Nakala




Imeandaliwa na Alhidaya.


Imepitiwa na Abubakari shabani Rukonkwa.


Ingia Katika Milango Mingi Ya Kheri


Ramadhaan


Mwezi mtukufu wa Ramadhaan unakaribia kutufikia.


Chukua fursa ya kujichumia thawabu nyingi kwa sababu


malipo ya amali inayotekelezwa humo yanaanzia mara kumi


mpaka mara mia saba. Juu ya hivyo, kuna malipo maalum


yatokayo kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) kama


ilivyothibiti katika Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu


'alayhi wa aalihi wa sallam):





Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu


‘anhu): ((Kila amali njema ya mwanaadamu inalipwa mara


kumi na inaongezewa thawabu kutoka kumi hadi mia saba,


na Allaah (‘Azza wa Jalla) Anasema: Isipokuwa Swawm,


2


kwani hiyo ni kwa ajili Yangu na Mimi Ndiye


Nitakayemlipa.


Ameacha matamanio yake na chakula chake kwa ajili


Yangu. Kwa aliyefunga swawm atapata furaha mbili; furaha


anapofuturu na furaha atakapoonana na Mola wake, harufu


inayotoka kinywani mwa aliyefunga ni nzuri mbele ya


Allaah kuliko harufu ya misk))


[Muslim na Ahmad]


Kwanza kabisa inatupasa kutia niyyah ya ikhlasi moyoni (si


kuitamka) kwa sababu ni sharti mojawapo la kutakabaliwa


amali yoyote, na ili kupata Radhi za Allaah (Subhaanahu wa


Ta’aala) kama Anavyosema:





Na hawakuamrishwa (chochote kile) isipokuwa wamwabudu


Allaah mukhliswiyn (wenye kumtakasia) Dini, hunafaa1 na


wasimamishe Swalaah na watoe Zakaah; na hiyo ndiyo Dini


iliyosimama imara.


Wakielemea haki na kujiengua na upotofu -١


3


[Al-Bayyinah:5]


Weka azimio la nguvu kutekeleza amali zifuatazo katika


mwezi wa Ramadhaan.


1-Kufunga Swawm kwa imaani na matarajio ili kufutiwa


madhambi





Amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa


sallam): ((Atakayefunga Ramadhaan kwa iymaan na kutaraji


malipo ataghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia ))


Al Bukhaariy na Muslim.


2-Qiyaamul-Layl (Kusimama usiku katika Swalah);


Tarawiyh na Tahajjud





Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallaam)


amesema: ((Atakayesimama [kwa Swalah ya usiku] kwa


4


iymaan na kutaraji malipo, ataghufuriwa madhambi yake


yaliyotangulia)) [Al-Bukhaariy na Muslim]


3-Kutoa sadaka





Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallaam)


amesema:


((Sadaka bora kabisa ni ile inayotolewa katika mwezi wa


Ramadhaan))


[At-Tirmidhiy kutoka kwa Anas]


4-Kumfuturisha aliyefunga Swawm:





Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallaam)


amesema: ((Atakaye mfuturisha aliyefunga Swawm, atapata


5


ujira kama ujira wake bila ya kupungua chochote katika ujira


wa yule aliyefunga))


[Ahmad, An-Nasaaiy – Ameipa daraja ya Swahiyh Shaykh


Al-Albaaniy]


Na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema:





Na wanalisha chakula juu ya mapenzi yao (kwa hicho


wanacholisha) masikini na mayatima na mateka. “Hakika


sisi tunakulisheni kwa ajili ya Allaah, hatutaki kwenu jazaa


na wala shukurani. “Hakika sisi tunakhofu kwa Mola wetu


siku inayokunjisha uso ngumu nzito. . Basi Allaah


Atawakinga na shari ya siku hiyo, na Atawakutanisha na


mng’ao na furaha. Na Atawalipa Jannah na (nguo za) hariri


kwa kusubiri kwao.


[Al-Insaan: 8-12]


Vile vile Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa


sallam) amesema:





((Muumin yeyote atakayemlisha Muumin mwenzake


mwenye njaa, Allaah Atamlisha katika matunda ya Peponi,


na atakayemnywesha Muumin mwenye kiu Allaah


Atamnywesha kutoka katika 'Rahiyqul-


Makhtuum' [Kinywaji safi kilichofunikwa kwa kizibo


madhubuti])) [At-Tirmidhiy na Isnaad yake ni nzuri]


5-Kusoma Qur-aan kwa wingi na kujifunza maana yake.


Mwezi wa Ramadhaan ni mwezi ulioteremshwa Qur-aan


kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):





Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan


ili iwe Hidaaya kwa watu na hoja bayana za Hidaaya na Al-


Furqaan (Upambanuzi). [Al-Baqarah: 185]


Jitahidi ndugu Muislam uzidishe kusoma Qur-aan na


ujitahidi kukhitimisha japo mara moja katika mwezi huu.


Jibriyl (‘alayhis-salaam) alikuwa akimfikia Mtume (Swalla


Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa ajili ya


kumsikiliza na kumfundisha Qur-aan katika mwezi wa


7


Ramadhaan. Vile vile Maswahaba na Salafus-Swaalih


(Wema waliotangulia) walikuwa wakijihimiza sana kusoma


Qur-aan katika mwezi wa Ramadhaan; 'Uthmaan bin


'Affaan (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwa akikhitimisha Quraan


kila siku moja. Na baadhi ya Salaf wakikhitimisha Qurraan


kila siku tatu katika Qiyaamul-layl. Wengineo


walikuwa wakikhitimisha siku saba, na wengine siku kumi.


Na walikuwa wakiisoma katika Swalah na nje ya Swalah.


6-Kukaa kwa kumdhukuru Allaah baada ya Swala ya


Alfajiri hadi jua litoke





Imetoka kwa Anas kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi


wa aalihi wa sallam) amesema:((Atakayeswali Alfajiri


katika Jamaa'ah kisha akakaa anamkumbuka Allaah mpaka


likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira


kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili


kamili))


8


[Imetolewa na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy].


(Kuswali Jama'ah kumesisitizwa kwa wanaume, ama


mwanamke anaweza naye kupata ujira wa thawabu


zilizotajwa akiswali nyumbani kwake)


Thawabu hizo za kama Hajj na ‘Umrah ni katika siku za


kawaida ndugu Muislamu, seuze mwezi wa Ramadhaan?


Usiache fursa hii ikupite. Ukishindwa kuitekeleza kila siku,


basi jitahidi japo wiki mara moja, hapo utakuwa una


thawabu za Hajj na 'Umrah mara nne kwa mwezi, na


ukiendelea hivyo miezi yote kumi na mbili basi utakuwa na


thawabu za Hajj na 'Umrah mara 48 kwa mwaka.


7- Kubakia Masjid kwa ajili ya Itikaaf:





Kutoka kwa 'Aashah (Radhiya Allaahu 'anhaa) kwamba:


"Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa


sallam)alikuwa akikaa Itikaaf kila Ramadhaan katika siku


kumi za mwisho, na mwaka ambao aliondoka duniani alikaa


Itikaaf siku ishirini.


9


[Al- Bukhaariy]


Unapokuwa umo katika I'itikaaf utaweza kutekeleza amali


nyingi zitakazokufanya ubakie katika taqwa na iymaan


kuzidi moyoni. Utaweza kusoma Qur-aan kwa wingi,


kuswali Swalaah za Sunnah, kumdhukuru Allaah


(Subhaanahu wa Ta’ala), kuomba du’aa na maghfira.


Fadhila za I’tikaaf zinazidi inapokuwa katika kumi la


mwisho kwa sababu ya usiku mtukufu unaojulikana kama


ni: ’Laylatul-Qadr’.


8-'Umrah katika mwezi wa Ramadhaan


Ukiwa na uwezo, tekeleza ‘Umrah. Imethibiti katika Hadiyth


ya Mtume (walla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)


kwamba thawabu za kutekeleza 'Umrah katika Ramadhaan


ni sawa na thawabu za kutekeleza Hijjah.





(('Umrah katika Ramadhaan ni sawa [kwa thawabu] na


Hijjah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]


9-Kupata Baraka za Suhuwr (Daku)


10


Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)


amesema:





((Kuleni daku kwani katika huko kula daku, kuna


baraka)) [Al-Bukhaariy na Muslim]


10-Kuomba Du'aa


Ramadhaan ni mwezi wa Du'aa. Allaah (Subhaanahu wa


Ta’ala) Anataja kuhusu kumuomba du’aa baada ya


kutufaridhisha Swawm:





Na watakapokuuliza (Ee Muhammad GH و E وآ EGA لله JGK (


waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Qariyb (Yu karibu


daima kwa elimu Yake); Naitikia maombi ya muombaji


anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi,


wapate kuongoka.


[Al-Baqarah:186]


11


Zinaendelea Aayah za kuhusu Swawm baada yake.


11-Kuomba maghfirah na tawbah:


Omba maghfira na tawbah kabla ya alfajiri. Kufanya hivi


utakuwa miongoni mwa waja wema Anaowasifu Allaah


(Subhaanahu wa Ta’ala):





Na kabla ya Alfajiri wakiomba maghfira


[Adh-Dhaariyaat: 18]


Vile vile Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Huteremka


nyakatii hizo kuweko katika mbingu ya kwanza:





Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu


‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa


sallam amesema: ((Allaah Tabaaraka wa Ta’ala Huteremka


kila siku katika mbingu ya dunia inapobakia thuluthi ya


mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba


Nimtakabalie? Nani ana shida Nimtekelezee? Nani


ananiomba maghfira Nimghufurie?))


[Al-Bukhaariy Na Muslim]


12-Kuunga undugu na jamaa:


Jambo muhimu kulitekeleza siku zote. Mtume (Swalla


Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametahadharisha kwa


anayekata mawasiliano na ndugu au jamaa:





((Fuko la uzazi linaning'inia katika 'Arshi linasema:


“Atakayeniunga, Allaah Atamuunga, na


atakayenitenga Naye Allaah Atamtenga [Atamkatia]”))


[Al-Bukhaariy na Muslim]


13- Kukesha siku kumiza mwisho:


13


Utaweza kudiriki Laylatul-Qadr, usiku ambao ‘ibaadah yake


ni bora kuliko ‘ibaadah utakazoifanya miezi elfu. Anasema


Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):





Hakika Sisi Tumeiteremsha (Qur-aan) katika Laylatil-Qadr


(usiku wa cheo). Na nini kitakachokujulisha ni nini huo


(usiku wa) Laylatul-Qadr? (Usiku wa) Laylatul-Qadr ni


(usiku) mbora kuliko miezi elfu Wanateremka humo


Malaika na Ruwh (Jibriyl) kwa idhini ya Mola wao kwa kila


amri (jambo). (Usiku huo ni) Amani mpaka kuchomoza


Alfajiri. [Al-Qadr: 97]


Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Atujaalie


tawfiyq kutekeleza yote hayo na Atutakabalie. Aamiyn.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI