Nakala

بسم الله الرحمن الرحيم


BID'A YA MAWLIDI Imeandikwa na: Shaykh 'Abdullaah Swaalih Faarsiy Imepitiwa na: Abubakari shabani Rukonkwa 1. Kusoma Mawlid Mawlid ni uzushi (Bid’ah) uliyozuka baada ya kupita hao watu mabora aliowasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kama tulivyobainisha katika Dhikiri namba moja. “KUDHIKIRI” Hata mjukuu wa huyu aliyetunga Mawlid ya Barzanjiy akaifanyia sharh yake akiita “Al-Kawkabul-Anwaar” aliandika katika sahifa 4 maneno haya “Jua kuwa kusoma Mawlid ni bid’ah (uzushi) kwani halijapokelewa jambo hili kwa hao Ulamaa waliokuwa karne tatu tukufu za mbele huko zilizosifiwa na Mtume”. Basi inatosha shahada hii ya huyu mjukuu khasa wa huyu mwenye Barzanjiy. Imekuwa “Washahida shaahidun min ahlih” yaani akashuhudia shahidi wao wenyewe. Basi wacha kushughulikia mambo yasiyokuwa ndiyo, khasa ilivyokuwa yanatokea ndani yake mambo mabaya kabisa yasiyokuwa ndiyo. Kama mchanganyiko wa wanaume na wanawake unaotokea wakafanya mambo yasiyokuwa ndiyo. Na mambo haya si kificho, hakuna asiyejua. Na ubaya wake mkubwa zaidi kule kuwadhanisha watu kuwa hilo ni jambo zuri lilohimizwa na Mtume, kumbe kinyume


nyume. Usitoe pesa lako kwa jambo lilokwenda kinyume na


alivyosema Mtume.


2. Zeffe (Zafa)


Nani asiyejua namna Zeffe inavyoutia aibu Uislamu? Fujo la


wanaume na wanawake, mbali fujo la wahuni. Fujo la


wanaocheza ngoma za uchafu, na chakacha na dansa na


nyinginezo. Yuko mwenye akili yake timamu akayaona mazuri


haya?


3. Kupiga Dufu (Daf) Na Mazumari


Kupiga daf msikitini ni haramu kwa wanavyouni wote


wanaotegemewa kama ilivyo sahifa 273 ya Juzuu ya tatu ya


“I’anatut-Twalibyn” Alisema: “Halipigwi Daf msikitini, seuze


kupiga mazumari” Ati Gasba; Gasba ndiye nduguye zumari na


zumari ndiye nduguye Gasba. Ila huyu mfupi huyu mrefu.


Ama kupigwa nje ya Msikiti kwa jambo la arusi na la furaha


(kwa wanawake) haikatazwi maadam hapana mchanganyiko wa


wanaume na wanawake.


Ama kwa jambo linaloitikadiwa kuwa la Dini basi hakuna


yeyote mwenye kutegemewa aliyesema ni jambo zuri hilo seuze


kusema ni Sunnah. Mufti mkubwa wa Hadhramauti wa zama


hizo – Sayyid ‘Abdur-Rahmaan Mashhuur - Alisema katika


sahifa 322 ya kitabu chake: “Bughyatul-Mustarshidyn”: “Na


kwa kila hali mambo hayo ima haramu au karaha au Sivyo


ilivyo bora”.


Basi uko wapi huo uzuri hapa? Seuze Usunnah? Si Sharifu wa


Hadhramauti huyu? Na Mufti huko pia? Na ndiye Sheikh wa


Sayyid Mansab, Sayyid Ahmad bin Sumeit na Shaykh


‘Abdallaah Bakathiyr na walimfuata vyema kwani ndiyo haki.


Hawakuhudhuria kwenye matari wala hawakuya kubalisha


mpaka wameondoka ulimwenguni.


Na huyu mufti alizaliwa Hadhramaut mwaka 1250 akafa 1320.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI