Nakala

1


Kujitoa Muhanga Kunamuweka Mtu Mbali Na Allaah Mzungumzaji: Imaam Muhammad Swaalih bin bin ´Uthaymiyn Imefasiriwa na: Wanachuoni.com Imepitiwa na: Yunus Kanuni Ngenda


2


بسم الله الرحمن الرحيم


Utangulizi


Kuhusu matendo [ambayo mtu humuonyesha Allaah hasira


kwayo], ni pamoja na kuchana nguo, kupiga mashavu, kukokota


nywele na mfano wa hayo. Baadhi ya watu wanafanya hivi. Hata


hivyo lililo kubwa, chafu na baya zaidi ni kujiua. Kuna watu


wanaojiua wakati wanapopatwa na misiba wasiyoweza kukabiliana


nayo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametueleza


kuhusu mtu aliyejeruhiwa na hakuweza kuvumilia. Akafanya kitu


ambacho hakijuzu na Allaah Akamuwajibishia Moto.


Mwenye kujitoa muhanga ili kuepukana na msiba huu - hivi kweli


ataepukana nao? Jibu! Hapana. Hatouepuka. Anafikiria kuwa


atapata kupumua baada ya kujiua. Pamoja na kwamba sivyo. Akifa


ataadhibiwa Motoni kwa kile alichojiua nacho. Humo


atadumishwa milele.


Kwa ajili hiyo tunawakataza ndugu zetu wanaoenda Palestina ili


kujilipua kati ya mayahudi. Wanafikiri kwa kufanya hivo


wanajikurubisha kwa Allaah. Uhakika wa mambo ni kwamba hili


linawatia mbali na Allaah. Wanajiua wao wenyewe! Kujiua ni


miongoni mwa madhambi makubwa. Mtu ataadhibiwa Motoni kwa


kile alichojiua nacho. Pamoja na hivyo hatusemi kuwa hawa


wanaingia katika kundi la watu hawa kwa kuwa wanafanya hivo


kwa Ijtihaad. Wanafikiria kuwa kitendo hichi ni kizuri. Mtu


mwenye kufanya kitu kwa kuelewa makosa pengine akasamehewa.


Hata hivyo kitendo hichi ni haramu Kishari´ah na sio katika Jihaad


katika njia ya Allaah.


3


Kitendo hichi vilevile hakiingii akilini. Ni mayahudi wangapi


anawaua pale anapojilipua? Ikiwa ni wengi ni watu 50-100.


Matokeo yake mayahudi hufanya nini? Wataua mamia na wanazidi


kuwa wenye kuchupa mipaka kuliko unavowaona sasa kwa kuteka


mji.


Lakini watu wengi hawatazami matokeo. Hawafikirii mbali.


Talare: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn


Imefasiriwa na: Wanachuoni.com


Milipuko Inayofanywa Haijawapatia Waislamu Faida Yoyote


Zaidi Ya Madhara Juu Ya Madhara


Kuhusiana na yale yanayofanywa na baadhi ya watu kujitoa


muhanga kwa kujiweka mabomu na kuwaendea makafiri kisha


wanajilipua pindi wanapokuwa kati yao, huku inachukuliwa ni


kujiua - na tunaomba kinga kwa Allaah. Mwenye kuiua nafsi yake


atadumishwa Motoni milele kama ilivyokuja katika Hadiyth yake


(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).


Huyu aliyeiua nafsi yake hakuleta faida yoyote kwa Waislamu


hata kwa wasiokuwa Waislamu. Kwa sababu akiua watu kumi,


ishirini, mia au mia mbili, Uislamu haufaidiki chochote kwa hilo.


Wala hilo haliwafanyi watu kuingia katika Uislamu. Tofauti na


kile kisa cha yule kijana, yeye alisababisha watu wote wakaingia


katika Uislamu. Hata hivyo haihitajiki kuua adui kumi, ishirini,


mia au mia mbili kwa ajili watu waingie katika Uislamu. Kinyume


chake huenda maudhi ya maadui ndiyo yakazidi kuwa mengi.


4


Jambo hili ambalo Waislamu hawa wanafanya linapelekea


makafiri kuzidisha maudhi yao dhidi ya Waislamu.


Mfano wa hili ni kama sasa jinsi mayahudi wanavofanya dhidi ya


wapalestina. Mpalestina mmoja anapojilipua na kuua [mayahudi]


sita mpaka saba, matokeo yake wanajilipiza kwa kuua wapalestina


sitini, sabini au zaidi. Kwa hali hiyo kunakuwa hakuna faida


yoyote kwa Waislamu wala hao waliojilipua. Ndio maana naona


yeyote atakayefanya kitendo kama hicho atakuwa amejiua bila ya


haki. Hili litasababisha yeye kuingia Motoni - na tunaomba kinga


kwa Allaah. Aliyefanya hivo sio shahidi.


Lakini ikiwa mtu atafanya kitendo hiki kwa ujinga na huku


akifikiria kuwa inajuzu, tunatumai kuwa hatopata madhambi. Hata


hivyo hatofikia daraja ya aliyekufa shahidi kwa sababu


hakufanya kama anayekufa shahidi anavyopaswa kufanya. Lakini


hatopama madhambi kwa kuwa amefanya hivo kwa kufahamu


makosa. Yule mwenye kujitahidi na akakosea, anapata thawabu


moja.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI