Nakala




بسم الله الرحمن الرحيم


Imeandaliwa na alhidaya.com


Imepitiwa na Abubakari Shabani Rukonkwa.


MIEZI MITUKUFU IMEINGIA YATAMBUE MATENDO MEMA YANAYO TAKIWA KWA MUISLAM. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): 


((Hakika idadi ya miezi kwa Allaah ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya Allaah, tangu Alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko minne mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) [At-Tawbah: 36]. Miezi minne hiyo imetajwa katika Hadiyth ifuatayo: 





Kutoka kwa Abu Bakrah ambaye amesema: “Mtume


(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema


alipokuwa katika Hijjah ya kuaga (Hijjah wa mwisho):


((Mgawanyo wa nyakati umerudikama ulivyo (wakati)


Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi


kumi na mbili, minne ambayo ni mitukufu; mitatu


inafuatana pamoja (nayo ni) Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na


Muharram, na (wa nne ni) Rajab wa (kabila la) Mudhwar


ambao upo baina ya Jumaada na Sha'abaan)). [Al-


Bukhaariy)


Hivyo tunaona kwamba ni kuanzia mwezi huu tulioingia


wa Dhul-Qa'adah na miezi miwili ijayo inayofuatia kisha


tena hadi tutakapojaaliwa kufika mwezi wa Rajab In shaa


Allaah.


Katika miezi yote kumi na mbili Allaah (Subhaanahu wa


Ta'ala) Ameichagua hii minne na Ameifanya kuwa ni


mitukufu na kusisitiza kuitakasa, na kwamba dhambi


zitakazofanyika humo ni zaidi na hali kadhalika thawabu za


vitendo vyema zinakuwa maradufu na zaidi. [Atw-


Twabariy 14: 238]


Ni sawa kama Anavyoonya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)


kufanya maasi katika sehemu tukufu Alipotaja Masjidul-


Haraam (Msikiti Mtukufu Makkah):





((Hakika wale waliokufuru na wakazuilia Njia ya Allaah


na Msikiti Mtakatifu, ambao Tumeufanya kwa ajili ya


3


watu wote sawasawa, kwa wakaao humo na wageni. Na


kila atakayetaka kufanya upotofu humo kwa dhulma,


basi Tutamwonjesha adhabu iumizayo)). [Al-Hajj: 25].


Qataadah amesema kuhusu kauli ya Allaah:





((Basi msidhulumu nafsi zenu humo))


“Dhulma itakayotendeka katika miezi mitukufu ni mbaya


na kubwa (au hatari) kuliko dhulma itakayotendeka katika


miezi mingine. Hakika dhulma daima ni makosa, lakini


Allaah Hufanya baadhi ya vitu kuwa ni vizito kuliko


vingine kama Anavyopenda.”


Akaendelea kusema: “Allaah Amechagua baadhi ya


viumbe Vyake na baadhi ya vitu kuwa bora zaidi kuliko


vingine, Amechagua Wajumbe kutoka Malaika na kutoka


binaadamu.Vile vile Amechagua baadhi ya kauli Zake


kuwa ni bora kuliko nyingine, Misikiti kuwa bora kuliko


sehemu nyingine za ardhi, Ramadhaan na miezi mitukufu


kuwa bora kuliko miezi mingine, siku ya Ijumaa kuwa ni


bora kuliko siku nyingine na usiku wa Laylatul-Qadr kuwa


ni bora kuliko nyusiku zingine. Kwa hiyo takasa vile


Alivyovitakasa Allaah, kwani kufanya hivyo ni vitendo vya


watu wenye akili na wenye kufahamu.”[Tafsiyr ya Ibn


Kathiyr].


4


Miongoni mwa yaliyokatazwa katika miezi hii mitukufu


ni kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):





((Wanakuuliza juu ya kupigana vita katika mwezi


mtakatifu. Sema: Kupigana vita wakati huo ni dhambi


kubwa Lakini kuzuilia watu wasiende katika Njia ya


Allaah na kumkanusha Yeye, na kuzuilia watu wasende


kwenye Msikiti Mtakatifu na kuwatoa watu wake humo,


ni makubwa zaidi mbele ya Allaah. Na fitina ni mbaya


zaidi kuliko kuua)) [Al-Baqarah: 217].


Maasi Mengine Ambayo Tunatakiwa Tujikumbushe


Kuyaacha


Kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wata'ala)


kama kwenda kwa wachawi na waganga na


kuwaamini wanayoyatabiri kwa watu.


Kuiba;


Kuzini;


Kulewa;


Kumdhulumu mtu haki yake;


Kugombana, kutukanana, kuvunjiana heshima,


kudharauliana n.k.;


Kusengenya (Ghiybah);


Kusema uongo, na kila aina ya uovu mwengine.


5


Mambo Mema Ya Kukumbushana Kufanya Katika Miezi Hii Mitukufu Kuongeza Sunnah za Swalah; *(tazama maelezo chini) Kufunga Swawm za Sunnah kama Jumatatu na Alkhamiys, Ayyaamul-Biydhw (tarehe 13,14 na 15) na Swawm ya Nabii Daawuwd (kufunga kila baada ya siku moja); Kujielimisha mambo ya dini kwa kusoma vitabu na kusikiliza mawaidha; Kuomba Maghfirah na Tawbah; Kufanya kila aina ya dhikr (kumkumbuka na kumtaja Allaah), kwa kusoma Qur-aan kwa wingi, kumshukuru, kumtukuza, kuomba du'aa n.k.; Kuwasiliana na ndugu na jamaa; Kutenda wema kwa jirani, marafiki na watu wote kwa ujumla; Kutoa sadaka; Kulisha masikini; Kupatanisha waliogombana; Kuamrishana mema na kukatazana maovu, na mengi mengineyo katika vitendo vyema.


6


* Swalah za Sunnah Ratiba Ya Swalah Za Sunnah Zilizosisitizwa Na Zisizosisitizwa NYAKATI ZA SWALAH *MUAKKADAH (ZILOSISITIZWA) GHAYR MUAKKADAH (ZISOSISITIZWA) KABLA BAADA KABLA BAADA


ALFAJIRI








Fadhila Zake ))


((Hatoswali mja Rakaa 12 zisizo za fardhi kwa siku, ila atajengewa [na Allaah] nyumba peponi))[Muslim] Nazo ni hizo Muakkadah (Zilosisitizwa) jumla yake ni 12 


** ((Rakaa mbili (za Sunnah) kabla ya Alfajirr ni kheri kuliko duniya na yaliyomo ndani yake) [Muslim]





((Mja yeyote atakayesujudu sijda moja ataandikiwa wema mmoja, na atafutiwa baya moja, na atapandishwa daraja yake, kwa hiyo zidisheni kusujudu)) [Ibn Maajah] Swalah ya Tahajjud 


((Swalah iliyo bora kabisa baada ya Fardh ni Swalah ya usiku)). [Muslim]


8


Swalah Ya Dhwuhaa na Swalah Ya Witri ع





Kutoka kwa Abu Hurayrah (radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba “Ameniusia rafiki yangu Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam [mambo matatu]; kufunga siku tatu katika kila mwezi, Rakaa mbili Dhwuhaa na niswali Witr kabla ya kulala” [Al-Bukhaariy na Muslim] Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kujitenga na maasi na kuzidisha mema katika miezi hii mitukufu. Aamiyn.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI