Nakala

1


NI YUPI RAFIKI MWEMA? الصديق الصالح


IMEANDALIWA NA: YUNUS KANUNI NGENDA IMEPITIWA NA: ABUBAKARI SHABANI RUKONKWA


2


بسم الله الرحمن الرحيم


Utangulizi


Ndugu zangu katika imani ni kawaida kwa binadam na ni


muhim kuwa na rafiki, Lakini kwa Muislam kuchagua


rafiki mzuri ni lazima kwa ajili ya kuhifadhi Dini yetu.


Kufanya urafiki na watu wema wenye tabia nzuri, wenye


dini na heshima ni moja ya mambo yanayotufanya sisi


Waislam kuwa katika njia iliyonyooka, na kuwa mfano


bora katika jamii.


Mtume (Swalla Allahu Alaihi Wa Sallam) amesema:


"Mtu yamkini (inawezekana) kufuata dini ya rafiki yake,


kwa hivyo muangalie unayemfanya rafiki." {Abu Dawud


na Tirmidhiy}


Ukiona rafiki yako ana matendo maovu, jaribu


kumkumbusha,kumpa nasaha na mawaidha, asipobadilika


na akaendelea kufanya maovu, ni vema kumuepuka kwa


sababu unaweza ukaiga tabia zake ambazo zinakwenda


kinyume na Dini yako (ya kiislam). Lakini pamoja na


kumuepuka inakupasa kumfanyia wema na kumuombea


kwa Allah uongofu.


Allah (Subhanahu Wa Ta'ala) amesema:


"Na Siku ambayo mwenye kudhulumu atajiuma mikono


yake, na huku anasema: 'Laiti ningelishika njia pamoja na


3


Mtume (S.a.w) Ee Ole wangu! Laiti nisingelimfanya fulani


kuwa rafiki! Amenipoteza nikaacha Ukumbusho, baada ya


kwisha nijia, (kunijia) na kweli shetani ni khaini (mwenye


khiyana) kwa mwanaadamu."


{Surat Al-Furqaan 25:27-29}


Allah (Subhanahu Wa Ta'ala) tena Anasema:


"Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao,


isipokuwa wachaji Allah (wacha Mungu)" {Surat Az-


Zukhruf 43:67}


Muumini ni kioo cha ndugu yake muumini, akiona makosa


ya mwenzake inampasa amueleze kwa uzuri na kumsaidia


kurekebisha kosa hilo.


Huo ndio urafiki unaotakiwa katika Uislam, na muumini


wa kweli lazima ataangalia nani wa kumfanya rafiki.


Lakini kwa masikitikiko makubwa vijana wa kiislam wa


leo hawana habari na jambo kama hili, imefikia hatua


marafiki wa zama hizi wanatumia muda mwingi kusaidiana


katika mambo yasiyofaa, badala ya kusaidiana katika


mambo ya dini na ya kheri.


Tunamuomba Allah atuongoze pamoja na marafiki zetu.


Ameen!!!



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI