Nakala




SHARTI ZA KUSIHI KWA FUNGA -


SEHEMU YA KWANZA


Makala imeandaliwa na Raudhwah islamic


Group


Imepitiwa na Abubakari Shabani Rukonkwa.


Ili swaum isihi kuna sharti zake zitimizwe ndipo funga hiyo


itasihi. Na sharti hizi zisipokamilika basi funga haitosihi au


funga itabatilika na itamlazimu mwenye kufunga aje kuilipa


funga hiyo.


Hivyo hatutokuja kueleza yanayofunguza. Bali makala hii in


shaa Allah itamtosheleza msomaji kujua sharti za kusihi kwa


funga na kubatilika kwa funga. Pia katika baadhi ya vitabu


wametumia neno NGUZO ZA FUNGA zote hizo ni sawa na


wanakusudia kukieleza kitu hicho hicho.


1-KUTIA NIA KILA SIKU


Ni lazima kwa mwenye kufunga atie nia kwa kila siku


anayofunga. Iwe funga hiyo ya sunna au faradhi kama


Ramadhan. Na hatokuwa na funga yule atakaekuwa hajatia


nia. Kwani katika hadithi kutoka kwa Sayyidina Omar (radhi


za Allah ziwe juu yake) amesema: “Nimemsikia Mjumbe wa


Allah akisema: “ Hakika kila jambo huambatana na nia na


kila mtu atalipwa kutokana na kile alichokinuwia … .”


[Bukhari na Muslim].


Na inamuwajibikia mwenye kufunga Ramadhan atie nia


kabla ya kuanza kwa alfajiri ya kweli. Na endapo mwenye


kutaka kufunga hatotia nia kabla ya wakati huo basi


hatokuwa na funga. Na itamuwajibikia kwake yeye kuja


kuilipa funga hiyo. Kwa ushahidi wa Hadithi ya Mtume


(swalla Allahu alayhi wasallam): “Yeyote ambae hatoweka


nia ya kufunga kabla ya alfajiri hatokuwa na funga.”


Imepokewa na Imam Ahmad na An-Nasai.


Hivyo inamlazimu atie nia kwa kuzingatia kabla ya kuanza


kwa funga na nia hiyo iwe kwa kila siku atakayoifunga.


Ama mwenye kufunga sunna anaweza kutia nia kabla ya


kupambazukwa kwa jua,mpaka wakati wa zawali (kabla ya


Adhuhuri)


Kwa nini mtu atie nia kila siku ndani ya Ramadhani? Swala


humalizika kwa mtu kutoa salam. Na anapotaka kuingia


katika swala nyengine basi analazimika kutia nia ya swala


nyengine. Hivyo hivyo kwa mwenye kufunga, swaumu


humalizika kwa kuzama kwa jua hivyo basi anaetaka


kufunga siku ya pili lazima atie nia nyengine. Kwani


anakuwa ameanza swaumu nyengine. Na hii ndio kauli


yenye nguvu.


Imethibiti hadithi ya mtume (swalla Allahu alayhi wasallam)


akisema:


م NRZ "[رواه ا QF ا R ST ا UVW       م NL Y : " FG و IFJ لله KFL ل NO


. Nًb`O`R     J   لله iVJ jWi R ج ١ ص ٢٨٨ ^ ط`     ا ab cNR


Alisema mtume (swalla Allahu alayhi wasallam):Hana funga


yoyote ambae alie lala bila kuweka nia usiku.


[Imepokelewa na imamu maliki katika kitabu chake cha


muwatwaa 1/288]


Je kutia nia ni kwa kutamka au moyoni tu inatosha?


Kwanza ni jambo lisilokuwa na shaka kuwa nia mahali pake


ni moyoni. Ama suala la kutamka kwa kauli za maulamaa


wengi ni jambo ambalo halikuthibiti katika dini. Hivyo basi


mwenye kufunga atatia nia moyoni mwake kwani Allah


anajua yale yote yaliyomo ndani ya nafsi zetu na hakifichiki


kwake kitu chochote.


Nakauli iliyo sahihi nikwamba kutamka niya ni BIDAA


kwasababu nia nikatika matendo ya moyo.


2- KUJIZUIA KULA NA KUNYWA


Ni lazima kwa mtu mwenye kufunga ajizuie kula na kunywa


kuanzia kuingia kwa alfajiri ya kweli hadi kuzama kwa jua.


Kwa kauli ya Allah (subhanahu wata‘ala): “Na kuleni na


kunyweni mpaka kubainike kwenu weupe wa alfajiri katika


weusi wa usiku, Kisha timizeni saumu mpaka usiku.”


(Suratul Baqara : 187).


Nini hukmu ya kula kwa kusahau


Yule ambae atakula kwa kusahau iwe kidogo au sana basi


haitobatilika funga yake kwa ushahidi wa hadithi ya Abu


Hurayrah (radhi za Allah ziwe juu yake) amesema :


Amesema Mtume (Swalla Allahu alayhi wa sallam):


“Mwenye kusahau nae amefunga, basi akala au akanywa na


aikamilishe funga yake.”


[Al Bukhariy na Muslim].


Na katika riwaya nyengine “Kwani hakika Allah amemlisha


na amemnywisha.” Ila Muislamu azingatie asije kujiigiza


kuwa amesahau kwani ataweza kuwadanganya watu lakini


Allah hawezi kumdanganya hata kidogo.


Je kupiga mswaki ndani ya Ramadhan kwa kutumia dawa


inasihi?


Ama Kupiga mswaki ndani ya funga hilo linasihi kwani


Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam) alikuwa akipiga


mswaki nae amefunga. Ama suala linakuja kwenye kupiga


mswaki kutumia dawa.


Dawa ya mswaki haibatilishi swaum ikiwa wakati anasafisha


meno atatema na wala hamezi. Ama ikiwa atakusudia


kumeza, swaumu yake itabatilika.


Na yule ambae anakhofia anaweza kumeza basi bora


asitumie dawa. Na kilichopendekezwa zaidi na maulamaa


mtu apige mswaki kwa kutumia dawa kabla ya kuanza kwa


saumu na itakapoingia saumu apige mswaki bila ya kutumia


dawa ili asije kutumia dawa na kuimeza.


Je kuonja chakula wakati mtu amefunga inasihi?


Kuonja chakula wakati mtu amefunga inasihi kwa sharti


ahakikishe kuwa hamezi kile alichokiweka kwenye ulimi


kwa ajili ya kuonja.


Je kukoga katika mchana wa Ramadhan inasihi?


Kukoga au kukosha uso ikiwa mtu yumo kwenye funga


inasihi. Ila ahakikishe maji hayaingii katika matundu ya


mwili kama masikioni nk.


Ama yakiingia bila ya kukusudia hilo halina tatizo. Na


yakiingia kwa kusudia basi atakuwa amefungua.


Ni ipi hukmu ya mwenye kufunga kutia dawa kwenye


macho?


Anaruhusika kutumia na haitobatilika funga yake.


Nini hukmu ya kuchoma sindano wakati mtu amefunga?


Ikiwa sindano ni ya dawa tu basi haifunguzi. Ila sindano


ikiwa imewekewa kitu chochote ambacho ndani yake


kitampa mwenye kufunga nguvu kama glucose basi hapo


itakuwa amefungua. Allah ni mjuzi zaidi.


3-KUJIZUIA NA KUJITAPISHA KWA MAKUSUDI


Pia ni wajibu kwa mwenye kufunga kujizuia na kujitapisha


kwa makusudi. Ama akitapika bila ya kukusudia basi


ataendelea na funga yake kama kawaida. Na akijitapisha


kwa makusudi ni lazima ailipe funga hiyo.


Kutoka kwa Abu Hurayrah (radhiya Allahu anhu) amesema:


Amesema Mtume (Swalla Allahu alayhi wa sallam): "... na


mwenye kujitapisha basi inamuwajibikia kulipa." Bukhari na


Muslim.


4-KUWA MUISLAMU


Ikiwa mtu sio Muislamu basi kwake yeye haimuwajibikii


kufunga. Na akija kusilimu basi hatolipa kwa zile siku


ambazo hakufunga kwani alipokuwa sio Muislamu


haikumuwajibikia kufunga.


Ama Muislamu ambae ataritadi wakati amefunga basi moja


kwa moja funga yake itabatilika na akija kutubu na kuamua


kurudi kwenye Uislamu basi inamuwajibikia kuzilipa siku


zote ambazo aliziwacha wakati ametoka kwenye Uislamu.


5-KUWA NA AKILI KATIKA MCHANA MZIMA WA


RAMADHAN


Pia ili swaumu isihi lazima mwenye kufunga awe na akili na


ikiwa atarukwa na akili basi funga yake itabatilika. Na


hakuna tatizo kwa mtu kuzimia kwa muda mchache katika


mchana wa mwezi wa Ramadhan.


SHARTI ZA KUSIHI KWA FUNGA- SEHEMU YA PILI


3 – KUJIZUIA KUFANYA TENDO LA NDOA KWA


MAKUSUDI NA KUJITOA MANII


Ikiwa mtu atafanya jimai bila ya kukusudia basi mtu huyo


atakuwa amesameheka. Kwa kauli ya Allah:


رًا `ُz| نَ للهَُّ َ N وَ َ ْ ُ ُ `ُFُO تْ iَ     َّ ƒَ َ „ NR َ ْ َ ِ  وَ Iِ ِ  ُ ْ „ْ^†َ ‡ أَ ْ N    َ ِb حٌ NَT‹ ُ ْ ُ َ ْ FJ َ Œَ ْ  ...{و


}N    ً  رَ ِ


''Wala si lawama juu yenu kwa mlivyo kosea. Lakini ipo


lawama katika yale ziliyo fanya nyoyo zenu kwa makusudi.


Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye


kurehemu''


(Suratul Ahzaab : 5).


Ama yule ambae atafanya jimai kwa makusudi basi huyo


funga yake itabatilika na itamlazimu kwake yeye kuilipa


funga hiyo pamoja na kutoa kafara.


Kafara kwa yule ambae atafanya tendo la ndoa katika


mchana wa Ramadhani ni :


i. Kuacha huru mtumwa.


ii. Kufunga miezi miwili mfululizo.


iii. Alishe maskini 60 kila mmoja kibaba kimoja.


Ikiwa mke au mume mmoja wao amemlazimisha kwa nguvu


mwenzake kufanya tendo la ndoa ndani ya mchana wa


Ramadhan na wamo katika funga basi yule aliemlazimisha


mwenzake ndio itamuwajibikia kutoa kafara.


Na mwanamke hatakiwi akubali kufanya tendo la ndoa


wakati amefunga ndani ya Ramadhani. Na maulamaa


wengine wakaengeza kwa kusema hata ikiwa anaweza


kupigana na mume wake basi ampige, Kuonesha uzito wa


funga.


Na wala mtu asitumie kivuli kuwa amelazimishwa kujitetea


ajue kuwa Allah (subhanahu wata‘ala) anajua kila kilichomo


ndani ya nafsi ya mja wake.


Ikiwa mtu atafanya tendo la ndoa hali ya kuwa amefunga


ndani ya Ramadhani kwa siku mbili tofauti basi ni juu yake


kafara mbili. Kila funga moja basi na kafara yake moja.


Pia ikiwa mtu anafanya tendo la ndoa na baadae


ikambainikia kuingia kwa alfajiri basi kinachotakiwa ni


kuacha tendo la ndoa hapo hapo akakoge janaba na aendelee


na funga yake.


Je ni wakati gani jimai ya mchana wa Ramadhani


inaruhusika?


Ikiwa mke na mume wote wana dharura za kisheria za


kutofunga kwa mfano wote wamesafiri basi hakuna ubaya


na hawatotoa kafara. Kwani ruhusa ya kutofunga


ishakuwepo kwao wao.


Ikiwa mume amerudi safari na mke wake hakufunga siku


hiyo kwa sababu ya hedhi na ametwaharika baada ya funga


kuanza, basi tendo la ndoa kwao wao linaruhusika kwani


mume hajafunga na mke hakufunga.


Ama kinyume na hali hizo wakifanya tendo la ndoa ndani ya


mchana wa Ramadhani wakiridhia wenyewe basi kwa kila


mmoja juu yake kafara ama mmoja amemlazimisha


mwenzake basi yule aliyemlazimisha mwenzake ni juu yake


kutoa kafara.


Kujitoa maniii kwa makusudi kunabatilisha funga. Hivyo


basi yeyote ambae amefunga anatakiwa ajizuie na kujitoa


manii kwa makusudi. Na mfano wa kujitoa manii kwa


makusudi ni puunyeto, au kwa kumkumbatia au kumchezea


mkewe au mwanamke mpaka akatokwa na manii.


1-SUALI


Walifanya jimai kabla ya kuanza kwa funga na baadae


hawakuwahi kukoga janaba wakalala mpaka ikaingia alfajiri.


Je nini hukmu ya funga yao?


JIBU


Ikiwa walitia nia ya kufunga basi funga yao itasihi.


Kinachowalazimu ni kukoga janaba ili waweze kuswali na


waendelee na funga yao.


Na hili ni kwa ushahidi wa hadithi ya Bibi Aysha na Ummu


Salamah (radhiya Allahu anhuma) “kwamba Mtume (Swalla


Allahu alayhi wasallam) alikuwa akiamka na janaba


kutokana na kukutana kimwili na wake zake, kisha anakoga


na kufunga.”


(Al Bukhariy na Muslim).


2-SUALI


Alifanya jimai bila ya kujua kwamba alfajiri imeingia. Na


baadae akajua kuwa alifanya jimai wakati tayari alfajiri


ishaingia. Nini hukmu yake?


Ikiwa wakati anafanya hajui kama wakati umeingia basi


atakoga na ataendelea na funga yake. Kwani hakuna kosa


kwa mtu kutojua.Ama akifanya kwa kusudi basi funga


itabatilika funga yake na itamlazimu kutoa kafara na kuilipa


funga hiyo.


4-KUEPUKANA NA HEDHI NA NIFASI


Ni lazima kwa mwanamke anaetaka kufunga awe


ametwaharika kutokana na hedhi na nifasi. Na pindi


mwanamke anapokuwa na hedhi au nifasi basi huwa ni


wajibu kwake kuacha kufunga. Na hii ni amri kutoka kwa


Allah (subhanahu wata‘ala) na mwanamke akitwaharika


ataendelea na kufunga.


Pia siku ambazo ameziacha kwa kutofunga atakuja kuzilipa


baada ya Ramadhani.


SUALI


Bado muda mdogo sana kumalizika kwa funga. Mwanamke


akapatwa na hedhi. Je itahesabika funga yake ile?


JIBU


Hapana, haitohesabika funga ile kwa sababu wakati


haujatimia. Na itamlazimu mwanamke huyo aje kuilipa


funga hiyo baada ya kumalizika kwa Ramadhani.


SUALI


Mwanamke amepatwa na maumivu au dalili nyengine za


kuonyesha atapatwa na hedhi ila hakupata wala hakutokwa


na damu. Nini hukmu yake?


JIBU


Hatowajibika kuilipa na funga yake itakuwa sahihi.


SUALI


Ikiwa mwanamke siku zake za hedhi zimekaribia. Akaona


matone ya damu ila damu haikutoka. Nini hukmu ya funga


yake?


JIBU


Lazima ailipe funga hiyo kwani matone hayo ya damu


yatahesabika kama ni damu ya hedhi.


SUALI


Miaka yote Ramadhan napata kufunga siku 10 tu au 11. Na


zinazobaki nakuwa katika siku za hedhi. Sipati kufanya


ibada ambazo zina fadhila kubwa kuliko miezi mingine.


Nakuwa mnyonge kutokana na hali hiyo.


Je naweza kutumia vidonge vya kuzuia hedhi ?


JIBU


Kuhusu hedhi muda wake wajuu kabisa ni siku kumi na


tano, zikizidi hapo huwa ni ugonjwa, kwa maelezo yako


unakuwa ukitokwa na damu kwa takriban siku 20, hii


inaonesha una tatizo jitahidi kutafuta tiba ya ugonjwa huo.


Ama ikiwa zitabaki siku 15 au chini ya hapo tutaizingatia


kuwa ni hedhi, na kipindi unachokua ndani ya hedhi kuacha


yale sheria iliokutaka kuyaacha ni ibada, hivyo ibada


iliyokuzuilia kufanya ibada nyengine fadhila zake ni kubwa


zaidi kwa wakati huo.


Pili.


Kuhusu kutumia vidonge vya hedhi wako maulamaa


wanasema kuwa haifai kutumia vidonge hivyo kwani


vimethibitika vina madhara.


Ama tukisema havina madhara basi ushauri wetu ni bora


kuiacha hedhi katika utaratibu wake ndio bora zaidi kiibada


na kiafya pia. Kwani ndio maumbile yake mwanamke


alivyoumbwa na Allah (subhanahu wata‘ala). Na Allah ndie


mjuzi zaidi.


SUALI


Ikiwa mwanamke amemaliza nifasi kwa siku chache mfano


siku saba je anaweza kufunga?


JIBU


Ikiwa kweli imesita damu ya nifasi mwanamke huyo


anaweza kufunga. Na Allah ni mjuzi zaidi.


SUALI


Ni ipi hukmu ya funga kwa mwanamke aliyeharibu mimba?


JIBU


Ikiwa mimba imeharibika kabla ya mtoto kuumbika basi


damu hiyo si damu ya nifasi na mwanamke atakoga


kujisafisha na kuendelea na funga yake.


Ikiwa mimba imeharibika baada ya mtoto kuumbika basi


damu hiyo itakuwa ni ya nifasi na itambidi ajizuie kufunga


mpaka pale itakaposita damu ya nifasi. Na Allah ni mjuzi


zaidi.


SUALI


Mwanamke ametoharika kabla ya kuanza kwa alfajiri ya


kweli. Akatia nia ya kufunga ila akachelewa kukoga josho.


Je anaweza kufunga?


JIBU


Ndio anaweza kufunga. Kitakachomlazimu ni kukoga josho


kabla ya kutoka kwa swala ya alfajiri ili asiache swala na


ataendelea na funga yake. Na Allah ni mjuzi zaidi.


Hayo ndio masharti ambayo yanalazimika kutimizwa ili


funga ya Muislamu isihi. Na kinyume cha masharti hayo ni


kubatilika kwa funga hiyo. Na kama tulivyoeleza


itamuwajibikia mtu huyo kulipa. Ama yule ambae kwa


sababu ya kufanya tendo la ndoa yeye itamuwajibikia kulipa


pamoja na kafara. Na Allah ni mjuzi zaidi.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI