Nakala

1


بسم الله الرحمن الرحيم


UMMATI MUHAMMAD UTAKUWA WA KWANZA KUINGIA PEPONI. Imeandaliwa na alhidaaya.com Imepitiwa na Yunus Kanuni Ngenda Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): 


((Watu wote walikuwa ni Umma mmoja. Allaah Akapeleka Manabii wabashiri na waonyaji. Na pamoja nao Akateremsha Kitabu kwa Haki, ili kihukumu baina ya watu katika yale waliokhitalifiana. Na wala hawakukhitalifiana ila wale waliopewa Kitabu hicho baada ya kuwafikia hoja zilizo wazi, kwa sababu ya uhasidi baina yao. Ndipo Allaah kwa idhini Yake Akawaongoa walioamini kuiendea haki katika mambo waliyokhitalifiana. Na Allaah Humwongoa Amtakaye kwenye Njia Iliyonyooka)) [Al-Baqarah: 213] Ibn 'Abbaas amesema kuhusu kauli hii: "Kulikuweko na vizazi (karne) kumi baina ya Aadam (‘AlayhisSalaam) na Nuuh (‘Alayhis Salaam), wote wakiwa katika dini ya haki. Kisha tena wakakhitilafiana, hivyo Allah Akatuma Mitume kama waonyaji na wabashiriaji" [Tafsiyr Ibn Kathiyr].


2


Idadi ya Mitume ni 124,000 wakiwemo Wajumbe


313 kama ilivyo kauli ya wengi wa Maulamaa wa Ahlus-Sunnah


wal Jama’ah. Mitume 25 wametajwa majina yao katika Qur-aan.


[Aysarut-Tafaasiyr – Abu Bakr Al-Jazaairy 1:191]


Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) alisema kuhusu kauli:





((Ndipo Allaah kwa idhini Yake Akawaongoa walioamini


kuiendea haki katika mambo waliyokhitalifiana))


Akasema kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa


sallam) amesema:





((Sisi ni (Ummah) wa mwisho lakini ni wa kwanza siku ya


Qiyaamah. Sisi ni wa kwanza kuingia Peponi ingawa wao


(Mayahudi na Manaswara) walipewa Kitabu kabla yetu nasi


tumepewa baada yao. Allaah Ametuongoza katika haki katika


waliyokhitilafiana kwa idhini Yake. Hii ni siku (Ijumaa)


waliyokhitilafiana, nasi Allah Ametuongoza nayo Hivyo watu


wanatufuata kwani kesho (Jumamosi) ni siku ya Mayahudi na


inayofuatia (Jumapili) ni ya Manaswara)) [Al-Bukhaariy, Muslim,


Musnad Ahmad na wengineo]


3


Ibn Wahb amesema kwamba 'Abdur-Rahmaan bin Zayd bin


Aslam amesema kuwa baba yake amesema kuhusu Aayah hii:


)) ا ف ا ه ا دى الُلّه الََِّّي ا ن آ ا منُواْ لِ ا ما اخْتالافُواْ فِيهِ مِ ا ن الْْاقِّ بِإِذْنِهِ ((


((Ndipo Allaah kwa idhini Yake Akawaongoa walioamini


kuiendea haki katika mambo waliyokhitalifiana))


 Wamekhitilafiana kuhusu siku ya Jamaa (Ijumaa); Mayahudi


wamesema ni Jumamosi, Manaswara wamesema ni Jumapili,


Allaah Akaongoza Ummah wa Muhammad (Swalla Allaahu


'alayhi wa aalihi wa sallam) kufuata Ijumaa.


 Wamekhitilafiana kuhusu Qiblah; Manaswara wameelekea


Mashariki na Mayahudi wameelekea Baytul-Maqdis (Palestina),


Allaah Akaongoza Ummah wa Muhammad (Swalla Allaahu


'alayhi wa aalihi wa sallam) katika Qiblah sahihi (Ka'bah


iliyoko Makkah).


 Wamekhitilafiana kuhusu Swalah; wengine wanarukuu lakini


hawasujudu, wengine wanasujudu lakini hawarukuu, wengine


wanaswali huku wakizungumza na wengine huku wanatembea.


Allaah Amewaongoza Ummah wa Muhammad (Swalla Allaahu


'alayhi wa aalihi wa sallam) katika haki.


 Wamekhitilafiana pia katika kufunga (Swawm); wengine


wanafunga sehemu tu ya siku, wengine wanafunga kujizuia tu


baadhi ya vyakula (vingine wanakula). Allaah Ameongoza


Ummah wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa


sallam) katika haki.


4


 Wamekhitilafiana pia kuhusu Nabii Ibraahiym; Mayahudi


wamesema "Alikuwa ni Myahudi" na Wakristo wakidai ni


Mnaswara. Allaah Amemfanya ni Haniyfam-


Musliman (Muongofu Muislamu) Allaah Ameongoza Ummah wa


Muhammad katika haki.


 Wamekhitilafiana pia kuhusu Nabii 'Iysaa; Mayahudi


wamemkanusha na kumzulia mama yake kuwa kafanya madhambi


makubwa (ya zinaa), Manaswara wamemfanya ni Mungu na mtoto


wa mungu. Allaah Amemfanya kwa maneno Yake ni roho kutoka


Kwake (Kwa Alivyoviumba) Allaah Ameongoza Ummah wa


Muhammad katika haki"


Kisha (muelezeaji) akamalizia maelezo hayo kwa kusema (Kwa


idhini Yake [Allaah]) (kamailivyoendeleza Aayah hiyo tukufu


kuwa sisi Ummah wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa


aalihi wa sallam) tumeongozwa na Allaah kwa Idhini Yake).





((Ndipo Allaah kwa idhini Yake Akawaongoa walioamini


kuiendea haki katika mambo waliyokhitalifiana))


Bibi 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anhaa) amesimulia kuwa


Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa


anapoamka usiku akisoma duaa ifuatayo:





Allaahuuma Rabbi Jibraaiyl wa Miykaaiyl, wa Israafiyl,


Fatwiras-Samawaati wal-ardhw, 'Aalimal-Ghaybi wash-


Shahaadah, Anta Tahkumu bayna 'Ibaadika fiymaa kaanu fiyhi


yakhtalifuun. Ihdiniy lima-khtulifa fiyhi minal-Haqq Biidhnika,


Innaka Tahdiy man Tashaau ilaa Swiraatwim Mustaqiym.


Ee Allaah Mola wa Jibriyl na Mikaaiyl na Israafiyl, Muumba


wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa mambo yaliyojificha na yaliyowazi,


Wewe Unahukumu baina ya waja Wako katika mambo ambayo


walikuwa wakitofautiana, niongoze mimi kwenye haki katika yale


waliotofautiana kwa ruhusa Yako. Hakika Wewe Unamuongoza


Umtakae kwenye Njia Ilionyoka.


Zaidi ya du'aa hiyo inatupasa pia tuombe du'aa ifuatayo daima ili


tubakie katika haki,





Allaahumma Arinal-Haqqa Haqqan War-Zuqnat-tibaa'ah. Wa


Arinal-Baatwila baatwilan War-Zuqnaj-tinaabah. Wa laa taj'alhu


mutalabbisan 'alaynaa Fanadhwilla Waj-'alnaa Lil-Muttaqiyna


Imaama.


Ee Allaah, Tuonyeshe yale yaliyo haki, Uturuzuku tuweze


kufuata (na kutekeleza).


Na Tuonyeshe yaliyo batili (maovu) na Utuongoze tujiepushe


nayo.


Usituchanganye (usitufunike tusiiujue) hakika ya uovu ili


tusipotee kuufuata, na Tujaaliye tuwe viongozi wa Wamumini))


[Takhiryj Al-Ihyaaa 3: 1318].



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI