Nakala

Yohana 14:16  "Nami nitamwomba Baba, naye atawapeni Msaidizi mwingine akae nanyi siku zote." 





 Katika aya hii, Yesu anaahidi kwamba “Msaidizi” mwingine atatokea, na hivyo, ni lazima tuzungumze baadhi ya masuala kuhusu huyu “Msaidizi”.





Neno la Kigiriki paravklhtoß, ho parakletos, limetafsiriwa kama 'Msaidizi.' Parakletos kwa usahihi ina maana 'yule anayeomba kwa niaba ya mwingine, mwombezi.'[1] Ho parakletos (Msaidizi ) ni mtu katika lugha ya Kigiriki, si kipengele kisichokuwa na mwili. Katika lugha ya Kigiriki, kila nomino ina jinsia; yaani, ni kiume, kike au ni huru. Katika Injili ya Yohana, Sura 14, 15 na 16 ho parakletos ni mtu halisi. Viwakilishi vyote kwa Kigiriki lazima vikubaliane kijinsia na neno ambalo vinawakilisha, na kiwakilishi “yeye(kiume)” kimetumika kurejelea parakletos. Agano jipya linatumia neno pneuma, ambalo linamaanisha “pumzi” au “roho,” na lina maana sawa na neno ruah, neno la Kiebrania linalo maanisha “roho” linalotumiwa katika Agano la kale. Pneuma ni neno la kisarufi huru na daima linawakilishwa na kiwakilishi “ni.”





  Biblia zote za kisasa zimekusanywa kutoka “miswada ya kale,”ambapo mswada wa zamani zaidi ni wa karne ya nne B.K. Hakuna miswada miwili ya kale inayofanana. [2] Biblia zote za leo zinaandikwa kwa kuchanganya miswada bila kumbukumbu moja ya uhakika. Watafsiri wa Biblia hujaribu “kuchagua” toleo sahihi. Kwa maana nyingine, kwa kuwa hawajui ni “mswada wa kale” upi ndio sahihi, wanaamua kwa niaba yetu ni “toleo” lipi la aya fulani ndio sahihi.  Chukua Yohana 14:26 kama mfano. Yohana 14:26 ndiyo aya pekee ya Biblia inayohusisha Parakletos na Roho Mtakatifu. Lakini “miswada ya kale” hayakubali kuwa “Parakletos” ndiye 'Roho Mtakatifu. ' Kwa mfano, Kodeks Syriakus, iliyoandikwa takriban karne ya tano B.K., na kugunduliwa  mwaka wa 1812 juu ya mlima Sinai, maandishi ya 14:26 yanasoma; “Paraklete, Roho”; na si “Paraklete, Roho Mtakatifu.”





Kwa nini hii ni muhimu? Kwa sababu katika lugha ya Biblia, “roho,” inamaanisha tu “nabii.”





“Wapendwa, msiamini kila roho bali zipimieni roho zote kwa makini muone kama zinatoka kwa Mungu: Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea duniani."[3]





Ni jambo la kuelimisha kujua kwamba wasomi kadhaa wa Bibilia waliona parakletos kuwa 'mwokovu huru (aliye na uwezo wa kuokoa), 'na si Roho Mtakatifu.[4]





Swali, basi, ni: Je, parakletos wa Yesu, Msaidizi,alikuwa ni 'Roho Mtakatifu' au mtu - nabii - ambaye angekuja baada yake? Ili kujibu swali, ni lazima tuelewe maelezo ya ho parakletos  na kuona kama yanaafikiana na roho au mwanadamu.





Tunapoendelea kusoma zaidi ya sura ya 14:16 na sura ya 16:7, tunaona kwamba Yesu anatabiri maelezo maalum ya kuwasili kwa na utambulisho wa parakletos. Kwa hiyo, kulingana na Yohana 14 na 16  tunagundua mambo yafuatayo.





1.      Yesu alisema parakletos ni mwanadamu:


Yohana 16:13 "Atanena..."





Yohana 16:7 "…kwa maana nisipoondoka, yule Msaidizi hatakuja kwenu."





Haiwezekani kwamba Msaidizi awe ni “Roho Mtakatifu” kwa sababu Roho Mtakatifu alikuwepo kwa muda mrefu kabla ya Yesu na wakati wa huduma yake.[5]





Yohana 16:13 Yesu alimwongelea paraklete kama 'yeye' na si kama 'kitu' kwa mara saba, hakuna mstari mwingine katika Biblia ambao una viwakilishi saba vya kiume. Kwa hivyo, paraklete ni mtu, na sio roho.





2.      Yesu anaitwa parakletos:


"Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye mtetezi (parakletos) wetu kwa baba, Yesu Kristo mwenye haki." (1 Yohana 2:1)





Hapa tunaona kwamba parakletos ni mwombezi aliye na mwili na ni mwanadamu.





3.      Uungu wa Yesu ni Uvumbuzi uliokuja baadaye


Yesu hakukubaliwa kuwa mungu hadi Baraza la Nikea, 325 BK, lakini kila mtu, isipokuwa Wayahudi, anakubaliana kuwa alikuwa nabii wa Mungu, kama ilivyoonyeshwa na Biblia:





Matayo 21:11 "...Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya."





Luka 24:19 "...Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele za wanadamu."





4.      Yesu alimwomba Mungu awape parakletos mwingine:


Yohana 14:16 "Nami nitamwomba Baba, naye atawapeni Msaidizi mwingine akae nanyi siku zote."





5.      Yesu anaeleza jukumu la Yule Parakletos Mwingine:


Yohana 16:13 "Atawaongoza muijue kweli yote."





Mwenyezi Mungu anasema katika Kurani kuhusu Muhammad:





"Enyi Watu! Amekwisha kujieni Mtume huyu na haki itokayo kwa Mola wenu Mlezi. Basi aminini, ndiyo kheri yenu.!..." (Kurani 4:170)





Yohana 16:14 "Atanitukuza mimi."





Kurani aliyokuja nayo Muhammad inamtukuza Yesu:





"…Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).." (Kurani 3:45)





Muhammad pia alimtukuza Yesu:





"Yeyote atakaye shuhudia ya kwamba hakuna anayestahili kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu, ambaye hana mshiriki, na kuwa Muhammad ni mja wake na Mtume wake, na Isa ni mja wa Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na neno lake alilo mpea Maryamu, na roho iliyotoka kwake, na kuwa Pepo ni kweli, na Jahannamu ni kweli, Mwenyezi Mungu atamkaribisha kwa Pepo kulingana na yale aliyo yatenda.." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)





Yohana 16:8 "Naye akija atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, na haki na hukumu ."





Kurani inaeleza:





"Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu! Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru. !’" (Kurani 5:72)





Yohana 16:13 "Yeye hatanena kwa uwezo wake mwenyewe, bali atanena yote atakayosikia."





Kurani inasema kuhusu Muhammad:





"Wala hatamki kwa matamanio.Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa." (Kurani 53:3-4)





Yohana 14:26 "atawafundisha mambo yote, na kuwakumbusha yote."





Maneno ya Kurani:





"…Na hali Masihi mwenyewe alisema, ‘Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi.’" (Kurani 5:72)





…yanawakumbusha watu amri kuu na ya kwanza ya Yesu, ambayo wameisahau:





"Ya kwanza ndiyo hii: ‘Sikiliza Israeli! Bwana Mungu wetu, ndiye peke yake Bwana.’" (Marko 12:29)





Yohana 16:13 "atawafundisha kuhusu mambo yote yajayo."





Kurani inasema:





"Hizi ni katika khabari za ghaibu tulizo kufunulia, [Ewe Muhammad]…" (Kurani 12:102)





Hudhaifa, mwanafunzi wa Mtume Muhammad, anatuambia:





"Mtume, rehma ziwe juu yake, aliwahi kusimama kati yetu na kutoa hotuba, ambapo hakuacha chochote bali alituambya yote yatakayotokea hadi siku ya kiama ." (Saheeh Al-Bukhari)





Yohana 14:16 "akae nanyi siku zote."





…maana yake ni kuwa mafundisho yake ya awali yatabaki milele. Muhammad alikuwa nabii wa mwisho wa Mungu kwa wanadamu. [1] Mafundisho yake yamehifadhiwa kikamilifu. Anaishi ndani ya mioyo na akili za wafuasi wake wanaomwabudu Mungu kwa kumuiga Muhammad kisawasawa. Hakuna mtu, ikiwa ni pamoja na Yesu au Muhammad, anayeishi milele duniani. Na Parakletos si kesi ya kipekee pia. Hili haliwezi kuwa linamzungumzia Roho Mtakatifu, kwani imani ya kisasa ya Roho Mtakatifu haikuwepo kabla ya Baraza la Kalsedoni , mnamo 451 BK, karne nne na nusu baada ya Yesu.





Yohana 14:17 "huyo ndiye roho wa kweli"





…maana atakuwa nabii wa kweli, tazama 1 Yohana 4: 1-3.





Yohana 14:17 "ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea kwa kuwa haumwoni..."





Watu wengi duniani leo hawamjui Muhammad.





Yohana 14:17 "...wala haumtambui"





Wachache zaidi ndio wanaomtambua Muhammad wa kweli, Mtume wa Rehema wa Mungu.





Yohana 14:26 "yule Msaidizi (parakletos)"





Muhammad ndiye atakuwa mtetezi wa wanadamu kwa ujumla na Waumini wenye madhambi siku ya kiama:





Watu watawatafuta wanaoweza kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu kwa niaba yao ili kupunguza dhiki na mateso Siku ya Kiyama. Adamu, Nuhu, Ibrahimu, Musa na Yesu watajitoa na kupeana udhuru zao.





Kisha watakuja kwa Nabii wetu, naye atasema: 'Hakika mimi ndiye mwenye uwezo'. Kisha atawaombea watu katika uwanja mkubwa ambapo watu wamekusanyika, hukumu itolewe. Hiki ndicho 'Cheo kilicho sifika ' ambacho Mungu anamuahidi katika Qur'an:





"…Huenda Mola wako Mlezi akakunyanyua cheo kinacho sifika (heshima ya kuwa mwombezi siku ya kiyama)" (Kurani 17:79)[2]





Mtume Muhammad alisema:





"Maombezi yangu yatakuwa kwa wale wa taifa langu waliotenda dhambi kuu." (Al-Tirmidhi)





"Mimi nitakuwa mwombezi wa kwanza katika Peponi.." (Saheeh Muslim)





Baadhi ya wasomi wa Kiislamu wanaonyesha kuwa kile ambacho Yesu alisema kwa Kiaramu kinawakilisha kwa karibu zaidi neno la Kigiriki periklytos ambalo linamaanisha 'anayependwa.' Kwa Kiarabu neno 'Muhammad' linamaanisha 'anayesifiwa, anayeheshimiwa. ' Kwa maana nyingine, periklytos ni “Muhammad” kwa Kigiriki. Tuna sababu mbili kuu za kuunga mkono jambo hili. Kwanza, kutokana na matukio kadhaa yaliyorekodiwa ya kubadilisha maneno yanayofanana katika Bibilia, inawezekana kwamba maneno yote mawili yalikuwa katika maandishi ya awali lakini yaliwachwa na mwandishi kwa sababu ya desturi ya kale ya kuandika maneno yakikaribiana, bila nafasi katikati. Katika hali kama hiyo maandishi ya awali yangekuwa, “na atawapa msaidizi mwingine (parakletos), anayependwa (periklytos).” Pili, tuna ushuhuda wa kuaminika wa angalau wasomi wanne wa Kiislamu kutoka kwa vipindi tofauti ambao waliwahesabia wasomi wa Wakristo kuwa 'wa kusifiwa' ndio maana inayowezekana ya neno la Kigiriki au la Kisyriak .[3]





Wafuatao ni kati ya wale walioshuhudia kwamba Paraklete inamrejelea Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake:





Shahidi wa Kwanza


Anselm Turmeda (1352/55-1425 BK), kuhani na msomi wa Kikristo, alikuwa shahidi wa utabiri huu. Baada ya kukubali Uislamu aliandika kitabu, "Tuhfat al-arib fi al-radd ‘ala Ahl al-Salib."





Shahidi wa Pili


Abdul-Ahad Dawud, ambaye ni Mchungaji wa zamani David Abdu Benjamin Keldani, BD, padri Mkatoliki wa madhehebu ya Umoja wa Wakaldayo. [4] Baada ya kukubali Uislamu, aliandika kitabu, 'Muhammad katika Biblia. ' Anaandika yafuatayo katika kitabu chake:





“Hakuna shaka hata kidogo kwamba neno “Periqlyte,” inamlenga Nabii Muhammad, yaani Ahmad."





Shahidi wa Tatu


Muhtasari wa maisha ya Muhammad Asad tayari imetolewa hapo juu. Akitoa maoni yake kuhusu mstari huo:





"…Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad" (Kurani 61:6)





…ambapo Yesu anatabiri kuja kwa Muhammad, Asad anaelezea kuwa neno Parakletos:





"…bila shaka ni Periklytos ('anayesifiwa kwa wingi'), iliyo badilishwa, na ni tafsiri halisi ya Kigiriki ya neno au jina la Kiaramu la Mawhamana. (Ikumbukwe kwamba Kiaramu ilikuwa lugha iliyotumiwa Palestina wakati wa Yesu, na kwa karne kadhaa baada yake, na hivyo bila shaka ilikuwa lugha ambayo maandiko ya kiasili -ambayo yamepotea kwa sasa - ya Injili yalitungwa.) Kwa mtazamo wa ukaribu wa kimatamshi kati ya Periklytos na Parakletos, ni rahisi kuelewa jinsi mfasiri - au, labda zaidi, mwandishi wa baadaye - aliyachanganya maneno haya mawili. Ni muhimu kwamba maneno ya Kiaramu Mawhamana na Periklytos ya Kigiriki yana maana sawa na ni majina mawili ya Mtume wa Mwisho, Muhammad na Ahmad, ambayo yote yametokana na kitenzi cha Kiebrania hamida ('alisifu') na nomino ya Kiebrania hamd ('sifu').”



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI