Nakala

Biblia ni maandiko matakatifu ya Uyahudi na Ukristo. Biblia ya Kikristo ina Agano la Kale na Agano Jipya, huku matoleo ya Kikatoliki na ya Kiorthodoksi ya Mashariki ya Agano la Kale yakiwa makubwa kidogo kwa sababu ya kukubalika kwa vitabu fulani ambavyo havikubaliwi kama maandiko na Waprotestanti. Biblia ya Kiyahudi inajumuisha tu vitabu vinavyojulikana kwa Wakristo kama Agano la Kale. Zaidi ya hayo, mipangilio ya vitabu vinavyokubalika vya Wayahudi na vya Wakristo vinatofautiana sana.[1] Mtume Muhammad ametabiriwa katika Agano la Kale na Agano Jipya.





 Yesu na Mitume wake wanaaminiwa kuwa waliongea Kiaramu. Kiaramu kiliendelea kutumika katika matumizi makubwa hadi takriban 650  BK, kilipobadilishwa na Kiarabu. [2] Biblia ya leo, hata hivyo, haitoki kwa miswada ya Kiaramu, bali kwa matoleo ya Kigiriki na Kilatini.





 Kunukuu utabiri wa Biblia haumaanishi ya kwamba Waislamu wanakubali kuwa Biblia ya leo kwa ukamilifu wake ni ufunuo wa Mungu. Kwa imani ya Kiislamu kuhusu maandiko yaliyopita, tafadhali bofya hapa





 Sio sharti kwa nabii kukubalika kuwa lazima atabiriwe na manabii wa awali. Musa alikuwa nabii kwa Farao ingawa hakutabiriwa na mtu yeyote kabla yake. Ibrahimu alikuwa nabii wa Mungu kwa Nimrodi, lakini hakuna mtu aliyetabiri kuja kwake. Nuhu na Lutu na wengine walikuwa manabii wa kweli wa Mungu, lakini hawakutabiriwa. Ushahidi wa ukweli wa nabii hautegemei utabiri wa manabii wa zamani, lakini unajumuisha ujumbe halisi ulioletwa naye, miujiza na zaidi.





 Kujadili mambo ya unabii ni suala nyeti. Inahitaji kuangalia kwa kina matoleo ya Biblia na tafsiri zake, miswada iliyogunduliwa hivi karibuni na kutafuta maneno ya Kiebrania, ya Kigiriki, na ya Kiaramu na kuyachunguza. Kazi inakuwa ngumu zaidi wakati: “kabla ya vyombo vya uchapishaji kuvumbuliwa (karne ya 15), nakala zote za Biblia zinaonyesha tofauti za kimaandishi. “[3] Hili si jambo rahisi kwa watu wa kawaida. Kwa sababu hiyo, ushuhuda bora unatoka kwa wataalamu wa kale na wa kisasa katika mambo hayo ambao walikubali utabiri.





 Tuna kumbukumbu za Wayahudi na Wakristo wa kale, watawa na marabi, ambao walishuhudia kwamba Muhammad alikuwa utimilifu wa utabiri mahususi wa Biblia. Wafuatao ni baadhi ya mifano ya watu hawa.





Mtume Anayesubiriwa


Wayahudi na Wakristo wa Arabia kabla ya Uislamu  walikuwa wakisubiri mtume. Kabla ya kutokea kwa Muhammad, Arabia ilikuwa makao ya Wayahudi, Wakristo, na Waarabu Walioabudu masanamu ambao, mara kwa mara, walikwenda vita kati yao. Wayahudi na Wakristo wangesema: 'Wakati umefika wa Nabii asiye andika wala kusoma atakayefufua dini ya Ibrahimu kutokea. Na tutaungana naye, na tutapigana vita vikali dhidi yenu.' Muhammad alipotokea, baadhi yao walimuamini, na wengine walikataa. Hii ndiyo sababu Mungu alifunua:





"Na kilipo wajia Kitabu [Kurani] kitokacho kwa Mwenyezi Mungu kinacho thibitisha waliyo nayo- na wao walikuwa wakitafutia ushindi kuwashinda makafiri- yalipo wajia yale waliyo kuwa wakiyajua waliyakanusha. Basi laana ya Mwenyezi Mungu juu yao wakanushao." (Kurani 2:89)





Shahidi wa kwanza alikuwa Buhra, mtawa Mkristo, aliyetambua unabii wa Muhammad alipokuwa bado mdogo na kumwambia mjomba wake:





"…Mpwa wako ana bahati kubwa mbele yake, hivyo mrudishe nyumbani haraka."[4]





Shahidi wa pili alikuwa Waraqah ibn Nawfal, msomi Mkristo aliyefariki punde baada ya mkutano wa faragha na Muhammad. Waraqah alimshuhudia Muhammad kuwa alikuwa Nabii wa wakati wake na kupokea ufunuo kama Musa na Yesu.[5]





Wayahudi wa Madina walikuwa wakisubiri kwa hamu kuwasili kwa nabii. Mashahidi wa tatu na wa nne walikuwa Marabi wao maarufu wa Kiyahudi, Abdullah ibn Salam na Mukhayriq.[6]





 Mashahidi wa sita na wa saba walikuwa pia rabi wa Kiyahudi wa Yemeni, Wahb ibn Munabbih, na Ka'b al-Ahbar (alikufa 656 BK). Ka'b alipata vifungu vingi vya sifa na maelezo ya Nabii yaliyotabiriwa na Musa katika Biblia.[7]





Quran inasema:





"Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?" (Quran 26:197)





Kumbukumbu la Torati 18:18  "Mimi (Mwenyezi Mungu) nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe (Musa), nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.'





Wakristo wengi wanaamini utabiri huu uliotabiriwa na Musa unahusu Yesu. Hakika Yesu alitabiriwa katika Agano la Kale, lakini kama itakavyokuwa wazi, utabiri huu haufanani naye, bali unaafikiana zaidi na Muhammad, rehema na baraka za Mungu ziwe juu yake. Musa alitabiri yafuatayo:





1.       Mtume huyo atakuwa kama Musa


.





Kipengele cha Ulinganisho





Musa





Yesu





Muhammad





Kuzaliwa





alizaliwa kawaida





alizaliwa kimiujiza, mama yake alikuwa bikira





alizaliwa kawaida





Lengo





Mtume tu





Inasemekana ni mtoto wa Mungu





Mtume tu





Wazazi





baba na mama





mama pekee





baba na mama





Maisha ya kifamilia





alioa na kuzaa watoto





hakuoa





alioa na kuzaa watoto





Kukubaliwa na watu wake





Wayahudi walimkubali





Wayahudi walimkataa[1]





Waarabu walimkubali





Mamlaka ya kisiasa





Musa alikuwa nao (Hesabu 15:36)





Yesu aliukataa[2]





Muhammad alikuwa nao





Ushindi juu ya wapinzani wake





Farao alikufa majini





inasemekana alisulubiwa





Watu wa Makka walishindwa





Kifo





Kifo cha kawaida





inadaiwa kuwa alisulubiwa





Kifo cha kawaida





Kuzikwa





alizikwa kwa kaburi





kaburi tupu





alizikwa kwa kaburi





Uungu





si mungu





wakristo wanaamini ni mtoto wa mungu





si Mungu





Alianza uhubiri kwa umri wa





40





30





40





Kufufuka duniani





hakufufuka





inadaiwa alifufuka





hakufufuka








2.       Nabii aliyesubiriwa atatoka kati ya Ndugu wa Wayahudi


Aya tunayoongelea ni wazi kwa kusema kwamba nabii atatokea miongoni mwa Ndugu wa Wayahudi. Ibrahimu alikuwa na wana wawili: Ishmaeli na Isaka. Wayahudi ni wazao wa mwana wa Isaka, Yakobo. Waarabu ni watoto wa Ishmaeli. Hivyo, Waarabu ni ndugu wa taifa la Kiyahudi.[3] Bibilia inasema:





‘Naye (Ishmaeli) atakaa mbele ya uso wa ndugu zake wote.’ (Mwanzo 16:12)





‘Naye (Ishmaeli) akakata pumzi, akafa. Akakusanywa kwa watu wake.’ (Mwanzo 25:18)





Wana wa Isaka ni ndugu wa Waishmaeli. Vivyo hivyo, Muhammad ni miongoni mwa ndugu wa Waisraeli, kwa sababu alikuwa mzao wa Ishmaeli mwana wa Ibrahimu.





 


3.       Mungu Ataweka Maneno Yake katika Mdomo wa Nabii Anayesubiriwa


Kurani inasema kuhusu Muhammad:





"Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ufunuo ulio funuliwa (Kurani 53:3-4)





Hii inafanana sana na fungu la Kumbukumbu la Torati 18:18:





"nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao, mfano wako wewe (Musa), nami nitatia maneno yangu kinywani mwake; naye atawaambia yote nitakayomwamuru." (Kumbukumbu la Torati 18:18)





 Nabii Muhammad alikuja na ujumbe kwa walimwengu wote, na kutoka kwao, Wayahudi. Wote, ikiwa ni pamoja na Wayahudi, wanapaswa kukubali unabii wake, na hii inasadikishwa na maneno yafuatayo:





"MWENYEZI MUNGU, Mungu wenu atawateulieni nabii aliye kama mimi kutoka miongoni mwenu, nanyi mtamsikiliza huyo." (Kumbukumbu la Torati 18:15)





 


4.       Onyo kwa Watakaokataa


Utabiri unaendelea:





Kumbukumbu la Torati 18:19  "Yeyote ambaye hatasikia maneno atakayosema nabii huyo kwa jina langu, mimi mwenyewe nitamwadhibu."





Waislamu, kwa upande mwingine, huanza kila sura katika Kurani kwa jina la Mungu kwa kusema:





Bismillah ir-Rahman ir-Raheem





"‘Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu"





 Yafuatayo ni masimulizi ya baadhi ya wasomi walioamini kuwa utabiri huu unamfaa Muhammad.





Shahidi wa Kwanza





Abdul-Ahad Dawud, ambaye alikuwa Mchungaji zamani, ambapo aliitwa kwa wakati huo David Benjamin Keldani, BD, padri Mkatoliki wa madhehebu ya Umoja wa Wakaldayo (soma wasifu wake hapa).Baada ya kukubali Uislamu, aliandika kitabu kinachoitwa, 'Muhammad katika Biblia. ' Anaandika kuhusu utabiri huu:





“Kama maneno haya hayamuongelei Muhammad, basi bado hayajatimia. Yesu mwenyewe hakudai kamwe kuwa yeye ndiye nabii aliyetajwa. Hata wanafunzi wake walikuwa na maoni sawa: walisubiri ujio wa pili wa Yesu ili utabiri utimie (Matendo ya Mitume 3:17-24). Hadi sasa ni dhahiri kwamba ujio wa kwanza wa Yesu haukuwa ujio wa Nabii huyo na ujio wake wa pili hauwezi kutimiza maneno hayo. Yesu, kama inavyoaminiwa na Kanisa lake, atatokea kama Hakimu wala si kama mtoaji sheria; lakini aliyeahidiwa atakuja na “sheria ya moto” katika mkono wake wa kuume."[4]





Shahidi wa Pili





Muhammad Asad alizaliwa kama Leopold Weiss mwezi Julai 1900 katika mji wa Lvov (Lemberg ya Kijerumani), ambao sasa upo nchini Poland, ambayo ilikuwa chini ya Dola la Austria. Alikuwa mzawa wa ukoo ambao ulikuwa na mstari mrefu wa marabi , mstari uliovunjwa na baba yake, ambaye alichagua kuwa wakili. Asad mwenyewe alipata elimu nyingi ya dini ambayo ingemruhusu kuendeleza mila ya familia ya urabbi. Alikuwa mjuzi katika Kiebrania akiwa mdogo na pia alikuwa akifahamu Kiaramu. Alikuwa amejifunza Agano la Kale  katika mfumo wake asili pamoja na maandishi na maoni ya Talmud, Mishna na Gemara, na alikuwa amejiingiza katika mambo ya undani ya ufafanuzi wa Biblia, Targum.[5]





Akiongelea aya ya Kurani:





"Wala msichanganye kweli na uwongo na mkaificha kweli nanyi mnajua." (Kurani 2:42)





Muhammad Asad anaandika:





“Kwa 'kuichanganya ukweli kwa uwongo '  maana ni kupotosha maandishi ya Biblia, ambayo Qur'ani mara nyingi huwashtaki Wayahudi (na ambayo tangu hapo imethibitishwa kwa upinzani wa kweli wa maandishi), huku 'kuficha ukweli' inahusu kutokujali kwao au kupeana tafsiri ya uongo kwa makusudi kuhusu maneno ya Musa katika kifungu cha Biblia, 'Mungu wenu atawateulieni nabii aliye kama mimi kutoka miongoni mwenu, nanyi mtamsikiliza huyo." (Kumbukumbu la Torati 18:15) na maneno yanayosemekana ni ya Mungu mwenyewe, 'nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao, mfano wako wewe (Musa), nami nitatia maneno yangu kinywani mwake; naye atawaambia yote nitakayomwamuru." (Kumbukumbu la Torati 18:18) “Ndugu” wa wana wa Israeli ni wazi kuwa ni Waarabu, na hasa kundi la Musta'riba ('Walioarabishwa') miongoni mwao, ambalo linaingilia ukoo wa Ishmaeli na Ibrahimu; na kwa kuwa ni kundi hili ambalo kabila la Nabii wa Arabia linatoka, yaani Quraish, vifungu vilivyo juu vya Biblia vinapaswa kuchukuliwa kumaanisha ujio wake."[6]





Yohana 14:16  "Nami nitamwomba Baba, naye atawapeni Msaidizi mwingine akae nanyi siku zote." 





 Katika aya hii, Yesu anaahidi kwamba “Msaidizi” mwingine atatokea, na hivyo, ni lazima tuzungumze baadhi ya masuala kuhusu huyu “Msaidizi”.





Neno la Kigiriki paravklhtoß, ho parakletos, limetafsiriwa kama 'Msaidizi.' Parakletos kwa usahihi ina maana 'yule anayeomba kwa niaba ya mwingine, mwombezi.'[1] Ho parakletos (Msaidizi ) ni mtu katika lugha ya Kigiriki, si kipengele kisichokuwa na mwili. Katika lugha ya Kigiriki, kila nomino ina jinsia; yaani, ni kiume, kike au ni huru. Katika Injili ya Yohana, Sura 14, 15 na 16 ho parakletos ni mtu halisi. Viwakilishi vyote kwa Kigiriki lazima vikubaliane kijinsia na neno ambalo vinawakilisha, na kiwakilishi “yeye(kiume)” kimetumika kurejelea parakletos. Agano jipya linatumia neno pneuma, ambalo linamaanisha “pumzi” au “roho,” na lina maana sawa na neno ruah, neno la Kiebrania linalo maanisha “roho” linalotumiwa katika Agano la kale. Pneuma ni neno la kisarufi huru na daima linawakilishwa na kiwakilishi “ni.”





  Biblia zote za kisasa zimekusanywa kutoka “miswada ya kale,”ambapo mswada wa zamani zaidi ni wa karne ya nne B.K. Hakuna miswada miwili ya kale inayofanana. [2] Biblia zote za leo zinaandikwa kwa kuchanganya miswada bila kumbukumbu moja ya uhakika. Watafsiri wa Biblia hujaribu “kuchagua” toleo sahihi. Kwa maana nyingine, kwa kuwa hawajui ni “mswada wa kale” upi ndio sahihi, wanaamua kwa niaba yetu ni “toleo” lipi la aya fulani ndio sahihi.  Chukua Yohana 14:26 kama mfano. Yohana 14:26 ndiyo aya pekee ya Biblia inayohusisha Parakletos na Roho Mtakatifu. Lakini “miswada ya kale” hayakubali kuwa “Parakletos” ndiye 'Roho Mtakatifu. ' Kwa mfano, Kodeks Syriakus, iliyoandikwa takriban karne ya tano B.K., na kugunduliwa  mwaka wa 1812 juu ya mlima Sinai, maandishi ya 14:26 yanasoma; “Paraklete, Roho”; na si “Paraklete, Roho Mtakatifu.”





Kwa nini hii ni muhimu? Kwa sababu katika lugha ya Biblia, “roho,” inamaanisha tu “nabii.”





“Wapendwa, msiamini kila roho bali zipimieni roho zote kwa makini muone kama zinatoka kwa Mungu: Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea duniani."[3]





Ni jambo la kuelimisha kujua kwamba wasomi kadhaa wa Bibilia waliona parakletos kuwa 'mwokovu huru (aliye na uwezo wa kuokoa), 'na si Roho Mtakatifu.[4]





Swali, basi, ni: Je, parakletos wa Yesu, Msaidizi,alikuwa ni 'Roho Mtakatifu' au mtu - nabii - ambaye angekuja baada yake? Ili kujibu swali, ni lazima tuelewe maelezo ya ho parakletos  na kuona kama yanaafikiana na roho au mwanadamu.





Tunapoendelea kusoma zaidi ya sura ya 14:16 na sura ya 16:7, tunaona kwamba Yesu anatabiri maelezo maalum ya kuwasili kwa na utambulisho wa parakletos. Kwa hiyo, kulingana na Yohana 14 na 16  tunagundua mambo yafuatayo.





1.      Yesu alisema parakletos ni mwanadamu:


Yohana 16:13 "Atanena..."





Yohana 16:7 "…kwa maana nisipoondoka, yule Msaidizi hatakuja kwenu."





Haiwezekani kwamba Msaidizi awe ni “Roho Mtakatifu” kwa sababu Roho Mtakatifu alikuwepo kwa muda mrefu kabla ya Yesu na wakati wa huduma yake.[5]





Yohana 16:13 Yesu alimwongelea paraklete kama 'yeye' na si kama 'kitu' kwa mara saba, hakuna mstari mwingine katika Biblia ambao una viwakilishi saba vya kiume. Kwa hivyo, paraklete ni mtu, na sio roho.





2.      Yesu anaitwa parakletos:


"Lakini kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye mtetezi (parakletos) wetu kwa baba, Yesu Kristo mwenye haki." (1 Yohana 2:1)





Hapa tunaona kwamba parakletos ni mwombezi aliye na mwili na ni mwanadamu.





3.      Uungu wa Yesu ni Uvumbuzi uliokuja baadaye


Yesu hakukubaliwa kuwa mungu hadi Baraza la Nikea, 325 BK, lakini kila mtu, isipokuwa Wayahudi, anakubaliana kuwa alikuwa nabii wa Mungu, kama ilivyoonyeshwa na Biblia:





Matayo 21:11 "...Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya."





Luka 24:19 "...Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele za wanadamu."





4.      Yesu alimwomba Mungu awape parakletos mwingine:


Yohana 14:16 "Nami nitamwomba Baba, naye atawapeni Msaidizi mwingine akae nanyi siku zote."





5.      Yesu anaeleza jukumu la Yule Parakletos Mwingine:


Yohana 16:13 "Atawaongoza muijue kweli yote."





Mwenyezi Mungu anasema katika Kurani kuhusu Muhammad:





"Enyi Watu! Amekwisha kujieni Mtume huyu na haki itokayo kwa Mola wenu Mlezi. Basi aminini, ndiyo kheri yenu.!..." (Kurani 4:170)





Yohana 16:14 "Atanitukuza mimi."





Kurani aliyokuja nayo Muhammad inamtukuza Yesu:





"…Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).." (Kurani 3:45)





Muhammad pia alimtukuza Yesu:





"Yeyote atakaye shuhudia ya kwamba hakuna anayestahili kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu, ambaye hana mshiriki, na kuwa Muhammad ni mja wake na Mtume wake, na Isa ni mja wa Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na neno lake alilo mpea Maryamu, na roho iliyotoka kwake, na kuwa Pepo ni kweli, na Jahannamu ni kweli, Mwenyezi Mungu atamkaribisha kwa Pepo kulingana na yale aliyo yatenda.." (Saheeh Al-Bukhari, Saheeh Muslim)





Yohana 16:8 "Naye akija atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, na haki na hukumu ."





Kurani inaeleza:





"Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu! Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru. !’" (Kurani 5:72)





Yohana 16:13 "Yeye hatanena kwa uwezo wake mwenyewe, bali atanena yote atakayosikia."





Kurani inasema kuhusu Muhammad:





"Wala hatamki kwa matamanio.Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa." (Kurani 53:3-4)





Yohana 14:26 "atawafundisha mambo yote, na kuwakumbusha yote."





Maneno ya Kurani:





"…Na hali Masihi mwenyewe alisema, ‘Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi.’" (Kurani 5:72)





…yanawakumbusha watu amri kuu na ya kwanza ya Yesu, ambayo wameisahau:





"Ya kwanza ndiyo hii: ‘Sikiliza Israeli! Bwana Mungu wetu, ndiye peke yake Bwana.’" (Marko 12:29)





Yohana 16:13 "atawafundisha kuhusu mambo yote yajayo."





Kurani inasema:





"Hizi ni katika khabari za ghaibu tulizo kufunulia, [Ewe Muhammad]…" (Kurani 12:102)





Hudhaifa, mwanafunzi wa Mtume Muhammad, anatuambia:





"Mtume, rehma ziwe juu yake, aliwahi kusimama kati yetu na kutoa hotuba, ambapo hakuacha chochote bali alituambya yote yatakayotokea hadi siku ya kiama ." (Saheeh Al-Bukhari)





Yohana 14:16 "akae nanyi siku zote."





…maana yake ni kuwa mafundisho yake ya awali yatabaki milele. Muhammad alikuwa nabii wa mwisho wa Mungu kwa wanadamu. [1] Mafundisho yake yamehifadhiwa kikamilifu. Anaishi ndani ya mioyo na akili za wafuasi wake wanaomwabudu Mungu kwa kumuiga Muhammad kisawasawa. Hakuna mtu, ikiwa ni pamoja na Yesu au Muhammad, anayeishi milele duniani. Na Parakletos si kesi ya kipekee pia. Hili haliwezi kuwa linamzungumzia Roho Mtakatifu, kwani imani ya kisasa ya Roho Mtakatifu haikuwepo kabla ya Baraza la Kalsedoni , mnamo 451 BK, karne nne na nusu baada ya Yesu.





Yohana 14:17 "huyo ndiye roho wa kweli"





…maana atakuwa nabii wa kweli, tazama 1 Yohana 4: 1-3.





Yohana 14:17 "ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea kwa kuwa haumwoni..."





Watu wengi duniani leo hawamjui Muhammad.





Yohana 14:17 "...wala haumtambui"





Wachache zaidi ndio wanaomtambua Muhammad wa kweli, Mtume wa Rehema wa Mungu.





Yohana 14:26 "yule Msaidizi (parakletos)"





Muhammad ndiye atakuwa mtetezi wa wanadamu kwa ujumla na Waumini wenye madhambi siku ya kiama:





Watu watawatafuta wanaoweza kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu kwa niaba yao ili kupunguza dhiki na mateso Siku ya Kiyama. Adamu, Nuhu, Ibrahimu, Musa na Yesu watajitoa na kupeana udhuru zao.





Kisha watakuja kwa Nabii wetu, naye atasema: 'Hakika mimi ndiye mwenye uwezo'. Kisha atawaombea watu katika uwanja mkubwa ambapo watu wamekusanyika, hukumu itolewe. Hiki ndicho 'Cheo kilicho sifika ' ambacho Mungu anamuahidi katika Qur'an:





"…Huenda Mola wako Mlezi akakunyanyua cheo kinacho sifika (heshima ya kuwa mwombezi siku ya kiyama)" (Kurani 17:79)[2]





Mtume Muhammad alisema:





"Maombezi yangu yatakuwa kwa wale wa taifa langu waliotenda dhambi kuu." (Al-Tirmidhi)





"Mimi nitakuwa mwombezi wa kwanza katika Peponi.." (Saheeh Muslim)





Baadhi ya wasomi wa Kiislamu wanaonyesha kuwa kile ambacho Yesu alisema kwa Kiaramu kinawakilisha kwa karibu zaidi neno la Kigiriki periklytos ambalo linamaanisha 'anayependwa.' Kwa Kiarabu neno 'Muhammad' linamaanisha 'anayesifiwa, anayeheshimiwa. ' Kwa maana nyingine, periklytos ni “Muhammad” kwa Kigiriki. Tuna sababu mbili kuu za kuunga mkono jambo hili. Kwanza, kutokana na matukio kadhaa yaliyorekodiwa ya kubadilisha maneno yanayofanana katika Bibilia, inawezekana kwamba maneno yote mawili yalikuwa katika maandishi ya awali lakini yaliwachwa na mwandishi kwa sababu ya desturi ya kale ya kuandika maneno yakikaribiana, bila nafasi katikati. Katika hali kama hiyo maandishi ya awali yangekuwa, “na atawapa msaidizi mwingine (parakletos), anayependwa (periklytos).” Pili, tuna ushuhuda wa kuaminika wa angalau wasomi wanne wa Kiislamu kutoka kwa vipindi tofauti ambao waliwahesabia wasomi wa Wakristo kuwa 'wa kusifiwa' ndio maana inayowezekana ya neno la Kigiriki au la Kisyriak .[3]





Wafuatao ni kati ya wale walioshuhudia kwamba Paraklete inamrejelea Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake:





Shahidi wa Kwanza


Anselm Turmeda (1352/55-1425 BK), kuhani na msomi wa Kikristo, alikuwa shahidi wa utabiri huu. Baada ya kukubali Uislamu aliandika kitabu, "Tuhfat al-arib fi al-radd ‘ala Ahl al-Salib."





Shahidi wa Pili


Abdul-Ahad Dawud, ambaye ni Mchungaji wa zamani David Abdu Benjamin Keldani, BD, padri Mkatoliki wa madhehebu ya Umoja wa Wakaldayo. [4] Baada ya kukubali Uislamu, aliandika kitabu, 'Muhammad katika Biblia. ' Anaandika yafuatayo katika kitabu chake:





“Hakuna shaka hata kidogo kwamba neno “Periqlyte,” inamlenga Nabii Muhammad, yaani Ahmad."





Shahidi wa Tatu


Muhtasari wa maisha ya Muhammad Asad tayari imetolewa hapo juu. Akitoa maoni yake kuhusu mstari huo:





"…Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad" (Kurani 61:6)





…ambapo Yesu anatabiri kuja kwa Muhammad, Asad anaelezea kuwa neno Parakletos:





"…bila shaka ni Periklytos ('anayesifiwa kwa wingi'), iliyo badilishwa, na ni tafsiri halisi ya Kigiriki ya neno au jina la Kiaramu la Mawhamana. (Ikumbukwe kwamba Kiaramu ilikuwa lugha iliyotumiwa Palestina wakati wa Yesu, na kwa karne kadhaa baada yake, na hivyo bila shaka ilikuwa lugha ambayo maandiko ya kiasili -ambayo yamepotea kwa sasa - ya Injili yalitungwa.) Kwa mtazamo wa ukaribu wa kimatamshi kati ya Periklytos na Parakletos, ni rahisi kuelewa jinsi mfasiri - au, labda zaidi, mwandishi wa baadaye - aliyachanganya maneno haya mawili. Ni muhimu kwamba maneno ya Kiaramu Mawhamana na Periklytos ya Kigiriki yana maana sawa na ni majina mawili ya Mtume wa Mwisho, Muhammad na Ahmad, ambayo yote yametokana na kitenzi cha Kiebrania hamida ('alisifu') na nomino ya Kiebrania hamd ('sifu').”



Machapisho ya hivi karibuni

FADHILA YA KUFUNGA SI ...

FADHILA YA KUFUNGA SIKU SITA ZA SHAWAL

Masuala kumi muhimu n ...

Masuala kumi muhimu na mafupi kuhusu mwezi wa Muharram

UJUMBE KWA ALIYEICHOM ...

UJUMBE KWA ALIYEICHOMA KURANI

KWANINI UISLAMU? UZU ...

KWANINI UISLAMU? UZURI NA FAIDA ZA UISLAMU