Nakala




FADHILA ZA KULA DAKU


Kiswahili.


Imeandikwa na: Imaam Swaalih bin Fawzan Al-Fawzaan.


Imetafsiriwa na: Yasini Twaha Hassani


Imepitiwa na: Yunus Kanuni Ngenda


1


بسم الله الرحمن الرحيم


Utangulizi


Sifa zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe


vyote, na rehma na amani zimwendee Mtume wetu


Muhammad (s.a.w) na watu wake na Maswahaba wake wote.


Amma baad:


Mtu ni mwenye haja ya kula na kunywa. Kwa ajili hii Allaah


Hakumkataza mfungaji kula, kunywa na kufanya jimaa wakati


wa usiku isipokuwa tu wakati wa mchana, kuanzia pale


ambapo alfajiri inapoingia mpaka wakati jua linapozama.


Allaah Anapenda watu wale daku. Mtume (Swalla Allaahu


´alayhi wa sallam) amesema kuhusu daku:


“Kuleni daku. Hakika katika kula daku kuna baraka”.


Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:


“Allaah (´Azza wa Jalla) na Malaika Wake wanawaswalia


wenye kula daku.”


(Ibn Hibbaan (3467),


Atw-Twabaraaniy i ”


Al-Awsatw” (6434) na


Abu Nu´aym (8/320). Hasan kwa mujibu wa al-Albaaniy


katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb” (1070).


Kwa nini daku?


Daku si ni chakula tu ambacho mtu anakula kwa matamanio?.


2


Kwa sababu nia yake ni kutekeleza maamrisho ya Allaah


ambayo ni kufunga, ili aweze kupata nguvu za kumuabudu


Allaah. Kwa ajili hio kila ambavyo daku itacheleweshwa ndio


bora zaidi:





”Na kuleni na kunyweni mpaka ibainike kwenu weupe (wa


Afajiri) kutokana na weusi (wa usiku).” (02:187)


Ama yule anayekula usiku mzima na kujaza tumbo lake kisha


analala nyuma na wala haamki kula daku pamoja na Waislamu


wenzake na wala haswali hata al-Fajr, huyu kwa hakika


hakutekeleza maamrisho ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).


Amechofanya ni kutekeleza maamrisho na hawaa ya nafsi


yake. Yuko macho usiku mzima ambapo anakesha kwa


kumuasi Allaah na analala wakati ambapo anatakiwa kumtii


Allaah (´Azza wa Jalla).


CHANZO:


http://www.alfawzan.af.org.sa/node/%205824



Machapisho ya hivi karibuni

Mafungamani ya Shahad ...

Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.

Namna ya swala ya mtu ...

Namna ya swala ya mtume (s.a.w). na Namna ya kutawadha

FADHILA YA SUNNA ZA M ...

FADHILA YA SUNNA ZA MTUME (S.A.W)

MAZUNGUMZO KATIKA PEP ...

MAZUNGUMZO KATIKA PEPO NA JAHANNAMU (SEHEMU YA 3 KATI YA 3): NA SITAWAHI WAKASIRIKIA TENA.