Nakala

1


ADABU ZA KULA





BISMI LLAHI RRAH MANI RRAHIIM


Utangulizi


Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumtakia Rehma


na amani Nabii Muhammad (s.a.w) pamoja na familia yake na


Maswahaba zake na Waislamu wote watakao fuata mwenendo


wake mpaka siku ya mwisho tuna muomba Mwenyezi Mungu


atujaalie nasi tuwe miongoni mwahao Aamiin.


Kutoka kwa AbaHuraira (r.a) amesema: Amesema Mtume


Muhammad (s.a.w): (Hakika jambo la kwanza atakalo ulizwa


mja siku ya kiyama miongoni mwa neema, ataambiwa:


Jee! Sijakupa afya njema na kukunywesha maji ya baridi?).


kapokea hadithi hii Imam Tirmidhi.


MIONGONI MWA ADABU ZA KULA:


1: Kutaja jina la Mwenyezi Mungu Mwanzo wa kula kwako.


Kutoka kwa Bibi Aisha (r.a) kwamba Mtume (s.a.w) amesema:


(atapo kula Mmoja wenu ataje jina la Mwenyezi Mungu


Mtukufu, akisahau kutaja jina la Mwenyezi Mungu Mwanzo wa


kula, asema: kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzo wake na


mwisho wake). Kapokea hadithi hii Imam Tirmidhi, na Ahmad,


na Daramy.


2: kusema Bismi llahi, ni kila mtu, sio kwamba akisema Mmoja


anawatosheleza wengine anao kula nao, kwa sababu Sunna hii


niya kila mtu inatakiwa aiseme, wala usiifananishe na Salamu,


Hadithi ya Amru bin Salama (r.a) wakati aliambiwa na Mtume


(s.a.w): (Ewe kijana! Sema: Bismillahi, na ule kwa mkono wako


wa kulia, na ule mbele yako).


3


3: NAMNA YA KUSEMA BISMILLAHI WAKATI WA


KULA NA KUNYWA:


Aseme: Bismillah, wala asizidishe Arrahmani rrahiim. Laity


akisema: Bismillahi Rrahmani Rrahiim, atakuwa kenda kinyume


na Sunna.


Kwa hakika limepokelewa tamko la wazi la (Bismillah) katika


hadithi alio ipokea Imam Abii Daud na Tirmidhi, na


kaisahihisha Shekh Albani (r.h) kwa hadithi ya Bibi Aisha (r.a)


amesema: amesema Mtume (s.a.w):


(Atapo kula Mmoja wenu chakula, na aseme: Bismillah).


Na katika hadithi nyingine, kutoka kwa Amru (r.a) amesema:


nilikuwa kijana mdogo katika malezi ya Mtume (s.a.w) mkono


wangu ulikuwa hautulii kwenye sahani ya chakula, akaniambia


Mtume (s.a.w): (Ewe kijana! Utakapo anza kula, useme:


Bismillah).


Kapokea hadithi hii Imam Twabarani, na akasema Shekh Albani


upokezi wake ni sahihi, kwa sharti za Imam Bukhari na Muslim,


zingatia hili kwa sababu ni muhimu sana kwa wale wanao


tukuza Sunna, na wala hawakubali kuzidisha zaidi ya Bismillah.


Angalia Irwail-Ghaliil, (3/31).


Kwa haya machache tuna muomba Mwenyezi Mungu atujaalie


tuyafanyie kazi haya na mengine Inshaallah!.


Ewe Mola wetu zipeleke Rehma na Amani kwa Mtume wetu


Muhammad (s.a.w) pamoja Familia yake na Maswahaba haze na


Waislamu wote hadi siku ya mwisho. Aamiin.



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI