ijayo nitafanya


vizuri, na nitamuabudu Allah kikamilifu, lakini


tunayakumbuka haya au pia tunasubiri ya mwakani, ili


tufanye vizuri kwa kua Ramadhan hii tuko na mishughuliko


ya world cup, hatuna muda wa kumuabudu Allah.


Na tuipambeni Ramadhan yetu kwa Qur-an na qiyamul-layl.


Adhkaar na madarsa na vikao vya kheri,Tutieni nia ya


kuzidisha kheri na miongoni mwa mambo tunaotakiwa


kuyaazimia kuyafanya ni kutekeleza sunna ya itikafu, sunna


ambayo hakuiachapo Mtume baada ya kuhamia Madina na


mwaka aloiwacha ikabidi ailipe lakini ndio sunna


iliyokimbiwa na wengi.


5-Kuwahurumia wanyonge na kuacha israfu.


Anasema Allah (subhanahu wataala) “…. Na


amewanyanyua daraja baadhi yenu juu ya wengine ili


akufanyieni mtihani kwa hayo alokupeni…” (An-aam


165).Na akasema tena katika Suratu-Nahli aya ya 71 “Na


Allah amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine katika


rizki, Je wale walofadhilishwa,hawarejeshi rizki zao,kwa


wale wanaowamiliki kwa mikono yao ya kulia?”.


Kutofautiana kwa kipato ni dalili za uwepo wa Allah


kuonesha anampa amtakae na humnyima amtakae na


kwamba kupata si kwa utashi wa mtu, bali ni mipango ya


Allah. Na akawataka waja wake wasaidiane. Bila shaka


miongoni mwa jamii za kiislamu tunazoishi nazo wako


wanaofunga lakini wasijue wataftari nini, na wanafunga


hawana daku ya kula ili waweze kufunga vizuri.


Wanafunga kwa kua ni amri ya Allah (subhanahu wataala)


lakini kipato chao na uwezo wao hauwaruhusu kufanya


hivyo. Watu aina hiyo wanahitaji kuangaliwa kwa jicho la


huruma na wale wenye uwezo. Si vibaya kila siku kumlisha


maskini mmoja kwani sadaka ya kulisha chakula ina


thamani kubwa mbele ya Allah (subhanahu wataala). Na


Amesema Mtume wa Allah katika hadithi inayosimuliwa na


Saad bin Khalid:”Atakaemfutarisha aliefunga, basi atapata


ujira sawa na wake, pasi na kupungua ujira wa mfungaji


chochote”(Tirmidhy,Nasai na Ibnu-Majah).


Ikiwa ni hivyo basi na kuftarsha kwetu tusiwasahau maskini


na sio shughuli zetu za kuftarisha kujazwa matajiri na wenye


uwezo wao ambao hata hicho chakula hawakihitaji. Kwa


kutumia kiyasa ya hadith ya Rasuul inayosimuliwa na Abu-


Hurayrah kua chakula kibaya ni chakula cha harusini, kwani


wanaalikwa wasiokihitaji; basi na ftari zetu kesi ndio


hiyohiyo, tunawasahau maskini na wote wanaoalikwa


hawakihitaji. Tusitosheke na thawabu za kuftarisha mtu bali


tutake na thawabu za kulisha maskini kwani tukialika


matajiri tutapata thawabu za kuftarisha tu lakini kualika


maskini itakua ni thawabu za kuftarisha na za kulisha


maskini.


Ama kuhusu israfu tumeona maudhui yake katika mada


zilopita


6-Kukumbuka njaa na kiu siku ya Qiyamah.


Moja kati ya mambo walohusishwa Mitume na ndo ikawa


kama zawadi yao hapa duniani amesema Allah subhanah


“Hakika tuliwachagua kwa lile jambo zuri kabisa la


kuikumbuka Akhera” (Swaad :46). Ni zawadi ambayo


imewafanya kutojali maisha ya dunia ni kutoshughulishwa


na starehe za duniani.


Amesema Allah (subhanahu wataala) hii kuonesha kua kila


kitu chao walikua wakifiri akhera.Na hivyo ndio


anavyotakiwa muislamu wa kweli awe. Awe anafikiri


akhera,kwani nguzo zote za kiislamu kuanzia sala,swaumu


na hata hajji vinamkumbusha mtu mambo yatakayotokezea


siku ya kiyama. Funga inatakiwa imkumbushe mtu njaa na


kiu, kitakachowakuta watu wa motoni na kutokana na kiu


hiyo wataomba kwa watu wa peponi kama anavyotusimulia


Allah (subhanahu wataala) katka suratu A’raf aya ya 50 “Na


watanadi watu wa motoni kuwaita wa peponi: Tumiminieni


maji au chochote katika alivyokuruzukuni Allah. Watasema


watu wa peponi: Hakika Allah ameviharamisha vyote viwili


(yani chakula na maji) kwa makafiri”. Hivyo basi mtu


anapokaa na njaa na kiu akumbuke kua akhera watu waovu


watakaa na njaa na kiu.(Allah atuhifadhi)


Allah atuwafikishe kuyatekeleza haya na mengineyo ya


kheri.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI