Nakala




NASIHA FUPI KWA WAISLMU WAPYA


Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.


1. kumbuka kwamba Uislamu ni wa Allah, Sub-hanahu wa Ta'ala. kwa


hivyo ni muhimu wewe uingie katika Uislamu kwa sababu (na makusudio)


ya Allah pekee, na wala sio kwa kutaka manufaa yoyote ya kibinafsi au kwa


lengo la yasiyokuwa Twaa (kumtii Muumbaji).


2. Binadamu anapoupata ukweli huwa ni wajibu kwake kuushikilia na


kuutetea kwa vyovyote vile, bila kujali yatakavyokuwa matokeo. Zaidi ya


hayo, sharti awe na subira ili aweze kuwa na uthabiti katika huo ukweli


(ambao amupata).


3. kuwapendelea wenzako mema unayoyapenda wewe, ni sehemu ya


shukurani kwa Allah, Aliye juu, Mtukufu aliye mkuu, kwa neema hii ya


Uislamu aliyokutunuku (aliyokupa). Kwa hivyo wakaribishe wenzako, ili nao


wapate sehemu yao ya Neema hii Tukufu (Uislamu).


4. Uislamu sio mali ya mtu yeyote. Sio Mali ya Waarabu kwa kuwatenga


wasiokuwa Waarabu, wala sio Mali ya Matajiri kwa kuwatenga masikini.


Kwa hakika ni uwanja ulio wazi kwa wote, na zaidi ni kwamba aliye Mtukufu


mbele ya Allah kuwashinda wenzie ni yule anayewazidi wenzake katika


kushikamana na mafundisho, kwa kuwa anatenda kama inavyohitajika na


ndiye anayetarajiwa zaidi kuwa katika daraja ya juu siku ya kiama (siku ya


kufufuliwa).


5. Kumbuka kwamba baada ya wewe kuwa Muislamu utapata marafiki


wapya kama watakavyozuka pia maadui - kiongozi wao akiwa Shetwani - na


atajaribu kuweka kizuizi baina yako na Uislamu, au kwa kiwango cha chini


sana, kukuzuilia maendeleo ndani ya dini yako, ili pia usiwanufaishe


wenzako.


6. Allah, mwenye Uwezo wote na Utukufu na Ufalme ndiye Msaidizi wako,


asiyekuwa na shaka. kwa hivyo, kumbuka kwamba ikiwa Allah Atatambua


kwamba wewe ni muaminifu Rohoni mwako, fahamu naye Atakutendea


wema unaofaa Duniani na Akhera.


7. Uislamu ni mfumo wa maisha uliopangwa vizuri, utokao kwa Mola wa


ulimwengu. Na pia ni kama vile katiba. Kuhusu waislamu wote, wao ni


binadamu tu ambao baadhi ya wakati, wanafanya makosa au wanakosea


wakijitahidi kufanya mema. Baadhi yao wanaushikilia Uislamu vyema na


hali kunao walio wapungufu, ki-elimu au ki-tabia au ki-ibada. Kwa hivyo


yeyote miongoni mwao anayetenda yaliyo sawa, ni kutokana na kuwa


anafahamu Uislamu vyema. Na vitendo anavyovitenda vinakuwa ndiyo


sawa. Vile vile anayetenda yasiyo sawa, basi makosa yake yatamletea yeye


madhara. Haiwezekani kuulaumu Uislamu kwa makosa yanayotendwa na


mtu au watu ambao hawakutekeleza vyema mafundisho ya Uislamu.


8. Pengine Waislamu walifurahi sana kwa wewe kujiunga na mila hii (ya


Nabii Ibrahim), na pengine walikukaribisha sana pale mwanzo. Haya ni


kutokana na wanavyokupenda. pamoja na hivyo ni muhimu Allah, Mwenye


Nguvu na Utukufu, aone uaminifu wako katika Roho yako na katika vitendo


vyako.


9. Uislamu ni mfumo ulio na mpangilio wa maisha bora, kama vile Mashule


yanavyokuwa na mpangilio wa kuwalea wanafunzi (yaani Manhaj au


syllabus). Na ni njia ya maisha inayofaa kufuatwa na kufuatiliwa katika


maisha yote. Kwa hivyo, kama unavyoamrisha Uislamu Mtu kuswali,


kufunga (saum), kutoa zaka na sadaka, na kwenda kuhiji Makka, pia


unaamrisha Mtu kuwa muaminifu na mkweli katika maongezi (kauli),


mwenye huruma kwa walio wadhaifu na maskini. Aliye na heshima kwa


wazee na anaishi na watu vizuri. Vile vile kama unavyokataza Uislamu Mtu


kulewa na kuzini (na mke wa watu au binti yao), hivyo hivyo ndivyo


unavyokataza Dhulma, Wivu, Uhasidi na Tabia mbaya. Kwa ufupi Uislamu


unaamrisha kila wema na maarifa yenye manufaa na unakataza kila ubaya


unaodhuru watu (iwe ni Maneno au Vitendo au Itiqadi).


10. Allah Amefanya Maisha ya hii Dunia kuwa pahala pa kufanyiwa Watu


Mtihani ili kupambanua Ukweli na Uwongo, na yaliyo sawa na yaliyo


makosa. Vile vile Allah, Sub-hanahu wa taala, Ametenga mtihani maalumu


kwa Waumini, ili kuchunguza (imani ya) Roho zao. Kwa njaa au umasikini


au maradhi au kuondokewa na wapenzi, kwa mauti au mitihani


aliyoichagua Allah, ili kuwapandisha ngazi (peponi ikiwa walikuwa na


subira na kudumu katika Imani na haki na vitendo vizuri). kwa hivyo


kumbuka ukweli huu unapokuwa Maishani mapya.


11. Ni jambo la dharura kuwa Muislamu anahitajika kuwa mwenye nguvu,


anayefurahia (kujivunia) Maisha yake mapya. Sio lazima kila wakati kuwa


anachukua nafasi ya kujilinda. Badala yake anafaa pia kuwapa watu


aliyonayo yeye (yaani Uislamu), akiwa na heshima zake na kujivunia Dini


yake. kwa ukweli yeye ndiye aliye na bidhaa tukufu na takatifu zaidi. Wakati


huo huo anafaa kuwa mwenye Hikima na mwenye Subira wakati anaongea


na kutekeleza lolote na binadamu wenzake.


12. Uislamu sio tu kutamka LA ILAHA ILLA ALLAH, MUHAMMAD RASUULU


LLAHI. Kwa kweli mfumo wa amri kutoka mbinguni (SHARIA) ndiyo


unaoendesha maisha ya mwanadamu vyema na kikamilifu. Uislamu unazo


hukumu (ahkaam), Aadabu (adabu au mpangilio wa kutekeleza mambo),


Ibaadat (vitendo vya kuabudia) na Muamalaat, yaani tartibu za kutendeana


baina ya Mtu na Watu (katika jamii au biashara). Kwa hivyo inahitaji mtu


kujifundisha Uislamu hatua kwa hatua.


13. Mwisho tunakuhimiza ujiunge na chuo cha kufunza Waislamu wapya.


vyuo ambavyo huwa vimeanzishwa pahali tofauti tofauti katika vituo vya


Da'awa (vituo vya makaribisho), ili upate kuelimika kuhusu mambo yote ya


Uislamu.





ISLAMIC PROPAGATION OFFICE IN RABWAH


P.O. BOX 29465 ARRIYADH 11457-TEL 4454900-4916065


FAX 4970126-e-mail: rabwah @ islamhouse.org


NASIHA FUPI KWA WAISLAMU WAPYA


Tafsiri ya : A brief advice for the new Muslim


Mfasiri : Saleh M. Kyambo


mobile No : +966594370352


Lugha : KISWAHILI








 



Machapisho ya hivi karibuni

UJUMBE KUTOKA KWA MUH ...

UJUMBE KUTOKA KWA MUHUBIRI MUISLAMU KWA MKRISTO

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI