Nakala




NYAKATI TATU MUHIMU ZA IBADA


ZISIKUPITE KATIKA RAMADHANI


Imeandaliwa na Alhidaya.com


Imepitiwa na Abubakari shabani


Rukonkwa


Nyakati tatu hizi ni muhimu sana za kufanya


ibada kutokana na fadhila zake kuu. Mwenye


kupenda kuchuma thawabu nyingi asizikose


khaswa katika mwezi huu Mtukufu Wa


Ramadhaan ambao ni mwezi wenye malipo


maradufu


1-Wakati wa mwanzo: Baina ya Alfajiri na


jua kuchomoza:


Usimulizi uliothibiti kutoka katika Swahiyh


Muslim (564/1) kwamba Mtume (Swalla Allaahu


'alayhi wa sallam) na Maswahaba walikuwa


2


wakibakia macho wakati huo hadi jua


kuchomoza kwani ni wakati mja anapogaiwa


rizki yake, na ni wakati wenye kheri nyingi,


unampa siha nzuri ya mwili binaadamu, na kwa


ujumla ni wakati wenye baraka nyingi za kila


aina kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa


sallam) aliomba:





((Ee Allaah, wabarikie Ummah wangu nyakati za


asubuhi mapema)) [At-Tirmidhiy, Ahmad, Abu


Daawuud, Ibn Maajah na imethibitishwa kuwa ni


Hadiyth Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]


Usimulizi huu umetoka kwa Maswahaba kadhaa


ambao wameelezea kwamba: "Mtume (Swalla


Allaahu 'alayhi wa sallam) alipotaka kupeleka


kikosi au jeshi aliwapeleka mwanzo wa asubuhi".


3


Vile vile wamesimulia kwamba:"Swakhar


alikuwa mtu tajiri ambaye alikuwa akipelekea


biashara zake mwanzo wa asubuhi na matokeo


yake ilikuwa ni kufuzu katika biashara na kupata


faida kubwa sana".


Wamesimulia Salafus-Swaalih kwamba Ibn


'Abbaas naye alimkataza mtu kulala nyakati hizo


alipomwambia:





"Inuka! Je, unalala katika saa ambayo rizki


inagaiwa?"


Ikiwa wakati huo ni kama hivyo ilivyoelezwa


juu, basi vipi Muislamu aache wakati huu umpite


hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramdhaan?


Ibnul-Qayyim (Rahimahu-Allaah) katika kitabu


chake 'Zaad Al-Ma'aad' amesema: "Usingizi wa


4


asubuhi unanyima rizki kwani huo ni wakati


ambao Muumba anaombwa rizki na wakati wa


kugaiwa rizki. Hivyo usingizi unanyima rizki


isipokuwa kwa dharura. Usingizi wakati huo pia


ni madhara kwa mwili…"


Faida nyingine kubwa ya kubakia


macho ukimdhukuru Allaah wakati huu:


Kwa muda wa saaa moja na nusu takriban


utakuwa umepata thawabu za Hajj na ‘Umrah


zikiwa kamilifu:





Imetoka kwa Anas kwamba Mtume (Swalla


Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema:


((Atakayeswali Alfajiri katika Jamaa'ah kisha


5


akakaa anamdhukuru Allaah mpaka likachomoza


jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira


kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio


kamili kamili kamili)) [Imetolewa na At-


Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy]


Pindi ukifanya hivyo kwa mwezi mzima utakuwa


umechuma thawabu za Hajj na ‘Umrah za muda


wa mwezi mzima. Hizo ni fadhila za siku za


kawaida, seuze ukifanya mwezi mtukufu huu wa


Ramadhaan? Jitahidi ndugu Muislamu kadiri


uwezavyo kuchuma hizi thawabu kubwa ambazo


zingelikukalifu mali, tabu za safari na mashaka


ya kufika Makkah kutekeleza ibada hizo. Lakini


kwa Rehma ya Allaah Amejaalia thawabu hizo


ziweze kuchumwa tukiwa majumbani mwetu


tena kwa wepesi kabisa. Wanaume inawapasa


waswali msikitini kuzipata thawabu hizo kwa


kuwa Hadiyth imetaja atakayeswali jamaa’ah.


Ama wanawake, wanazipata fadhila hizo hata


wakiswali majumbani mwao. Hata hivyo, juu ya


kuweko fadhila kama hiyo, tusisahau kuwa


haivunji wala haifuti fardh ya kwenda Hajj kwa


6


mwenye uwezo, asije mtu akadhani kufanya hayo


kutakuwa kumetengua wajibu wake wa kuhiji au


kufanya ‘Umrah.


2- Wakati wa pili: Kabla ya Jua kuzama


(Magharibi):


Huu ni wakati ambao bado Muislamu yuko


katika Swawm na du'aa yake anayoiomba


hairudi:





Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)


amesema: (([Watu] watatu du'aa zao hazirudi;


mwenye kufunga Swawm hadi afuturu. Kiongozi


muadilifu na aliyedhulumiwa)) [At-Tirmidhiy


kwa isnaad nzuri]


7


Ni fursa kwa Muislamu atumie wakati huo


kuomba du'aa wakati huu hasa kwa vile ni wakati


ambao Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)


Amehimiza Atukuzwe kama Anavyosema:





... na msabbih kwa kumsifu Mola wako kabla ya


kuchomoza jua na kabla ya kuchwa [Qaaf: 39]





…Na msabbih Mola wako kwa kumsifu kabla ya


kuchomoza jua, na kabla halijachwa, na nyakati


za usiku pia umsabbih na ncha za mchana ili


upate ya kukuridhisha [Twaahaa: 130].





Na omba maghfirah kwa dhambi zako, na


umsabbih Mola wako kwa kumsifu jioni na


asubuhi)) [Ghaafir: 55]


3- Wakati wa tatu: Suhuur - Kabla ya Alfajiri


Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amewaaahidi


wenye taqwa Pepo kwa sababu miongoni mwa


sifa zao ni kuomba maghfira kabla ya Alfajiri:





Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na


chemchem. Wanapokea Aliyowapa Mola wao.


Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya


9


wakifanya mema. Walikuwa wakilala kidogo tu


usiku. Na kabla ya Alfajiri wakiomba


maghfira. [Adh-Dhaariyaat: 15-18]


Kisha wamesifiwa tena kwa sifa kama hiyo


pamoja na nyinginezo:





Wanaosubiri, wanaosema kweli, na watiifu, na


wanaotoa sadaka, na wanaoomba maghafira


kabla ya Alfajiri.[Al-'Imraan: 17]


Muislamu asiache wakati huo umpite kwani ni


wakati muhimu na wenye fadhila na faida kubwa


kwa vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)


Huteremka wakati huo kutoka mbingu ya saba na


kuweko mbingu ya ardhi kututakabalia maombi


ya anayemuomba:


10





Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu


'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi


wa sallam) amesema: (Allaah (Subhaanahu wa


Ta'ala) Huteremka (kwa namna inavyolingana na


utukufu Wake) kila siku katika mbingu ya dunia


(mbingu ya kwanza) inapobakia thuluthi ya


mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba


Nimtakabalie? Nani ana shida Nimtekelezee?


Nani ananiomba maghfirah Nimghufurie?)) [Al-


Bukhaariy na Muslim]


Nani miongoni mwetu asiyemhitaji Mola wake


kumtakabalia haja zake au kumuondeshea shida


zake? Nani asiyekuwa na madhambi asiyemhitaji


Mola wake kumghufuria? Hivyo usiache wakati


huu ukakupita hasa kwa vile ni mwezi wa


Ramadhaan ambao kila jambo ulifanyalo lina


fadhila na thawabu marudufu.


11


Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)


Atuwezeshe kudiriki nyakati hizo tatu na


nyingine, tuwe katika ibada katika mwezi huu wa


Ramadhaan na miezi yote mingineyo na


Atujaalie kheri na Baraka nyingi, Atutakabalie


haja zetu, Atuondoshee shida zetu na Atughufurie


madhambi yetu yote. Aamiyn.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI