Nakala

1


بسم الله الرحمن الرحيم


WALIVYOOMBA MASWAHABA ILI WAKUBALIWE SWAUM YA MWEZI WA RAMADHANI Imeandikwa na: Imaam Swaalih Bin Fawzaan Al-Fawzaan Imetafsiriwa na: Idara ya Wanachuoni.com Imepitiwa na: Yunus Kanuni Ngenda Salaf-us-Swaalih (Rahimahumu Allaah) walikuwa wakimuomba Allaah miezi sita Awafikishe katika Ramadhaan, kisha wanamuomba tena kwa miezi sita Awakubalie Swawm ya Ramadhaan. Walikuwa wakitilia umuhimu wa matendo kukubaliwa zaidi kuliko utekelezaji. Allaah (Jalla wa ´Alaa) Amesema: إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللَّهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ


“Hakika Allaah Anatakabalia wenye uchaji Allaah”. (05:27) Allaah Anakubali kutoka kwa wachaji Allaah ambao wanamcha Allaah, wanamukhofu, wanamuogopa na wanamuabudu ukweli wa kumuabudu. Wameitwa ´wachaji Allaah` kwa kuwa wamechukua kinga inayowakinga na adhabu na khasira za


2


Allaah kwa kumtii, kutekeleza maamrisho Yake na kujiepusha


na makatazo Yake.


Salaf (Rahimahumu Allaah) walikuwa wakiogopa matendo yao


kurudishwa kwa sababu ya upungufu wake, ima kwa sababu ya


kutotakasa nia kwa kuingiliwa ndani yake na Riyaa au Sum´aa.


Hii ni khatari kubwa ambayo inayoweza kumsibu mwanaadamu.


Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:


“Hakika ya kila ´amali inalipwa kwa nia na kila mmoja atalipwa


kwa kile alichonuia.”


Nia ndio msingi wa ´amali. Inaweza kuingiwa ndani yake na


kitu katika Riyaa au Sum´aa au ´amali inayofanyiwa asiyekuwa


Allaah (´Azza wa Jalla) na hivyo ´amali hiyo iwe ni yenye


kurudishwa kwa mwenye nayo. Kuna khatari vilevile ´amali


ikawa sio yenye kuafikiana na Sunnah za Mtume (Swalla


Allaahu ´alayhi wa sallam) na hivyo ikawa ni yenye kurudishwa.


Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:


“Mwenye kufanya ´amali isiyokuwa humo Amri yetu


itarudishwa.”


Vilevile wanaogopa kuwa wamewadhulumu watu na hivyo


matendo yao wakapewa wale waliowadhulumu. Inawezekana


wakawa wamemdhulumu mtu katika mali yake au heshima yake


au wamemfanyia uadui. Katika hali hii siku ya Qiyaamah yule


mdhulumiwaji atapewa matendo mazuri ya yule mdhulumaji.


Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:


“Yule aliyemdhulumu ndugu yake basi amrudishie haki yake leo


kabla [ya Siku] ambapo hakutokuwa dinari wala dirhamu. Ikiwa


alifanya matendo mazuri yatachukuliwa na apewe yule


3


aliyemdhulumu na ikiwa hana matendo mazuri yatachukuliwa


madhambi ya yule rafiki yake na apewe yeye.” (al-Bukhaariy


(2317)


Imesimuliwa katika Hadiyth ya kwamba kuna watu watakuja


siku ya Qiyaamaha na matendo mfano wa jibali katika Swalah,


Swadaqah na Swawm, lakini amemdhulumu huyu, amempiga


huyu na amechukua mali ya huyu. Wote hawa watachukua


sehemu ya matendo yake mazuri. Yakiisha kabla ya


kuhukumiwa yatachukuliwa madhambi yao na kuongezewa.


Baada ya hapo atupwe Motoni. Hii ni khatari kubwa. Kwa ajili


hiyo ndio maana Salaf walikuwa wakitilia umuhimu mkubwa


katika ´ibaadah na hata hivyo wakiogopa isije kukubaliwa.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI