Nakala

1


1


إياكم و الغلو


JIEPUSHENI NA KUCHUPA MIPAKA


MUANDISHI SHEKH: YASINI TWAHA


KIMEREJEWA NA SHEKH: ABUBAKARI SHABANI


2


2


Kwajina la Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma


mwenye kurehemu.


Tunamshukuru Mwenyezi Mungu Mmoja, Rehma na


Amani za Allah zimuendee nabii Muhammad (s.a.w)


hakuna nabii baada yake, pamoja na ahli zake na


maswahaba zake na Waislamu woote watakao fuata


mwenendo wake hadi siku ya kiyama. Amma baad:


Hakika Uislamu ni Dini ya uadilifu na ya kati kwa kati


na kuacha kuchupa mipaka.


Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na vivyo hivyo


tumekufanyeni muwe Umma wa wasitani).


(Al-Baqara: 143).


Maana yake: Waadilifu walio bora.


Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Sema: Mola


wangu ameamrisha uadilifu). (Al-Aaraf: 29).


Na Uislamu ni Dini nyepesi yenye huruma na kuondoa


uzito.


Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Wala hakuweka


juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya


baba yenu Ibrahim. Yeye (Mwenyezi Mungu) alikuiteni


Waislam tangu zamani). (Al-Hajj: 78).


Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Mwenyezi


Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya


iwezavyo). (Al-Baqara: 286).


3


3


Na akasema: (Mwenyezi Mungu hamkalifishi mtu


isipokuwa kwa kadiri ya alicho mpa. Mwenyezi Mungu


atajaalia baada ya dhiki faraji). (Attalaaq: 7).


Na Mtume (s.a.w) alikuwa ni mfano wa kimatendo


katika hii dini, kwa hakika yeye (s.a.w) alipo mtuma


Mudhi pamoja na Abaa Mussa kwenda Yemen


aliwahusia kwa kusema: (Fanyeni wepesi na msifanyi


uzito, wabashirieni watu yalio mazuri na wala


msiwakimbize, saidianeni na wala msitofautiane).


Kapokea hadithi hii imam Bukhari na Muslim.


Usio huu sio kwa wawili hawa tu, bali kwa kila alio


lazimishwa na sheria, inaonyesha jambo hilo kauli yake


Mtume (s.a.w): (Hakika Dini ni nyepesi, na hakuna


atakae fanya uzito isipokuwa itamshinda, fanyeni yalio


ya sawa sawa, fanyeni yalio ya karibu, wabashirieni watu


yalio ya kheri).


Kapokea hadithi hii imam Bukhari.


Hakika sheria ya Uislamu inapinga kuchupa mipaka


katika dini, kwa sababu jambo hilo huondoa Uislamu


katika usawa na uadilifu, kwa sababu hiyo kawakataza


Mwenyezi Mungu walio pewa kitabu kutochupa mipaka


katika dini yao, kwa sababu kuchupa mipaka hupelekea


katika ukafiri na upotevu na kumzulia Mwenyezi Mungu


kwa namna nyingi za uzushi.


Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Enyi Watu wa


Kitabu! Msipituke mipaka katika dini yenu, wala


msimseme Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa lilio


kweli). (An-Nisaa: 171).


Na akawakataza Mwenyezi Mungu wajawake waumini


4


4


kutochupa mipaka katika dini kwa kuharamisha yalio


mazuri, na akaeleza ya kwamba vitendo hivi nivya


wakeukao wasio pendwa na Mwenyezi Mungu.


Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Enyi mlio amini!


Msiharimishe vizuri alivyo kuhalalishieni Mwenyezi


Mungu, wala msikiuke mipaka. Hakika Mwenyezi


Mungu hawapendi wakiukao mipaka). (Al-Maaida: 87).


Mwenyezi Mungu atujaalie tuwe niwenye kufuata sheria


zaka bila kuchupa mipaka, tuwe watu wa kati kwa


kati,Rehma na Amani za Mwenyezi Mungu zimshukie


nabii Muhammad (s.a.w) pamoja na Ahli zake na


Maswahaba zake na Waislam woote hadi siku ya


Mwisho.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI