Nakala

1





FADHILA YA SUNNA ZA MTUME (S.A.W)


Imeandaliwa na: Abubakari Shabani Rukonkwa


Imepitiwa na: Yunus Kanuni Ngenda


Utangulizi:


Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote, na rehma na amani zimwendee kiongozi wa umma huu Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na watu wake na Maswahaba zake wote,! Amma baad.


Ni wazi kwamba Sunna za Mtume wetu Muhammad (s.a.w) ndio kielelezo na uhimili katika dini yetu ya kiislam, pia ndio tafsiri ya mwongozo mzima wa maisha ya mwislam kidini na kijamii kwa ujumla, hivyo mwislam hawezi kuwa na imani thabiti kama hajafuata sunna za Mtume Muhammad (s.a.w).


Hii inamaana kwamba yeyote aliye mbali na sunna basi yuko mbali na dini, na aliyekaribu na sunna yupo karibu na dini, Mwenyezi Mungu mtukufu anatilia mkazo na kuamrisha katika Qur’an pale alipo sema:


2





Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni


jiepusheni nacho. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika


Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.


[Surat Hashri: 7.


Ayah hii tukufu imekusanya sunna zote alizokuja nazo Mtume


wetu Muhammad (s.a.w) ya kwamba hatuna budi kuzipokea na


kuzifanyia kazi, ikiwa ni pamoja na kuzilinda, kuzinusuru na


kuzieneza ulimwenguni kote.


Hili ni jambo kubwa lenye fadhila nyingi kwa yeyote mwenye


kujishughulisha nalo, na ni sababu ya pata mwisho mwema na


kuipata Jannah (Pepo).





Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehma na amani ziwe


juu yake:





Uislam ulianza ni mgeni na utarudi ni mgeni kama ulivyoanza,


lakini habari njema ni kwa wale wanao onekana ni wageni


(maghurabaa). (Pia inasemekana kwamba “TWUUBAA” ni mti


katika miti ya peponi.


3


Na katika riwaya nyingine akaulizwa Mtume (s.a.w): Ewe


Mtume wa Mwenyezi Mungu ni kina nani hao wanao onekana


wageni (maghurabaa)? Akasema Mtume (s.a.w):





Ni watu ambao wanatengeneza (palipo haribika) wanapoharibu


watu (Dini).


Na katika lafdhi nyingine: Hao ni watu ambao wanatengeneza


yaliyo haribiwa na watu kutokana na sunna zangu.





Chanzo: Majumuu fatawa Ibun Baaz namba 3/158.


Na katika Hadithi nyengine.





Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehma na amani ziwe


juu yake: “Umati wangu wote wataingia Peponi isipokua atakae


4


kata”, wakasema (Maswahaba): Ewe Mjumbe wa Mwenyezi


Mungu ni nani basi atake kata? Akasema: “Mwenye kunitii


ataingia Peponi na mwenye kuniasi basi huyo amekataa.”


Ameipoke Imamu Bukhari, katika Hadhithi iliyotokana na Abuu


Hurayra.


Kitabu ni: Swahihi Bukhari ukurasa namba 7280.


Hivyo shime ndugu zngu katika imani tushikamaneni na sunna


za bwana Mtume Muhammad (s.a.w) hata kama jamii itakuona


umekuja na mambo mageni, au hata ukipewa majina yasofaa


hilo usijali bali hata Mtume (S.A.W) aliitwa mchawi a kaitwa


mwendawazimu lakin aliendelea kuitangaza dini na kueneza


Sunna zake (s.a.w).


Mfano ulio hai ni wanislam wanaoifanyia kazi kauli ya bwana


Mtume (s.a.w) ya kupunguza nguo iliyozidi katika kongo mbili


za miguu kwa wanaume utakuta baadhi ya watu wana watukana


na kuwabeza kwa kuwapa majina yasiyofaa kama : njiwa, au


kavaa nguo ya mtoto, au kavaa kimini sketi nk.


Hayo yakikukuta basi usikate tama unatakiwa kushikamana na


sunna tu bila kujali matusi na kebehi za maadui wa haki.


Au kauli za baadhi ya watu kuwa eti huu sio wakati wa


kuambiana kuhusu ndevu, kukata nguo inayozidi chini, na


mfano wa hayo.


5


Hizi zote ni sauti za shari zinazokurudisha nyuma katika kufata


maamrisho ya Mtume wetu Muhammad swallah llah alayhi


wasalam.


Bali juwa kuwa ukifanya bidaa moja basi umeuwa suna


iliyostahiki kuwa mahala hapo.


Na ukishika sunna basi juwa umefanya juhudi kubwa ya kuzuia


bidaa.


Tunamuomba Mwenyezi Mungu mshindi na mtukufu


atudumishe katika Sunna za Mtume wetu Muhammad (s.a.w) na


atukutanishe nae katika Pepo ya Firdausi, pamoja na wema


waliokuja baada yake, Ameen!!.



Machapisho ya hivi karibuni

Mafungamani ya Shahad ...

Mafungamani ya Shahada na Aina za Tawhiid.

Namna ya swala ya mtu ...

Namna ya swala ya mtume (s.a.w). na Namna ya kutawadha

FADHILA YA SUNNA ZA M ...

FADHILA YA SUNNA ZA MTUME (S.A.W)

MAZUNGUMZO KATIKA PEP ...

MAZUNGUMZO KATIKA PEPO NA JAHANNAMU (SEHEMU YA 3 KATI YA 3): NA SITAWAHI WAKASIRIKIA TENA.