Nakala

1


KUWA NA TAWHID YA KWELI NI SABABU YA KUPATA MWISHO MWEMA


Imeandaliwa na: Yunus Kanuni Ngenda


Imepitiwa na: Abubakari Shabani Rukonkwa


Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote, na rehma na amani zimwendee kiongozi wa umma huu Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na watu wake na Maswahaba zake wote,! Amma baad.


Muislamu anapokuwa na msimamo katika tawhid, na imani, na ucha Mungu, hubashiriwa Pepo wakati anapofikwa na mauti. Anasema Mwenyezi Mungu mtukufu:





Hakika wale waliosema: “Rabbuna (Mola) wetu ni Allaah.” Kisha wakanyooka (wakawa na msimamo); Malaika huwateremkia


2


(wakati wa kutolewa roho kuwaambia) kwamba: “Msikhofu, na


wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo


mlikuwa mkiahidiwa (kwayo). “Sisi ni marafiki walinzi wenu


katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale


yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale


mnatayoyaomba. “Ni mapokezi kutoka kwa Ghafuwrir-Rahiym


(Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu).” [Fusw-Swilat: 30-


32].


Na amesema Mwenyezi Mungu mtukufu:





Hakika walio sema: “Mola wetu Mlezi ni Mwenyezi Mungu;


kisha wakatengenea (wakawa na msimamo), hawatakuwa na


khofu, wala hawatahuzunika. Hao ndio watu wa Peponi,


watadumu humo, kuwa ni malipo kwa waliyo kuwa


wakiyatenda.” [Surat Ahqaaf: 13-14]


Ukitafakari kwa umakini Aya hizo tukufu, utatambua ya


kwamba mtu kusema “RABBUNA LLAH” pekee! haitoshi kwake


yeye kupata bishara njema, isipokuwa lazima neno hilo


liambatane na:


1.Tauhid ya dhati.


2.Imani ya kweli.


3


3-Msimamo ulio madhubuti.


5.Na matendo yaliyo mema.


Ndiyo maana Mwenyezi Mungu mtukufu mwisho wa Aya


anasema:


“Hao ndio watu wa Peponi, watadumu humo, kuwa ni malipo


kwa waliyo kuwa wakiyatenda.” [Surat Ahqaaf: 13-14]


Tunamuomba Mwenyezi Mungu mtukufu atujaalie tuwe na


tauhid ya kweli katika nyoyo zetu, na atufishe hali ya kuwa ni


waislam wenye imani thabiti, na atuwezeshe kwa rehma zake


tuweze kutenda matendo yaliyo mema ili tupate mwisho


mwema, na atufufue Mola wetu pamoja na Mtume wetu


Muhammad (s.a.w) siku ya Kiyama, Ameen!



 



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI