Nakala




HUKUMU YA ANAEFUNGA HALI YA KUWA HASWALI.


SWAHILI.


IMEANDIWA NA:


DAUDI ABUBAKARI.


IMEPITIWA NA:


ABUBAKARI SHABANI





بسم الله الرحمن الرحيم


Utangulizi


Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe


vyote, na rehma na amani zimwendee Mtume wetu


Muhammad (s.a.w) na watu wake na Maswahaba wake wote.


Amma baad:


Fatawa ya Sheikh Uthaymiyn katika Hukmu ya Mfungaji


Saum ambaye Haswali.


Swali:-


Nini Hukmu ya Mtu anaefunga lakini Haswali?


Jibu:-


Mwenye kuacha swala huku anafunga sio Sahih Saumu yake


wala Haikubaliki,Kwa hakika mwenye Kuacha Swala ni Kafir


Murtad, kwa Kauli ya Allah inayosema





Anasema Allah "Wakitubu na Wakasimamisha Swala na


wakatoa Zaka basi hao ni ndugu zenu katika Dini" (Tawbah


Aya 11).


2


Na Kauli ya Mtume (s.a.w) aliposema"Ahadi iliyopo Kati yetu


na wao ni Swala na Yeyote atakaeacha Swala amekufuru"


Na akasema tena





"Kati ya Mtu na Shirk na Kufru ni kuacha Swala"


Na hii ni Kauli ya Jumla ya Maswhaba kwa yule asiyekuwa


pamoja nao.


Anasema Abdullah Ibn Shaqiyq (r.a) Naye alikuwa miongoni


mwa Tabi'in ambaye ni Maarufu;-"Walikuwa Maswhaba wa


Mtume (s.a.w) Hawakuona Kitu ambacho Mtu anaweza


kuacha akawa Kafir Kinyume na mwenye Kuacha Swala.


Na kwa hili anapofunga Mtu na hali ya kuwa Haswali


Swaumu yake ni yenye Kurudishwa haikubaliki wala Haina


manufaa mbele ya Allah siku ya Qiyamah,


Nasisi tunasema: Swala Kisha Saumu na Amma atakaefunga


akawa Haswali basi Saumu yake anarejeshewa


mwenyewe,Kwa hakika Kafir Haikubaliwi Ibada yake.


Pia Allah amewaandalia adhabu kali wenye kuswali ilihali


wanazisahau swala zao, amesema Allah mtukufu :





(Basi, ole wao wanao Sali Ambao wanapuuza Sala zao).


Katika hizi aya Allah ameeleza adhabu ambayo watafikia


wale ambao wanaswali ila swala zao wanazisahau na


kupuuzia mpaka muda wake unapita, sasa ikiwa hali yao


nikama hiyo wale wasio swali kabisa hawawezi kuwa waislam.


3


Tunamuomba Allah atudumishe katika swala na tuwe


niwenye kutekeleza swala katika wakati wake.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI